Kama songesha hakuna namna unazweza kujitoa. Nimehangaika sana wasinikopeshe lakini imeshindikana. Kama kuna mtu najua aniambie. Lakini asiseme unsubscribe. Hiyo najua
Umetafsiri vibaya wazo la WM. Mimi nakubaliana nalo. Shughuli nyingi tunazozifanya za kila siku ni elimu ya veta.
Ukiwa na gari ukajifunza kuendesha, VETA hiyo. Kuna kosa gani ukiwa mhitimu wa Uhasibu, ukaenda VETA kutengeneza makochi, halafu ukatumia uhasibu wako kutunza hesabu za biashara...
Sera ya no reform no election inawaoeleka shimoni. Fanyeni vitu vyo lakini maneno hayo hayaeleweki hata nie wenyeqe chadema mnashindwa kuyafafanua vema. Yaondoeni kwenye sera zenu.
Miaka ya hivi karibuni inashuhudia matajiri wakiongezeka. Wanatunza fedha benki. Ndio maana BONDS zikitangazwa fedha zinatolewa zaidi ya bond. Ina maana watamzania wana fedha kwenye mabenki.
Nawashauri watanzania weusi. Wasioogope kuwekeza kwenye viwanda. Matajiri wakubwa ni wenye viwanda...
Huduma za treni kwenda Pugu zimekuwa mbovu sana siku za karibuni. Treni zinachelewa. Zinaenda mwendo wa kusuasua. Mabehewa ovyo. Abiria wanaingia bure.
Hiyo treni bado inahitajika iimarisheni. Itengeezeeni COST CENTRE yake muine kama inalipa ili ipewe ruzuku ya serikali au mpandishe bei.
Sio kwamba wafanyabiashara hawajui. Tatizo ni namna ya kuwasafirisha na gjarama zake. Hizi ndege za kuungaunga hadi Morocco sio rahisi. Miuondo mbinu ya usafirishaji wa meli poa migumu.
Mie najiuliza kama serikali yetu sikivu inaweza kuwasilikilza Hospitali ya Aghakan/NHIF, wamachinga wa Kariakoo/TRA inashindwaje kuwasikiliza chadema? Ingewaacha hakuna mtu angejua kuna tukio la chadema Mbeya. Tumuimbe Rais wetu awe anaingilia mapema matukio yanayorudisha 4R zake.
Walikuwa na ibada zao. Walichagua vitu ambavyo havikuwa vya kawaida kwenye jamii kama miti mikubwa, mawe, jua, nyota, mwezi, milima kuwa miungu yao. Ingawa wanaweza kuwa hawakuwa sahihi kwa mapokeo ya sasa lakini bado walikuwa na ibada zao. Nyingine zipo mpaka leo kulingana na makabila yao.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.