Nijuavyo mimi mfanyakazi akihama Kutoka alipokuwa anafanya kazi akahamia sehemu nyingine aidha ni kampuni binafsi au Serikalini hawezi kupata mafao kwa kuwa ataendelea kuchangiwa michango yake kwa hiyo mtu wangu ndio hivyo hata ukienda uliza utasikia majibu yao
Kuna jamaa yangu amesaidiwa juzi kupitia ukurasa wa instagram wa NSSF @nssftz mwambie atume huko taarifa zake muhimu kama namba ya uanachama na majina yake kamili pamoja na mahali alikuwa anafanyia kazi atapata msaada wa haraka
Jamaa wanasema kwa mujibu wa sheria inasema mafao ya kupoteza ajira yanatolewa kwa mwanachama aliyeachishwa kwa sababu yoyote isipokuwa kuacha yeye mwenyewe, jitazame kama upo kundi gani
Mzee ungeuliza kwanza kabla ya kufanya maamuzi, juzi kati nilikuwa nasoma soma taarifa ya hii mifuko miwili hasa huu wa NSSF nikaona kuwa kuna Pensheni iliyohairishwa yaani endapo mwanachama atakuwa ametimiza Credit 180 hata kama atakuwa na umri wa miaka 40 kwa mfano anaweza kuomba pensheni hiyo...
Ebwana kwa uelewa wangu Mwanachama atapata mafao yake endapo ataachishwa kazi kwa sababu yoyote ile isipo kuwa kuacha kazi yeye mwenyewe hapo atakuwa hana sifa ya kupata mafao, pili mwanachama atapata mafao yake endapo atafikisha umri wa kustaafu kwa hiari miaka 55-59 kwa hiari na miaka 60 kwa...
Ebwana pole sana ila naungana na mdau aliyeseama kama umeshawahi soma hata vigezo na masharti, kwa uelewa wangu na itawasaidia watu wengi kama wewe, ipo hivi nijuavyo mimi kwanza kabisa ikiwa mfanyakazi ameacha kazi kwa hiari yake yeye mwenyewe anakuwa hana sifa za kupata mafao yake hii ipo...
Ushauri wa Bure kama unauhakika unacho kiandika haudanganyi nakushauri ukaandike barua ya kukata shauri na uwe na vithibitisho kweli wewe sio mtaalam, lakini kama hauna uhakika wa hilo unataka mseleleko basi usifanye hivyo jamaa wapo smart sana wale mifumo yao inasomana. So akili kichwani mtu wangu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.