Gharama ya usajili wa kampuni hutegemeana na mtaji wa kampuni husika, tembelea katika tovuti yetu ya www.brela.go.tz kuona gharama za usajili wa kampuni pamoja na aina za kampuni na kupata taarifa zaidi.
Usajili wa kampuni unafanyika moja kwa moja kwa njia ya mtandao kupitia BRELA ORS au http://www.brela.go.tz, unatakiwa kuwa na:- 1.Katiba ya kampuni (Memorandum and Articles of association) 2.Namba ya kitambulisho cha taifa (NIN) kwa wahusika ambao ni watanzania kwa wahusika ambao sio watanzania...
Habari, zoezi la kufungua kampuni ni rahisi na ufanyika kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wetu wa ors.brela.go.tz, pindi unapojaza taarifa za usajili wa kampuni yako na kukutana na changamoto usisite kuwasiliana nasi kupitia namba yetu ya kituo cha miito BRELA 0222212800 kwa msaada zaidi.
Habari, pole kwa changamoto uliyokutana nayo, watoa huduma wetu katika kitengo cha TEHAMA walikua wanahudumia wateja wengine, tunaomba kufahamu changamoto uliyokutana nayo katika mfumo wetu kwaajili ya msaada zaidi.
Habari, unatakiwa kutengeneza akaunti yako ya BRELA ORS kisha andika barua ya maombi kuja BRELA kwaajili ya kuomba akaunti yako kuwezeshwa (access) kwaajili ya kufanya maombi ambayo unahitaji katika mfumo wetu.
Habari, pole kwa changamoto uliyokutana nayo, tunaomba tutumie namba ya kampuni yako pamoja na jina la kampuni husika kwa njia ya ujumbe (DM) kwaajili ya msaada zaidi.
Habari, katika usajili wa jina la biashara (business name) shughuli mwisho ni nne, ndio unaweza kusajili kampuni mpya BRELA kwa kutumia jina la biashara yako ambalo tayari limesajili BRELA, utatakiwa kufunga jina la biashara husika (ceasation of business name) kisha utaendelea na usajili wa kampuni.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.