RIP mzee Moi, pamoja na mambo mengine lakini ulionesha njia kwa viongozi wa Africa ambavyo wanatakiwa kuwa baada ya kishindwa uchaguzi, nakumbuka uliposhindwa uchaguzi na kuulizwa kwanini hujakataa matokeo, ulijibu jibu rahisi kwamba 'hiyo ndiyo demokrasia '
Weka takwimu acha mambo ya kwenye vijiwe vya kahawa, unaposema IGP ndiye aliyefanya vibaya kuliko wote unatumia vigezo vipi kuthibitisha ulichoandika, pia unapohusihanisha gari la zimamoto na IGP unataka kutuonyesha uwelewa wako finyu kuwa hujui jeshi la zimamoto lina kamishina jenerali wake...
Njoo Tanzania uendelee kutembelea maeeneo yaliyotolewa tahadhari ni siyo wewe uko nchi salama halafu unatuamisha utumbo wako hapa, polisi wenyewe wamekiri taarifa hizi zipo na wanazo sasa wewe unawashwa nini hadi uanze mitizamo isiyo chanya wakati ikitokea kweli tulioko huku ndo tutaathirika
Uhakika upo kwasababu wao wenyewe wamekiri kuwa huwa wanalazimika kukwepa ama kudaganya kulipa kodi sababu ya nyie watumishi wa TRA huwa mnawabambikia kodi kwa kutafsiri kivyenu sheria ili kukaribisha mazungumzo ya rushwa kwa faida zenu binafsi
Wewe January Makamba stress zitakuuwa, fanya kazi uliyopewa, na siyo kuona unastahili sana kuliko watu wengine, kwa mfano ulisha wahi kubuni nini ulikopita kote ukiondoa kufacilitate bao la mkono ulilofaulu kwa asilimia zote
Naona leo watumishi wa TRA mnahangaika sana jf kutaka kuhalalisha uozo wenu, tatizo siyo mfumo wala nini bali tatizo ni nyie watumishi wa TRA kutumia sheria zilizopo vibaya ili kupata vipato visivyo halali, na asilimia 99.9 mkiambiwa muelezee mali mlizo jilimbikizia mmezipata wapi hamuwezi,
Acha janja janja wewe, siku ile ya mkutano wa Jiwe , wafanya biashara wamekuwa so clear kwamba TRA kwenye biashara wanazokadiria mlipa kodi alipe nini , wamekuwa wakiweka makadirio ya juu sana kiasi kwamba mfanya biashara kutishika na kuanza kubembeleza kupelekea kutoa rushwa kwa nyie...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.