Sasa nimeelewa. Kuna hizi bei za online na bei za kwenye 'field'. Asante. Nilimpigia simu mdau wangu ambaye yuko huko akanipa majibu kama ya kwako kabisa.
Nakubaliana na wewe. Mpe mtoto jina ambalo kwanza ni nadra, pili liwe lina-sound poa, tatu usitafute liwe na maana kubwa sana. Likiwa na hizo sifa mbili, hata kama linamaanisha jiwe, meza, shamba, inatosha. Mradi lisimaanishe kitu kibaya kama mwizi, mavi, shetani nk.
Wakuu, katika makala yangu iliyopita tuliyojadili kuhusu programu hatari ya udukuzi kutoka Israeli iitwayo Pegasus, niligusia tukio hili kwa kulitaja tu, maana mwishoni mwa makala ile nilitaja wakuu wa nchi mbalimbali waliowahi kudukuliwa na programu hii.
Kama nilivyosema, mnamo mwaka 2021...
Hawakuwepo. Walinzi hawakutakiwa kuwepo ili kuondoa attention.
Ndio maana lilikuwa jengo baya, na limekaa pia mahali pa hovyo.
Lingekuwa zuri, mara walinzi, tayari maswali yangeibuka kuwa kuna nini hapa.
Fikiri mfano huu: umeshika simu yako, ghafla tu unasikia imeita, kabla hata hujapokea inakatwa. Unaachana nayo. Hujabonyeza chochote.
Lakini!!
Simu yako ndio imeshadukuliwa hivyo!! Meseji zako zote za kawaida na za whatsapp, zinasomwa. E-mails zako zote zinasomwa! Simu zako zote zinasikilizwa...
Operesheni ya Nyaraka za Kinyuklia za Iran ya mwaka 2018 ni moja ya misheni za kusisimua mno na za kijasiri zaidi katika historia ya kintelijensia ya Mossad. Huu ni uvamizi wa usiku mmoja, ambapo majasusi wa Israel waliingia ndani kabisa ya mji mkuu wa Iran, Tehran, na kuondoka na nusu tani ya...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.