Haya muone huyu nae anashindwa hata kutofautisha kati ya kuanzishwa na Matajiri na kuendeshwa na taasisi za kidini. Hizo hapo juu zimeasisiwa na kuendeshwa na madhehebu ya Ki-kristo. Majina yanayojitokeza ni kuwaenzi waumini watajwa kwa michango yao katika dini husika.
Hizi ndio mbinu zakupata kura............kwa watu wa dizaini hii.............1) wenye uchumi mdogo 2) shule ndogo. Hapa tayari jamaa ameshajihakikishia block ya kura za Mufti. Anatafuta block jingine... come 2015 he is the president, hamna cha fisadi wala shangazi yake fisadi! siku 90...
Mgosi na kamati yako ninawafagilia na kuwakubali angalau kwa hili. Hili ni moja na dogo sana lakini kubwa ni pale serekali inapokuwa na kigugumizi kuwashughulikia wahusika. Inauma na inakera sana kuona kazi nzuri kama hiyo ya kufichuwa madudu inaishia kwenye makaratasi ambayo baada ya muda...
Majuva kanena kweli nami kuanzia sasa najaribu kuwavumilia kama mlivyotuvumilia miaka nenda rudi. Waswahili wanausemi usemao mazoea yana tabu..... mtusamehe wenzetu tulizoea hivyo kwamba nchi hii ni yetu peke yetu wengine ni kuburuzwa tu, ni kama vile wamasai wanavyoamini kuwa ng'ombe wote ni wa...
Msimamo wetu ungalileta maana japo kwa mbaali kama waliohusika na wizi huu kwa upande wetu wangeadabishwa kwa aina yoyote ile. Si rahisi kwa wazungu kutuibia bila ya ushirikiano na watu wetu. Au kukata mzizi wa fitina naona ni bora akabidhiwe kitita mama Claire Short kwani ndie aliejitokeza...
Breaking news si lazima ziwe na reliable source. Nami pia nimezipata na source yangu ni mwanagu anaesoma pale. Nahisi hii ni virus kama wale wa Tunisia na Misri, kaingia UDOM na anaweza kusambaa pande yoyote ndani ya nchi hii kwani kote kuna mazingira rafiki ya kirusi kuishi na ku-multiply.
Inawezekana nadharia hii ni ya kweli, pita pita yangu kitaani pale Sinza kwa wajanja nikapishana na lori limendikwa " MTALAKA HATONGOZWI" Kazi kwetu tulio na mywife zetu.
Unanikumbusha katika pitapita yangu kitaani pale Sinzawa wajanja nikaona nikakutana na lori lenye maandishi haya " MTALAKA HATONGOZWI" kazi kweli kweli tuliona na mywife zetu.
Hivi tuseme mkuu wa kaya hayajui haya, jibu haiwezekani kuwa hayajui; na kama anayajua anachukua hatua gani! Ninamashaka kwa ukimya huu nae yumo. ....tanganyika ya wadanganyika......kwishnei
Tuwalipe hao Dowans inauma sana Mh! alafu afya bure na elimu bure haiwezekani, tunawapa kazi vitukuu vyetu wakija watajiuliza hawa baba zetu na mama zetu walikuwa na vichwa kama vyetu au vyao vilikuwa mstatili kwa mambo serikali yetu inavyofanya Mh! tutafika tu lakini tukiwa hoi bin...
Sidhani kama hawa wazungu maporofesa wana agenda ya siri katika hili. Nashauri tulijadili kwa kina hili swala, kwani katika kufanya hivyo itatoa taswira ni kiasi gani tunajijali na kujali rasilimali yetu kwa vizazi vijavyo. Katika yote kama mwisho wa mjadala tutabaliana barabara isijengwe...
Naongezea, nisingalipenda kusikia neno msaada pale Serikali au Mbunge anapofanya wajibu wake kwa wananchi. Kwa mfano utasikia waziri akisema "Serikali itawasaidia wananchi kujenga barabara" Kwa mtizamo wangu ni wajibu wa serikali kufanya hivyo vinginevyo isichukue kodi kwa wananchi iache...
Mjadala mzuri aliouanzisha BM ingawa ni kweli anajichanganya pale anapokubali haja ya mabadiliko wakati huo huo anashabikia CCM. lakini pia nafurahi kuwa amekubali kuwa kipindi hiki tutarajie kupata wabunge wengi wa upinzani. Kama ndivyo basi hii itakuwa njia moja ya kuleta mabadiliko kwani...
Mhh, nami naanza kuwa na wasiwasi na huu msisitizo wa kinadada, kama unataka kina dada tu si useme badala ya kuwapotezea njemba muda wao kukutumia CV zao. Ni bora uwe very specific man. If I were you I would have simply ask for Female IT specialist, kwisha.
Mtaji wa CCM ni umaskini wa wawaDanganyika. Ni pale wenye nchi yao watakapo komboka kiuchumi ndipo CCM watakapo-ondoka madarakani. CCM wanalifahamu hili na ndio maana hawanadhamira ya dhati kuwakomboa wananchi kiuchumi. Pili ni kukosa elimu, wanatumia kuwahofisha wenye nchi yao vijijini kuwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.