Ilikuwa Samsung 125 ina kaantena. Siku moja nikawa napita pale shule ya uhuru kuelekea kituo cha basi ambacho sasa wamekihamisha huku nimeweka simu yangu kwenye mfuko wa shati kaantena kanachungulia. Jamaa akanitega na mguu wake, namuuliza vipi kumbe ni danganya toto, mwenzake akachomoa ile simu...
Najua watu wasiotaka kuambiwa ukweli watakataa lakini huu ndio ukweli wenyewe. Wote wanaweza kuhamasisha maandamano ila wanachozidiana kwa hili ni jee hayo maandamano yana tija yoyote au ni kujitafutia umaarufu?
Tamko la wanausalama linaeleweka vzr ila ni hao wanaojiita wanaharakati hawakulielewa na wameamua kulitafsiri vibaya. Hizi siyo civil societies ni vyama vya siasa. Wanajeshi wanahusika pia na usalama wa raia ndiyo maana hata wakati wa maafa wanajishughulisha na uokoaji. Kwenye tamko lao...
Sidhani kama kuna nchi yeyote hapa duniani ambapo hakuna maskini, maradhi na ujinga, kama ipo nitajie. Tuache blabla mafanikio yapo sana ukilinganisha na huko tulikotoka na pia nji zingine. BRAVO CCM NA JAKAYA.
Angola na Mali wamecheza jana na matokeo ni draw ya goli 4 kwa 4. Angola waliongoza kwa goli 4 mpaka dakika ya 79 ndiyo Mali wakaanza kurudisha goli moja baada ya lingine. Very suprizing lakini ndiyo maana wanasema mpira ni dakika 90!
Kawaida ya ndoa ni kuaminiana ili muishi vizuri. Inapofikia mambo ya kupima DNA UJUE KUNA TATIZO KUBWA SANA ambalo kama hukutatua litaleta matatizo. Vinginevyo hakuna haja ya kupima wala kuongelea suala hilo kwa manufaa ya watoto.
Hata mimi imeniacha speechless. Huyu jamaa yako namfahamu ingawa siyo kwa karibu sana. Wape pole sana nashindwa kifikiria hali aliyokuwa nayo kwa sasa.
Naona mashahidi kwenye kesi hizi huwa wamapangwa kizidhoofisha. Inashangaza kuona mchunguzi anashindwa kujibu maswali obvious kabisa kwa mtu wa taaluma yake. Kweli na hii inaelekea kwenye Uzombe zombe!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.