Ni mzuri ndiyo maana hata sisi tulikuwa tunataka aje kwetu. Mmefanikiwa kutunyang'anya tonge mdomoni.
Sasa endelezeni pia tabia yenu ya kututupia wachezaji wenu wabovu kama kina Kai, Noni na Jorginho. Sasa tupeni Malo Gusto na Estevao. Hata Caicedo na Enzo ni wabovu mnaweza kutupa hao...
Hakumsikia kuwa sisi tunamipango ya kumsajili Rogers? Au mlisikia na bado mkaamua kutuzidi dau? Naona bado hamtaki kuacha tabia ya kuingilia dili zetu.
Hongereni lakini. Rogers ni mchezaji mzuri.
Na msimu ujao bado Arsenal tutabeba ubingwa. Mbona hatuna Caicedo, hatuna Fernandes, hatuna Isak na bado sisi ndio mabingwa wa sasa? Tumebeba kombe na kina Martinelli na akina Trossard na akina Ben White huko.
Simon ndiye kocha anampenda na kuona anafaa mfumo wa timu ya taifa. Hata ikiwa Raya akimzidi kidogo kiuwezo, si kiasi cha kutosha kumfanya kocha abadilishe kipa anayemuona anafaa mfumo wake.
Shida ni habari ya mjini ni ubingwa wa Arsenal lakini mna chuki na sisi so hamtaki kutujadili.
Habari ingine ya mjini ni kwamba hali yenu ya kiuchumi ni mbaya kinoma. Hilo pia hamuwezi kulijadili.
Sasa hakuna kingine cha kuongea humu.
Aah wapi. Hapo tumepata mshiko wa kutosha kumchukua Kvaratskhelia 😁😁😁.
Yaani tusingezingua jumamosi tukabeba kombe, hata sitaki kufikiria dunia ingekuwaje aisee.
Nimesikiliza dakika 10 tu mpaka sasa...ila hali yenu ni mbaya mno .
Boehly amechezea sana pesa za wawekezaji na hakuna faida yoyote mliyopata bali hasara ya pauni milioni 355.:oops::oops::eek:
Nategemea ndani ya misimu miwili mtakuwa mnacheza championsihip...
Tuanze kuagana mapema tu...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.