kuelekea 2025

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Amani Golugwa: CHADEMA kutosaini kanuni za uchaguzi Mkuu 2025, tupo sawa

    Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani Golugwa amesema msimamo wa chama hicho kutosaini kanuni za uchaguzi Mkuu 2025, wanajiona wako sawa huku akikisisitiza hawatakimbilia kusaini zaidi ya kufichua yasiyofaa. “Tunaona tunaenda sawa kabisa na watu...
  2. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Heche awataka wananchi kuunga mkono msimamo wa 'No Reforms No Election'

    Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, amewataka wananchi kuendelea kuwaunga mkono katika kuhakikisha yanafanyika mabadiliko ya sheria za uchaguzi, ili kufanya siasa safi na kushiriki uchaguzi ambao watapatikana viongozi bora na watakaoleta mabadiliko kwa...
  3. M

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Tuseme ukweli: CHADEMA msithubutu kugomea uchaguzi maana hata Ulaya na Marekani sasa hivi wana matatizo yao kiuchaguzi na hakuna wa kuwaogopa tena

    Kila taifa SASA HIVI linajiendesha kwa mtazamo na matakwa yake kiuchaguzi... Dunia imebadilika kwa haraka sana...ULAYA na MAREKANI nao zile rafu tulizozea kuchezwa Afrika kwao ndio zinachezwa kwa uwazi Kila kiumbe kinaona.. Angalieni chaguzi za HIVI karibuni za Afrika licha ya mapungufu kibao...
  4. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Amos Makalla: CCM haijiweki yenyewe madarakani, Watanzania ndio wanaamua

    Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla amesema madai kwamba Chama Cha Mapinduzi kinajiweka madarakani ni dhana potofu. Akizungumza katika mkutano wa hadhara mjini Newala mkoani Mtwara leo Jumanne Aprili 16, 2025, Makalla amesema: "Wapo wanaosema wamekichoka CCM...
  5. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Musukuma: CHADEMA waruhusiwe hata kwa mlango wa nyuma, tukutane nao majukwaani

    Mbunge wa Geita Vijijini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Joseph Kasheku ‘Musukuma’ amesema kwa niaba ya Wabunge wa CCM, hawana hofu na vyama vya upinzani na kwamba wako tayari kukutana nao majukwaani endapo uchaguzi mkuu utafanyika. Akizungumza leo Aprili 16, 2025, Bungeni jijini Dodoma...
  6. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Mwenyekiti wa UVCCM Mohammed Kawaida: Viongozi bora hawawezi kutoka nje ya CCM

    Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohammed Kawaida akizungumza na Wakazi wa Lugarawa - Ludewa Njombe. Sisi tumeshakaa mguu sawa kwenda uchaguzi wa mwaka 2025. Twendeni kwenye uchaguzi tukiwa katika hali ya amani, hali ya umoja kuchakua viongozi wetu watakao tuletea maendeleo na nyinyi mtakubalina na...
  7. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Mchungaji Peter Msigwa: Hao wanaosema haki, kwao hakuna haki. Wanaosema demokrasia, kwao hakuna demokrasia

    Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mchungaji Peter Msigwa, amewataka wananchi wa Wilaya ya Tandahimba, mkoani Mtwara, kuendelea kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na chama hicho tawala, akieleza kuwa mafanikio ya sekta ya korosho ni ushahidi tosha wa uongozi imara na wenye...
  8. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Waziri Aweso apanda na Suti yake kwenye Tenki kukagua mradi wa Maji Dodoma

    Waziri wa Maji Jumaa Aweso ametembelea na kukagua ujenzi wa Miradi ya Majisafi katika Kata ya Nala na Nkuhungu ili kuona maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo. Katika ziara hiyo Waziri wa Maji ameambatana na Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde. Aweso ametoa wiki...
  9. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Mbowe amjulia hali Tundu Lissu, Wateta kwa saa moja Gerezani

    Wakuu! Hawa G-55 watakuwa na hali gani huko waliko kama kweli Mbowe, anayedaiwa kuwa nyuma yao ameenda kumtembelea TAL? === Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe akiambatana na Salum Mwalimu aliyekuwa Naibu katibu Mkuu wa Chama hicho Zanzibar pamoja na...
  10. JamiiForums Tanzania Katibu wa CCM kata ya Mlali alalamika kupigwa na Diwani walipokuwa kwenye kikao

    Katibu wa Chama cha Mapinduzi Kata ya Mlali Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Herieth Ngonde amedai kushambuliwa na Diwani wa kata hiyo aliyetambulika kwa Frank Mwananziche kwa kupigwa wakati wa kikao cha siasa kilichokuwa kinajadili maendeleo ya chama hicho Akizungumza na wanahabari katibu wa...
  11. JamiiForums Tanzania Wana CCM Mnadhani ni ipi ilikua njia mbadala ya NO REFORMS NO ELECTION ?

    Daima huwa nnawalaumu Sana Wana Chadema kwakuwa wabwatukaji, na watu wa maneno ya fedheha na dhihaka Huku wakikosa kabisa kuwa watu wenye kutoa hoja na kusimama hoja zao. Hiki ni kilema serious Sana kwa Hawa mambwana as per my very own personal observation and experience upon being around...
  12. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Stephen Wasira akutana na Kadinali Protase Rugambwa Tabora

    Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amekutana na kufanya mazungumzo na Muadhama Kadinali Protase Rugambwa katika Jimbo Kuu Katoliki la Tabora. Wasira amekutana na Kadinali Rugambwa leo Aprili 16, 2025 katika Jimbo Kuu Katoliki Tabora akiwa katika ziara...
  13. JamiiForums Tanzania Utaratibu mpya wa kupata Wagombea Ubunge na Udiwani CCM ni kupunguza Rushwa au Kuengua wote wanaoonesha Upinzani kwa Serikali?

    Wakuu, Machi 7 Amos Makalla alisema CCM kwenye kikao cha ndani ilifanya marekebisho makubwa mawili katika mchakato wa uteuzi. Kwanza, kutakuwa na uchujaji wa wagombea kabla ya kura za maoni, tofauti na awali ambapo jina moja lilikuwa likirudishwa moja kwa moja. Pili, hakuna mgombea atakayepita...
  14. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Musukuma ataka wateule wa Rais wanaotaka ubunge wakaguliwe na CAG

    Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Musukuma amemshauri Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohammed Mchengerwa kuwapima wateule wa Rais wanaotaka kugombea ubunge kabla ya kuruhusiwa. Ameyasema hayo leo, Jumatano Aprili 15, 2025 bungeni alipokuwa...
  15. S

    JamiiForums Tanzania Makalla: CCM imesogeza mbele muda wa kuchukua fomu

    Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza kusogeza mbele ratiba ya mchakato wa ndani wa uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge, ujumbe wa Baraza la Wawakilishi na udiwani kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, baada ya kupitia ushauri kutoka kwa wanachama wake.
  16. R

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Msukuma ataka watumishi wa umma na wateule wa Rais wadhibitiwe wasichukue pesa za serikali kwenda kugombea ubunge

    Mzee Msukuma amekiri kwamba wabunge wa Tanzania wana kinga dhidi ya tuhuma za rushwa Kimantiki amesema wapo viongozi wanakwapua fedha za umma kwenda kuzitumia kugombea ubunge Ameeleza viongozi wengi wa umma wameomba kugombea lakini akataka wasipewe idhini hadi wafanyiwe special audit Je...
  17. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Gambo aibua tuhuma za ufisadi wa mabilioni Arusha, Spika Tulia amwagiza Mchengerwa kuandaa ripoti iwasilishwe Bungeni

    Mbunge wa Arusha Mjini (CCM), Mrisho Gambo, amedai kuwepo kwa harufu ya upigaji fedha katika Ujenzi wa Jengo la Utawala Arusha. Akiwasilisha hoja yake leo, Jumatano Aprili 16, 2025, wakati akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na...
  18. S

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Frank Nyalusi: Lissu atakuja kuwa Rais wa nchi hii

    Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Jimbo la Iringa mjini , Frank Nyalusi amefunguka katika mahojiano na Shamba fm kupitia kipindi cha Amka na Shamba. "Tumegundua wazi watu wote waliopewa kesi za uhaini walikuja kuwa Marais. I swear to God mimi ni mkristo Tundu Lissu atakuja...
  19. S

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Stambuli awatahadharisha wanahomia vyama vingine wakati huu asema hawatoambulia kitu huko waendako

    Master Stambuli ametoa neno kwa wanasiasa wanaohama vyama vyao na kukimbilia vyama vingine katika dakika hizi za lala salama. Amesema kama wanataka kwenda kupata nafasi ya kugombea huko wanakokwenda, hawataambulia chochote kwani hata huko wameshajiandaa na watu wao.
  20. JamiiForums Tanzania PreGE2025 Makalla aburuzwa Mahakamani kwa kauli yake kuwa CHADEMA inataka kununua Virusi vya Mpox na Ebola ili kuzuia uchaguzi

    Dawson Kagine kupitia Mtandao wa X, amesema kuwa ''Amos Makalla ashtakiwa Kwa kesi ya Jinai. Mimi na ndugu Yangu wa damu Martin Maranja tumemshataki Ndugu Amos Makalla Kwa matamshi yake ya kijinai kwa kuwaambia Watanzania kwamba CHADEMA inachangisha tone tone ili inunue virusi vya MPOX na...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…