Hodihodi Jamvini, naomba nipokeeni,
Mja wenu najirudi, mwenzenu nisameheni,
Nimechanganya maneno, niliyotoa jamvini,
Sikutumia busara, matusi kuyathamini,
Nikaanika jamvini, maneno yasoakili,
Nikasahau watoto, eti napinga ugali,
Huyu shetani gani, nimtafutie nauli,
Aende zake mwituni, akale...