Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,402
- 114,343
Hongera Mkuu kwa kukubali, lakini hiyo ni mojawapo ya kuufanya mnakasha unoge na kuwa na mashiko.
Kweli Mkuu, watu walibisha sana kwa kudanganywa na kura za maoni, hawakujua kuwa chombo chaeza zama kingali karibu kutia nanga.Nakubali kuchemka ila pia kuna watu nawacheka kwa dharau sana humu ndani leo.
Siku zaidi ya 500 na ushee kabla ya uchaguzi kuna watu walikuwa wanaziangalia hizo zinazoitwa kura za maoni na kuchekelea eti Hillary atashinda kwa vile tu zilikuwa zinamwonyesha yuko juu.
Nikajaribu kuwaambia kuwa kura pekee zenye maana na zinazohesabika ni zile zinazopigwa siku ya uchaguzi na si hizo za maoni, lakini nikawa nabishiwa.
Nani analia na nani anacheka leo?
Ujinga ni mbaya sana na hao wajinga leo nawacheka kwa dharau.
Mkuu fakalava naona umeamua kwenda kufukua makaburi. Niliongea sana, na nikiwasihi sana watu waachane na hizo media watafute habari zaidi lakini hawakunielewa. Hata George Betram leo amekumbushia hili. Kama hizo posts zote ulizozi quote hapo ni mimi peke yangu naonekana kumuunga mkono Trump na kuelewa kinachoendelea huku nikiwasihi wengine wajaribu kuanalia kwa macho na akili zao badala ya media lakini wapi...Kuna wadau humu hasa kwenye huu mnakasha waliwahi kupost kuhusu Donald Trump kama zinavyosomeka.
Big up sana...Nakubali kabisa kuwa nilichemka.
Hongera Mkuu, maana ulikuwa kama jeshi la mtu mmoja.Mkuu fakalava naona umeamua kwenda kufukua makaburi. Niliongea sana, na nikiwasihi sana watu waachane na hizo media watafute habari zaidi lakini hawakunielewa. Hata George Betram leo amekumbushia hili. Kama hizo posts zote ulizozi quote hapo ni mimi peke yangu naonekana kumuunga mkono Trump na kuelewa kinachoendelea huku nikiwasihi wengine wajaribu kuanalia kwa macho na akili zao badala ya media lakini wapi...
Eitherway, yameshakuwa yaliyopangwa kuwa.
"Clinton also spoke directly to the women who supported her historic candidacy, calling it “one of the greatest honors” of her life and asking them to not give up their fight. “To all the little girls watching this, never doubt that you are powerful and valuable and deserving of every chance in the world.”
Very true kui, but it won't be easy especially taking into consideration that Dems right now they don't have a leader.
Jamaa anamwaga mapovu balaa. Nakumbuka alialikwa hadi kwenye debate.
America inayoweza kuongozwa na mwanamke apa duniani ni American chips tu ya kinondoni
Si mlisema haya semeni tena TB Joshua nyieInaonekana na wewe ni conspiracy theorist, baadhi ya tuhuma ulizoandika dhidi ya mama Clinton hazina uthibitisho isipokuwa ni uzushi tu kutoka right wing websites.
Trump ni racist toka zamani miaka ya 70 hakutaka blacks wapange kwenye majengo yake, kuwaita Mexicans, Latinos kwamba ni rapist (hapo amepoteza makundi mawili yenye nguvu sana kwenye ballot box). Trump ni sexist sana kwa kuwajaji wanawake kutokana na muonekano wao na pia ame wadhalilisha wanawake wengi tu kijinsia kwa kuwashika, kuwabusu bila ridhaa zao. Kashfa kama hii ilimuondoa Herman kaine kwenye uchaguzi wa chama cha Republican mwaka 2012.
Hawezi kushinda uchaguzi kwa sababu ame alienate makundi makubwa na muhimu sana katika uchaguzi ambayo ni blacks, Latinos na women.