JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji. Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi
Tumefanikiwa kuipata picha hii ambayo inaaminika huyu ndio Gustave. Kuna Mamba katika Ziwa Tanganyika anayeitwa "Gustave" ambaye inadaiwa ameua zaidi ya watu 300 katika miongo kadhaa iliyopita. Kumekuwa na majaribio kadhaa ya kumuua au kumkamata bila mafanikio. Gustave ni mamba wa kiume yupo tangu mwaka 1955 ambaye huzurura katika fukwe ndani ya Ziwa Tanganyika. Inasemekana kuwa Gustave aliua watu 300, amepata hadhi ya kuzungumzwa na anaogopwa sana na watu. Uwezo wake ni mkubwa sana wa kukamata na nguvu zake hazieleziki. Urefu wake ni mita 6.1 ana uzito wa kilo 907 kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika. Ana uwezo wa kukamata mnyama yeyote yule wa nchi kavu na majini ikiwemo Kiboko. tembo n.k. Wazungu wamelichukulia swala hili ni maajabu...
Tangu nikiwa mdogo nilisikia na kuamini kwamba ute/ mapovu yanayokuwa kwenye mimea ni mate ya nyoka. Mpaka kufika wakati huu bado sijajua kama suala hili lina ukweli ama la. Naomba wataalamu mnisaidie kujua uhalisia wa jambo hili Kielelezo 1: Picha ikionesha mmea umeachiwa mapovu Kielelezo 2: Picha ikionesha mdudu aina ya Spittlebugs anayetengeneza Povu kwenye mimea Video ikionesha namna wadudu aina ya Spittlebugs wanavyotengeneza povu
Nimesikia sehemu kuwa binadamu anaweza kupata usugu wa vimelea kutokana na kutumia mazao yatokanayo na wanyama mbalimbali, mfano wa mazao hayo ni nyama nk. Hofu yangu ni kuwa wafugaji wengi siku hizi wamekuwa si waaminifu kabisa, wamekuwa wakitumia madawa hatari kwa ajili ya kukuzia haraka wanyama ili waingize sokoni, au wakati mwingine wamekuwa wakitumia madawa kwa ajili ya kuhifadhi mazao hayo ili yakae muda mrefu bila kuharibika. Kumekuwepo cases nyingi za nguruwe na kuku kuchanganyiwa dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI. JamiiCheck.com naomba mniondoe wasiwasi huu maana tunakoelekea huko mbeleni ni hatari.
Nimeona mtandaoni Mkuu wa kitengo cha Digital, Crown Fm ameandika kuwa Mara ya mwisho Yanga SC kufungwa kwenye Ligi Kuu ni Oktoba 4, 2023 bado siku 3 itimize mwaka mmoja pasipo kupoteza mchezo kwenye Ligi Ligi Kuu ya NBC PL. Eti wadau huyu anasema kweli au anatupanga maana huwa naona kama mnazi wa Yanga isijekuwa mapenzi ya timu yamefanya achakachue takwimu atupange. JamiiCheck fanyenyi jambo tujue Ukweli.
Salama wakubwa wa JamiiCheck? Katika pitapita zangu mitandaoni kuna mtu nimeona akishauri kuwa ni vizuri kumnyoa mtoto mchanga nywele alizozaliwa nazo ili mtoto akue vizuri. Amedai kuwa mtoto asiponyolewa nywele hizo anaweza pata madhara ya ngozi ya kichwa, ukuaji duni lakini mwisho ni mambo ya kiimani. Binafsi nipo njiapanda maana nimekuwa nikiona watoto wengine wakinyolewa ndani ya wiki moja baada ya kuzaliwa, lakini wengine hawajawahi guswa nywele zao mpaka wanakuwa wakubwa.
Wakati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kikitangaza kufanya Maandamano ya amani leo Jijini Dar Es salaam chini ya Mwenyekiti wake Freeman Mbowe, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amechapisha mtandaoni mwake akisema anazo taarifa kuwa Mwenyekiti Mbowe yupo Arusha na hivyo kumualika ofisini kwake Jijini Arusha. Makonda ameandika "Kaka yangu Mbowe kumbe umeingia Arusha na hausemi. Karibu Ofisini basi ukiamua Kutoka" Ikumbukwe kuwa saa chache zilizopita, nyumba ya Freeman Mbowe iliyopo Mikocheni ilizingirwa na Jeshi La Polisi huku mkewe Dr Lilian Mtei akiripotiwa kuzuia kutoka nyumbani kwake. Source: Jambo TV
Back
Top Bottom