Umenena vema. Nimesikitika sana kwani thread nyingi siku ya leo ni za kukosoa kile kilichofanyika jana badala ya Watanzania wote kusimama pamoja kuunga mkono harakati za kuzuia WIZI MKUBWA ambao tumekuwa tukifanyiwa na majizi makomavu. Leo ni siku ambayo ilipasa pakuche Watanzania wakiwa...
Taifa la ajabu lenye watu wanaoshabikia kuibiwa na kushangilia kuwa ombaomba. Katika hili Watanzania wote tunapaswa kuungana dhidi ya WIZI ambao umekuwa ukifanyika wa raslimali zetu badala ya kubeza. Unaweza kuja kukuta tumeibiwa zaidi ya hiyo iliyobainishwa jana kwenye ripoti. TUWEKENI ITIKADI...
Ijapo Mhe. Rais JPM alipiga maandamano marufuku, nadhani wakati umefika wa watu kukaidi marufuku hiyo na kuingia barabarani kuunga mkono jitihada hizi kubwa alizofanya za kubainisha na kukabili wizi wa raslimali za taifa letu.
Naona ni wakati wa Watanzania wote, pasipo kujali itikadi zetu za...
Hatukuacha kuelewa kuwa hilo litatokea. Wangefanya tofauti ndio tungeona ajabu. Mheshimiwa Lema wewe tulia na utambue kuwa UPUUZI NI MALI YA WAPUUZI. Waache walivyo na endelea kuwa muungwana kwa kuwa UUNGWANA NI MALI YA WAUNGWANA! Barikiwa na siku zote ujue TUPO PAMOJA!
Bila shaka ni wakati mzuri wa viongozi na watumishi wa umma kuujua ukweli kwamba ni vigumu kuzuia kusemwa. Tufanyapo jambo zuri watu watasema kwa uzuri wake na tufanyapo jambo ambalo sio sawa kwa mujibu wa mtazamo wa watu tutasemwa vibaya. Kamwe hatuwezi kuzuia kusemwa kwani mwanadamu hakuumbwa...
Ni kweli amefanya mazuri yastahiliyo pongezi. SHIDA NI PALE ANAPODHARAU KATIBA NA KUTOHESHIMU UTAWALA WA SHERIA! Hilo linafuta mazuri yote ayatendayo. Huwezi kuwa baba uletaye matumizi yote nyumbani lakini unawatukana na kuwasimangia wa nyumbani mwako yale unayowafanyia.
Maadam Makonda alijua mtazamo wa aliyemteua kuhusiana na hatua yake ya kuvamia kituo cha Clouds, basi tuliobakia hatuna haki ya kumlaumu kuwa kakosea. HAKUKOSEA. Alitenda lile limpendezalo aliyemteua huku akijua kuwa hatofanywa kitu. TUSIMLAUMU. Wito wangu aendelee mbele azidi kusifiwa. Hongera...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.