Recent content by Fadhilim

  1. Fadhilim

    Kwa nilichokishuhudia na bado naendelea Kukishuhudia kwa Wanaume mlio mbali na Wake zenu hakika nawapeni Pole nyingi sana

    Duh haya mambo ndo yanasababisha muda mwingine watu wasioe, ukimuacha mke nyumbani kwenda kwenye majukumu nje ya eneo wahuni ni kupeleka moto tu
  2. Fadhilim

    Kwa nilichokishuhudia na bado naendelea Kukishuhudia kwa Wanaume mlio mbali na Wake zenu hakika nawapeni Pole nyingi sana

    Haya mambo ni shida kwa kweli na ukizingatia miaka hii uaminifu nao hakuna basi shida tupu, ni mwendo wa wadau kula tunda kimasihara
  3. Fadhilim

    KERO Responded Naomba uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili uondoe CCTV Camera zilizowekwa chooni

    Ifike hatua wabongo tuwe wastaarabu pia, sasa unang'oa koki ili kiwe nini ndo maana watu wakaona suluhisho ni kuweka kamera, ukishindwa kujiheshimu hakuna ambaye atakuheshimu.
  4. Fadhilim

    Walimu naomba mjirekebishe na hili la kuomba tip

    Sidhani kama kulikuwa na haja ya kujumuisha walimu wote, kwa upande wangu hii leo ndo naisikia mwalimu kuomba fedha kwa mzazi/mlezi.
  5. Fadhilim

    Manyara: Baba mbaroni kwa kuwabaka binti zake watatu

    Masharti ya mganga hayo. Haiwezi kuwa akili yake, unasimamia kucha kabisa kwa mtoto wako.
  6. Fadhilim

    Ofisi ya Kata wanashirikiana na baba yangu mzazi kuninyima haki yangu ya mali

    Kwa majibu ambayo mtoa mada aliyapata kwenye thread yake ya awali, sikutarajia kama angeandika uzi unaofanana na wa awali. Kwa umri huo hata uende mahakama kuu, watasikiliza tu halafu waendelee na mengine. Huwezi pata chochote,maana haingii akilini udai mali ambazo sio zako. Ukizingatia mwenye...
  7. Fadhilim

    Je, Rais yupo humu? Kama yupo ina maana hatuoni?

    Nilikuwa najiuliza sana hili swali, kwa nini wenye elimu ndogo wanakuwa na roho mbaya. Kuna mmoja mpaka kesho na certificate yake ana kinyongo na mimi, kwa vile nilikabidhiwa ofisi pindi Boss yuko likizo.Heshima kwa wafanyakazi wote wenye elimu kuanzia Degree na kuendelea.
  8. Fadhilim

    Hayati Magufuli aliweza kujenga miradi kwa fedha za ndani, hizo fedha za ndani kwa sasa zinafanya kazi gani au mapato yameshuka?

    Kwa hiyo mkuu nawe ulikuwa unaamini ni fedha za ndani. Na huku wakizunguka kwenye makorido ya benki ya dunia, shirika ka fedha duniani kukopa fedha za miradi.
  9. Fadhilim

    Mwanza: Chalamila akabidhi ofisi kwa RC mteule

    Mkuu hilo sina majibu nalo labda tuwaulize watu wa Lumumba buku 7 watatusaidia. Ukirejea enzi za mwendazake alishasema kuwa hakuna kuvaa kofia mbili.
  10. Fadhilim

    TANZIA Mtangazaji Fred Fidelis ''Fredwaa'' afariki dunia kwa ajali ya gari

    Huyu jamaa alikuwa bonge la mtangazaji, hususani enzi zile yuko RFA. Japo umauti umemkuta akifanya kazi Clouds, na siku za usoni alikuwa hasikiki kwenye kile kipindi cha Power Breakfast. Hakika sisi sote ni wa mwenyezimungu na kwake tutarejea.
  11. Fadhilim

    Kwanini Rais Samia amesema hataki mabango, Je hii ndiyo demokrasia?

    Kiongozi mbona kauli ya rais Samia Suluhu iko wazi. Uwepo wa mabango tafsiri yake ni kwamba wateule wake hawawajibiki. Kwa mantiki ya kwamba viongozi wa ngazi za chini wapige kazi kutatua kero za wananchi. Ndo maana akasema kila bango litaondoka na mtu/kiongozi.
  12. Fadhilim

    Mwanza: Vivuko viwili vyasimamishwa

    Kama vinahatarisha usalama wa raia na mali zao bora visimamishwe kusubiri marekebisho. Kufumbia uozo wa vivuko ni kuweka maisha ya watu rehani. Ila naibu waziri asitoe tu zile kauli alizowahi kutoa kiongozi mmoja pale Dar ferry kwenda kigamboni. Anayeona nauli ya kivuko ni kubwa apige mbizi.
  13. Fadhilim

    Mamlaka za Usafiri Dar hazijali muda wa abiria

    Duh mkuu kumbe siku hizi hiyo ruti ndo ina ujinga huo wa kurudi tena Ubungo utokapo mawasiliano. Mara ya mwisho kupanda hizo gari ilikuwa ukitoka simu 2000, unaingia barabara ya shekilango/Sinza -mlimani city na kuelekea Kawe/Makumbusho.
  14. Fadhilim

    Depression inaniathiri, nakaribia kujiua

    Kijana pole sana kwa hiyo changamoto unayopitia.Ushauri wangu ni kwamba wawe usijishtukie uonapo watu wanacheka. Kwa vile bado uko shuleni soma sana na ipo siku hao wanaokucheka watakuja kukupigia magoti kukuomba msaada. Mwisho tambua tu kuwa mungu kamuumba kila mtu kwa mfanowe.
  15. Fadhilim

    TBC na Vyama vya Upinzani kuna ugomvi gani, au ni maagizo toka juu?

    Inawezekana ikawa ndio masharti ya mikataba ya wafanyakazi. Ukitangaza/kuripoti habari za chama cha upinzani kibarua kimeota nyasi.
Back
Top Bottom