Hivi karibuni Mh. Waziri Lukuvi ameagiza gharama za urasimishaji zisizidi Tzs.150,000 nchini kote. Ila Manispaa ya Iringa bado wanatoza Tzs.250,000 kwa sqm 400. Nimeona mama mmoja mnyonge ameshindwa kabisa kutoa hiyo hela. Swali langu ni kwamba hivi ni upigaji au ndo gharama zimebadilika...
Sijaelewa ni kwa nini hili suala linakaliwa kimya namna hii. Kuna baadhi ya wahadhili wa vyuo vikuu hasa UDSM na campus zake wanawalazimisha wanafunzi eti ili ufaulu lazima ununue pamphlet langu.
Na ukinunua anakuandika jina kabisa ili siku anaposahihisha ajue adui yake ni nani ili amkamate...
Picha za kanisa la EAGT zilivyonaswa toka katika chanzo chetu, Nasikia ni la Mafia, Limechomwa kipindi cha Pasaka. Wenye habari zaidi watujuze, mliopo huko
Jamani wana jamvi, nahitaji tuition ya form six kwa masomo ya HGE hapa Dar es Salaam inapatikana wapi. Nahitaji kwa muhula huu wa likizo ya mwezi June.
Jamani wanajamvi naomba kujulishwa kwa wale wakristo, hivi ni wapi imeandikwa heri mchawi kuliko mwongo? Maana Dr wetu amenukuu katika kuchangia hoja bungeni jana. Nisaidieni jamani
Kila siku nikipita mitaa mbali mbali ya Dar es Salaam nasikia harufu ya fresh kinyesi, hivi ni nini hasa, ukichukulia mvua sasa hivi hazinyeshi ila mitaa inanuka kana kwamba jamaa wanajisaidia kwenye mitaro. Si uswahilini, si masaki, si mikocheni,, kote kunanuka tu. Hivi nani muhusika mkuu...
Kwa habari nilizonazo, ni kwamba kuna kundi la watu wanasemekana ni waislamu wenye msimamo mkali wamepiga kambi maeneo ya Chuo kikuu huko Changanyikeni kwa ajili ya kufanya matukio kama yale ya Mbagala na sehemu zingine. Kuweni macho, ......(tafadhali msipuuze)
Source.. Mimi mwenyewe
Nimekuwa nasoma post mbalimbali kuhusu wizi wa hawa jamaa wa Vituo vya mafuta vya OILCOM, nikapuuza leo yamenikuta. Nimetoka na gari yangu mpaka Oilcom pale tiptop manzese, nikajaza mafuta ya 12,000 yaani lita 6. Natoka hapo nikijua hayo yatanifikisha mpaka kesho, nafika Jangwani taa ya mafuta...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.