Serikali chini ya chama chao imeshindwa kukemea ufisadi na utekaji. Zaidi, imeshindwa kuboresha huduma muhimu za afya, maji n.k kwa wananchi.
Kazi kubwa imebaki kutishia wananchi, na kutoa dharau na kejeli kanakwamba wananchi hawana mamlaka kama katiba inavyosema.
Mdude na Soka hawajulikani waliko. Mzee Kibao kutekwa mchana kweupe, sijui mwelekeo wa nchi kwenye usalama wa raia ni upi. Tuhuma nzito za ufisadi kila kona, maisha ya watanzania ni magumu. Kwa kipindi kifupi taifa linakosa mwelekeo.
Wawe ni panya road au sio, kuna utawala wa sheria. Walipaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria baada ya uchunguzi na sio kuuawa kikatili namna hiyo. Tusitumie hisia kujadili mambo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.