Peniela (Story ya kijasusi)

LEGE

JF-Expert Member
Oct 14, 2011
5,123
9,168
SEASON 1
SEHEMU YA KWANZA
MTUNZI : PATRICK.CK
Ni saa sita za usiku sasa bado jaji Elibariki chukuswa yuko sebuleni akiendelea kupitia kitabu chake cha sheria .Katika meza ndogo kulikuwa na vitabu vingine zaidi ya saba vya sheria.Aliendelea kufungua ukurasa baada ya ukurasa.Alionekana kuwa na mawazo mengi mno.Wakati akiendelea kupitia kurasa za kitabu kile mke wake akaingia pale sebuleni akiwa na kikombe cha kahawa, akakiweka mezani halafu akainama na kumbusu mumewe.

“ You need to take a rest now.Tommorow is your big day” akasema Flaviana mwanamke mwenye uzuri wa kipekee.Elibariki akakifunika kitabu chake na kumtazama mkewe ,akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kusema

“ Natamani sana nipumzike lakini sina hakika kama nitapata usingizi.”
Mke wake akamuangalia kwa makini halafu akasema
“ Kuna jambo nataka nikuulize mume wangu”
“ Uliza usihofu ”
“ Najua kesi hii ni moja kati ya kesi kubwa na ngumu kwako.Hukumu unayotarajia kuitoa kesho inasubiriwa kwa hamu kubwa sana na umma wa watanzania.Wewe ni jaji na nina imani maamuzi yako utakayoyachukua ni sahihi kabisa,lakini swali langu ni je Yule msichana ana hatia?
Swali lile lilionekana gumu sana kwa jaji Elibariki.Akainama akafikiri kidogo halafu akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kumtazama mkewe.

“ My love kesi hii ni ngumu sana na imejaa utata mwingi na ndiyo maana unaniona mpaka hivi sasa bado niko hapa.” Akasema Elibariki
Flaviana akamtazama mume wake na akagundua kwamba hakuwa tayari kumjibu swali alilouliza.Akas
imama na kusema

“ Sina wasi wasi na maamuzi utakayoyatoa kesho lakini nakuomba utoe haki kwa upande wenye haki.”
Elibariki hakumjibu kitu akabaki akimuangalia
“ Come to bed when you are done,but don’t stay till very late.You have a big day tomorrow.” Akasema Flaviana na kuelekea chumbani .Elibariki akavuta pumzi ndefu na kuchukua kitabu chake cha sheria akaendelea kukisoma.
“ Katika maisha yangu ndani ya sheria sijawahi kukutana na kesi ngumu yenye mitihani kama hii.Hata hivyo niliapa kusimamia sheria na kutenda haki kwa kila mwenye haki.

Katika maamuzi yangu ya kesho lazima nifanye kwa haki japokuwa nina hakika nitakuwa katika matatizo makubwa baada ya hukumu ya kesho lakini siwezi kupindisha sheria eti tu kwa sababu ya shinikizo toka kwa mtu au kikundi cha watu.Mungu ataniongoza na kunisimamia ili nitoe hukumu ya haki” akawaza Elibariki na kufunga vitabu vyake akaelekea chumbani kulala.tayari Flaviana mke wake amekwisha lala.Akamtazama kwa makini na kujisemea moyoni

“ Nina hakika hata wewe hautanitazama vizuri baada ya hukumu ya kesho,lakini sina namna nyingine zaidi ya kutenda haki.Utanisamehe mke wangu” akawaza Elibariki na kupanda kitandani kulala.

***********

“ Eli my love,amka kumekucha !! ..Ilikuwa ni sauti tamu na laini ya Flaviana akimuamsha mumewe.Jaji Elibariki ambaye asubuhi hii alionekana kuzama katika usingizi mzito akafumbua macho huku akiguna na kutazama saa ya ukutani.Ni saa kumi na mbili na dakika ishirini za asubuhi.
“ jana sikupata usingizi kabisa.Usiku wangu ulikuwa mrefu sana” akasema kwa sauti ya uchovu.

“ Please wake up honey.Today its going to be a very long day” akasema Flaviana.Elibariki akainuka na kuelekea katika chumba chake cha mazoezi akafanya mazoezi kidogo halafu akaelekea bafuni.Bado kichwa chake kiliendelea kuwa na mawazo mengi sana.Kisha oga akarejea chumbani na kukutana na suti nzuri aliyoandaliwa na mke wake akavaa na kujitazama katika kioo kikubwa kilichokuwamo chumbani mwao.Aliganda pale katika kioo hadi mke wake alipoingia naye akaanza kujiandaa.

“ Leo unakwenda kazini? Akauliza Jaji Elibariki.Flaviana akacheka kidogo na kusema
“ Usinichekeshe mume wangu,yaani niende kazini leo? Siwezi kufanya hivyo hata kidogo.Leo ni siku yako kubwa.Ni siku yetu kubwa.Ni siku ambayo jina lako litaingia katika vitabu vya historia kwa hukumu unayokwenda kuitoa.Vyombo vyote vya habari vitakuwepo mahakamani ,lazima na mimi niwepo nikuunge mkono pamoja na mdogo wangu Anna.” Akasema Flaviana.Elibariki hakujibu kitu akaendelea kujitazama katika kioo.

“Are you nervous my love? Akauliza Flaviana
“ No I’m not” akajibu Elibariki halafu wakaongozana kuelekea katika chumba cha chakula kwa ajili yakupata kifungua kinywa.Wakati wakiendelea na kupata kifungua kinywa simu ya Jaji Elibariki ikaita.Akaitazama ikiita akasita kuipokea.
“ Mbona hupokei hiyo simu? Akauliza Flaviana
“ Its your father.Mr President” akajibu Elibariki
“ Usiogope.Ongea naye .Si kawaida yake kupiga simu mida kama hii.Inawezekana ana jambo la maana la kukwambia” Akasema Flaviana.Elibariki akaichukua simu na kubonyeza kitufe cha kupokelea huku akiinuka na kuelekea sebuleni.

“ Hallo Mr President” akasema Jaji Elibarki
“ Hallo Jaji.Mnaendeleaje vijana wangu?
“ Tunaendelea vizuri mzee.Ninyi mnaendeleaje?
“ Tunaendelea vizuri sana”
“ Nashukuru kusikia hivyo” akasema Elibariki na kimya kifupi kikapita
“ Elibariki,today its your big day” akasema Mheshimiwa rais.
“ Najua unakwenda kutoa hukumu katika kesi ngumu inayovuta hisia za watu wengi na hasa kwa kuwa binti wa rais naye kesi hii inamuhusu kwani mchumba wake ndiye aliyeuawa.Sikufundishi kuifanya kazi yako lakini fanya maamuzi ya haki kwa namna uonavyo wewe.Pamoja na hayo kuna jambo ambalo nataka kukuomba kijana wangu” Akasema Dr Joshua Johakim rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“ Nakusikiliza mzee” akasema Jaji Elibariki kwa wasi wasi .
“ Nilikuteua kuwa jaji kwa sababu wewe ni msomi mzuri na unazifahamu sheria za nchi kwa hiyo sitaki kuingilia maamuzi yako lakini nakuomba kijana wangu,try in anyway you can to make my daughter Happy.Alimpenda sana Edson.Ni hilo tu ninalotaka kukuomba kijana wangu.Nakutakia siku njema” akasema mheshimiwa rais na kukata simu.Jaji Elibariki alibaki ameduwaa asijue afanye nini.Maneno yale ya rais ambaye ni baba mkwe wake yalimfanya ahisi kuchanganyikiwa.

“ Huu ni mtihani mgumu sana lakini Mungu atanitangulia nitatenda haki” akawaza Elibariki na kurejea mezani
“ Amekwambia nini baba? Mbona sura yako imebadilika namna hiyo? Akauliza Flaviana
“ Nothing.Just greetings” akajibu Elibariki na kuendelea kupata kifungua kinywa.Baada ya kumaliza akarejea chumbani na kujitazama tena katika kioo na kuvuta pumzi ndefu.

“ Please help me Lord.I’m in a very difficult situation” akasema Elibariki kwa sauti ndogo na mara mke wake akaingia mle chumbani
“ Its time my love.Are you ready?
“ Let’s go” akasema Elibariki ,wakatoka wakaingia garibni na kuondoka.

**********

Hakukuwa na nafasi tena ya kukaa ndani ya chumba cha mahakama kutokana na watu kujaa.Ni siku ya hukumu ya kesi ya mauaji inayomkabili mmiliki wa maduka makubwa ya mavazi ya Penny Fashion,Peniela Salimote.Kesi hii iliyovuta hisia za watu wengi na kuwafanya wafurike ili kuja kusikia hukumu ilikuwa inaonyeshwa moja kwa moja katika runinga.ILikuwa ni kesi ya kwanza kubwa kurushwa moja kwa moja katika runinga.Katika kila kona ya nchi watu walikuwa wakifuatilia matangazo ya moja kwa moja ya kesi hii ambayo hukumu yake ilikuwa inasubiriwa na watu wengi.

Ndani ya chumba cha mahakama ilikuwepo familia ya rais ikiongozwa na mke wa rais,Dr Flora Johakim ambaye alikuwa ameambatana na binti zake wawili Flaviana na Anna.Familia ya Edson Kobe kijana anayedaiwa kuuliwa na Peniela nayo ilikuwepo mahakamani hapo ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka.Familia ya Edson na ile ya rais zilikuwa ni familia rafiki kwa muda mrefu sana.Kwa upande wa Penny hakukuwa na ndugu yake yeyote aliyefika mahakamani pale zaidi ya rafiki zake wachache.

Tayari mtuhumiwa amekwisha ingizwa mahakamani na aliyekuwa akisubiriwa ni jaji anayeisikiliza kesi ile aweze kuingia na kuisoma hukumu.Wakati wakimsubiri Jaji aingie,Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny alikuwa akibadilishana mawili matatu na mteja wake .
“ Jason,kabla hukumu haijaanza ninaomba nikwambie kitu.” Akanyamaza kidogo na kuendelea.

“ Nakushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia.Umenisimamia katika kesi hii kwa kila namna ulivyoweza.Najua chochote kinaweza kikatokea siku ya leo hivyo nakuomba endapo ikitokea nikakutwa na hatia na kufungwa kifungo cha maisha au kifo uhakikishe yale yote niliyokuandikia katika karatasi unayatimiza.Wewe ni zaidi ya rafiki.Wewe ni ndugu yangu pekee ninayekutambua.Ninakukabidhi kila kilicho changu endapo mambo yataenda kinyume na matarajio yetu." Akasema Penny huku machozi yakimtoka
“ Penny naomba usikate tamaa hata kidogo.Nimepambana vya kutosha kuhakikisha kwamba tunashinda kesi hii lakini kama mambo yataenda tofauti na matarajio yetu hautakuwa ni mwisho.Nitapambana hadi nihakikishe haki imepatikana.” Akasema Jason na mara jaji akaingia.

Wakati Jaji akiingia Penny akamnong’oneza Jason sikioni
“ I didn’t do it.I didn’t kill him”
“ I know Penny and I believe you” akasema Jason na mara mahakama ikaanza.”
 
SEASON 1
SEHEMU YA PILI
MTUNZI : PATRICK CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Tayari mtuhumiwa amekwisha ingizwa mahakamani na aliyekuwa akisubiriwa ni jaji anayeisikiliza kesi ile aweze kuingia na kuisoma hukumu.Wakati wakimsubiri Jaji aingie,Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny alikuwa akibadilishana mawili matatu na mteja wake .
“ Jason,kabla hukumu haijaanza ninaomba nikwambie kitu.” Akanyamaza kidogo na kuendelea.

“ Nakushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia.
Umenisimamia katika kesi hii kwa kila namna ulivyoweza.Naju
a chochote kinaweza kikatokea siku ya leo hivyo nakuomba endapo ikitokea nikakutwa na hatia na kufungwa kifungo cha maisha au kifo uhakikishe yale yote niliyokuandikia katika karatasi unayatimiza.Wewe ni zaidi ya rafiki.Wewe ni ndugu yangu pekee ninayekutambua.Ninakukabidhi kila kilicho changu endapo mambo yataenda kinyume na matarajio yetu." Akasema Penny huku machozi yakimtoka

“ Penny naomba usikate tamaa hata kidogo.Nimepambana vya kutosha kuhakikisha kwamba tunashinda kesi hii lakini kama mambo yataenda tofauti na matarajio yetu hautakuwa ni mwisho.Nitapambana hadi nihakikishe haki imepatikana.” Akasema Jason na mara jaji akaingia.Wakati Jaji akiingia Penny akamnong’oneza Jason sikioni
“ I didn’t do it.I didn’t kill him”
“ I know Penny and I believe you” akasema Jason na mara mahakama ikaanza.”
ENDELEA…………………………..

Masaa manne yamekwisha katika sasa toka Jaji Elibariki alipoanza kuisoma hukumu .Ndani ya chumba cha mahakama kulikuwa na ukimya mkubwa kila mtu akifuatilia kwa umakini mkubwa kila alichokisema Jaji.Baada ya maelezo marefu kuhusiana na mwenendo mzima wa kesi ,hatimaye ukafika wakati wa kuhitimisha hukumu,wakati ambao ni mgumu kwa kila mtu mle mahakamani.Mke wa rais Dr Flora Joakin alishikana mikono na wanae Flaviana na Anna wakipeana moyo.Familia ya Edson halikadhalika walikuwa katika wasi wasi mkubwa kwani hakuna aliyejua jaji anakwenda kusema nini.

Toka alipoingia ndani ya chumba cha mahakama,Anna mtoto wa rais amekuwa akimtazama kwa hasira Peniela aliyekaa ndani ya kizimba kilichokuwa mbele kabisa ya mahakama.

“ Leo ndiyo siku yako ya mwisho kahaba wewe,mdanida waume za watu.Ndani ya muda mfupi ujao utayaanza maisha mapya gerezani paka wewe.Nilikuahidi kwamba utaozea gerezani na sasa utayaamini maneno yangu.Mwangalie kwanza alivyopauka na kukondeana kama muwa.” Akawaza Anna akiendelea kumtazama Penny kwa hasira
“ Ulinitenganisha na Edson mwanaume niliyempenda kuliko wote duniani.Urafiki wetu ulianza toka utotoni lakini ulivuruga kila kitu na mwishowe Edson akaniacha.Ninakuchukia wewe mwanamke na na laiti ningekuwa na uwezo ningekukata masikio “ Anna aliendelea kuwaza na akashindwa kuyazuia machozi kumtoka .Kitendo cha kumuona tena Peniela kilimrejeshea taswira ya Edson mwanaume aliywahi kumpena kupindukia.Akainama na kufuta machozi

Wakati kila mtu moyo ukimuenda mbio akisubiri maamuzi ya Jaji,Peniela alikuwa amefumba macho michirizi ya machozi ikionekana mashavuni pake.Alikuwa akiomba.

“ Ee Mungu baba,wewe ndiye mwenye uwezo wa kuona kila kitu hadi ndani ya mioyo yetu.Baba unafahamu sijatenda kosa hili ninaloshtakiwa nalo.Nimeteseka gerezani kwa mwaka mzima na hakuna anayeonekana kuniamini kwamba sikumuua Edson.Baba imetosha sasa na ninaomba kwa mapenzi yako itolewe hukumu ya haki”
Jason mwanasheria wake alikuwa amemuelekezea macho akimtazama na kumuonea huruma sana.

“ She’s Innocent.She didn’t kill him.Please Lord help her” akawaza Jason.Penny aliendelea kuyafumba macho yake machozi yakiendelea kumtoka na mikono yake akiwa ameifumbata kifuani .Jaji Elibariki aliendelea kumalizia kuisoma hukumu yake
Taratibu Penny alihisi miguu yake inaisha nguvu pale Jaji alipotamka kwamba upande wa mashtaka umeshindwa kuithibitishia mahakama kwamba Penny alimuua Edson licha ya kuwasilisha ushahidi na vielelezo vingi.Jaji Elibariki alikwenda mbali zaidi na kuainisha namna ushahidi uliotolewa mahakamani ulivyokosa nguvu ya kuweza kumtia hatiani mshtakiwa kwa hiyo kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa anamuachia huru Penny.Alipotamka tu maneno hayo Penny akaanguka na kupoteza fahamu.

**********

Mtu wa kwanza kumtambua baada ya kurejewa na fahamu akiwa hospitalini alikuwa ni Jason mwanasheria wake.Mara tu alipopoteza fahamu baada ya Jaji kumuachia huru ,Penny alikimbizwa katika hospitali ya karibu kwa ajili ya huduma ya kwanza.

“ Jason ..!.akasema Penny kwa sauti dhaifu huku akitaka kuinuka lakini akashindwa mwili haukuwa na nguvu.
“ Penny relax ..!!!..Endelea kupumzika…” kabla hajamaliza sentensi yake Penny akapoteza tena fahamu.

“ Amepatwa na mstuko mkubwa huyu binti.Tunahitaji kumuweka hapa kwa muda tuendelee kumuangalia” akashauri daktari.
Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny hata naye bado alikuwa katika kutoamini kama ni kweli Penny ameachiwa huru.Alifanya kazi kubwa ya kumtetea Penny lakini ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka ulikuwa mzito na uliotosha kabisa kumtia hatiani mteja wake.

Alimshukuru Mungu kwa muujiza ule mkubwa.Alimshuk
uru vile vile jaji Elibariki kwa maamuzi yale ya haki.
“ Haki imetendeka.Jaji Elibariki ameweka historia kwa kutoa hukumu ambayo wengi hawakuitegemea” akawaza Jason na mara daktari akamfuata na kumwambia kwamba kuna kundi la waandishi wa habari nje wanaohitaji kuongea na Penny.Akatoka na kwenda kukutana nao na kuwataarifu kwamba Penny hakuwa tayari kuongea na waandishi wa habari kwa wakati huo.

**********

Jaji Elibariki alipomaliza kutoa hukumu yake akatoka ndani ya mahakama huku nyuma yake akiacha vilio na mshangao kwa wengi hasa wale wa upande wa Edson.Asilimia kubwa ya wale waliokuwa waki fuatilia kesi ile waliamini kwamba lazima mahakama ingemkuta na hatia Penny. Flaviana mke wa Jaji Elibariki alikuwa amesimama amejishika kiuno asiamini kile kilichokuwa kimetokea

“ How could you do this to us Eli…!! Akasema kwa sauti ndogo na kupandwa na hasira alipomtazama mdogo wake Anna ambaye alikuwa ameanguka chini ameishiwa nguvu .Familia ya Edson nao hawakuamini kilichokuwa kimetokea.Walik

umbatiana na kulia kwa pamoja .Hawakuamini kama ni kweli mtu anayesadikiwa kumuua mtoto wao ameachiwa huru.
Dr Flora Joakim mke wa rais akakumbatiana na mama wa Edson na kumfariji akimuhakikishia kwamba huo haukuwa mwisho.Watapambana hadi haki ipatikane.

**********

Kitambaa cha mkononi cha jaji Elibariki kilikuwa kimeloa jasho lililokuwa linamtiririka kwa wingi licha ya ofisi hiyo kuwa na kipoza hewa.
“ I did it !!..” akasema kwa sauti ndogo
“ Nashukuru nimemaliza kesi.Penny hakuwa na hatia.Hakumuua Edson.” Akawaza huku akiendelea kujifuta jasho
“ Nimetoa hukumu ambayo wengi hawakuitarajia.Wengi waliamini lazima Penny angekutwa na hatia na kupewa adhabu kali akiwemo rais na familia yake.

Hata mke wangu akiwa ni sehemu ya familia ya rais naye alitegemea nimpatie Penny adhabu kali sana.Nimekwenda kinyume na matakwa yao kwa hiyo toka sasa nitaonekana msaliti na inanibidi kujiandaa kwa matatizo yatakayonikuta lakini sintoogopa kitu chochote kile kitakachonitokea kwa kuitenda vyema kazi yangu na wala sintafanya kazi kwa shinikizo la mtu au kikundi cha watu.Si rais wala mtu mwingine yeyote atakayenishinikiza nifanye atakavyo yeye” akawaza Elibariki na kujifuta jasho ,akainuka na kwenda dirishani akachungulia nje.

“Niliziona sura za familia ya mke wangu namna zilivyobadilika baada ya kutangaza kwamba Penny yuko huru.After today we’ll never be the same again” akawaza na mara sura ya Penny ikamjia, akatabasamu
“ Moyo wangu una furaha kwa kumrejeshea tena uhuru wake Penny ambaye ameteseka mwaka mzima gerezani bila hatia.Nisingeitendea haki taaluma hii kama ningekubali shinikizo la kumfunga maisha gerezani.”

Akainuka na kuanza kuzunguka zunguka mle ofisini
“ Kuna kitu nimekuwa nikijiuliza kwa mida mrefu bila kupata majibu.Ni kwa nini kumekuwa na shinikizo kubwa la kutaka Penny afungwe au ahukumiwe kifo? Toka ndani ya moyo wangu ninaamini kabisa Penny si muuaji wa Edson .Swali linakuja kama si yeye nani alimuua Edson? Akajiuliza Jaji Elibariki na kuvuta pumzi ndefu.Lilikuwa ni swali gumu lisilo na jawabu
“ Maswali haya ni magumu lakini yanahitaji majawabu.

Kesi tayari imekwisha lakini kuna kila ulazima wa kwenda mbali zaidi na kutafuta majibu ya maswali haya.Ninaamini kuna jambo linajificha hapa na bila kupata majibu ya maswali haya basi maisha ya Penny hayatakuwa salama.Kumuachia huru pekee haitoshi inabidi kuhakikisha pia na usalama wake baada ya kuwa huru.Atakuwa huru tukimpata muuaji wa Edson bila hivyo Penny atauawa tu” Akainuka na kwenda tena dirishani akachungulia nje

“ Sielewi ni kwa nini ninataka kujiingiza katika jambo kama hili ambalo ninajua lazima litaniletea matatizo makubwa lakini nafsi inanituma lazima nifanye hivi kwa ajili ya usalama wa Penny.Sina taaluma ya kuchunguza na kumpata muuaji lakini nitatumia kila mbinu ili niweze kufanikisha suala hili.I must dig deeper” akawaza Elibariki.

************

Ni saa tatu za usiku ,chupa ya mvinyo iliendelea kushuka taratibu.Toka aliporudi nyumbani Jaji Elibariki alikuwa amejifungia chumbani kwake akiendelea kupata mvinyo huku akitazama mpira katika runinga kubwa iliyokuwamo humo chumbani.Kazi kubwa aliyokuwa nayo usiku huu ni kupokea simu toka kwa watu mbali mbali marafiki zake waliokuwa wakimpongeza kwa hukumu ile ya kihistoria.

Wakati akiongea na mmoja wa rafiki zake simu nyingine ikaita,akatazama mpigaji alikuwa ni baba mkwe wake,Profesa Joshua Joakim rasi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

“ Kazi imeanza” akawaza na kumuomba samahani Yule rafiki yake aliyekuwa akiongea naye na kuichukua simu ile iliyokuwa ikiita akabonyeza kitufe cha kupokelea.

“ Hallo mzee” akasema Jaji Elibariki.Zikapita kama sekunde kadhaa akasikia sauti ya rais.Haikuwa ile sauti yake aliyoizoea kuisikia
 
SEASON 1
SEHEMU YA TATU
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Ni saa tatu za usiku ,chupa ya mvinyo iliendelea kushuka taratibu.Toka aliporudi nyumbani Jaji Elibariki alikuwa amejifungia chumbani kwake akiendelea kupata mvinyo huku akitazama mpira katika runinga kubwa iliyokuwamo humo chumbani.Kazi kubwa aliyokuwa nayo usiku huu ni kupokea simu toka kwa watu mbali mbali marafiki zake waliokuwa wakimpongeza kwa hukumu ile ya kihistoria.Wakati akiongea na mmoja wa rafiki zake simu nyingine ikaita,akatazama mpigaji alikuwa ni baba mkwe wake,Profesa Joshua Joakim rasi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
“ Kazi imeanza” akawaza na kumuomba samahani Yule rafiki yake aliyekuwa akiongea naye na kuichukua simu ile iliyokuwa ikiita akabonyeza kitufe cha kupokelea.

“ Hallo mzee” akasema Jason.Zikapita kama sekunde kadhaa akasikia sauti ya rais.Haikuwa ile sauti yake aliyoizoea kuisikia.

ENDELEA………………………………………….

“ Hallow mheshimiwa Jaji habari za jioni?
“ Habari nzuri mheshimiwa rais.Pole na majukumu”
“Ahsante sana kijana wangu nimekwisha poa” akasema mheshimiwa rais halafu kimya kifupi kikapita.Rais akauvunja ukimya
“ Elibariki nimekupigia simu kuna jambo nataka tuongee”
“ Ndiyo nakusikiliza mzee”
“ Naomba kwanza nikupongeze kwa kuimaliza kesi ngumu iliyovuta hisia za watu wengi.Pamoja na pongezi hizo, naomba niwe wazi kwako kwamba sijafurahishwa hata kidogo na maamuzi uliyoyafanya.

To ka awali nilikuomba ufanye kila linalowezekana ili shemeji yako Anna aweze kupunguza machungu ya kifo cha mpenzi wake Edson.Alimpenda sana Edson na walikuwa na ndoto nyingi siku za usoni.Sina maana ya kudharau maamuzi yako kama jaji,lakini kitendo cha kumuacha huru muuaji wa mpenzi wa mwanangu kimenifadhaisha sana mimi na familia yangu kwa ujumla.Elibariki umemuoa mwanangu kwa hiyo nakuhesabu nawe ni sehemu ya familia yangu.Kama mwanangu ulitakiwa kusimama upande wa familia yako na kumuadhibu muuaji lakini pamoja na ushahidi wote uliowasilishwa mahakamani bado umeupuuza ukamuachia huru Yule msichana.

Naomba tu ufahamu kwamba maamuzi haya yamenifadhaisha sana mimi na familia yangu kwa ujumla.Ni hayo tu niliyotaka kukwambia usiku huu.Kwa heri Jaji” akasema mheshimiwa rais na kukata simu.Jaji Elibariki alihisi kijasho kikimchuruzika.Akainua glasi yake ya mvinyo na kunywa fundo kubwa.

“ Nilijua tu lazima mambo kama haya yangejitokeza kwani rais na familia yake walitegemea ningefanya kama walivyokuwa wakishinikiza wao kwamba nimpatie Penny adhabu kali.Kwa maamuzi ya kumuachia huru nimekwisha tangaza vita na familia hii na nina hakika maisha yangu yatakuwa magumu sana kuanzia sasa.Lakini vyovyote itakavyokuwa siyajutii maamuzi yangu.Nimetenda haki na siku zote nitasimama katika haki.Nitatenda haki bila kujali uwezo wa mtu na sintokubali kufanya kazi yangu kwa shinikizo toka kwa mtu yeyote .

Si rais wa nchi wala mtu yeyote atanishinikiza nifanye kazi kwa matakwa yake.Ninafanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi.” Akawaza Jaji Elibariki akiwa na hasira na kunywa tena fundo lingine
“ Ndiyo maana ninataka nifanye uchunguzi ili kumbaini muuaji wa Edson.Hapo ndipo nitakapowadhihirishia kwamba maamuzi yangu ya kumuachia Penny yalikuwa sahihi kabisa.Nisipofanya hivyo nitajiweka mahala pabaya na hata Penny maisha yake hayatakuwa na amani na salama.Lazima watamuandama tu.”

Akiwa bado katika mawazo mara mlango ukafunguliwa na akaingia mke wake Flaviana.Bila kumsalimu mumewe akajitupa kitandani .Alionekana mchovu sana na usoni alionekana ni mwenye hasira.Baada ya dakika kama tano hivi za ukimya mle chumbani kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwao Elibariki akaamua kuuvunja ukimya na kumuuliza mke wake
“ Umechelewa wapi?

“ Nilikuwa nyumbani kwa baba nikilia na familia yangu” akajibu Flaviana kwa sauti ya ukali
“ Kwa nini hukunitaarifu kama utachelewa ili nisiwe na wasi wasi kuhusu usalama wako?
Flaviana akacheka kidogo kicheko cha dharau na kusema
“ Sikuona umuhimu wa kukutaarifu.”
Jibu lile likamstua sana Jaji Elibariki.Hata siku moja mke wake hakuwahi kumjibu kijeuri namna ile
“ Hukuona umuhimu wa kunitaarifu mahala uliko? Tabia hii imeanza lini? Akauliza Elibariki
“ Ndiyo sikuona umuhimu huo”
“ Flaviana naomba uwe makini na kauli zako.Mimi ni mumeo na ni lazima nijue kila kitu unachokifanya.

Mimi nina maadui wengi nitajuaje kama umedhurika huko njiani? Nimekaa hapa mawazo tele nikiwazia usalama wako” akasema Jaji Eli
“ Kwa maana hiyo unataka kumaanisha kwamba mimi ni wa muhimu kwako? Akauliza Flaviana
“ Maswali gani hayo unayouliza Flaviana? You are my wife and you are important to me”
“ Save your breath Eli.I’m not important to you at all.I mean nothing to you”
“Una hakika na hayo unayoyasema ? akauliza Eli
“ Ningekuwa ni wa thamani kwako basi ungeithamini na familia yangu pia na usingefanya maamuzi kama uliyoyafanya.Sikutegema kama ungemuachia huru Yule kahaba.

How could you let her go? Kahaba Yule alimuua Edson na kuna kila ushahidi wa kutosha ulikuwepo kumtia hatiani lakini kwa makusudi kabisa umeamua kumuacha huru.You have broken my sister’s heart and mine as well.I’m disappointed,very disappointed” akasema Flaviana kwa hasira.Elibariki akanywa fundo kubwa la mvinyo halafu akazima runinga na kumgeukia mkewe
“ Flaviana naomba iwe ni mwanzo na mwisho wewe na familia yako kuingilia kazi yangu.Mimi ndiye ninayehukumu na si mtu mwingine kwa mantiki hiyo basi hakuna anayeweza kunishinikiza nifanye anavyotaka yeye.Si wewe wala baba yako wala mtu yeyote Yule anayeweza akanifundisha namna ya kuifanya kazi yangu.Halafu naomba iwe ni mara ya kwanza na ya mwisho kumuita Penny kahaba.She’s a respectable woman and you’ll have to respect her” akasema kwa ukali Jaji Elibariki.

“ Huwezi kunizuia kuongea Eli. Nitaongea chochote nikitakacho na hutanifanya kitu.That woman is just a prostitute .Nashangaa unavyosimama na kumtetea kwa nguvu.Who is she to you? Akafoka Flaviana
Maneno yale ya mke wake yakamuumiza sana Jaji Elibariki akamsogelea mkewe
“ Flaviana nakupa onyo la mwisho.Naomba tafadhali usithubutu kunijibu namna hiyo.”

“Usinitishe Elibariki.Huwezi kunifanya lolote” .Flaviana akongea kwa ukali na kwa kujiamini.Elibariki akamshika shingoni kwa hasira
“ I married you because I love you,and not because you’re a president’s daughter so don’t dare disrespect me again.If you do that again I’ll forget that your father is the president and I’ll break your neck.” Akasema Elibariki kwa hasira na kutoka mle chumbani. Pamoja na ujasiri wote aliokuwa Flaviana akajikuta akiogopa ghafla kwani hakuwahi kumuona muwe akiwa amekasirika namna ile .

“ What a stupid husband” akasema kwa sauti ndogo Flaviana baada ya Eli kutoka mle chumbani
“ Sijawahi kudharauliwa kama alivyonidharau Flaviana leo.Lakini nilijua tu mambo kama haya lazima yatakuja.Ninachopaswa kufanya ni kukabiliana nayo,.Huu ni mwanzo tu.Mengi yatakuja makubwa zaidi ya haya.” Akawaza Jaji Elibariki akiwa amekaa sebuleni amefura kwa hasira

***********

Ilipata saa nane na dakika kumi na tatu za usiku kwa mujibu wa saa kubwa ya ukutani,hali ya chumba ikiwa ni ya ubariki uliotokana na kipoza hewa huku kukiwa na mwanga hafifu na muziki laini kwa mbali,msichana mrembo Peniela alikuwa amejilaza kitandani.Baada ya kusota gerezani kwa takribani mwaka mzima hatimaye leo kama ndoto amerejea tena katika chumba chake
Kwa muda wa masaa mawili sasa amekuwa simuni akiongea na wakili wake Jason Patrick

“ Penny muda umekwenda sana nadhani ni wakati sasa wa kukuacha upumzike.Siku ya leo ilikuwa ndefu sana” akasema Jason
“ Ouh C’mon Jason,unadhani ninaweza kupata usingizi leo? Siwezi kabisa kupata usingizi kwa furaha niliyonayo na pili bado niko katika mstuko.Bado siamini kama ni kweli niko huru.Itanichukua siku kadhaa ili niamini kama ni kweli niko huru.” Akasema Penny.Jason akacheka kidogo na kusema
“Penny amini kwamba kesi imekwisha na uko huru.Mahakama imekukuta huna hatia na imekuachia huru”

“ Nakubaliana nawe Jason lakini kwa upande mwingine bado nina wasi wasi sana na maisha yangu.Sina hakika kama maisha yangu yatakuwa sawa tena.”
“ Kwa nini unasema hivyo Penny?
“ Nimewashinda watu wakubwa waliotaka kuniangamiza .Ninaamni jambo hili halitaishia hapa.Wataendele
a kuniandama usiku na mchana hadi wahakikishe kwamba wametimiza lengo lao.Anna mtoto wa rais aliapa kwamba ataniangamiza na ndiyo maana umeshuhudia nguvu kubwa ikitumika katika kuhakikisha ninafungwa gerezani.Uliona wewe mwenyewe ushahidi mzito uliotolewa mahakamani lakini pamoja na jitihada zao zote Mahakama imeniachia huru.Nina hakika mapambano yetu hayatishia hapo tu.

Nitaendelea kuandamwa kokote nitakakokuwa.My life will be a living hell”
“ Penny nashukuru kama umelifahamu hilo.Kitu cha msingi unachotakiwa kufanya ni kujiweka mbali kabisa na mambo yoyote yale yanayoweza kuwafanya wapate sababu ya kufanya lolote juu yako.Najua watatumia uwezo wao kuyafanya maisha yako yawe magumu lakini usihofu wala usiogope.Mimi nipo pamoja nawe siku zote.Vita hii ni yetu na tutashinda sote” akasema Jason

Sijui nikushukuruje Jason kwa msaada wako mkubwa.Hata nikikulipa mamilioni ya pesa ,hayataweza kufikia ukubwa wa msaada ulionisaidia.Dunia nzima ilinitenga baada ya kuaminishwa kwamba mimi ni muuaji lakini wewe pekee ndiye uliyeniamni kwamba sikutenda kosa lile na ukasimama pamoja nami.Ahsante sana Jason “ akasema Penny na kwa mbali machozi yakamlenga akikumbuka namna Jason alivyompigania hadi akawa huru

“Penny toka siku ya kwanza nilipokuona machoni niliamini hukutenda kiosa hilo na ndiyo maana nimepambana kufa na kupona kuhakikisha kwamba binti malaika asiye na hatia anaachiwa huru. Hata hivyo hayo yameshapita na ninachokuomba uyasahu yote na tuangalie mambo ya mbele.Tunatakiwa kuangalia nini kitafuata baada ya wewe kuwa huru.Tutakaa pamoja na kuangalia ni namna gani tutafanya ili uweze kujiweka vizuri kiuchumi..Mwaka mzima uliokaa gerezani najua mambo yako mengi yameyumba lakini usihofu niko pamoja nawe ,nitakusaidia hadi hapo utakapoweza kusimama tena”

“ Ouh Jason,you are so sweet.Ahsante sana kwa kujitolea kunisaidia lakini naomba kwa hili niseme hapana.Jason umenipigania mpaka nimekuwa huru.Sitaki niendelee kuwa mzigo kwako” akasema Penny
“ Penny tafadhali usirudie tena kutamka hilo neno eti wewe ni mzigo kwangu.Ninajiona ni mwenye bahati sana kuwa na rafiki kama wewe.Zaidi ya yote wewe bado ni jukumu langu.Kukusaidia kushinda kesi bado haitoshi lazima nihakikishe kwamba umeweza kujiimarisha kiuchumi .Pesa ni vitu vya kupita kwa hiyo naomba ukubali nikusaidie Penny” akasema Jason.Penny akacheka kidogo na kusema

“ Jason siku zote hutaki kushindwa.Ok tutakaa na kuliongelea suala hili”
“ Ahsante sana Penny.Pumzika sasa tutaonana kesho” akasema Jason wakaagana na kukata simu
“ Afadhali sasa nitaweza kulala usingizi.Kesi ya Penny iliyokuwa ikininyima usingizi imekwisha “ akawaza Jason
“ Nitamsaidia kwa kadiri niwezavyo hadi nihakikishe amerejea katika maisha yake ya awali.Uchumi wake umeyumba sana baada ya kukaa mwaka mzima gerezani.Bado Penny anahitaji sana msaada wangu” Akawaza halafu akastuka baada ya kukumbuka kitu
“ Kuna kitu nimekuwa najiuliza sana kuhusu Penny.Toka nimemfahamu sijawahi kuwaona ndugu zake,wala wazazi wake.Mwaka mzima nimehangaika naye katika kesi na sijawahi kumuona ndugu yake yeyote wala hajawahi kutamka lolote kuhusu ndugu zake.Jambo hili linanifanya nijiulize maswali mengi kuhusiana na maisha yake.Je hana ndugu? Kama anao wako wapi?

Kwa nini walimuacha wakati wa kipindi kigumu alichokuwa nacho?Nadhani ninahitaji kumfahamu Penny kwa undani zaidi.Kuna mambo mengi kumhusu yeye ambayo nahitaji kuyafahamu” akawaza Jason
 
SEASON 1
SEHEMU YA 4
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Afadhali sasa nitaweza kulala usingizi.Kesi ya Penny iliyokuwa ikininyima usingizi imekwisha “ akawaza Jason
“ Nitamsaidia kwa kadiri niwezavyo hadi nihakikishe amerejea katika maisha yake ya awali.Uchumi wake umeyumba sana baada ya kukaa mwaka mzima gerezani.Bado Penny anahitaji sana msaada wangu” Akawaza halafu akastuka baada ya kukumbuka kitu
“ Kuna kitu nimekuwa najiuliza sana kuhusu Penny.Toka nimemfahamu sijawahi kuwaona ndugu zake,wala wazazi wake.

Mwaka mzima nimehangaika naye katika kesi na sijawahi kumuona ndugu yake yeyote wala hajawahi kutamka lolote kuhusu ndugu zake.Jambo hili linanifanya nijiulize maswali mengi kuhusiana na maisha yake.Je hana ndugu? Kama anao wako wapi? Kwa nini walimuacha wakati wa kipindi kigumu alichokuwa nacho?Nadhani ninahitaji kumfahamu Penny kwa undani zaidi.Kuna mambo mengi kumhusu yeye ambayo nahitaji kuyafahamu” akawaza Jason.

ENDELEA……………………………….

Jaji Elibariki aliamka asubuhi na mapema na kufanya mazoezi ya viungo kama ilivyo kawaida yake halafu akajiandaa kwa ajili ya siku hiyo na kuondoka akimuacha mkewe Flaviana akiwa bado amelala.Hakuweza kupata usingizi usiku huo kutokana na kichwa chake kuwa na mawazo mengi sana.
“ Siamini kama mimi na Flaviana tumefikia hatua hii.Dharau zake zimezidi.Dharau alizonionyesha jana zimevuka mipaka. Nadhani kinachompa kiburi na kumfanya awe na dharau ni kuwa mtoto wa rais na baba yake ndiye aliyeniteua kuwa Jaji.

Kwa kigezo hicho walitegemea wanitumie watakavyo.Hapana.Siwezi kukubali kutumika.Nimekwisha vumilia mambo mengi sana toka kwa Flaviana na sasa nadhani imetosha.Nilijitahidi kuvumilia ili kuinusuru ndoa yetu lakini kwa sasa litakalotokea na litokee tu.Kuna mambo mawili ambayo natakiwa kuyafanya .Moja ni kutafuta nani muuaji wa Edson.Pili ni kuanza maandalizi ya maisha mapya kwani nina hakika muafaka kati yangu na Flaviana hautapatikana. Akawaza Jaji Elibariki wakati akikata kona kuingia Mandarini Hoteli kwa ajili ya kupata kifungua kinywa
Alihudumiwa haraka haraka na wakati akiendelea kupata kifungua kinywa akachukua simu yake na kumpigia rafiki yake Stanley
“ Halo Stanley.

Habari za asubuhi?

“ Habari za asubuhi nzuri Jaji.Nimestuka kidogo kwa simu ya asubuhi asubuhi namna hii” akasema Stanley
“ Stanley nimekupigia ninakuomba msaada wako.”
“ Nakusikiliza Jaji”
“ Kuna Yule wakili wa Yule msichana Peniela ambaye kesi yake imekwisha jana akachiwa huru, anaitwa Jason Patrick,unaweza ukanisaidia kupata mawasiliano yake?
“ Usihofu.

Nitakupatia mawasiliano yake ndani ya nusu saa” akajibu Stanley na kukata simu
Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kuwaza
“ Nadhani Jason ni sehemu nzuri ya kuanzia uchunguzi wangu.Yeye ni wakili wa Penny na nina hakika kuna mambo mengi anayoyafahamu kuhusiana na maisha ya Penny.Ninaweza kupata kitu toka kwake kitakachonisaidia katika uchunguzi wangu.Nitapenda vile vile nionane na Peniela ana kwa ana lakini makutano yetu yawe katika sehemu ya siri.

Sitaki nionekane nikiongea naye watu wanaweza wakahisi vibaya kwamba pengine nilifanya makusudi kumuachia kwa kuwa nina mahusiano naye Fulani” akawaza Jaji Elibariki na kutabasamu baada ya kumkumbuka Penny.
“ Penny ni msichana mrembo sana aliyebarikiwa uzuri wa aina yake.Ningefanya kosa kubwa sana kama ningemfunga gerezani msichana kama Yule” akawaza jaji Elibariki halafu akamaliza kupata kifungua kinywa na kuondoka kuelekea ofisini kwake.

“ Clara sihitaji kuonana na mtu yeyote siku ya leo.” Akampa maelekezo katibu muhtasi wake kisha akajifungia ofisini kwake.Hakutaka kufanya kazi yoyote siku ya leo,kichwa chake kilikuwa na wazo moja tu kumtafuta muuaji wa Edson.

“ Sina hakika kama nitampata muuaji wa Edson lakini nitajitahidi kwa kila linalowezekana hadi nimpate.Si kazi rahisi na ni ya hatari sana lakini sina namna nyingine lazima niifanye.” Akawaza jaji Elibariki na mara simu yake ikaita alikuwa ni rafiki yake Stanley
“ Hallo Stanley” akasema Jaji Elibariki
“ Jaji tayari nimekwisha pata mawasiliano ya Jason Patrick na nitakutumia sasa hivi katika ujumbe mfupi” akasema Stanley.Baada ya dakika moja ujumbe mfupi ukaingia katika simu ya Elibariki ukiwa na mawasilinao ya Jason,kuanzia namba za simu barua pepe,n.k.

Jaji Elibariki akashusha pumzi na kuziandika namba za simu za Jason akapiga
“ hallow” ikasema sauti ya upande wa pili baada ya kupokea simu
“ hallow.Naongea na wakili Jason Patrick?
“ Ndiye mimi.Nani mwenzangu?
“ Jaji Elibariki.”
“ jaji Elibariki?!...

Jason akashangaa hakuwa ametegema hata siku moja jaji Elibariki angempigia simu kwani hawakuwa na mahusiano yoyote zaidi ya kukutana mahakamani
“ Ndiyo Jason.Ni mimi Elibariki”
“ Nafurahi kupata simu yako Jaji Elibariki.Nikusaidie nini?
“ Jason nina shida nahitaji kukuona.”
“ Shida gani hiyo? Hatuwezi kuzungumza katika simu kwa sababu leo nina mizunguko mingi”

“ Ni jambo ambalo hatuwezi kuliongea simuni Jason”akasema Elibariki
Jason akafikiri kidogo na kuuliza
“ What is that about?
“ Its about Penny “ akajibu Jaji Elibariki
Jason akafikiri kidogo na kusema
“ Ok mheshimiwa.Tuonane wapi?
“ Tukutane Mandarini hotel saa tano asubuhi hii.Nitakuwa juu ghorofani ” akasema Jaji

“ Ok jaji nitajitahidi kufika kwa wakati” akasema Jason na kukata simu
“ Hii ndiyo hatua ya kwanza.Baada ya kuonana na Jason nitajua nini cha kufanya” akawaza Jaji Elibariki

************

Saa tano na dakika saba ,Jason akawasili Mandarini hoteli,akaegesha gari na kushuka akapanda hadi sehemu ya juu alikoelekezwa na Jaji Elibariki ambaye tayari alikwisha wasili kitambo
“Hallo Jason.Karibu sana” akasema Jaji Elibariki akimkaribisha Jason
“ Ahsante sana mheshimiwa jaji.”

Akasema Jason na kuvuta kiti .Muhudumu hakuchelewa akafika na kumuhudumia kinywaji
“ Jason samahani sana kwa kukuharibia ratiba zako,najua wewe ni mtu mwenye shughuli nyingi” akaanzisha mzungumzo Jaji Elibariki
“ Usijali mheshimiwa.Najua usingefanya hivyo kama kusingekuwa na jambo la msingi.Hata hivyo ninashukuru kukutana nawe ana kwa ana.Tumekuwa tunakutana tu katika kesi mahakamani.” Akasema Jason
“ Ni kweli Jason ,kuna jambo la msingi lililonifanya nilazimike kukuita hapa.Hata mimi kwa upande wangu ninafurahi pia kukutana nawe.Ulinifurahisha sana namna ulivyoisimamia kesi ya Penny.Katika maisha yangu ndani ya sheria sijawahi kukutana na wakili mahri kama wewe.You are the best Jason.Hongera sana” akasema Jaji Elibariki na wote wakaangua kicheko.

“ Ahsante kwa pongezi mheshimiwa.Hata mimi vile vile napenda nikupongeze kwa namna ulivyoiendesha kesi ile na hukumu ya haki uliyoitoa.Hukumu ile imedhihirisha kwamba mahakama iko kwa ajili ya kutoa haki bila kujali cheo cha mtu,uwezo rangi au mahala atokako.Nakupongeza sana mheshimiwa” akasema Jason ,wakainuka na kushikana mikono.

“ Ahsante sana Jason.Nilitoa hukumu ile kutokana na namna ulivyoweza kuithibitishia mahakama kwamba Penny hakutenda lile kosa.Upande wa mashitaka uliwasilisha ushahidi mwingi ambao ungeweza kumtia hatiani Penny lakini kwa umahiri wako uliweza kuufanya ushahidi ule ukose nguvu na hivyo Penny akaachiwa huru”Akasema Jaji Elibariki halafu kikapita kimya kifupi kisha akasema

“ Jason kuna jambo ambalo nimekuitia hapa linalohusiana na Peniela.” Akasema Jaji na kukaa kimya kidogo halafu akaendelea
“ Katika kesi iliyomalizika kulikuwa na nguvu kubwa iliyotumika kuhakikisha kwamba Penny anakutwa na hatia ya mauaji,lakini toka ndani ya moyo wangu ninaamini Penny hakutenda kosa lile” akasema Jaji
“ Nashukuru Jaji kwa kulitambua hilo.Nadhani ni mimi na wewe pekee ambao tunaamini kwamba Penny hakuua.” Akasema Jason
“ Kweli kabisa Jason.

Wengi wanaamini kwamba Penny alimuua Edson kutokana na mazingira yenyewe ya tukio.Lakini mwisho wa yote ukweli utabaki pale pale kwamba Penny hakuua.Lakini kuna swali ambalo nimekuwa najiuliza bila majawabu na ambalo limenifanya nikuite hapa asubuhi hii,je kama Penny hakuua nani basi alimuua Edson??

Kimya cha dakika mbili kikapita kila mmoja akifikiria halafu Jason akasema
“ Jaji Elibariki,swali hilo ni gumu mno.Hata mimi nimekuwa nikijiuliza swali kama hilo je nani aliyemuua Edson na kesi akaangushiwa Penny lakini nimekosa majibu”
“ Jason ,ukweli ni kwamba Penny yuko huru lakini hayuko salama na hata sisi ambao tumefanikisha yeye kuwa huru bado hatuko salama pia.Kuna jambo nalihisi litakua nyuma ya mauaji yale na ndiyo maana nikakuita hapa ili tujadili na kwa pamoja tushirikiane tumpate muuaji wa edson.Ni hilo tu ndilo litamuhakikishia usalmaa Penny na sisi sote.Bila kumpata muuaji ,sikufichi maisha ya Penny yatakuwa hatarini.”

“ Nakubaliana nawe Jaji.Hata yeye mwenyewe amekwisha anza kuhisi kwamba ,maisha yake hayatakuwa na amani kwani aliahidiwa na mtoto wa rais kwamba lazima atayafanya maisha yake yawe magumu”
Jaji Elibariki akatabasamu kidogo na kusema
“ hayo ni mambo ya kawaida kwa wanawake kwani inasemakana Edson alikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Anna mtoto wa rais kabla ya kuanzisha mahusiano na Peniela kwa hiyo vitisho kama hivyo ni vya kawaida .Tunachohitaji sisi ni kumtafuta muuaji halisi wa Edson.

Jason wewe umekuwa wakili wa Penny na ninatumai kuna mambo mengi ambayo amekueleza .Je hajawahi kukueleza chochote kwamba anahisi nani anaweza kuwa muuaji wa Edson?

“ Hapana mheshimiwa jaji.Penny hajawahi kunieleza chochote kuhusiana na nani anahisi anaweza kuwa muuaji wa Edson.Maelezo aliyonipa mimi siku zote ndiyo yale aliyoyatoa mahakamani kwamba alimkuta Edson ameanguka ametapakaa damu kifuani pake kulikuwa na bastora na kwa taharuki aliyokuwa nayo alijikuta akiishika ile bastora bila ya kujua kwamba inaweza kumtia hatiani kwani alama zake za vidole zilibaki katika ile bastora na ikasadikika moja kwa moja kwamba yeye ndiye muuaji.Mpaka leo hafahamu nani aliyemuua Edson” akasema Jason

“ Jason ninamuamini Penny.Inawezekana ni kweli hafahamu ni nani muuaji wa Edson lakini naomba mimi na wewe tushirikiane tufanye uchunguzi wetu na tumpate muuaji.Hiyo ndiyo itakuwa salama ya Penny na sisi sote.Toka nimeingia katika sheria sijawahi kukutana na kesi ambayo nguvu kubwa imetumika ili kuhakikisha mshtakiwa anapatikana na hatia kama hii.Hii inanishawishi kuchimba kwa undani zaidi kuhusiana na kifo cha Edson.”
“ Nakubaliana nawe jaji.Niko tayari kuungana nawe ili kufanya uchunguzi na kumpata muuaji japokuwa si suala rahisi na ni la hatari kubwa.Je unashauri tufanye nini?

“ Ahsante sana Jason kwa kukubali.Kitu cha kwanza ambacho nataka unisaidie,nahitaji kuongea na Penniela ana kwa ana lakini katika sehemu yenye usiri .Sitaki kuonekana na watu niko naye kwani wataanza kuongea mambo mengine.”
“ Sawa Jaji nimekuelewa.Nitaongea na Penniela na kumuomba akutane nawe kisha nitapanga mahala ambako mtakutana na kuongea”

**********

Wakati akina Jason wakiwa katika mazungumzo hotelini juu ya kumpata muuaji wa Edson,Penny alikuwa amekaa sebuleni kwake akitazama runinga.Hakujisikia kutoka siku hii.Alitaka kubaki ndani akipumzika baada ya mwaka mzima kusota gerezani.Akiwa amejilaza sofani kengele ya mlangoni ikalia,akainuka akachungulia nje kupitia dirishani,na kukutana na sura ambayo ilimstua sana.

Alihisi mwili ukimtetemeka kwa uoga.
 
SEHEMU YA 5
ILIPISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Wakati akina Jason wakiwa katika mazungumzo hotelini juu ya kumpata muuaji wa Edson,Penny alikuwa amekaa sebuleni kwake akitazama runinga.Hakujisikia kutoka siku hii.Alitaka kubaki ndani akipumzika baada ya mwaka mzima kusota gerezani.Akiwa amejilaza sofani kengele ya mlangoni ikalia,akainuka akachungulia nje kupitia dirishani,na kukutana na sura ambayo ilimstua sana.Alihisi mwili ukimtetemeka kwa uoga.

ENDELEA………………………………….

“ Ivan!!..akasema Penny kwa sauti ndogo .Bado mwili uliendelea kumtetemeka.Aliogopa sana.Kengele ya mlangoni iliendelea kulia,akavuta pumzi ndefu na kwenda kuufungua mlango .Mtu mmoja mwembamba mrefu ,aliyevaa suti nzuri nyeusi na miwani myeusi alikuwa amesimama mlangoni akiwa ndani ya tabasamu .Mkononi alikuwa ameshika lundo la maua mazuri.Wakatazamana kwa sekunde kadhaa

“ Welcome back Penny.I missed you so much.Even after a year in prison you are still as pretty as you used to be ” akasema Yule mtu.Penny hakuonekana kujali alichokiongea Ivan akamuuliza kwa ukali
“ What are you doing here Ivan?

“ Ouh Penny bado hujaacha machachari yako tu? Akasema Ivan huku akiendelea kutabasamu
“Ivan sema kilichokuleta tafadhali na uondoke mara moja.I don’t want to see you here” akasema Penny kwa sauti iliyoonyesha lwamba hakuwa na masihara
“ Hunikaribishi hata ndani Penny? Hatujaonana kwa muda mrefu “ akasema Ivan

“ Ivan tafadhali nakuomba sema kilichokuleta na uondoke.” Akasema Penny.Ivan akatabasamu na kusema
“ Ok Penny nimetumwa nikuletee mzigo huu”
“ Nani kakutuma?
“ Ivan hakujibu kitu akampa Penny ule mzigo wa maua.Penny akaupokea na kuuangalia kwa hasira
“ Kwa heri Penny.Nimefurahi kukuona tena” akasema Ivan na kuanza kupiga hatua kuondoka
“ Ivan please don’t come back here again” akasema Penny lakini Ivan hakugeuka akaingia katika gari lake na kuondoka,akimuacha Penny bado amesimama mlangoni
Baada ya Ivan kuondoka ,Penny akafunga mlango na kuyatupa yale maua mezani.Akayaangalia na kusema kwa sauti ndogo
“ After one year in prison,leo ndiyo ananikumbuka bazazi mkubwa Yule” Toka ndani ya maua yale kikaanguka kikadi kidogo chenye maandishi” welcome back”.Akiwa bado amesimama akitafakari mara simu ya mezani ikaita akaenda kuipokea
“ Hallow” akasema penny
“ Hallow Penny” ikasema sauti ya upande wa pili ambayo Penny aliitambua.

Kikapita kimya kifupi
“ What do you want from me? Akauliza Penny
“ Is that how you say hello to the love of your life? Akauliza mtu Yule.
“ Niambie tafadhali ni kitu gani unakitaka toka kwangu? Akauliza Penny
“ Penny naomba kwanza nikupe pole nyingi kwa masahibu makubwa yaliyokupata lakini vile vile napenda kukukaribisha tena uraiani.Tatu, leo jioni nataka kukutana nawe kwa chakula.Nitamtuma dereva aje akuchukue saa moja na nusu za jioni” akasema Yule mtu na kukata simu.Penny akabaki amesimama ameushikilia mkono wa simu.

Alizama katika mawazo.Akiwa bado amesimama akiwaza mara kengele ya mlangoni ikalia na kumstua.Haraka haraka akayakusanya yale maua na kuyafungia kabatini halafu akaenda kufungua mlango akakutana na wakili Jason
“ Jason” akasema Penny kwa mshangao kidogo kwani hakuwa ametegemea kama Jason angefika kwake mida ile
“ Hi Penny”
“ Hi Jason” akasema Penny na kumkaribisha Jason ndani.
“ Utanisamehe Penny nimekuja bila taarifa”
“ Bila samahani Jason.Hapa ni nyumbani kwako na una ruhusa ya kuja muda wowote na unakaribishwa bila hata kubisha hodi” akasema penny na kumfanya Jason atabasamu
“ Ahsante sana penny”
“ Jason unatumia kinywaji gani?
“ Ahsante Penny lakini kwa sasa sihitaji kinywaji chochote ila nimepita tu kutokana na suala la dharura lililojitokeza asubuhi ya leo”
“ Dharura gani hiyo?

Kuna tatizo? Akauliza Penny kwa wasi wasi
“ Jaji Elibariki alinipigia simu asubuhi akataka nionane naye”
“ Jaji Elibariki?!!..Penny akashangaa
“ Ndiyo “
“ Kuna tatizo gani tena? Akauliza Penny
“ Kuna suala nyeti ambalo aliniitia”
“ Suala gani hilo?
“ Anataka tumtafute muuaji wa Edson”
“ Muuaji wa edson? Penny akazidi kushangaa
“ Ndiyo Penny.Jaji Elibariki amekuwa akijiuliza swali ambalo hata mimi nimekuwa nikijiuliza bila kupata majbu,kwamba nani alimuua Edson ? Wote tuna hakika kabisa kwamba hukumuua lakini sasa nani alimuua? Tunahitaji kufanya uchunguzi na kulibaini hilo.Penny akamtazama Jason kwa sekunde kadhaa na kusema

“ Jason,siwezi kupingana na mawazo yako wala ya jaji Elibariki kwani hata mimi nimekuwa nikijiuliza swali kama hilo bila kupata jibu lakini kesi imekwisha na mahakama haijanikuta na hatia,ni kazi ya vyombo vya dola sasa kufanya uchunguzi na kubaini ni nani muuaji wa Edson?.Nadhani katika suala hili tuviachie vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yake” akasema Penny

“ Nakubaliana nawe Penny kwamba mahakama haijakukuta na hatia na ndiyo maana ikakuachia huru lakini naomba nikuweke wazi kwamba hauko salama.Kulikuwa na nguvu kubwa iliyotaka kuhakikisha kwamba unakutwa na hatia lakini hilo likashindikana.Ni hilo ndilo lililomshangaza jaji Elibariki na kumfanya atake kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio lile na kumbaini muuaji halisi wa Edson.Watu waliofanya kila jitihada kuhakikisha kwamba unakutwa na hatia ya mauaji watakuandama usiku na mchana hadi wahakikishe wamekuangusha baada ya kushindwa mahakamani.Kwa upande wangu nimekubaliana kabisa na jaji Elibariki kwamba kuna ulazima wa kufanya uchunguzi wa siri na kumpata muuaji.

Hiyo ndiyo itakuwa salama kwako na kwetu pia” akasema Jason.Penny akasema
“ Jason nakubaliana nawe kwa kila kitu na ninakushukuru lakini kuhusu hili sina hakika kama lina umuhimu mkubwa kwa sasa.Kuhusiana na maisha yangu usihofu kabisa.I’ll be fine.”
“ No Penny you are not fine and you’ll never be fine hadi hapo tutakapomjua muuaji wa Edson.Please Penny let us do this for you.This is for your own safety “ akasema Jason
Penny akainama akafikiri kwa muda na kusema
“Jason ninaogopa kwa sababu ninajitahidi kwa kila niwezavyo kuifuta kumbu kumbu ya Edson kichwani mwangu .Sitaki tena kujihusisha na mambo yoyote yanayohusiana na Edson.He’s gone for good and I have to forget him”
“ Penny nalielewa hilo lakini hautaweza kuifuta kumbu kumbu hiyo kichwani mwako bila ya kumpata muuaji wa Edson.Utakuwa unajiuliza swali hili mara kwa mara na hautakuwa na amani”
“ Jason this isn’t an easy thing.Ni jambo zito na la hatari kubwa.

How are you going to do it?
“ Ni kweli si jambo jepesi hata kidogo na sisi ni wanasheria na hatuna utaalamu wa kufanya uchunguzi wa jambo kubwa kama hii lakini tukiunganisha nguvu zetu sote watatu tunaweza tukafanikiwa”
Penny akanyamaza akafikiri na kusema
“ Sina kipingamizi hata kidogo kuhusiana na suala hili japokuwa sikuwa nataka kujihusisha katika kitu chochote kinachohusiana na Edson lakini wewe ndiye mwanasheria wangu naamini umeona umuhimu wa jambo hili kwa hiyo naahidi kutoa ushirikiano wangu”
“ Ahsante sana kwa kukubali penny.

Kwa kuanzia,Jaji Elibariki anahitaji kukuona ana kwa ana kwa maongezi ”
“ Kuhusu nini?
“ Ni kuhusiana na suala hili .Kuna mambo ambayo anahitaji kuyafahamu kutoka kwako kabla ya kuangalia tufanye nini tena.”
“ Lini anahitaji kuonana nami?
“ Ni jioni ya leo.Tayari nimekwisha andaa chumba ,Moniz 5 star hotel ambako ndiko mtakakokutania.Jaji Elibarii alitaka makutano yenu yawe ya siri kubwa bila ya mtu yeyote kufahamu”
Penny akainama akazama katika mawazo.

Alikumbuka jioni ya ana ahadi ya kuonana na mtu kwa chakula cha jioni
“ Mambo yanaingiliana.Watu wawili wote wanataka kuonana nami usiku wa leo.Nionane na nani? Akajiuliza Penny
“ Lakini ngoja nikaonane na Jaji Elibariki.Bila yeye hivi sasa ningekuwa kifungoni.” Akawaza Penny halafu akamgeukia Jason
“ Ok Jason.Nitakwenda kuonana na Elibariki jioni ya leo”
“ Ahsante kwa kukubali Penny.Nitakupitia saa moja za jioni nikupeleke mkaonane na Jaji Elibariki halafu nitakurejesha nyumbani”
“ Sawa Jason” akajibu Penny halafu wakaagana na Jason akaondoka

*********

Katika moja ya jengo refu kabisa jijini Dar ,watu saba wameizunguka meza ya duara ndani ya ofisi nzuri iliyo katika ghorofa ya kumi na mbili.Mtu mmoja mrefu na mwenye umbo la wastani alikuwa akiongea na wengine wakimsikiliza kwa makini

“ Nimepigiwa simu na ofisi kuu asubuhi ya leo wakinionya kuhusiana na kutorudiwa tena kwa uzembe mkubwa uliopita kiasi cha kumuacha Penny akaingia katika matatizo makubwa na kuhatarisha mpango wetu wa miaka mingi.Endapo Penny angekutwa na hatia mahakamani na kufungwa ,kila kitu kingefikia mwisho.Juhudi zote za miaka zaidi ya ishirini zingekuwa ni kazi bure. Bila Penny kila kitu kitakwama .

Kwa hiyo basi maagizo niliyoyapata toka ofisi kuu ni kwamba tuhakikishe uzembe kama ule haujirudii tena na Penny apewe ulinzi wa kutosha na kumuepusha na mambo yote yanayoweza kumsababishia matatizo na kuhatarisha mpango mzima.Kazi kubwa imekwisha fanyika na tuko katika hatua za mwishoni.

Tunatakiwa kuongeza umakini maradufu.Tunatakiwa tufahamu na tuwepo kila mahala alipo Penny,tufahamu watu anaokutana nao na kwa kuanzia tunatakiwa kumfahamu Jaji Elibariki Chukuswa ambaye anakwenda kuonana na Penny jioni ya leo.”

Akasema Yule jamaa
 
SEASON 1
SEHEMU YA 6
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Nimepigiwa simu na ofisi kuu asubuhi ya leo wakinionya kuhusiana na kutorudiwa tena kwa uzembe mkubwa uliopita kiasi cha kumuacha Penny akaingia katika matatizo makubwa na kuhatarisha mpango wetu wa miaka mingi.Endapo Penny angekutwa na hatia mahakamani na kufungwa ,kila kitu kingefikia mwisho.Juhudi zote za miaka zaidi ya ishirini zingekuwa ni kazi bure. Bila Penny kila kitu kitakwama .Kwa hiyo basi maagizo niliyoyapata toka ofisi kuu ni kwamba tuhakikishe uzembe kama ule haujirudii tena na Penny apewe ulinzi wa kutosha na kumuepusha na mambo yote yanayoweza kumsababishia matatizo na kuhatarisha mpango mzima.

Kazi kubwa imekwisha fanyika na tuko katika hatua za mwishoni.Tunatakiwa kuongeza umakini maradufu.Tunatakiwa tufahamu na tuwepo kila mahala alipo Penny,tufahamu watu anaokutana nao na kwa kuanzia tunatakiwa kumfahamu Jaji Elibariki Chukuswa ambaye anakwenda kuonana na Penny jioni ya leo.” Akasema Yule jamaa

ENDELEA……………………………….

Kwa mara ya kwanza baada ya kukaa gerezani kwa mwaka mzima,Penny alisimama mbele ya kioo kikubwa cha kujitazamia kilichopo chumbani kwake akijitazama namna alivyokuwa amependeza.Alikuwa amevaa gauni refu jekundu maalum kwa kutokea usiku.Alijiangalia na kutabasamu halafu akageuka na nyuma akajiangalia
“ Nothing have changed.I’m still the hot Peniela” akawaza Penny huku akiikoleza rangi ya mdomo.
“ sasa niko tayari kwenda kuonana na Jaji Elibariki” akawaza
Akiwa bado anamalizia kujiremba,kengele ya mlangoni ikalia,akatoka na kwenda kufungua mlango .

Kwa sekunde kadhaa akabaki akitazamana na Jason ambaye hakuamini macho yake
“ Wow ! “ akasema Jason
“ Umependeza mno Penny.Sikuwahi kukuona ukiwa umependeza kama ulivyopendeza leo.Kumbuka Jaji Elibariki ni mtu mwenye ndoa yake kwa hiyo chunga asije akachanganyikiwa na uzuri wako na kubadili mawazo” akasema Jason na wote wakaangua kicheko.

“ Ni muda mrefu sijapendeza Jason ndiyo maana kwa usiku wa leo nimeona nirudie enzi zangu”
Akasema Penny
“ Uko tayari? Akauliza Jason
“ Ndiyo Jason,niko tayari lakini naomba unisubiri dakika mbili kuna kitu nimesahau chumbani.” Akasema Penny na kuelekea chumbani kwake.Wakati akiwa bado chumbani kengele ya mlangoni ikalia .Jason aliyekuwa sebuleni akaenda kuufungua mlango na kukutana na kijana mmoja mrefu mwembaba,aliyevaa suti nzuri nyeusi iliyomkaa vyema.
“ Hallo” akasema Jason
“ Hallo” akajibu Yule jamaa ambaye sura yake ilionyesha mshangao kidogo kwa kumkuta Jason pale ndani
“Karibu ndani” akasema Jason na Yule jamaa akaingia ndani
“ Nimemkuta Penny? Akauliza
“ Ndiyo.

Penny yupo ,anakuja sasa hivi” akasema Jason halafu kikapita kimya kifupi
“ I’m Jason” akasema Jason
“ I’m Kareem” akasema Yule jamaa na kabla maongezi hayajaendelea zaidi Penny akatokea.
“ Kareem!!..akasema Penny kwa furaha
“ Penny..!!” akasema Kareem na kumfuata Penny wakakumbatiana.
“ Welcome back Penny”
“ Ahsante sana Kareem” akajibu Penny
“ Pole sana kwa matatizo.Nilikosa kabisa hata muda wa kuja kukuona.”
“ Usijali Kareem.Ninaelewa ugumu wa kazi zenu.Nashukuru Mungu matatizo yamekwisha”
“ Nashukuru kwa kulitambua hilo.

Vipi uko tayari?
“ Kareem I’m sorry.Leo sintaweza kwenda ,nimepatwa na dharura.Samahani sana kwa usumbufu.Labda siku nyingine” akasema Penny na kumstua Kareem
“ What ?!!!..
“ I’m so sorry Kareemkwa leo sintaweza kwenda”
“ How could you do this Penny? What am I going to tell him? Akauliza Kareem
“ Tell him that I don’t have time today” akasema Penny na kumgeukia Jason
“ Jason can we go?

Jason akainuka na kumfuata wakatoka nje akamfungulia Penny mlango wa gari akaingia halafu wakaondoka na kumuacha Kareem akiwa amesimama mlangoni hajui afanye nni
“ Sorry Peny”
“ Sorry for what?!!..akauliza Peny
“ Nimekuvurugia ratiba zako.Kama ulikuwa na miadi na mtu ungenitaarifu mapema ili tuahirishe kazi yetu”
“ Usijali Jason.Kuna mtu nilikuwa nahitahi kuonana naye jioni ya leo lakini haikuwa na umuhimu mkubwa.
“ Your boyfriend? Akauliza Jason
“ I don’t have a boy friend Jason” akasema Penny na kumfanya Jason atabasamu

Waliwasili Moniz 5 star hotel,wakashuka garini wakapanda lifti hadi ghorofa ya tano wakashuka na kuanza kutembea katika varanda refu huku wakisoma namba za vyumba.Walisimama katika mlango wa chumba namba 204.Jason akabonyeza kengele ya mlangoni na baada ya dakika moja mlango ukafunguliwa na jaji Elibariki akajitokeza.Wakaingia ndani
“ Hallow Penny. habari yako? Akasema jaji Elibariki
“ habari nzuri Jaji Elibariki.Pole na majukumu”
“ Ahsante sana Penny.Vipi unaendeleaje na maisha mapya?
“ Ninaendela vizuri sana jaji.Mwanzo unakuwa mgumu lakini baada ya muda nitazoea na kurudia hali yangu ya kawaida.” Akasema Penny.Jason akapiga simu hotelini na bila kuchelewa muhudumu akafika akiwa na toroli lenye vinywaji akaviweka mezani.

Jason akaomba awaache Jaji Elibariki na Penny yeye kaenda kuendelea na majukumu mengine
“ Penny ni mara ya kwanza mimi na wewe kukutana,lakini utakuwa mi mwanzo wetu pia kufahamiana rasmi” akaanzisha mazungumzo Jaji Elibariki baada ya Jason kuondoka na kuwaacha wao wawili pekee mle chumbani
“ Ni kweli mheshimiwa Jaji,Sikuwa nakufahamu hapo kabla na nilikufahamu tu pale ulipoanza kuisikiliza kesi iliyokuwa inanikabili.Nafurahi sana kukutana nawe ana kwa ana.Nilistuka Jason aliponiambia kwamba unahitaji kuniona,lakini kwa upande mwingine nikafurahi kwa sababu hata mimi nilikuwa na wazo la kukutafuta na kukushukuru kwa kuniachia huru.” Akasema Penny Jaji Elibariki akatabasamu
“ Penny si mimi niliyekuachia huru bali ni Mahakama baada ya kujiridhisha kwamba hukutenda kosa. Na hiyo inatokea si kwako tu bali kwa wote wanaofikishwa mahakamani na kukutwa hawana makosa,mahakama huwaachia huru.” Akasema jaji kikapita kimya cha sekunde kadhaa
“ Penny nadhani Jason amekwisha kueleza kwa ufupi kuhusiana na kilichotufanya tukutane leo hii.” Akasema Elibariki
“ ndiyo,alinieleza kwa ufupi” akajibu Penny
“ Nimeifuatilia kesi hii toka ilipoanza na nikagundua kwamba kuna nguvu kubwa iliyotumika ili kuhakikisha kwamba unapatikana na hatia na hatimaye kufungwa.

Nimejiuliza sana ni kwa nini nguvu kubwa itumike namna hii ikiwa ni pamoja na kuwasilisha kila aina ya ushahidi ambao kama Jaji usipokuwa makini unaweza kabisa kumtia mtu hatiani. Kutokana na mwenendo mzima wa kesi namna ulivyokuwa,nime
shawishika kuamini kwamba kuna kitu kipo nyma ya kesi hii.Kuna kundi la watu ambao walifahamu kabisa kwamba hukutenda lile kosa lakini walisimama imara kuhakikisha kwamba unabambikiwa kesi ile na kukutwa na hatia na hatimaye kuhukumiwa kwa mauaji.Ninachojiuliza,je watu hawa ni akina nani? Kwa nini walitaka ufungwe? Nani alimuua Jason? Akasema jaji Elibariki na kunywa mvinyo kidogo halafu akaendelea
“ Kutokana na maswali hayo ambayo nimekuwa nikijiuliza bila ya kupata majibu,ninalazimika kuamini kwamba pamoja na kukuacha huru lakini bado usalama wako uko mashakani.Watu hawa bado wako nyuma yako na watakuandama usiku na mchana bila kulala hadi wahakikishe kwamba lengo lao limetimia.

Kwa hiyo basi nimekuita hapa kukutaarifu kwamba mimi na wakili wako Jason tumeamua kufanya uchunguzi kisiri siri na kumjua muuaji wa Edson.Ni hiyo tu ndiyo itakuwa salama yako na sisi sote pia.Unaweza ukaona kwamba hali ni shwari lakini naomba nikuhakikishie kwamba hali yetu kiusalama si nzuri hata kidogo.Ninachokiomba toka kwako ni ushirikiano wako ili kwa pamoja tuweze kumtafuta na kumpata muuaji na kumfikisha mbele ya mkono wa sheria.Tukimpata muuaji tutajua sababu ya wewe kubambikiwa kesi ya mauaji.

Tutauweka ukweli wazi ili jina lako lisafishwe katika jamii”
Penny akanywa kinywaji kidogo na kusema
“ Jaji Elibariki,kama nilivyomwambia Jason kwamba nakubaliana na wazo hilo la kufanya uchunguzi wa kumbaini mtu aliyefanya mauaji yale.Niko tayari kutoa ushirikiano wangu wa kila namna ili tuweze kumbaini mtu huyo” akasema penny
“ Nashukuru sana Penny kwa hilo.” Akasema jaji Elibariki na kunywa funda moja la mvinyo
“ Kabla ya kuanza kwa uchunguzi au kuamua nini tufanye,ningependa kwanza kufahamu machache kutoka kwako kuhusiana nanamna tukio lile lilivyotokea na wewe ukajikuta ukitiwa hatiani.Samahani lakini kwa kukukumbusha mambo ambayo unajitahidi kuyasahau.” Akasema jaji Elibariki

Penny akafumba macho na kufikiri kwa muda halafu akasema
“ Ilikuwa ni siku ya Jumamosi,mimi na edson tulipanga tutoke kwa chakula cha jioni.Sikujua anataka kunipeleka sehemu gani kwani alisema angenifanyia surprise.Vile vile alisema kwamba kuna jambo analotaka kunieleza usiku huo” Penny akanyamaza akanywa mvinyo kidogo na kuendelea
“ Alitaka kunipitia nyumbani kwangu lakini nikakataa na kumwambia nitampitia yeye nyumbani kwake na siku hiyo tutatumia gari langu jipya.Saa moja na nusu niliwasili nyumbani kwake na kubonyeza kengele ya getini ambayo iliita kwa dakika kadhaa bila majibu.Nikajaribu kufungua eti na kukuta liko wazi.

Mlango wa kuingilia sebuleni ulikuwa umefungwa kwa funguo nikahisi labda Eddy atakuwa ametoka na kwenda maeneo ya karibu.Nilikuwa na funguo aliyonipa yeye mwenyewe nikafungua na kuingia ndani.Nilikaa sebuleni kwa takribani dakika kumi bila kutokea nikaamua kumpigia simu ambayo iliita bila kupokelewa.Nili
patwa na wasi wasi ikanibidi kupanda ghorofani katika chumba chake cha kulala.Nilipoingia tu ndani nikakutana na picha ambayo sintakuja kuisahau katika maisha yangu.”

Akanyamaza kidogo na kunywa mvinyo halafu akaendelea
“ Nilimkuta Edson akiwa amelala kitandani,huku mwili wake ukiwa umetapakaa damu.Kifuani pake kulikuwa na bastora .Nilipatwa na taharuki nikaenda kuishika bastora ile nikaiweka pembeni na kuanza kumuangalia Eddy kama bado mzima.Nilichanganyikiwa na kutaka kutoka ili nikatafute msaada.Wakati nashuka ngazi nikikimbia kwenda kutafuta msaada nikakutana na watu wanne waliodai kwamba wamesikia mlio wa risasi.Nilishindwa kuongea .Wakanikamata na kudai kwamba nimemuua Eddy.Nilipelekwa polisi na kufunguliwa mashitaka na kilichoendelea baada ya hapo unakifahamu hadi pale uliponiachia huru..”akasema Penny na mara simu yake ikaita..

“ Samahani nilisahau kuizima simu” akasema Penny na kuitoa simu ile akatazama mpigaji na mara sura ikambadilika.Hakuipokea simu ile akaikata na kuizima kabisa.Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Pole sana Penny kwa yote yaliyotokea.Lakini kuna jambo moja nataka kulifahamu.Unahisi ni kitu gani Edson alitaka kukueleza?
Penny akafikiri na kusema
“ Hapana sifahamu alitaka kunieleza nini lakini alisema kwamba ana jambo la muhimu la kuniambia usiku huo”
“ Kwa muda gani ulikuwa naye katika uhusiano?
“ Ni zaidi ya mwaka mmoja.Tulianza kwa siri lakini baada ya yeye kuachana na mpenzi wake Anna,tukaamua kuweka wazi mahusiano yetu”
“Hapo kabla uliwahi kuwa na mpenzi ambaye mliachana?
“Hapana ,sijawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi hapo kabla.Edson alikuwa ni mwanaume wangu wa kwanza”
“ Uliwahi kupokea vitisho vyovyote toka kwa mpenzi wa zamani wa Edson au mtu mwingine yeyote?
“ Maneno na vitisho haviwezi kukosekana.Tulikuwa tunatumiana jumbe mbali mbali za kutishana,kutuk
anana na hata kupigiana simu za vitisho”
“ Unadhani Anna anaweza akawa na mkono wake katika kifo cha Edson?
Penny akafikiri kidogo na kusema
“ Hapana ,sidhani kama anaweza kuwa amehusika na kifo kile “
“ kwa nini?
“Kwa sababu alimpenda sana Edson “
“Hufikiri kwamba Anna aliumizwa sana baada ya kuachwa na Edson na hivyo akaamua kumuua ili kulipiza kisasi?
“ Sidhanikama Anna anaweza akafanya hivyo kwa namna alivyompenda Edson.” Akajibu Penny na kimya kidogo kikapita
“ Kama si Anna ,unahisi nani anaweza akawa ni muuaji?

Akauliza Jaji Elibariki.Penny akainama akafikiri kwa muda na kusema
“ Hapana mheshimiwa sifahamu kabisa nani anaweza kuwa muuaji”
Kimya kifupi kikapita halafu jaji Elibariki akasema
“ Penny kuna jambo lolote ambalo hukuwahi kumueleza mtu yeyote Yule ambalo ungependa kuniambia na linaloweza kutusaidia katika uchunguzi wetu?
Swali lile likamfanya Penny anyamaze kwa muda wa zaidi ya dakika mbili halafu akasema
“ Hapana mheshimiwa,mambo yote nimekwisha yasema.

Hakuna ambalo sijalisema”
Waliendelea kuongea mambo mengi na muda ulipofika Jason akarejea na kumchukua Penny akamrejesha kwake.Akiwa njiani kurejea nyumbani kwake ,Jaji Elibariki akampigia simu
“ Halo jaji” akasema Jason
“ Jason,umemfikisha penny salama?
“ Ndiyo nimemfikisha salama.Niko njiani kuelekea nyumbani “
“ Ok Jason.Nimezungumza mambo mengi na Penny lakini kuna jambo moja nimeligundua toka kwake”
“ jambo gani Jaji?
“ Kuna kitu anakifahamu kuhusiana na kifo cha Edson lakini hayuko tayari kuliweka wazi”
“Are you sure? Akauliza Jason
“ yah ! I’m sure.

Kuna kitu anakifahamu lakini hayuko wazi kukisema.”
“ sasa tutafanya nini?
“ Tutaendela na uchunguzi wetu kimya kmya bila ya kumshirikisha Penny.” Akasema Jaji Elibariki
Jason akafikiri na kusema
“ Ok Jaji.Tutaonana kesho na tutajadili kwa kirefu” akasema Jason na kukata simu

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
SEASON 1
SEHEMU YA 7
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Akiwa njiani kurejea nyumbani kwake ,Jaji Elibariki akampigia simu
“ Halo jaji” akasema Jason
“ Jason,umemfikisha penny salama?
“ Ndiyo nimemfikisha salama.

Niko njiani kuelekea nyumbani “
“ Ok Jason.Nimezungumza mambo mengi na Penny lakini kuna jambo moja nimeligundua toka kwake”
“ jambo gani Jaji?
“ Kuna kitu anakifahamu kuhusiana na kifo cha Edson lakini hayuko tayari kuliweka wazi”
“Are you sure? Akauliza Jason
“ yah ! I’m sure.Kuna kitu anakifahamu lakini hayuko wazi kukisema.”
“ sasa tutafanya nini?

“ Tutaendela na uchunguzi wetu kimya kmya bila ya kumshirikisha Penny.” Akasema Jaji Elibariki
Jason akafikiri na kusema
“ Ok Jaji.Tutaonana kesho na tutajadili kwa kirefu” akasema Jason na kukata simu

ENDELEA……………………….

Baada ya Jason kuondoka,Penny akaenda chumbani kwake akajitupa kitandani.Alionekana kuwa uso wenye tabasamu
“ Ni mara ya kwanza nimetoka out baada ya mwaka mzima.Wow it was wonderfull. Elibariki is real a gentleman. Nimefurahi sana kukaa meza moja naye.Nii mtu ambaye ndiye aliyenifanya niwe huru.Bila yeye kwa sasa ningekuwa gerezani maisha yangu yote au nikisubiri kunyongwa.Sintaweza kumsahahu katika maisha yangu.

Hata hivyo he’s so cute.Ni jaji kijana na mwenye moyo wa huruma” akawaza Penny huku akitabasamu lakini mara akabadilika na kuonekana kuwa na mawazo
“ Jason na Jaji Elibariki wanataka kujiingiza katika jambo la hatari kubwa.Suala la kifo cha Edson si suala rahisi kama wanavyolichukulia.Ni jambo zito na la hatari .Mjadala wake ulikwisha fungwa na hakuna tena uchunguzi wowote utakaofanyika tena.Natamani kuwaambia wasiendelee na kitu wanachotaka kukifanya lakini nashindwa.Ninachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kwamba hawafanikiwi katika usala hili na hivyo kukata tamaa na kuacha kabisa kuchimba undani wa kifo cha Edson.Hii itakuwa ni kwa ajili ya usalama wao wenyewe” Akawaza Penny na kustuliwa na mlio wa simu.

Akatazama mpigaji akakutana na namba ambazo hazikuwa na jina mara moja akawa amemtambua mpigaji. Akavuta pumzi ndefu halafu akabonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow “ akasema kwa sauti ya uchovu.Sekunde kadhaa zikapita halafu sauti ya upande wa pili ikasema

“ Hallow Penny.How are you?
“ I’m fine.How are you? Akajibu Penny
Kimya kifupi ikapita tena na mtu Yule akauliza
“ Penny kwa nini umenifanyia dharau kubwa kama leo? Lini utaufungua moyo wako kwangu? Lini utakuwa tayari kukaa na kunisikiliza? Ikauliza sauti ile nzito iliyoongea kwa upole.Penny akashindwa kujibu
“ Kwa nini umeshindwa kuja kuonana nami kama tulivyokuwa tumepanga? Akauliza mtu Yule.Penny akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Mr President can we stop this?

“ Stop what ?
“ Mr President we can go on like this.Its time to end things now” akasema Penny
“ Penny ni hapo tu unaponiudhi “
“ Dr Joshu …” akataka kusema kitu Penny lakini Dr Joshua akamzuia
“ Don’t say anything Penny.You know exactly how much I love you and I’ll never stop loving you” akasema Dr Joshua kwa sauti yenye ukali kidogo.
“ Acha kunidanganya Dr Joshua !! “ Penny naye akasema kwa sauti yenye ukali kidogo ndani yake

“ Sikudanganyi Penny na sijawahi kukudanganya kwamba ninakupenda kwa moyo wangu wote.”
“ Liar !!..” akasema Penny
“ Kama unayoyasema yana ukweli usingekubali kuona nikitaka kuangamia.Unsingethubutu kuniona nikiozea gerezani na kunusurika kufungwa maisha wakati ukijua kabisa kwamba sikutenda lile kosa.Sikumuua Edson .Pamoja na kufahamu hilo lakini bado hukufanya lolote kunisaidia na badala yake ukakubali nibambikiwe kesi ile ili nikafungwe.You don’t love me at all” akasema Penny kwa hasira
“ Penny I love you.

real do.Najua hutaamini lakini fahamu kwamba niliumia kukuona ukiwa gerezani lakini nilishindwa namna ya kukusaidia kwa sababu kwa wakati ule bado ulikuwa umenikasirisha mno na nilitamani hata ufungwe gerezani ili nisikuone tena katika maisha yangu yote.Kitendo cha kuanzisha mahusiano na Yule kijana Edson kiliniumiza sana na ndiyo maana yakatokea yale yaliyotokea lengo likiwa ni kukufunza adabu kidogo ili uwe na heshima kwa watu wazima na wenye nguvu.” Akasema Dr Joshua .Penny akafuta machozi.Dr Joshua akaendelea

“ Penny naomba nikuweke wazi kwamba moyo wangu uliumia mno na kuvunjika pale ulipoingia katika mahusiano na yule kijana Edson na ukanisaliti na kwa sababu yako akamuacha hadi mwanangu Anna.Pamoja na yote yaliyotokea bado ninashindwa kukutoa moyoni mwangu.Bado nakuhitaji Penny katika maisha yangu.Ni wewe tu ambaye unaweza kunipa furaha ninayoihitaji.Tafadhali Penny naomba tuyasahau yote yaliyopita na tuufungue ukurasa mpya.”

Penny akafikiri kidogo na kusema
“ so you killed him !..” akasema Penny huku machozi yakimdondoka mashavuni
“.Yes I did.You are mine Penny,and mine alone.yeyote ambaye atataka kuchukua nafasi yangu kwako sintasita kumfanya kama nilivyomfanya Edson na ukumbuke kwamba siku ukifungua mdomo wako ndiyo utakuwa mwisho wako kwa hiyo basi …….” Dr Joshua akakatishwa na Penny ambaye machozi yalikuwa yanamtoka

“ You are a devil..!!” akasema Penny kwa ukali
“ Penny naomba unielewe kwamba nina kupenda na nitafanya kila linalowezekana ili mimi na wewe tuwe pamoja.My wife is sick and will die soon.Hawezi kunipatia kile ninachohitaji na ninachokipata toka kwako.She’ll die soon and you’ll be the first lady so please open your heart for me….” Akasema Dr Joshua

“ Dr Joshua,naomba hii iwe ni mara ya mwisho kunipigia simu.Wewe ni rais wa nchi na una mke wako wa ndoa kwa hiyo naomba uachane kabisa na mimi.Tafadhali angalia masuala makubwa ya nchi na mke wako mgonjwa.She needs you” akasema Penny
“ Penny kwa nini hutaki kunielewa? Nimekwisha kwambia kwamba hakuna kitu zaidi ya kifo kitakachoweza kunitenganisha na wewe.Nimekuchagua wewe tu na nitafanya kila niwezalo na nitatumia nguvu zote nilizonazo mpaka niwe nawe tena.Najua unanichukia sana kwa sasa lakini tutayamiliza mambo haya na tutakuwa wamoja tena. No woman will say no to me” akasema Dr Joshua.

Penny akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Let us have a deal Dr Joshua”
“ A deal !!..
“Yes a deal. I’ll keep my mouth shut.I’ll never tell anybody that its you who killed Edson and I’ll die with my secret if you’ll let me go”
“ hahaha Penny unanifurahisha sana.I’ll never let you go and you’ll keep your mouth shut because I did that for us,me and you.So we don’t have a deal.I know down deep in your heart that you do love me.”
“ I don’t love you Joshua and I’ll never love you”
“ Who do you love? Wakili wako Jason?

Au jaji Elibariki? Penny akastuka baada ya kutajiwa jina la Elibariki
“ So you are following me ?!! akauliza Penny
“ Penny ninafahamu kila hatua unayoipiga.Ninafahamu jioni hii umekataa mwaliko wangu na ukaenda kuonana na Jaji Elibariki.Be careful.Jaji Elibariki amemuoa mwanangu lakini sintosita kumuadhibu pale atakapoamua kuvuka mipaka na kumsaliti mwanangu kama Edson alivyomsaliti mwanangu Anna.”
Penny akahisi kuishiwa nguvu akashindwa aseme nini.
“ Penny nitakuwa na safari ya kwenda Arusha wiki ijayo kwa hiyo jiandae nawe utakwenda Arusha.Kareem atashughulikia kila kitu kuhusu safari hiyo.Kwa heri Penny” akasema Dr Joshua na kukata simu.Penny alihisi jasho likimchuruzika .

“ I’m back to a living hell.!..Nayachukia sana maisha haya lakini sina namna tena tayari nimenaswa.Endap
o nitaenda kinyume na huyu mzee kuna uwezekano yakanifika makubwa .Nimeponea chupu chupu kesi ya mauaji na safari hii lazima niwe makini sana kwa kila ninachokifanya.” akawaza Penny huku kijasho kikimchuruzika na mara simu yake ikaita,akatazama mpigani na kubonyeza kitufe cha kupokelea

“ Hallow” akasema
“ Penny don’t say No to Mr president.Fanya kila atakachokuamuru ufanye.We’re so close” ikasema sauti ile na kukata simu.Penny akahisi kuchanganyikiwa.

TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO
 
SEASON 1
SEHEMU YA 8
ILIPOISHIA SEHEMU ILIPOISHIA
“ Penny nitakuwa na safari ya kwenda Arusha wiki ijayo kwa hiyo jiandae nawe utakwenda Arusha.Kareem atashughulikia kila kitu kuhusu safari hiyo.Kwa heri Penny” akasema Dr Joshua na kukata simu.Penny alihisi jasho likimchuruzika .

“ I’m back to a living hell.!..Nayachukia sana maisha haya lakini sina namna tena tayari nimenaswa.Endap
o nitaenda kinyume na huyu mzee kuna uwezekano yakanifika makubwa .Nimeponea chupu chupu kesi ya mauaji na safari hii lazima niwe makini sana kwa kila ninachokifanya.” akawaza Penny huku kijasho kikimchuruzika na mara simu yake ikaita,akatazama mpigani na kubonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow” akasema
“ Penny don’t say No to Mr president.Fanya kila atakachokuamuru ufanye.We’re so close” ikasema sauti ile na kukata simu.Penny akahisi kuchanganyikiwa.

ENDELEA………………………

Penny alikaa kitandani akazama katika tafakari nzito.Simu mbili toka kwa watu wawili tofauti alioongea nao muda mfupi uliopita zilimchanganya sana.
“Sijui nini itakuwa hatima ya maisha yangu.Sijui nitaendelea na maisha haya hadi lini? Nimechoka sasa na maisha haya na ninahitaji kuwa huru na mimi niishi maisha ya kawaida.Nimepewa amri ya kuendeleza mahusiano na Dr Joshua japokuwa moyo wangu hautaki kabisa.Kamuua Edson kijana ambaye nilimpenda kwa moyo wangu wote.

I was deeply in love with him.Kama haitoshi nikaangushiwa kesi ile kubwa ya mauaji ambayo nusura inipeleke maisha gerezani.Yote hii ni kwa sababu ya wivu wa Dr Joshua.He’s a powerfull man and he can do anything.Sikuwa nataka kuwa na mahusiano naye ya namna yoyote ile baada ya kuachiwa huru lakini najikuta nikilazimishwa kukubali kuendeleza mahusiano naye ili kuikamilisha kazi .

I hate that bastard.” Akawaza Penny huku akijifuta jasho
“ Lakini kwa sasa ngoja niwe mpole na niendelee kumkubalia kwa kila anachotaka lakini iko siku moja atalia na kuomboleza. Kitendo alichokifanya cha kumuua Edson kimeniumiza mno na iko siku atalipia uovu huu.Ninachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kuhakikisha kwamba Jason na Jaji Elibariki wanaachana na kutafuta muuaji wa Edson.

Wanajiweka katika hatari kubwa sana bila wao wenyewe kujua.Hawa ni watu wangu wa muhimu sana na sintokubali kuona kwa namna yoyote ile mmoja wao yakimpata kama yaliyompata Edson.” Akawaza Penny na kuinuka akaelekea bafuni kuoga kwani jasho jingi lilikuwa linamtiririka
“ kuna nyakati huwa siamini kama ni kweli nimeweza kufanikiwa kumchanganya mkuu wa nchi,mtu anayeheshimika ndani na nje ya nchi, kwa kumpa penzi la kiwango cha juu .Mzee Yule amechanganyikiwa kiasi cha kumuombea mke wake anayesumbuliwa na saratani afariki mapema ili aweze kuwa na uhuru na mimi anioe na anifanye first lady.Hahaha laiti angejua angeyafuta kabisa mawazo yake.Ngoja nivumilie na kujifanya mjinga na kumsikiliza kila atakachokisema kwa sababu kimebaki kipindi kifupi sana kukamilisha kazi yangu” akawaza Penny akiendelea kuoga.

********
Saa mbili za asubuhi Jaji Elibariki aliondoka nyumbani kwake na kuelekea ofisini .Si kawaida yake kuondoka mapema hivi lakini kutokana na kutokuwa na maelewano mazuri na mke wake Flaviana ilimlazimu kuwahi kuondoka.
“ Siku ya pili sasa mimi na Flaviana hatuongei.Nimechoshwa na maisha haya ya mikwaruzano kila siku.Flaviana ni mwanamke ambaye anataka kuwa na sauti ndani ya nyumba na maamuzi yake yawe ndiyo ya mwisho.Yote hii ni kwa sababu yeye ni mtoto wa rais.

Siko tayari kuendelea kuvumilia dharau zake.Siko tayari kuendelea kuishi maisha yasiyokuwa na furaha hata kidogo eti kwa sababu ya kiapo cha ndoa. “Akawaza jaji Elibariki na mara sura ya Penny ikamjia
“ Sura ya Penny toka niliponana naye jana hainitoki kichwani.Ninamuwaza kila dakika.Yawezekana ni kutokana na uzuri wake.Ni mtoto mzuri mno.Ameumbwa akaumbika.

Ana uzuri wa kipekee mno ambao sijui nimfananishe na nani.Jana nilipomuona namna alivyokuwa amependeza niliogopa na kudhani labda ni malaika.Hakuwa Penny Yule ambaye nilizoea kumuona mahakamani ” akawaza Jaji Elibariki wakati akikata kona kuingia Lavenda Restaurant kupata kifungua kinywa kwani aliondoka nyumbani bila kupata mlo wa asubuhi.

“ Katika maongezi yangu na penny jana usiku sijaweza kugundua chochote cha kuweza kunipa mwanga kuhusu wapi nitaanzia uchunguzi wangu.Nilivyomsoma penny ni kama vile hataki tena kujihusisha na masuala yoyote yanayohusiana na kifo cha Edson.Nadhani anajitahidi kujisahaulisha yaliyopita lakini pamoja na hayo kuna kitu nimekiona katika macho yake ambacho kinanifanya niamni kwamba kuna kitu anakifahamu lakini hayuko wazi kukisema. Siwezi kumlazimisha kusema kila kitu anachokifahamu .Kama kuna kitu hataki kuniambia basi nitakifahamu kwa njia nyingine.Ninaapa nitalichimba suala hili hadi mzizi wa mwisho.Nataka nimdhihirishie rais na familia yake kwamba ninapofanya maamuzi huwa sikurupuki tu.

Lazima nimpate muuaji ” akawaza jaji Elibariki halafu akampigia simu Jason na kumfahamisha kwamba wakutane mahala walikokutana jana asubuhi
Kisha maliza kupata kifungua kinywa,akaondoka na kuelekea moja kwa moja katika sehemu waliyopanga wakutane na Jason.
Dakika kumi na mbili toka awasili mahala walikopanga kukutana,Jason akawasili.Wakasalimiana na bila kupoteza wakati wakaanza kujadili kile kilichowakutanisha pale

“ Vipi kuhusu jana,mambo yalikwendaje? Akauliza Jason.
“ Jana mambo yalikwenda vizuri ingawa si vizuri sana lakini si mbaya kwa kuanzia.Niliongea mambo mengi na Peniela na alikubali kushiriiana nasi ili kumbaini nani muuaji wa Edson.Alinieleza kwa ufupi tu namna mahusiano yake na Edson yalivyokuwa na hadi siku mauaji yalipotokea.Hakuna kitu kipya katika maelezo yake.Maneno aliyoniambia jana ndiyo yale yale ambayo aliyasema mahakamani.Lakini hata hivyo kuna kitu nilikigundua baada ya kuongea naye.Kuna kitu anakifahamu lakini hayuko tayari kukisema.Hiyo nayo inazidi kunipa mshawasha wa kutaka kufahamu kwa undani zaidi kuhusiana na jambo hili.” Akasema Jaji Elibariki.Jason akafikiri kidogo na kusema

“ Penny ni rafiki yangu na nimekuwa nikiisimamia kesi yake kwa muda wa mwaka mzima na ninakubaliana nawe kwamba Penny ni msiri sana.Ana ambo mengi ambayo hajawahi kuyaweka wazi na huwa hataki kabisa kuyaongelea.Kwanza ni kuhusiana na familia yake.Kwa muda wa mwaka mzima sijawahi kuiona familia yake au ndugu yake yeyote Yule .Najiuliza mara kwa mara ndugu zake wako wapi? Sijapata nafasi ya kumuuliza kuhusu suala hilo na wala hajawahi kunieleza chochote.Nakubaliana nawe kabisa kwamba kuna mambo ambayo penny anayafahamu lakini hayuko tayari kuyaweka wazi.”

“ Kama ni hivyo basi” akasema jaji Elibariki
“ itatubidi tufanye mambo mawili.Kwanza inatubidi tumfahamu huyu Edson alikuwa mtu wa namna gani.Tuyafahamu maisha yake alikuwa akiishi vipi,marafiki aliokuwa akiambatana nao,tutachunguza pia nyumbani kwake na mwisho tutafuatilia mawasiliano yake na watu mbali mbali ambao alikuwa akiwasiliana nao na hasa wale aliowasiliana nao siku tatu kabla ya kifo chake vile vile tutaipitia tena taarifa ya uchunguzi toka jeshi la polisi .Tunatakiwa tufahamu kila kitu kuhusiana na Edson.” Akasema Jaji Elibariki akanyamaza kidogo halafu akaendelea.

“ Jambo la pili ambalo tunatakiwa tulifanye ni kumchunguza Penny” akanyamaza na kumtazama Jason
“ Lazima tumfahamu Penny lakini ni baada ya kumfahamu Edson” akasema Jaji Elibariki.
Waliendelea na majadiliano na baadae wakaondoka kila mmoja akaelekea ofisini kwake .

Baada ya kuachana na Jaji Elibariki,Jason aliamua kuelekea nyumbani kwa Peniela.Hakuwa ameongea naye toka asubuhi hivyo akaamua kwenda kuonana naye kabla hajaendelea na mambo mengine .
“ Ninakubaliana na Jaji Elibariki kwamba Penny ni mwanamke msiri sana.Ninaamini hakumuua Edson lakini nina imani kuna mambo ambayo anayafahamu kuhusiana na kifo cha Edson lakini hayuko tayari kuyaweka wazi.Anyway tutachunguza na tutapata jibu” akawaza Jason akiwa njiani kuelekea kwa Penny

Ilimchukua dakika thelathini kuwasili katika makazi ya Penny.Katika geti la kuingilia ndani kulikuwa na makufuli makubwa manne kuashiria kwamba hakukuwa na mtu ndani.Jason akatoa simu yake na kumpigia lakini hata simu yake haikuwa ikipatikana.Jason akaingiwa na wasi wasi mkubwa.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
SEASON 1
SEHEMU YA 9
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Baada ya kuachana na Jaji Elibariki,Jason aliamua kuelekea nyumbani kwa Peniela.Hakuwa ameongea naye toka asubuhi hivyo akaamua kwenda kuonana naye .

“ Ninakubaliana na Jaji Elibariki kwamba Penny ni mwanamke msiri sana.Ninaamini hakumuua Edson lakini nina imani kuna mambo ambayo anayafahamu kuhusiana na kifo cha Edson lakini hatyuko tayatri kuyaweka wazi.Anyway tutachunguza na tutapata jibu” akawaza Jason akiwa njiani kueleka kwa Penny Ilimchukua dakika thelathini kuwasili katika makazi ya Penny.Katika geti la kuingilia ndani kulikuwa na makufuli makubwa manne kuashiria kwamba hakukuwa na mtu ndani.Jason akatoa simu yake na kumpigia lakini hata simu yake haikuwa ikipatikana.Jason akaingiwa na wasi wasi mkubwa

ENDELEA………………………………

Dakika zilizidi kuyoyoma na Jason bado aliendelea kusimama nje ya nyumba ya Penny ,asijue la kufanya.Alikuwa na wasi wasi mwingi pengine Penny amepatwa na matatizo lakini kilichompa moyo ni yale makufuli yaliyokuwa getini ambayo yaliashiria kwamba hakukuwa na mtu yeyote ndani
“ Penny kaenda wapi? Na kwa nini amezima simu yake? Akajiuliza
“ Nina wasi wasi asijekuwa amepatwa na matatizo kwani hali ya usalama wake bado si nzuri hata kidogo.Kuna haja ya kuimarisha ulinzi hapa nyumbani kwake hadi hapo hali ya usalama itakapokuwa shwari.Nitaongea naye na kama atakuwa tayari nitamkodishia walinzi toka katika kampuni binafsi ya ulinzi ili wailinde nyumba yake na kila sshemu aendako.” Akawaza Jason akiwa nje ya gari lake

“ Lakini kwa nini niwe na wasi wasi kuhusu maisha ya Penny kiasi hiki? Na kwa nini niko hapa mida hii? Sikuwa na ratiba ya kufika hapa siku ya leo lakini tazama mahala nilipo sasa hivi,nipo nje ya geti la Penny.What am I doing here? Akajiuliza Jason
“Kuna kitu kimoja tu kilichonileta hapa.Kumuona Penny.Lakini kumuona Penny kwa makusudi yapi? Hapo ndipo ninapokosa jibu.Sina sababu yoyote ya msingi iliyonileta hapa.Mahusiano yangu na Penny ni katika masuala ya kisheria tu nasi vinginevyo kwa hiyo sipaswi kuwa na hofu yoyote kuhusu yeye wala kuyafuatilia maisha yake wala kuja hapa kwake mara kwa mara na kwa muda ninaotaka.Kazi yangu ilikuwa kumsimamia kesi na baada ya kesi kuisha natakiwa nimuache aendelee na maisha yake kama kawaida.Siku akiwa na tatizo atanitafuta” akawaza Jason halafu akaingia garini na kuondoka

“ Lakini moyo wangu unakataa kabisa kukaa mbali na Penny.Nimekuwa naye katika kipindi chote alichopata matatizo makubwa na tayari tumejenga ukaribu mkubwa kati yetu kwa hiyo si rahisi kuachana naye” akawaza Jason huku akiongeza mwendo wa gari na kulipita gari la mbele yake
“ Kuna kitu kimoja ambacho nimekuwa nakihisi kwa muda mrefu sasa lakini nimekuwa nikikwepa kuwa wazi.I’m falling in love with Penny.Kwa muda wmrefu nimekuwa na hisia hizi lakini nimekuwa nikijizuia ili kumaliza kwanza masuala ya kesi iliyokuwa ikimkabili.Kwa sasa baada ya kesi kumalizka na Penny yuko huru,sina sababu ya kuendelea kuzificha hisia zangu kwake.Siwezi tena kuendelea kujizuia.” Akawaza Jason na mara sura ya penny ikamjia kichwani akatabasamu

“ Penny ni msichanamwenye uzuri wa kipekee kabisa ambaye sioni wa kumfananisha naye.Mimi na yeye tunaendana karibu katika kila kitu na ana kila sifa ninayoihitaji kwa mwanamke wa maisha yangu.Lakini kuna kitu kimoja ambacho kimekuwa kinanila akili yangu toka jana.Nikiwa pale kwake jana alikuja Yule kijana nadhifu kuja kumchukua ili kumpeleka mahala. Ni wazi alikuwa na miadi na mtu Fulani tena inaonekana ni mtu mwenye uwezo mkubwa kifedha.Je mtu huyo ni nani na wana mahusiano gani? Akajiuliza Jason na kuvuta pumzi ndefu

“ Nitamfuatilia mtu huyo hadi nimfahamu ni nani na ana mahusiano gani na penny.Nasikia wivu mkubwa kila nikiwaza kwamba yawezekana pengine mtu huyo na penny wakawa na mahusiano ya kimapenzi.Natak
a penny nimmiliki mimi peke yangu” akawaza Jason.Moja kwa moja alielekea ofisini kwake na kitu cha kwanza baada ya kuingia ofisini alitoa simu yake na kujaribu kupiga namba za simu ya Penny lakini hazikuwa zikipatikana “ Penny yulo wapi leo?Amepatwa na nini?Nitaendelea kumtafuta hadi nimpate.Sintolala usingizi leo hadi nitakapoongea naye simuni na kujua kama yuko salama.” Akawaza Jason na kuendelea na kazi zake.

**********

Ni saa tano za asubuhi,jiji la Arusha likiwa na ubaridi uliotokana na mvua za manyunyu zilizoendelea kunyesha,lakini sughuli za kujitafutia kipato ziliendelea kama kawaida.Katika hoteli ya kifahari ya Kobe Village ,Peniela msichana mwenye uzuri wa kipekee alikuwa ghorofani akilitazama jiji hili lililobarikiwa uzuri wa kipekee kabisa,likionekana kwa uzuri kutokea hotelini pale
“ geneva of Africa” akawaza Penny huku akitabasamu.
“ Nimerejea tena katika maisha yangu niliyoyazoea.Haya ndiyo maisha niliyokuwa nikiishi na ninayotaka kuendelea kuishi.To live like a queen.Nina hakika baada ya kumaliza shughuli yangu nitaishi maisha kama haya au hata zaidi ya haya.” Akawaza na mara dada mmoja mwenye kuvalia nadhifu kabisa akamfuata na kumsalimia
“ Madam,wewe ndiye Penny?

Akauliza Yule dada mwenye sauti ya upole baada ya kusalimiana
“ Ndiye mimi” akajibu penny
“ Ok.Naitwa Zulfa,ninafanya kazi katika dula la mavazi na urembo hapa jijini Arusha liitwalo Samia Fashion.”
“ Ouh Samia Fashion,ninawafahamu sana hawa.Wana maduka yao makubwa hata jijini Dare s salaama na Nairobi.Ulikuwa unasemaje Zulfa?”
“Nimeelekezwa na bosi wangu nije nikuchukue nikupeleke dukani kwetu kwa ajili ya kufanya manunuzi ya nguo na vitu vingine.Amesema uchukue chochote kile unachohitaji” akasema Zulfa.

Huku akitabasamu Penny akaingia chumbani kwake akajiweka tayari halafu wakaondoka
“ Hii ni kazi ya kareem kwani alinikataza kubeba mzigo wowote na kuniahidi kwamba nitanunua kila kitu huku Arusha” akawaza Penny akiwa garini kuelekea Samia fashion Hakuna aliyekuwa akifahamu kwamba penny yuko jijini Arusha.Kareem mlinzi wa rais ambaye anamuamini mno na ambaye huwa anamtuma katika mambo yake mengi ya siri,ndiye aliyemsafirisha Penny toka Dar hadi Arusha baada ya kupewa maelekezo na rais. Saa tisa za usiku alimpigia simu penny na kumtaka ajiandae kwa safari ya kuelekea Arusha.Hakuwa na kipingamizi kwani alikwishapewa maelekezo ya kukubali chochote atakachoambiwa na rais.

Saa kumi na moja juu ya alama lilifika gari na kumchukua kumpeleka uwanja wa ndege akapanda ndege maalum ya kukodi kuelekea Arusha ambako alikwisha andaliwa chumba katika hoteli ya kifahari ya Kobe village. Katika duka la Samia FashionPenny alifanya manunuzi makubwa na kurejea hotelini kwake

“ Dr Joshua safari hii amepania hasa kuusuuza moyo wangu na ndiyo maana ananifanyia mambo haya makubwa kiasi najihisi kama malkia.Atapata anachokitaka lakini na mimi nitakipata ninachokitaka na baada ya hapo mimi na yeye mkataba utavunjwa na nitaishi maisha ya hali ya juu kuzidi haya.” Akawaza Peny akiendelea kujaribisha mavazi aliyonunua.
“ safari hi sintofanya tena kosa nikipata tu nafasi namaliza kila kitu.Ninachotakiwa kufanya kwa sasa ni kumpa Dr Joshua penzi la kiwango cha juu ambalo hajawahoi kupewa na mwanamke yeyote chini ya jua .Ninafahamu udhaifu wake ulipo na hapo ndipo nitatumia kumshikia na kumfanya asifurukute na baadaya hapo yeye mwenyewe ataniachia njia na nitafanya ninachokitaka” akawaza.

***********

Jaji Elibariki akiwa ofisini kwake akapigiwa simu na katibu muhtasi wake na kumfahamisha kwamba kuna mgeni wake ambaye ni Anna mtoto wa rais.jaji Elibariki akatoa ruhusa aruhusiwe kuingia ofisini i.
“Shikamoo shemeji” akasema Anna ambaye uso wake ulionyesha dhahiri kwamba alikuwa na hasira
“ marahaba Anna.Hujambo? “ Sijambo “ akajibu kwa ufupi na kuvuta kiti akaketi “ Nimekuja kusikiliza ulichoniitia” akasema Anna kwa sauti ya juu kidogo
“ Anna nashukuru kwa kufika kwako.Nilikuwa na hofu pengine hutafika” akasema Jaji Elibariki “ Go straight to the point ,sina muda mwingi wa kukaa hapa” akasema anna kwa sauti iliyoonyesha dharau kidogo
“ Anna nimekuita hapa ili tuongelee kuhusiana na jambo liilotokea siku mbili zilizopita kuhusiana na kesi iliyomalizika iliyomuhusisha Penny.” Mara tu alipotamka jina la Penny ,Anna akabadilika usoni
“ Please !..

I don’t want to hear anything about penny” akasema anna kwa ukali.
“ Tafadhali naomba tuliza jazba Anna ili tuongee kwa undani kuhusu suala hili”
“Tuongee kuhusu nini tena ?Tayari umekwisha toa hukumu na muuaji umemuachia huru sasa unataka tuongee nini zaidi?
“ tafadhali naomba unisikilize Anna kile nilichokita hapa ” akasema Jaji Elibariki

“ Nitakusikiliza kama una lingine la kuniambia lakini si suala la hukumu uliyotoa ukamuachia muuaji.Hujui ni namna gani nilivyompenda Edson.Kitendo cha kumuachia huru muuaji aliyemuua mtu niliyempenda wakati kuna kila aina ya ushahidi kuthibitisha kwamba penny alimuua Edson kimenifanya nikutoe thamani kabisa na sina hakika kama unafaa kuwa mmoja wa wanafamilia yetu.Tulikutegemea utende haki lakini umepindisha haki ukampendelea Yule kahaba…..”

Akasema Anna na kumpandisha hasira Jaji Elibariki ambaye alisimama na kumnyooshea Anna kidole kwa hasira
“ Anna naomba iwe ni mara yako ya kwanza na ya mwisho kunionyeshea dharau namna hii.Nimekuita hapa kwa lengo zuri tu ili tuongee na tusaidiane kumpata muuaji wa Edson lakini wewe hutaki kunisikiliza na badala yake unanifanyia dharau.Nimechoka kuwavumilia wewe na familia yenu yote kwa dharau mnazonifanyia.Mimi ni jaji wa mahakama kuu na sifanyi maamuzi kwa shinikizo la mtu yeyote awe ni rais au nani.Ninatenda haki kwa kila mtu.Naomba vile vile iwe ni mwanzo na mwisho kumuita Penny kahaba.Mara nyingine ukithubutu kuja na kutoa matusi katika ofisi hii nitasahau kama baba yako ni rais wa nchi na nitakuharibu sura yako.Toka haraka ofisini kwangu !! ” akasema kwa hasira jaji Elibariki.

Aliku wa amekasirishwa mno na maneno aliyoyatamka Anna
“ Sawa ninaondoka lakini ukae ukijua kwamba huna muda mrefu katika kiti hicho ambacho umepewa tu kwa hisani ya baba yangu” akasema Anna huku akiondoka.Maneno yale yakazidi kumkasirisha sana jaji Elibariki.Alitamani amrukie na kumuadhibu vikali lakini akajitahdii kujizuia na kumuacha aondoke.

“ Dah ! Sijawahi kukutana nafamilia yenye dharau kama hii.Nilimuita kwa nia njema tu ya kuja kuongea masuala ya msingi ili tushirikiane kumbaini muuaji wa Robin lakini nimeambulia matusi na dharau.Sijawahi kudharauliwa kiasi hiki katika kazi yangu na sintokubali kamwe kuendelea kudharauliwa hasa na familia hii.” Akawaza jaji Elibariki huku amefura kwa hasira.Akachukua simu yake na kuzitafuta namba fulani akapiga “ Hallo Mathew” akasema Jaji Elibariki

“ hallo jaji.habari za siku? Leo umenikumbuka ndugu yangu lazima utakuwa na tatizo.”
“ Ni kweli nina shida ndugu yangu nahitaji kukuona” akasema Elibariki
“ Unataka tuonane saa ngapi?
“ sasa hivi.Uko wapi?
“ Niko nyumbani kwangu”
“ Ok njoo utanikuta lakini tafadhali naomba uje peke yako.Sitaki uwe umeambatana na mlinzi yeyote”
‘ Nitakuja mimi mwenyewe.dereva wangu ana matatizo ya kifamilia na nimempa likizo ya muda” akasema Elibariki
“ Good” akajibu Mathew na kukata simu.jaji Elibariki akainuka akavaa koti lake na kutoka “ It’s time for action now” akasema jaji Elibariki huku akiingia garini.
“Mbivu na mbichi lazimazijulikane katika kipindi kifupi” akasema kwa sauti ndogo

TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………
 
SEASON 1
SEHEMU YA 10
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Hallo Mathew” akasema Jaji Elibariki
“ hallo jaji.habari za siku? Leo umenikumbuka ndugu yangu lazima utakuwa na tatizo.”
“ Ni kweli nina shida ndugu yangu nahitaji kukuona” akasema Elibariki
“ Unataka tuonane saa ngapi?
“ sasa hivi.Uko wapi?
“ Niko nyumbani kwangu”
“ Ok njoo utanikuta lakini tafadhali naomba uje peke yako.Sitaki uwe umeambatana na mlinzi yeyote”

‘ Nitakuja mimi mwenyewe.dereva wangu ana matatizo ya kifamilia na nimempa likizo ya muda” akasema Elibariki
“ Good” akajibu Mathew na kukata simu.jaji Elibariki akainuka akavaa koti lake na kutoka
“ It’s time for action now” akasema jaji Elibariki huku akiingia garini.
“Mbivu na mbichi lazimazijulikane katika kipindi kifupi” akasema kwa sauti ndogo

ENDELEA…………………………………..

Jaji Elibariki waliwasili katika jumba moja kubwa lililozungushiwa ukuta mkubwa.Alipiga honi mara tatu na toka katika mlango mdogo wa geti akatokeza mlinzi akiwa na mbwa mkubwa akamfuata Elibariki katika gari
“ habari yako mkuu” Akasema Yule mlinzi aliyevalia sare za ulinzi za kampuni binafsi ya ulinzi
“ Habari nzuri.Nina miadi na ndugu Mathew” akasema jaji Elibariki
“ Wewe ndiye Elibariki? Akauliza Mlinzi
“Ndiye mimi”
“ Ok.taarifa zako ninazo” akasema Yule mlinzi huku akiingia ndani na kufungua geti.Jaji elibariki akaingia .

Mbwa watatu wakubwa wakalizingira gari lile na kuanza kubweka kwa nguvu.jaji Elibariki akaogopa kushuka ndani ya gari kwa namna mbwa wale walivyokuwa wakubwa.Mlinzi akafika mara moja na kuwatuliza akawapeleka katika nyumba yao.Elibariki akashuka na kuongozwa na mlinzi hadi ndani.Akakaribishwa sebuleni.Ilikuwa ni sebule kubwa yenye vitu vingi vya thamani.Baada ya dakika kama nne hivi Mathew akatokea.Ni mtu mmoja mfupi mwenye mwiliwa wastani.

“ Mheshimiwa jaji.habari za siku ndugu yangu?
“ habari nzuri Mathew.Maisha yanakwendaje?
“ maisha yanakwenda vizuri.Mungu ananiwezesha.Vipi wewe mambo yako yanakwendaje?
“ Mambo yangu yanakwenda vizuri lakinisi vizuri sana.”
‘Nini tatizo Elibariki? Mpaka uje kwangu lazima ni tatizo kubwa.Niambie nini tatizo? Niko tayari kukusaidia.Wewe ni rafiki yangu mkubwa.Hukuniacha wakati nina matatizo .” akasema Mathew huku akiwasha sigara yake na kuvuta
“ Mathew,kuna kijana mmoja anaitwa Edson alikuwa akifanya kazi katika idara ya mawasiliano ikulu,aliuawa kwa kupigwa risasi nyumbani kwake.Baada ya mauaji hayo mpenzi wake alituhumiwa kwamba ndiye muuaji na kufunguliwa mashtaka.

Kesi imeendeshwa kwa muda wa mwaka mzima na wiki hii nimetoa hukumu na kumuachia huru Yule msichana.Hakuwa na kosa lolote.Hakumuua Edson lakini nguvu kubwa ilitumika kushinikiza mahakama imkute na hatia na hatimaye afungwe maisha gerezani.Shinikizo kubwa lilitoka ndani ya familia ya rais kwani kijana huyo Edson aliwahi kuwa na mahusiano na binti wa rais kabla ya kuachana naye na kuingia katika mahusiano na Penny. Kwa hivi sasa hali si shwari ndani ya ndoa yangu.Mke wangu na ndugu zake wananichukia sana kwa maamuzi niliyoyafanya ya kumuachia huru Penny .Wao wanaamini kwamba penny ndiye aliyemuua Edson.Nimekuwa nikidharauliwa mno na watu hawa kutokana tu na kutenda haki. Baada y kutafakari sana nimeamua kufanya jambo moja la muhimu.

Kumtafuta mtu aliyemuua Edson ili kwanza kuudhihirishia umma wa watanzania kwamba sikukurupuka katika kufanya maamuzi yale na pili kumlinda Penny.Watu ambao walitaka akutwe na hatia na hatimaye apewe adhabu hawatamuacha hivi hivi.Lazima watamuandama na kuhakikisha wanamuondoa kwa namna nyingine.Mathew nimekuja kwako sina msaada mwingine,sina mtu mwingine ambaye anaweza akanisaidia katika jambo hili “ akasema jaji Elibariki.Mathew akainuka na kuelekea katika kabati kubwa akalifungua na kuchukua chupa kubwa ya mvinyo akamimina katika glasi mbili na moja akampatia Elibariki.Akagugumia pombe yote iliyoko katika glasi halafu akavuta mikupuo miwii ya sigara na kupuliza moshi mwingi hewani kisha akasema

“ This is a serious issue than I thought” akasema Mathew kwa sauti ndogo.
“ Si suala dogo hili Mathew na ndiyo maana nimekuja kwako ili unisaidia.Wewe umebobea katika masuala haya ya uchunguzi,umekwisha fanaya kazi katikaidara ya ujasusi ya taifa na una uzoefu mkubwa wa masuala kama haya.Naomba unisaidie kumbaini nani muuaji wa Edson na kwa nini alimuua.Tukifanikiwa katika hilo kila kitu kitakuwa shwari kabisa” akasema Elibariki.Mathew akainama akafikiri tena na kusema
“This girl ..Pe.. Jina lake nani ? Limenitoka kidogo” akasema Mathew
“ Anaitwa penny”
“ Good.This girl Penny who is she to you? Swali lile likamchanganya kidogo jaji Elibariki akafikiri na kusema
“ She’s just an Innocent girl.

Ni mtuhumiwa ambaye hakuwa na kosa na ndiyo maana nikamuachia huru”
“ Eli haujajibu swali langu.Ninafahamu alikuwa mtuhumiwa na hakuwa na kosa .Ninachotaka kufahamu ni mahusiano yako na msichana huyu.Ni ndugu yako,rafiki yako au mpenziwako.Usiogope kuwa muwazi kwangu.” Akasema Mathew
“ Hatukuwahi kufahamiana hapo kabla hadi nilipoanza kuisikiliza kesi yake.Hatukuwahi kuwa na urafiki lakini kwa sasa naweza kusema kwamba tumekuwa marafiki.”
“ Urafiki wa namna gani? Wa mtu na mpenzi wake au urafiki wa kawaida? Akauliza Mathew
“ Ni urafikiwa kawaida tu .” Mathew akavuta sigara na kupuliza moshi halafu akasema
“ Eli nakufahamu vyema,usingeweza kupoteza wakati wako kulishughulikia suala hili kama msichana huyu hana maana yoyote kwako.Please be honnest with me.

I want to help you” “ Ok Mathew,umetaka niwe muwazi na ninakuwa muwazi.Ni kweli msichana huyu ametokea kunivutia sana na tayari nimeanza kuwa na hisia za kimapenzi kwake na ndiyo maana ninajitahidi kufanya kila linalowezekana ili kumlinda”
“ Sawa Eli,ahsante kwa kuwa muwazi.Nitakusaidia.” akasema Mathew halafu akavuta mikupuo miwili ya sigara na kuizima akatoa nyingine katika pakiti akaiwasha.

“ Kwanza naomba ufahamu kwamba hili si suala rahisi kama unavyolichukulia. Ni suala zito na la hatari kubwa.Lakini nakuhakikishia kwamba tutamtafuta muuaji wa huyo kijana kokote alipo na nitahakikisha ninampata.Sikuwa nikitaka kufanya kazi yoyote ya hapa nchini lakini nitaifanya kazi hii kwa sababu yako” akasema Mathew huku akivuta sigara na kupuliza moshi mwingi hewani
“Mathew ninashukuru sana kukubali kunisaidia katika suala hili.Hata hivyo siko peke yangu katika suala hili.Nina mwenzangu aitwaye Jason ambaye ni wakili wa Penny.Ndiye aliyemsimamia Penny katika kesi hii.”
“ Sawa nimekuelewa Elibariki.Mimi niko tayari kufanya kazi hiyo kwa kutumia uwezo wangu wote.

Naomba unipe muda kidogo wa kutafakari namna nitakavyoweza kuifanya kazi hii.Naomba nionane nanyi kesho asubuhi ili niwape mchakato mzima namna nitakavyoifanya hii kazi. Akasema Mathew halafu wakaendelea na maongezi mawili matatu Jaji Elibariki akaondoka

*********

Saa moja na nusu za jioni,jiji ni Arusha bado mvua za manyunyu zinaendelea.Katika hoteli ya kifahari ya Kobe Village Peniela yuko chumban kwake amejilaza..Pembeni ya kitanda chake kulikuwa na meza ndogo iliyokuwa na chupa kubwa ya mvinyo akiendelea kunywa tarataibu huku akifurahia muziki katika runinga.Kengele ya mlangoni ikalia kuashiria kwamba kulikuwa na mtu.Akainuka na kwenda kufungua mlango akakutana na muhudumu aliyevaa suti nzuri nyeusi akiwa na kifurushi mkononi
“ madam kuna mzigo wako umeletwa”akasema Yule muhudumu huku akimpa Penny karatasi ya kusaini kwamba amepokea mzigo.Akasaini karatasi ile na kujifungia chumbani akakifungua kile kifurushi kilichofungwa vizuri.
“ Lazima mzigo huu utakuwa umetoka kwa Kareem” akawaza Penny wakati akikifungua.Ndani ya boksi lile kulikuwa na simu nzuri sana ya gharama kubwa

“ Wow ! what a nice phone” akasema Penny huku akitabasamu.Toka ndani ya lile boksi kulikuwa na kikaratasi kidogo kilichomuelekeza penny aiwashe simu ile.Akaiwasha na kuichunguza ndani,hakukuwa na namba yoyote ya simu iliyoandikwamo.Wakati akitafakari ikapigwa simu akaipokea.Aliitambua sauti ya mpigaji,alikuwa ni Kareem.
“ Hallo Penny” akasema kareem
“ Hi Kareem.”

“ Habari za Arusha?akauliza kareem
“ habari nzuri ila kuna baridi sana huku.?
“ Ok.Usizime hii simu.Mzee atazungumza nawe baada ya dakika chache.” Akasema Kareem na kukata simu.Baada ya dakika kama nne hivi simu ikaita tena kwa namba nyingine tofauti na zile za mwanzo,akabonyeza kitufe cha kupokelea

“ Hallo Penny” ikasema sauti ya upande wa pili ambayo Penny aliitambua ilikuwa ni ya mheshimiwa rais Dr Joshua.
“ Hallo Dr Joshua. Habari yako ? akasema Penny kwa sauti laini “ Habari yangu nzuri.habari za Arusha?
“ huku Arusha kwema kabisa .Habari za Dare s salaam?
“ Huku ni kawaida tu” akasema Dr Joshua
“ Penny mimi ninakuja huo kesho kutwa jioni kwa ajili ya mkutano wa marais wa afrika mashariki utakaofanyika kwa siku tatu kuanzia jumatatu ijayo.Katika siku hizo zote tatu nitakuwa nikionana nawe baada ya kumaliza shughuli zangu.

Nina mambo mengi sana ambayo nataka kuzungumza nawe na zadi ya yote ukumbuke ni mwaka mzima umepita sasa na sitapata ile raha ya aina yake toka kwako.Nataka unipe raha ,nifurahi “
“ Usijali Dr Joshua.Utapata kila unachokihitaji.Nimefurahishwa sana na namna unavyonijali na kunitunza.Nimeamini kwamba ni kweli umedhamiria kuufungua ukurasa mpya kati yetu.” Akasema Penny na kumfanya Dr Joshua acheke kidogo.

“ Ni furaha yangu kama umeridhika na huduma unayoipata Penny.Wewe ni malaika wangu tumia kitu chochote ukitakacho bila kujali gharama.Omba chochote ukitakacho nitakutimizia’ akasema Dr Joshua
“ Ahsante Dr Joshua.Mambo mengi tutaongea ukishakuja huku”
“ Ok Penny .Endelea kupumzika ,tutakuwa wote kesho kutwa.Nimefurahi kuongea na wewe” akasema Dr Joshua na kukata simu. Baada ya Dr Joshua kukata simu ikaingia tena simu nyingine toka kwa kareem
“ Halloo kareem” akasema Penny
“ Penny kuna jambo nimeona nikukumbushe.Simu hiyo ni maalum tu kwa ajili ya kuwasiliana na rais na mimi pekee.Usije ukathubutu kumpigia mtu mwingine yeyote.Isitoshe ukumbuke tulivyokubaliana hakuna kumpigia simu mtu yeyote Yule na kumweleza kwamba uko Arusha.Umenielewa penny?
“ Ndiyo kareem nimekuelewa” akasema Penny na kareem akakata simu
“ mambo yangu yote yanakwenda vizuri sana.Kila kitu kimekaa katika mstari na kinachofuatia sasa ni kuicheza karata yangu ya mwisho.Sitaki kufanya makosa safari hii.Hiki ndicho kipindi cha lala salama” akawaza Penny.

**********

Jaji Elibariki alirejea nyumbani kwake saa tatu za usiku na kumkuta mke wake Flaviana amekaa sebuleni akitazama filamu.Hakumsalimu akapita moja kwa moja hadi chumbani kwake akabadili nguo na kuingia bafuni akaoga halafu akajitupa kitandanina kuanza kusoma kitabu cha hadithi .Baada ya dakika kama ishirini hivi mke wake akaingia mle chumbani na kusimama pembeni ya kitanda.Alionekana wazi alikuwa na hasira
“ Eli ni tabia gani hiyo umeianza ya kuingia ndani bila hata salamu? Akauliza Flaviana.Jaji Elibariki akajifanya kama vile hajasikia akaendelea kujisomea kitabu chake cha hadithi

“Nakuuliza Eli ni tabia gani hiyo ya kuingia ndani bila hata ya kutoa salamu? Nini kinakupa kiburi siku hizi? Au ni hao wanawake unaowakingia kifua ndio wanaokupa kiburi siku hizi? akauliza kwa dharau Flaviana.Taratibu bila kuongea chochote Jaji Elibariki akainuka na kumfuata mkewe na kumzaba kibao kikali kinachomfanya apepesuke na kuangukia kitandani
“ Na iwe ni mwisho kunidharau nakunitolea maneno ya kashfa.Nimechoshoshwa na dharau zako .Nilikwisha kuonya kuhusiana na tabia hii ya dharau hukutaka kunisikia.”akasema kwa hasira Elibariki huku penny akiendelea kulia kwa nguvu.Ni mara ya kwanza toka wameoana Jaji Elibariki kumpiga kofi mke wake.

“ Ahsante Elibariki..ahsante sana..Wewe si mtu wa kunipiga mimi !...” akalia kwa uchungu Flaviana.
“ Toka nimezaliwa hata baba yangu hajawahi kunipiga kofi sembuse wewe ng’ombe ! ..Kauli ile ikampandisha hasira Elibariki na kuanza kumshushia mke wake kipigo kikali kilichomfanya apige ukelele mkubwa .Jaji Elibariki hakujali kelele zile akaendelea kumpa kipigo mkewe.Hadi anamuachia Flaviana alikuwa anavuja damu.

“ Siku nyingine usithubutu kabisa kunidharau paka wewe ..! akasema jaji Elibariki huku akitweta kwa hasira Huku akilia,Flaviana akaingia bafuni na kujifuta damu zilizotoka katika majeraha yaliyotokana na kipigo kikali
“ Eli umenipiga hadi kunitoa damu.Sasa nitakuonyesha mimi na wewe nani mwenye nguvu.I swear in heaven and earth lazima nikuonyeshe kazi na hautanisahau mpaka unaingia kaburini”akasema kwa hasira flaviana na kutoka kwa kasi akaingia katika gari lake na kuondoka kwa kasi
“ Nimechoshwa na dharau za familia hii.Yote hii ni kwa sababu baba yao ni rais .Hapana hawawezi kunitisha hata kidogo,hakuna aliye juu ya sheria.” Akasema jaji Elibariki kwa hasira.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
duuu
SEHEMU YA 5
ILIPISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Wakati akina Jason wakiwa katika mazungumzo hotelini juu ya kumpata muuaji wa Edson,Penny alikuwa amekaa sebuleni kwake akitazama runinga.Hakujisikia kutoka siku hii.Alitaka kubaki ndani akipumzika baada ya mwaka mzima kusota gerezani.Akiwa amejilaza sofani kengele ya mlangoni ikalia,akainuka akachungulia nje kupitia dirishani,na kukutana na sura ambayo ilimstua sana.Alihisi mwili ukimtetemeka kwa uoga.

ENDELEA………………………………….

“ Ivan!!..akasema Penny kwa sauti ndogo .Bado mwili uliendelea kumtetemeka.Aliogopa sana.Kengele ya mlangoni iliendelea kulia,akavuta pumzi ndefu na kwenda kuufungua mlango .Mtu mmoja mwembamba mrefu ,aliyevaa suti nzuri nyeusi na miwani myeusi alikuwa amesimama mlangoni akiwa ndani ya tabasamu .Mkononi alikuwa ameshika lundo la maua mazuri.Wakatazamana kwa sekunde kadhaa

“ Welcome back Penny.I missed you so much.Even after a year in prison you are still as pretty as you used to be ” akasema Yule mtu.Penny hakuonekana kujali alichokiongea Ivan akamuuliza kwa ukali
“ What are you doing here Ivan?

“ Ouh Penny bado hujaacha machachari yako tu? Akasema Ivan huku akiendelea kutabasamu
“Ivan sema kilichokuleta tafadhali na uondoke mara moja.I don’t want to see you here” akasema Penny kwa sauti iliyoonyesha lwamba hakuwa na masihara
“ Hunikaribishi hata ndani Penny? Hatujaonana kwa muda mrefu “ akasema Ivan

“ Ivan tafadhali nakuomba sema kilichokuleta na uondoke.” Akasema Penny.Ivan akatabasamu na kusema
“ Ok Penny nimetumwa nikuletee mzigo huu”
“ Nani kakutuma?
“ Ivan hakujibu kitu akampa Penny ule mzigo wa maua.Penny akaupokea na kuuangalia kwa hasira
“ Kwa heri Penny.Nimefurahi kukuona tena” akasema Ivan na kuanza kupiga hatua kuondoka
“ Ivan please don’t come back here again” akasema Penny lakini Ivan hakugeuka akaingia katika gari lake na kuondoka,akimuacha Penny bado amesimama mlangoni
Baada ya Ivan kuondoka ,Penny akafunga mlango na kuyatupa yale maua mezani.Akayaangalia na kusema kwa sauti ndogo
“ After one year in prison,leo ndiyo ananikumbuka bazazi mkubwa Yule” Toka ndani ya maua yale kikaanguka kikadi kidogo chenye maandishi” welcome back”.Akiwa bado amesimama akitafakari mara simu ya mezani ikaita akaenda kuipokea
“ Hallow” akasema penny
“ Hallow Penny” ikasema sauti ya upande wa pili ambayo Penny aliitambua.

Kikapita kimya kifupi
“ What do you want from me? Akauliza Penny
“ Is that how you say hello to the love of your life? Akauliza mtu Yule.
“ Niambie tafadhali ni kitu gani unakitaka toka kwangu? Akauliza Penny
“ Penny naomba kwanza nikupe pole nyingi kwa masahibu makubwa yaliyokupata lakini vile vile napenda kukukaribisha tena uraiani.Tatu, leo jioni nataka kukutana nawe kwa chakula.Nitamtuma dereva aje akuchukue saa moja na nusu za jioni” akasema Yule mtu na kukata simu.Penny akabaki amesimama ameushikilia mkono wa simu.

Alizama katika mawazo.Akiwa bado amesimama akiwaza mara kengele ya mlangoni ikalia na kumstua.Haraka haraka akayakusanya yale maua na kuyafungia kabatini halafu akaenda kufungua mlango akakutana na wakili Jason
“ Jason” akasema Penny kwa mshangao kidogo kwani hakuwa ametegemea kama Jason angefika kwake mida ile
“ Hi Penny”
“ Hi Jason” akasema Penny na kumkaribisha Jason ndani.
“ Utanisamehe Penny nimekuja bila taarifa”
“ Bila samahani Jason.Hapa ni nyumbani kwako na una ruhusa ya kuja muda wowote na unakaribishwa bila hata kubisha hodi” akasema penny na kumfanya Jason atabasamu
“ Ahsante sana penny”
“ Jason unatumia kinywaji gani?
“ Ahsante Penny lakini kwa sasa sihitaji kinywaji chochote ila nimepita tu kutokana na suala la dharura lililojitokeza asubuhi ya leo”
“ Dharura gani hiyo?

Kuna tatizo? Akauliza Penny kwa wasi wasi
“ Jaji Elibariki alinipigia simu asubuhi akataka nionane naye”
“ Jaji Elibariki?!!..Penny akashangaa
“ Ndiyo “
“ Kuna tatizo gani tena? Akauliza Penny
“ Kuna suala nyeti ambalo aliniitia”
“ Suala gani hilo?
“ Anataka tumtafute muuaji wa Edson”
“ Muuaji wa edson? Penny akazidi kushangaa
“ Ndiyo Penny.Jaji Elibariki amekuwa akijiuliza swali ambalo hata mimi nimekuwa nikijiuliza bila kupata majbu,kwamba nani alimuua Edson ? Wote tuna hakika kabisa kwamba hukumuua lakini sasa nani alimuua? Tunahitaji kufanya uchunguzi na kulibaini hilo.Penny akamtazama Jason kwa sekunde kadhaa na kusema

“ Jason,siwezi kupingana na mawazo yako wala ya jaji Elibariki kwani hata mimi nimekuwa nikijiuliza swali kama hilo bila kupata jibu lakini kesi imekwisha na mahakama haijanikuta na hatia,ni kazi ya vyombo vya dola sasa kufanya uchunguzi na kubaini ni nani muuaji wa Edson?.Nadhani katika suala hili tuviachie vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yake” akasema Penny

“ Nakubaliana nawe Penny kwamba mahakama haijakukuta na hatia na ndiyo maana ikakuachia huru lakini naomba nikuweke wazi kwamba hauko salama.Kulikuwa na nguvu kubwa iliyotaka kuhakikisha kwamba unakutwa na hatia lakini hilo likashindikana.Ni hilo ndilo lililomshangaza jaji Elibariki na kumfanya atake kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio lile na kumbaini muuaji halisi wa Edson.Watu waliofanya kila jitihada kuhakikisha kwamba unakutwa na hatia ya mauaji watakuandama usiku na mchana hadi wahakikishe wamekuangusha baada ya kushindwa mahakamani.Kwa upande wangu nimekubaliana kabisa na jaji Elibariki kwamba kuna ulazima wa kufanya uchunguzi wa siri na kumpata muuaji.

Hiyo ndiyo itakuwa salama kwako na kwetu pia” akasema Jason.Penny akasema
“ Jason nakubaliana nawe kwa kila kitu na ninakushukuru lakini kuhusu hili sina hakika kama lina umuhimu mkubwa kwa sasa.Kuhusiana na maisha yangu usihofu kabisa.I’ll be fine.”
“ No Penny you are not fine and you’ll never be fine hadi hapo tutakapomjua muuaji wa Edson.Please Penny let us do this for you.This is for your own safety “ akasema Jason
Penny akainama akafikiri kwa muda na kusema
“Jason ninaogopa kwa sababu ninajitahidi kwa kila niwezavyo kuifuta kumbu kumbu ya Edson kichwani mwangu .Sitaki tena kujihusisha na mambo yoyote yanayohusiana na Edson.He’s gone for good and I have to forget him”
“ Penny nalielewa hilo lakini hautaweza kuifuta kumbu kumbu hiyo kichwani mwako bila ya kumpata muuaji wa Edson.Utakuwa unajiuliza swali hili mara kwa mara na hautakuwa na amani”
“ Jason this isn’t an easy thing.Ni jambo zito na la hatari kubwa.

How are you going to do it?
“ Ni kweli si jambo jepesi hata kidogo na sisi ni wanasheria na hatuna utaalamu wa kufanya uchunguzi wa jambo kubwa kama hii lakini tukiunganisha nguvu zetu sote watatu tunaweza tukafanikiwa”
Penny akanyamaza akafikiri na kusema
“ Sina kipingamizi hata kidogo kuhusiana na suala hili japokuwa sikuwa nataka kujihusisha katika kitu chochote kinachohusiana na Edson lakini wewe ndiye mwanasheria wangu naamini umeona umuhimu wa jambo hili kwa hiyo naahidi kutoa ushirikiano wangu”
“ Ahsante sana kwa kukubali penny.

Kwa kuanzia,Jaji Elibariki anahitaji kukuona ana kwa ana kwa maongezi ”
“ Kuhusu nini?
“ Ni kuhusiana na suala hili .Kuna mambo ambayo anahitaji kuyafahamu kutoka kwako kabla ya kuangalia tufanye nini tena.”
“ Lini anahitaji kuonana nami?
“ Ni jioni ya leo.Tayari nimekwisha andaa chumba ,Moniz 5 star hotel ambako ndiko mtakakokutania.Jaji Elibarii alitaka makutano yenu yawe ya siri kubwa bila ya mtu yeyote kufahamu”
Penny akainama akazama katika mawazo.

Alikumbuka jioni ya ana ahadi ya kuonana na mtu kwa chakula cha jioni
“ Mambo yanaingiliana.Watu wawili wote wanataka kuonana nami usiku wa leo.Nionane na nani? Akajiuliza Penny
“ Lakini ngoja nikaonane na Jaji Elibariki.Bila yeye hivi sasa ningekuwa kifungoni.” Akawaza Penny halafu akamgeukia Jason
“ Ok Jason.Nitakwenda kuonana na Elibariki jioni ya leo”
“ Ahsante kwa kukubali Penny.Nitakupitia saa moja za jioni nikupeleke mkaonane na Jaji Elibariki halafu nitakurejesha nyumbani”
“ Sawa Jason” akajibu Penny halafu wakaagana na Jason akaondoka

*********

Katika moja ya jengo refu kabisa jijini Dar ,watu saba wameizunguka meza ya duara ndani ya ofisi nzuri iliyo katika ghorofa ya kumi na mbili.Mtu mmoja mrefu na mwenye umbo la wastani alikuwa akiongea na wengine wakimsikiliza kwa makini

“ Nimepigiwa simu na ofisi kuu asubuhi ya leo wakinionya kuhusiana na kutorudiwa tena kwa uzembe mkubwa uliopita kiasi cha kumuacha Penny akaingia katika matatizo makubwa na kuhatarisha mpango wetu wa miaka mingi.Endapo Penny angekutwa na hatia mahakamani na kufungwa ,kila kitu kingefikia mwisho.Juhudi zote za miaka zaidi ya ishirini zingekuwa ni kazi bure. Bila Penny kila kitu kitakwama .

Kwa hiyo basi maagizo niliyoyapata toka ofisi kuu ni kwamba tuhakikishe uzembe kama ule haujirudii tena na Penny apewe ulinzi wa kutosha na kumuepusha na mambo yote yanayoweza kumsababishia matatizo na kuhatarisha mpango mzima.Kazi kubwa imekwisha fanyika na tuko katika hatua za mwishoni.

Tunatakiwa kuongeza umakini maradufu.Tunatakiwa tufahamu na tuwepo kila mahala alipo Penny,tufahamu watu anaokutana nao na kwa kuanzia tunatakiwa kumfahamu Jaji Elibariki Chukuswa ambaye anakwenda kuonana na Penny jioni ya leo.”

Akasema Yule jamaa
uuuuuuuuuuuuu
 
Back
Top Bottom