Recent content by Getstart

  1. G

    Polisi yakiri watu 45 wafariki Dar wakati wa kumuaga hayati Magufuli

    Inanishangaza kuwa watendaji hawakumshauri Rais wetu kutuma salamu za rambirambi, au hata kulisemea tu kwa wazi, kwa msiba huu uliolipata jiji la Dar es Salaam.
  2. G

    Ripoti ya Hali ya Uchumi Tanzania: Benki ya Dunia yapendekeza mfumo wa ncha 3 kupambana na COVID-19 na Mporomoko wa Uchumi

    Je mwenendo wetu wa sasa katika sera na matendo ya kiuchumi haifuti hayo ya nyuma tuliyoyafanya kutufikisha hapa tulipo?
  3. G

    TANZIA Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Servacius Likwelile afariki dunia

    Nafikiri tutafute maana ingine ya ushindi. Huwezi kudai ulishinda wakati huna takwimu sahihi za watu wako waliopoteza maisha!
  4. G

    Dawa asilia sasa kuwekewa mkakati wa kupatikana katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya na Maduka ya Dawa za Binadamu

    Tutumai na kuomba aishie hapo. Wasiwasi wangu kuwa wasije wakatushauri oia tutumie mahabara na vipimo vya waganga wa asili. Wakati tunatumia madawa hayo tujiandae pia kwa madhara yake ya muda mrefu. Hakika utamaduni unadumu hata ukibafilika vipi!
  5. G

    Wizara ya Afya: Hakuna tishio la UVIKO-19, likiwepo tutatoa taarifa

    Ukiingia kwenye siasa unajifunza kuwa laghai hata kama wewe ni mwanasayansi inaikataa sayansi! Mbaya unawafanya watu wote ni wajinga na kwamba wewe tu ndiyo mwerevu
  6. G

    DPP aeleza sababu Nusrat Hanje kuachiwa huru

    Angefanya hivyo mapema na kwa kufuata taratibu ingeeleweka. Kubambikiwa kesi ni halisi na wanaofanya hayo wanashirikiana na ofisi yake au na 'yeye mwenyewe'
  7. G

    Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

    Tunanunua ugomvi ambao tunajua hatuwezi kushinda. Yesu alisema mfalme anayetaka kwenda vitani hufanya hesabu kwanza ya uwezo wa jeshi la adui. Akiona lina uwezo kumzidi hufanya majadiliano kabla ya kuingia vitani. Hii ndiyo hekima!
  8. G

    Uchaguzi 2020 Dkt. Bashiru: CCM mwaka huu itavunja rekodi kwa kupata ushindi mkubwa wa kihistoria kwa sababu tunashindana na vyama dhaifu sana!

    Sisi tunayoyaona huku mitaani hayahakisi hayo maoni yake. Labda ana wapiga kura wengine nje ya wananchi tunaoishi nao na wamaoudhuria mikutano ya wagombea!
  9. G

    Uchaguzi 2020 Vyama 8 vinavyoshiriki Uchaguzi vyamtaka Mbowe ajieleze kwa Msajili baada ya kuviita ni vyama bandia

    Yawezekana mkawa na uhalali wa kisheria lakini bado mkawa bandia! Kwa miaka zaidi ya 25 bado hamjapata mbunge hata mmoja wala madiwani mnapata wapi uhalali wa kisiasa kama siyo kutumika tu!
  10. G

    Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

    Dr Mahera usisahau kuwa wewe ni refa na mwamuzi. Wewe siyo kuwasemea wapiga kura wanachokitaka au siyo wewe unayeshauri vyama vya siasa viwe na sera zipi?
  11. G

    Uchaguzi 2020 Uzinduzi wa Ilani ya ACT–Wazalendo, Kutoa Ajira mpya milioni 10. Zitto asema CCM ilitekeleza 31% ya ilani ya mwaka 2015

    Huyu naye vipi? Yaani TBC wanasubiri kualikwa! Mara ya mwisho nilifikiri TBC ni chombo cha habari, tena cha umma na kina waandishi wa habari wanaotakiwa kutafuta taarifa na kutuletea sisi wananchi tunaowalipa. Kumbe wanasubiri kualikwa ili waende 'harusini' 🤔
  12. G

    Uchaguzi 2020 NEC yatoa siku 2 kwa Vyama vilivyopata changamoto kutambulisha Wagombea wao baada ya Watu wasioteuliwa kuchukua fomu za Uteuzi

    Sidhani kwamba ni tatizo la vyama vya siasa kutojipanga Mh Dr Mahera. Najua umetumia maneno hayo ili kuwalinda hao wasimamizi. Tume fikirieni hao wasimamizi ikiwa bado wana uhalali wa kusimamia maeneo hayo. Sijui kama vyama husika na wapiga kura wake winawaona kwamba hawana upande - yaani impartial
  13. G

    Dar es Salaam: Polisi waua majambazi wanne na kufanikiwa kukamata silaha mbalimbali

    Nafikiri kwa kulinda na kujali uhai wa kila mmoja wetu siyo lazima tusubiri ndugu wa marehemu. Ni wajibu wetu na serikali kuhakikisha uhai wa kila mmoja wetu unahifadhiwa na kulindwa. Kumbuka kuna watu wako mjini hawana hao ndugu wa kuwasemea kwa mara moja. Wanaweza kufa isijulikane, lakini...
  14. G

    Dar es Salaam: Polisi waua majambazi wanne na kufanikiwa kukamata silaha mbalimbali

    Ingekuwa vyema kama mauaji hayo yangekuwa yanachunguzwa kwa mujibu wa sheria ya vifo tatanishi. Kuna uwezrkano kwa watu wema kuuuawa. Ni vizuri pia kupatikana ukweli wa mauaji yoyote ya binadamu. Haya yatatuwezesha kuongeza ufanisi katika utendaji wa polisi na mambo mengine yanayohusiana na hayo.
Back
Top Bottom