Recent content by Jizaledo

  1. J

    JamiiForums Tanzania Kama Mama Malecela hafai, je Mbowe anafaa?

    Duh, JF sasa imeingiliwa. Watu wanatetea wafadhili wao utadhani vichwa kavu na hawasikii lolote. "Next" zimekuwa ndio hoja au tuseme ndio mbio na vificho.
  2. J

    JamiiForums Tanzania Rashid Othman: Umeshindwa Jiuzulu!

    Mwanakijiji, Nimekuwa nikifikiria kuwa michango yako ni ya uzalendo na inajaziishwa na uzalendo. Tafadhali niwezeshe niendelee na fikra hizo hizo, tafadhali andika yale unayoyajuwa kwani kuamini kwako na kutokuamini kwako si muhimu bali cha muhimu ni wewe kutueleza unayoyajuwa, uliyona hakika...
  3. J

    JamiiForums Tanzania Rashid Othman: Umeshindwa Jiuzulu!

    Kwanza heshima zenu wakuu kwa uzalendo mnaoonekana kuwa nao na pia mnavyoonekana kuelewa na kutueleza kazi za Idara ya Usalama wa Taifa na kufikia kutaka RO ajiuzulu kwa kuwa muonavyo ninyi hakutekeleza kazi hizo. Ni vizuri mkatueleza pia kazi za mshororo wa mfumo mzima wa serikali na uongozi wa...
  4. J

    JamiiForums Tanzania Buriani Amina Chifupa!

    NAMLILIA AMINA! Niliapo naliani, nalia nanyong'onyeka, Machozi tele usoni, kisimama naanguka, Hili ni balaa gani, wanandugu kutufika, Majonzi mengi moyoni, namlilia Chifupa. Miaka ya ishirini, thelathini hakufika, Ajulikana nchini, tadhani alizeeka, Asomjuwa ni nani, ni wengi...
  5. J

    JamiiForums Tanzania Buriani Amina Chifupa!

    AMINA Amina ametutoka, kufa ametangulia, Kama ua amefumba, baada ya kuchanua, Tunamuombea mwanga, peponi ende ingia, MSIMAMO ALOWEKA, HAKUNA WAKUCHANGUA
  6. J

    JamiiForums Tanzania KISWAHILI: Naomba maana ya maneno haya...

    Ila tu neno "vumbika" halihusiani na kuweka vumbi bali hutumika katika utayarishaji wa matunda machanga ili yalike na matumizi yake halisi hayahusiana na vumbi hata kidogo. Kuvumbika tunda kama vile embe ni kuliweka ili liive barabara. Kuiva kwa tunda hakuhusiani na kupikwa tunda hilo bali ni...
  7. J

    JamiiForums Tanzania Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

    Read what the Captain of Flight Tanzania, the President of the United Republic of Tanzania is talking. And we have said, the nervous passengers can cause our flight to crash. What every passenger should do is sit down, relax, enjoy the flight and wait for a happy landing. We will land if we...
  8. J

    JamiiForums Tanzania Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

    Ni kweli watu wanalewa madaraka na sasa imefika kikomo. Hawa maRC ndio wanaotakiwa kuchunga maisha ya Watanzania sio kuyaondowa kwa uchungu wa vitu visivyokuwa na maana. Hili linanifanya nilikumbuke jambo linaloniumiza kichwa sana ambalo linawachwa liendelee bila kukemewa nalo ni kuua watu...
  9. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Mkandara, Nilikwishasema kuwa hili darasa nimelifunga kwani uchache wako haurekebishiki kwa kuangalia haya unayoandika ambayo nimeyanukuhu hapa. Labda itakusaidia kama utakaa na kutafakari ili ujuwe mtu aliyekufuru huwa anaisabika vipi mbele ya Mwenyezi Mungu na tofauti yake ni nini na huyo...
  10. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Mkandara, Huwezi kunielewa kwasababu hutaki kuelewa kwani sioni unapata ugumu upi kujuwa kukufuru nini wakati nimekueleza kuwa kuna njia tatu kuu ambazo zinamtia mtu kwenye kufuru. Inavyoonekana wewe unabishabisha tu bila ya kuangalia maneno yako au bila ya kuelewa unachoandika. Kwa mfano...
  11. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Mswahili, Ukienda mbali kughorodhesha Nyerere alivyofadhiliwa na Waislamu itaonekana kama unawasimanga hawa ndugu zetu. Mimi nisingependa uende huko, si vizuri. Pia siafikiani nawe kuyaleta majina ya akina Magufuli hapa kwani zaidi ya wao kuwa wakristo si dhani ni mahali pa kuwajadili kwenye...
  12. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Mzeeshughuli Bwana, Nasaha zako safi ndugu yangu. Tatizo ni kuwa unaangalia upande mmoja na mifano yako iko kwenye mshazari huo huo. Ukiongelea Wapalestina inaonekana haikuyumkiini kabisa kuwa Northen Ireland zimepigwa na kulipuliwa mabomu ya kujiuwa kati ya Roman Catholic na Protetants. Pia...
  13. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Quarz, Kwa hiyo uliowaona wanajibishana kwenye mada hii ni Jizaledo na Mswahili tu. Kweli wewe kubwa yao. Hivi ni wapi niliposema kuwa Nyerere alinionea. Hapa tunajadili ukweli kuhusu Nyerere hatulalamiki kuonewa mtu bali tunajadili hitilafu na ufanisi wa mfumo wa uendeshwaji wa taifa...
  14. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Mkandara, 1. Soma dini tena kama wewe kweli ni Muislam ili uielewe na ili ujuwe kuwa wapo waliopewa madaraka kuwaongoza Waislamu hapa duniani na kuna mfumo wa kudhihirisha madaraka hayo katika Mwongozo wa waislam wote na kwenda kinyume na Mwongozo huo ni kuudhalilisha, kuukana na hivyo...
  15. J

    JamiiForums Tanzania Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

    Mkandara, Ninakutahadharisha tu kuwa ulimi hauna mfupa na hata siku moja simba awezi akawa tembo na tembo akawa simba kwani ulimi wake utamkosowa. Haya machache tu niliyoyanukuhu kutoka kwenye maandishi yako yanaonyesha wazi kuwa wewe si sunni wala muislam kwani ndani ya haya mna lack basic...
Back
Top Bottom