Nakumbuka iyo siku nilikuwa na kaka yangu nikamtania "Kaka leo si unajua siku ya UKIMWI duniani, nenda kapime '
Akanijibu kwa msisitizo kabisa..." Nani mimi?! Weeh nitapima vyote ila sio iyo kitu yaan, yaan waniambie nakufa kesho mimi? Ahna siwezi tena nakushauri na wewe na ilo limwili lako...
Ni kweli, ila pia kuna wanaume ni wabishi hata kupima kipindi cha mwanamke akiwa mjamzito, ivo mwanamke anajikuta katika ilo peke yake.
Nakumbuka kuna siku nilikuwa naongea na doctor ofisini kwake, akaja nesi kama emergency kua kuna mama Ana mtoto wa miezi mitatu anamnyonyesha wamempima...
Huwa kuna utaratibu wa kucheck cd4 kila baada ya muda flani.... Hata mimi ndo nimetoka kupewa majibu yangu hapa.... Zinapanda tu, namshukuru Mungu kwakweli
Na hayo magonjwa yanatokea kwa wale wasiojijua mapema, wale wabishi kupima afya zao, afu unakuta ni +. Kinga inapungua Kiasi kwamba magonjwa yakija yanapiga tu.
Binafsi! Mwanzoni ilikuwa ngumu, ila baada ya kukubali na kuitengeneza amani nayo, aiseee sioni tofauti na sijawahi kuwaza eti nitakufa kesho?!... Hahaha hapana aisee labda nipitiwe na roli, au mengine ila HIV is not a problem to me
data
I don't have IG account that I disclosed my status, because this is TANZANIA.
Watu wengi bado elimu yao juu ya ili ni ndogo, sasa ukitaka unyooshewe vidole everywhere bila sababu do that!
I did here, na kwa very closest people of mine ambao hata wao bado wananibishia, mmoja hadi alilia...
Usiogope kufa dear... Kwasababu kiumbe chochote hai kilichozaliwa kikaanza kuishi ipo siku kitaacha kuishi, kwaiyo haijalishi ur negative, or HIV positive.... Kifo kwetu ni pale pale.... Just ishi happy life to the fullest, Coz we only live once darling
Mh uyo itakua alikuwa na iyo issue zamani ila alikuwa hajui, na pengine kajua pindi cd4 zimeshashuka sana magonjwa kama hayo TB na mengine ndo yanashambulia sana, ila ukiwahi unadunda tu, ukajikubali hupati shida kabisa. Ila daah taking all of the ARV's at once mmh, zilivyokubwa vile...
Am good, everything is ok with me Haszu.... Being Positive haijanizuia chochote, am enjoying life to the fullest, just like everyone out there...! Na wala huwezi kujua unless nikwambie that nipo hivi nikupe na kadi usome, otherwise unakataa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.