Kama mashamba ni mengi , ni wazi miti imeongezeka , kwa hiyo, bei lazima ishuke maana ni maliggafi. Kama ni kupata faida lazima uuze mbao kama ilvyo kwa wakulima wa mahindi, anayepata faida ni muuza unga
Ukanda wote wa Afrika Mashariki na Kati si salama, vikundi vya kigaidi vinazidi kupata nguvu za kuijimarisha. Kwa hiyo, yanayotokea huku Msumbiji na tuweka katika hatari ya hata sisi huku TZ hasa mikoa ya kusini. Ni vizuri kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama unapoona dalili za uhalifu...
Kwanza wazo la biashara ni zuril Lakini ulitoka Dar kuja Arusha bila kuw ana taarifa za awali kama vile maharagae hayo yanapatikana Arusha sehemu gani, na kwa bei gani kwa gunia? Vile vile kama kuna gharama zingine mfano, tozo za Halmashauri kama zipo.
Nadhani alitaja umbali kakosea, yaani kilomit 10 hadi Mwanza alfu hamsini 58 hadi Geita. Kuna kitu hakijakaa sawa, inabidi wenyeji wa huko wafafanue ili kuondoa mchanganyiko huu.
Wafugaji wengi hawana malisho ya uhakika kwa mwaka mzima, hivyo, huhama hama kutafuta sehemu za malisho. Kwa vile mifugo inakuwa haina chakula inakimbilia kile penye chakula, na wale wanaowaswaga huwa wana uzembe au wanazidiwa maana ng'ombe huwa ni wengi hususani mifugo ya Maasai. Kunahitajika...
Nakushauri umalize kwanza masomo maana hata huko unakotaka kwenda kunatakiwa watu wenye elimu zao! Kuwa mvumilivu kwa muda umalize masomo , baadaye utapata ajira kulingana na fani (taaluma) yako. Vyombo vya ulinzi pia sasa vinajizatiti kwenye tekechnolojia ambayo ndiyo kila kitu leo hii
Halafu hiyo picha inaonesha askari akiwa amfuga ndevu, huko askari wanaruhusiwa kuwa 'o'. kwa mtindo huo, maadili yanakuwa kidogo au alikuwa mafichoni, hivyo, hajapata wembe wa kunyoa ndevu?!
Hii ina maana hata walizni wake pale Ikulu walikuwa wameshamchoka. Hii haina tofauti an yule rais wa Haiti aliyeuawa akiwa nyumbani kwake bila majibizano yo yote baina ya walinzi wa rais na wauwaji. Kwa kweli huheshimu utawala wa sheria na utawala bora n jambo jema sana.
kwa kweli iatabido kwa baadaye serikali iangalie kujenga stendi sehemu kama vile Boko ili kuhudumia magari ya njia ya kaskazini, vilevile kule Mbagala kunatakiwa kuwepo na stendi kwa ajili ya magari ya njia ya kusini.
Ni vigumu kwa Iran na Israel kulishambuiana maana hiyo vit aikauwa ni katia ya USA na Rusia pamoja na China. Ka hiyo, watabaki wakitishiana na kufanyia conspiracy
Kuwekeza kunawezakuwa na tija lakini ni vizuri wakajifunze kwa Mkoa wa Dar es Salaam ambao ulikuwa na vitega uchumi chini ya DDC. Vile vile kuna Chama cha Ushirika cha Mkoa Kilimanjaro, kilikuwa na KNCU Hotel lakini miradi hiyo haiingizi fedha tena kama ilivyokuwa imetarajiwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.