MILUZI MINGI
Nawaza nianze lipi, Kesho niwe wa maana.
Nimekazwa kwa mshipi, Na kaburi naliona.
Thamani yangu ni ngapi, Nihungame Maulana.
Miluzi sasa ni mingi, Napotea mawindoni.
Nawaza hadi magumu, Kuyasema nachelea.
Liwe moja baragumu, Ramani nitakosea.
Najua mwisho mgumu, Naweza pia potea...