Ningependa kumbakiza Martinelli niwauze Havertz au hata Gyokeres na Trossard ikibidi ndiyo aje Rojers. Nampenda Trossard ila naona Martinelli abaki kwa sababu ya umri wake na kiwango hayupo nyuma sana ya Trossard hivyo anaweza kumfukia kiwango chake na hata kumpita akikomaa, msimu ujao au ndani...
Umesahau madhara ya kina Captain Marvelous na Saint Anne na kocha wao bingwa ambaye sasa wanamwita Kichwa Mviringo jinsi wenge la kuwa na pesa lilivyowaponza wakaanza kununua wachezaji wa bei mbaya wakawajaza pale bandani mwao?
Yaani walikuwa kama mfanyakazi mlevi akishashika mshahara. Breki...
Kuna tetesi kuwa zile 115 charges dhidi yenu zinaelekea kufika mahala pabaya kwenu na huenda niyo sababu Pep kakimbia ligi mwaka mmoja mapema kabla ya mkataba wake kuisha.
Mnaweza kukatwa points 60 msimu ujao, kuzuiwa kushiriki transfers kwa miaka miwili, labda na faini kali juu.
Hii inamaana...
Yuko sahihi. Bruno ananikumbusha sisi enzi zetu tuna Fabregas halafu washambuliaji wetu ni kina Adebayor. Bonge la mido ila mastraika wa nafasi kumi goli moja.
Bei mbaya kinoma na kina ManU nao watataka kutoa 100m.
Nataka tusubiri kombe la dunia tucheki viSouth Americans vipambanaji mifano kama ya Alexis Sanchez na Cavani enzi wakiwa wamoto tuvichukue kwa bei za kishikaji zaidi.
Hii ni AI hii, sisi huwa ndiyo tunaadhibiwa na VAR kuliko timu yoyote, ila msimu huu tumetendewa haki kidogo zaidi ya misimu iliyopita. Pia ni kwamba tu ile moja ya West Ham kumkwida kipa wetu imetusaidia kupata ushindi badala ya sare na hatimae tukapata ubingwa, na hata hivyo uamuzi ule ulikuwa...
Tukikosa UCL msimu huu tutalazimika kupambana sana msimu ujao. Acha tu tuwapige hawa PSG fainali hii ili tupumue kidogo kama jinsi kubeba hiki ki Premier League trophy kilivyotusaidia kupumua kidogo. Sasa msimu ujao tutacheza bila presha.
Je, msimu ujao mtaweza kununua wachezaji wa bei mbaya au mtabana matumizi?
Najua mlitumia pesa nyingi kununua wachezaji wapya msimu huu lakini mlipata nyingi pia kwenye mauzo ya wachezaji wengine?
Au pesa za UCL msimu huu pamoja na kumaliza nafasi za kuingia UCL msimu ujao zitawatosha...
Aisee, acha kabisa. Tukibeba UEFA, viwanda vyote, baa zote na vibanda vyote vya maji ya kienyeji havitatutosha wanaGunners. Mashamba yote ya mmea takatifu hayatutosha wanaGunners.
False hopers aka bottlers aka Arsenyau aka sijui nini na nini.
Majina mengi walituita ila ArsenalNdoo au Asendooo wanatubania kutuita. Kina Labyrinth 84 na Flano waje basi watuite Asendoo wafurahi.
Kingine kizuri ni Arteta kumwahi Pep na kumshinda kabla hajakimbia ligi. Ameweza kumaliza juu ya Pep misimu miwili mfululizo. Ni kitu cha kujivunia maana yeye amepambana kwa muda mrefu kwa kuunda kikosi chake bora kilochopitia mengi njiani mpaka kufika nchi ya ahadi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.