Moto unawaka kwa sababu kuni haijaisha. Kuni ikiisha moto unaisha. Lakini kuni kwa yenyewe si moto.
Hapa ndipo hatupaswi kuchanganya maarifa ya Sayansi -"Jinsi gani", na Imani - "Kwa nini" bali kuyatumia kutafuta ukweli ambao ndio lengo letu la mwisho.
Kama kitu au jambo halipimiki au...
Huwezi kusema akili ya binadamu ni kama akili za viumbe wengine na hapo hapo unakiri kuwa binadamu ana uwezo wa juu sana wa akili.
Yaani kwa lugha rahisi maelezo yako yanakinzana.
Imani na hapa namaanisha imani kutoka kwa Mungu ni uelewa wa kina au wa hali ya juu wa mambo na elimu ya vitu (kujua). Kwa lugha rahisi ni jinsi mambo yalivyo, ukweli.
Ubongo wa binadamu ambao ndio mahali pa shughuli za kiakili unafanya kazi katika hali ya kusadiki (believe). Hii maana yake ni...
Binadamu ni sawa na viumbe vingine kwa msingi huu, wote wanatoka kwa chanzo kimoja. Lakini hadhi yao ni tofauti.
Panzi ana akili ya utambuzi. Tofauti na akili ya binadamu panzi hawezi kufikiri na kufanya uchunguzi na kujua na kujua kuleta au kuunda vitu vingine vipya kwa kutumia vitu vya asili...
Maana hii ya akili inamweka mtu kundi moja na wanyama wengine which is somehow correct.
Wanyama wote wana uwezo wa kupokea taarifa, kuchakata na kutoa maamuzi (utambuzi). Lakini akili ya binadamu ni nini?
Akili ya binadamu maana yake ni kufikiri na kufanya uchunguzi na kujua na kujua kufanya...
Watu wote wa nyakati zote tuko chini ya sheria moja (universal laws). Kile ambacho ni kosa dhidi ya akili kinawahusu watu wote wa nyakati zote.
Imani potofu huleta uelewa potofu na hivyo tamaduni na mila mbaya. Imani potofu na tamaduni mbaya sio sababu au kisingizio (excuse) cha makosa dhidi ya...
Mkuu sio sahihi kubishana. Yafaa kujiuliza na kufuatilia (kuchunguza): hapa tulipo ndio mwisho wa kila kitu?
Akili ya binadamu ni halisi?
Imani ni nini? Sayansi ni nini?
Imani inatoka wapi na sayansi inatoka wapi? Uthibitisho maana yake ni nini? Tunajuaje? Na tunajuaje kuwa tunajua?
Kwa nini...
Mfano wako wa kikombe cha babu wa Loliondo na maji ya Mwamposa ni ushahidi kuwa watu hao (watanzania wengi) hawana uelewa wa kina wa mambo na elimu ya vitu.
Jambo hilo la kikombe cha babu au maji ya Mwamposa sio mambo ya imani wala hayahusiani na imani kwa sababu hayana sifa hizo.
Imani sio...
Mtu aliyekuumiza au kujeruhi kihisia, kiakili au kimwili anaweza kufanya hivyo kwa sababu mbili. Moja kwa kujua. kwa makusudi-nia, ufundi na maarifa. Mbili kwa kutojua. Kutokuwa makini. Yote mawili hatahivyo hayakuondolei wajibu.
Maneno ya kusema mdomoni tu pasipo matendo ni maneno kama maneno mengine.
Ukweli wa mtu haumo katika maneno yake, umo katika matendo yake.
Ukweli wa maneno unathibitika kwa njia ya matendo.
Matendo yako wapi?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.