vinneboy
JF-Expert Member
- Aug 12, 2015
- 478
- 436
- Thread starter
- #61
SORRY MADAM (53)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Shamsa akajikuta akistuka baada ya kumuona
Phidaya akimfwata katika sehemu alipo shikiliwa
na polisi.
“Hawa ndio majambazi eheee?”
Phidaya alizungumza kwa sauti ya ukali, askari
mmoja akamuitikia, Phidaya bila hata kujiuliza
mara mbili, akamzaba kofi Shamsa, aliye kuwa
akimshangaa, pasipo kuamini kwamba huyo ni
Phidaya au laa, kwa maana wamefanana kila kitu.
Ilibidi baadhi ya askari wamzuie Phidaya
asiendelea kuwashambulia majambazi hao walio
ivamia hospitali yake.
ENDELEA
Shamsa na majambazi wengine watatu
wakaingizwa ndani ya gari tatu tofauti za polisi,
tukio hilo Sa Yoo aliweza kulishuhudia ila hakujau
ni kitu gani kimetokea hadi Shamsa kukamatwa na
askari, isitoshe akiwa katika mavazi ya unesi,
wakati si mavazi ambayo alikuwa nayo.
Gari za polisi zilizo beba wahalifu zikaondoka Sa
Yoo naye akaingia kwenye gari lake na kuzifwatilia
hadi kituoni. Shamsa na waalifu wengine wawili
wakaingizwa mahabusu, kusubiria mahojiano
yatakayo fwanywa dhidi yao.
Akilini mwa Shamsa kumbukumbu za Phidaya,
zilizidi kujirudia kichwani mwake. Hakuelewa ni
jambo gani ambalo limetokea hadi Phidaya kuwa
hai.
“Au sio yeye?”
Alijiuliza mwenyewe, huku akiwa amesimama
kwenye moja ya kona ya mahabusu, huku
mahabusu wezake wengine wakike wakiwa
wamejilaza, kwenye sakafu.
“Kwa usiku huu hautaweza kumuona”
Askari mmoja alimueleza Sa Yoo, ambaye alihitaji
kukutana na rafiki yake ili amuhoji kuhusu jambo
lililo jitokeza muda mchache ulio pita. Sa Yoo kwa
haraka akampigia simu daktari wa Shamsa,
akamueleza kila kitui kilicho tokea, daktri hiyo aliye
kabidhiwa jukumu la kumuangalia Shamsa, kwa
haraka akafika kituo cha polisi akiwa ameongozana
na mwanasheria wake kuhakikisha kwamba
Shamsa anaachiwa huru.
***
Maisha ya madam Mery yalizidi kuwa mazuri kadri
siku zilivyo zidi kwenda, jeraha la risasi aliyo
pigwa na Manka lilisha pona muda mrefu sana.
Maisha yake aliamua kuyahamishia mkoani
Mwanza, ambapo alifanikiwa kufungua mgahawa
mmoja mkubwa wa kisasa, ambao kwa siku una
uwezo wa kuhudumia wateja mia tisa hasi alfu
moja kwa siku.
Umaarufu wa mgahawa wake uliendana moja kwa
moja na jina lake, jumba kubwa la gorofa la
kifahari, lililopo maeneo ya majango mapya.
Aliliwekea ulinzi mkali kutoka katika mashirika
mawili tofauti yanayo jishuhulisha na ulinzi. Uzuri
wake uliwanyima usingizi wanaume wengi wa jijini
Mwanza, umri wa miaka arobaini na moja alio nao,
kwa haraka haraka ukimtazama utahisi ni
msichana mwenye umri wa miaka ishirini na tano.
Kwa siku hiyo, madam Mery alijawa na furaha sana
moyoni mwake, pale alipo toka katioka banki ya
Bacrays, na kukuta kiasi cha miliomi moja dola za
kimarekani zikiwa zimeingizwa kwenye akaunti
yake hiyo.
“Ranjiti nitakutesa hadi kufa kwako”
Madam Mery alizungumza baada ya kupokea risiti
yake inayo onyesha kiasi hicho kikubwa cha pesa
kikiwa kimeingizwa kwenye akaunti yake. Kwa
mwendo wa madaha akaanza kutembea huku
mlinzi wake wa kike akiwa ameibeba pochi lake
kubwa. Wakaingia kwenye gari, walipo muacha
dereva wake.
“Nirudishe nyumbani nahitaji kupumzika kwa sasa”
“Sawa madam”
Safari ya kutoka benk hadi nyumbani kwake
iliwachukua dakika ishirini, geti kubwa linalo
funguliwa na umeme likafunguka. Gari yake aina ya
Hammer, likaingia na dereva akalisimamisha
kwenye maegesho ya magari, ambapo kuna gari
nyingine nne za kifahari zikiwemo, Range rover
sport, Aud Q7, Ferrari spider na BMW X6. Milinzi
wake kwa haraka akashuka na kumfungulia
mlango.
“Lete tu pochi pumzika”
Madam Mery alizungumza huku akiichukua pochi
yake kwa mlinzi wake huyo, akaelekea ndani, alipo
pokelewa na mfanyakazi wake wa ndani.
“Mama utakula nikuandalie chakula?”
Hapana sijisikii kula”
Kwa furaha ambayo madam Mery anayo,
hakutamani siku hiyo kuweza kuingiza kiu
chochote mdoni mwake, kwani utajiri wake unazidi
kuongezeka mara dufu, akaingia chumbani kwake,
ajitupa kwenye tanda lake kubwa linalo nesa nesa.
“Mery sasa hivi mimi ni milionear”
Alizungumza huku akiliachilia tabasamu lake pana,
akakaa kitako, akaichukua rimoti ya Tv yake kubwa
ilipo ukutani, akaiwasha na kuanza kutafuta chaneli
ambayo ina kipindi kizuri cha kutazama. Chaguo la
chaneli likaangukia katika chaneli ya ITV, ambapo
amekuta mwenyekiti wa chama cha upinzani cha
TDPP(Tanzania Democras People Party), bwana
Kibwila, akizungumza na waandishi wa habari.
Masikio na macho ya Madam Mery yote yakaelekea
kwenye Tv yake, mapigo ya moyo yakaanza
kumdunda pale alipo muona Manka akiwa pembeni
ya kiongozi huyo.
“Huyu mtoto amefwata nini kwenye hichi chama?”
Madam Mery aalijiuliza huku akiongeza kidogo
sauti ya Tv hiyo. Mwenyekiti wa chama hicho
bwana Kibwila, akafikia wakati wa kumtangaza
mgombea uraisi wa chama chake.
“Mgombea wetu atakaye ipeperusha bendera ya
chama chetu atakuwa ndugu Godwin, gererali
mstaafu wa jeshi la wananchi Tanzania”
Madama Mery, akahisi kizunguzungu kikali kikitaka
kumchukua, baada ya kulisikia jina la Mzee
Godwin, kwa kudhibitishiwa kwamba mwenyekiti
huyo hajakosea kabisa, akaonyesha picha ya Mzee
Godwin, hapo ndipo furaha yote ya Madam Mery
ikayeyuka kama barafu liwekwapo juani.
***
Taratibu Rahab akamfikia Raisi Praygod kwenye
mlango alipo simama, kwa haraka akamkumbatia,
na kuanza kumwagikwa na machozi jambo lililo
mshangaza raisi Praygod.
“Mume wangu nisamehe”
Rahab alizungumza huku machozi yakimwagika,
raisi Praygod, alizidi kuendelea kushangaa,
kumuona Rahab akiwa amerejea katika hali ya
kawaida. Rahab, hakusita kuanza kuzinyonya lipsi
za mume wake, joto la hisia za kimapenzi likaanza
kupanda katikati yao. Kila mmoja akajikuta akiwa
na hamu ya kupata penzi la mwenzake, ambalo
walilikosa kwa kipindi fulani. Ndani ya dakika
kadhaa wote wawilili wakajikuta wakiwa hawana
nguo katika miili yao.
Kila mmoja alipo hakikisha kwamba amemuandaa
mwenzake vya kutosha, mechi ikaanza, si raisi
wala Rahab aliye onekana kuchoka, kila mmoja
alihakikisha kwamba anampa mwenzake kile kitu
roho inapenda, huku wote wakiwa wamejawa na
furaha mioyoni mwao.
***
Iliwalazimu Black Shadow kuhamishiwa katika
chumba kingine cha siri, kilichopo chini ya ardhi
ndani ya hospitali hiyo. Kazi hiyo ilifanywa na
dokta Ranjiti na wasaidizi wake, usiku huo huo,
baada ya tukio la uvamizi kutokea katika hospitali
yake. Polisi wakatoa tamko kwa watu ambao
walijitokeza kumuombea shujaa huyo, kwamba
warudi majumbani kwao na kuanzia siku hiyo watu
hawata ruhusiwa kuja kujazana katika hospitali
hiyo, hadi pale afya ya Black Shadow itakapo
imarika.
Lilikuwa ni pigo kwa mashabiki wa Black Shadow,
ila hawakuwa na jinsi, ni lazima waweze kutii
tamko hilo la askari. Ulinzi ukazidi kuimarishwa
kwenye hospitali hiyo, hata dhiara ya raisi,
ikakatishwa hadi pale mambo yatakapo kuja kuwa
sawa ndipo raisi aweze kumtembelea mpiganaji
huyo.
Uwepo wa Black Shadow katika chumba cha siri
ulijilukana kwa watu wachache tu akiwemo
Sabogo, ambaye yeye pekee ndiyo alipewa ruhusa
ya kwenda kumuona Black Shadow katika chumba
hicho. Asubuhi na mapema, Sabogo akawa yupo
ndani ya chumba hicho cha siri kilicho jaa taa
nyingi zenye mwanga mweupe.
Sabogo akatoa kinyago kingine kilicho tengenezwa,
kwa ajili ya Black Shadow, akamvua kinyago cha
mwanzo na kumvalishi kingine kipaya lilicho mkaa
vizuri, alipo hakikisha rafiki yake yupo salama,
akatoka ndani ya chumba hicho na kurudi kwa
daktari mkuu wa hospitali bwana Ranjiti.
“Itamchukua muda gani hadi kupata fahamu?”
“Itamchukua kipindi kidogo, ila kutokana bado
tunaendelea kumuangalia kwa usalama mkubwa,
basi tumuombe Mungu, kila jambo litakwenda
sawa”
“Sawa dokta ila hakikisha kwamba hakuna mtu
ambaye atagundua kwamba yupo chumba cha siri”
“Usijali kwa hilo”
Yote yakiwa yanazungumza ndani ya ofisi ya dokta
Ranjiti Phidaya aliweza kuyasikia akiwa nje ya
mlango, moyo wake ulizidi kumsumbua kila alipo
fikiria juu ya donge nono ambalo polisi
walilitangaza kwa mtu ambaye angelisaidia jeshi
hilo kumkamata Eddy.
Phidaya akarudi kwenye ofisi yake akiwa na
mawazo mengi, akilini mwake akaanza kulifikiria
tukio la jana alipo weza kuiona sura ya Black
Shadow, pili akafirikiria jinsi, majambazi walivyo
vamia kwenye hospitali yake, na kutaka kumuua
Black Shadow.
“Ina maana wanamjua kwamab ni Eddy nini?”
Phidaya alizungumza huku akinyanyuka kwenye
kiti chake na kuanza kuzunguka zunguka ndani ya
ofisi yake.
“Ngoja nikamueleze kila kitu mume wangu”
Phidaya alizungumza, kwa haraka akaanza kupiga
hatua hadi mlangoni kwake, akavuta kitasa cha
mlango huo, akaufungua na kuanza kutembea
kuelekea katika ofisi ya mume wake.
***
Baada ya Sabogo kutoka ofisini kwake, dokta
Ranjiti, akawasha Tv yake, moja ya taarifa aliyo
ikuta ni jinsi hospitali yake ilivyo vamiwa. Ila kati
ya majambazi walio kamatwa, mmoja wao
akamstua kidogo. Akajikuta akisimama kabisa na
kwenda kuikodolea macho Tv hiyo. Jina la Shamsa
Eddy, ndio kabisa zikazidi kumpagawisha. Na moja
ya picha ikapita kwenye taarifa hiyo ya habari jinsi
mke wake alivyo mtandika kofi jambazi huyo wa
kike.
‘Mungu wangu siri inakwenda kufichuka’
Dokta Ranjiti alizungumza huku kijasho kikianza
kumpiga na mapigo yake moyo yakizidi kwenda
mbio. Akaanza kujipapasa kuitafuta simu yake ya
mkononi sehemu alipo iweka, kwa bahati nzuri
akaikuta kwenye koti lake, akaichomoa kwa haraka
na kuminya baadhi ya namba kisha akaiweka
sikioni, baada ya muda ikapokelewa upande wa
pili.
“Ehee mkuu habari yako bwana”
‘Salama vipi dokta nikusaidie nini?’
“Naamini hao majambazi walio kuja kuvamia
hospitalini kwangu wapo mikononi mwako”
‘Ndio na wanaendelea kufanyiwa mahojiano, ila
huyu mmoja wa kike hana hatia ndio tumemuachia
mida hii’
“Mungu wangu…….!!!”
‘VVipi kuna tatizo kwani?’
“Aha…ahaaa hapana”
‘Basi kila litakalo kuwa linaendelea nitakujulisha’
“Sawa mkuu”
Dokta Ranjiti baada ya kukata simu alipo maliza
kuzungumza na mkuu wa kituo cha polisi, akili
yake ikaanza kufanya kazi kama compyuta pale
inapo tafuta, majina yaliyo hifadhiwa kwenye
kumbukumbu zake. Kwa haraka mkumbukumbu
zake zikatua kwenye moja ya mtu ambaye kazi
zake ni umafia na huzifanya kazi za matajiri wengi
ndani na nje ya Japani, pasipo kukosea wala
kukamatwa na askari polisi kutokana na
kujibadilisha badilisha sura na yeye huwa mara
nyingi huwa ndio mtu anaye mfanyia upasuaji wa
kumbadilisha sura.
“Ndio Kim upo wapi?’
‘Yokoma, vipi kuna tatizo dokta?’
“Ndio kuna tatizo bwana, kuna binti anaitwa
Shamsa Eddy nahitaji uweze kumuondoa dunia”
‘Amekufanyaje tena dokta?’
“Ni binti ambaye anaitambua siri ya yangu juu ya
mke wangu Phidaya, si unatambua kwamba huyu
Phidaya ni mwanamke niliye mpora waziri mmoja
nchini Tanzania”
‘Yap nalitambua hilo ulisha wahi kuniambia’
“Ndio basi binti huyo ni kati ya wale majambazi
walio kamatwa jana na polisi na yeye anamtambua
vizuri Phidaya kutokana ni mama yake”
Mazungumza ya simu ya dokta Ranjiti yakamfanya
Phidaya kusimama nje ya mlango, aliweza kusikia
kila kitu alicho kizungumza mume wake, ila
hakuweza kusikia mazungumzo na mtu wa pili.
‘Phidaya kutokana ni mama yake’
Maneno hayo yakaanza kujirudia kwa nguvu akilini
mwake, machozi yakaanza kumlanga lenga
Phidaya, hakuona haja ya kuendelea kukaa
mlangoni mwa mume wake kwa haraka akaanza
kutembea kurudi ofisini mwake. Akaufunga mlango
wake kwa ndani, akavuta kiti chake, akawa kama
mtu aliye changanyikiwa mara kadhaa akijiuliza
maswali mengi kuhusiana na kitui alicho kisikia.
“Shamsa Eddy”
‘Ni binti ambaye anaitambua siri yangu juu ya mke
wangu Phidaya’
Phidaya akajikuta akizidi kuyakumbuka maneno ya
mume wake bwana Ranjiti, kiu na hamu ya
kumuona Shamsa, ikaanza kumjaa moyoni mwake,
kwani anatambu ni kati ya majambazi ambao
walikamatwa jana na ni yule aliye mtandika kibao
jana usiku. Kwa haraka Phidaya akavua koti lake
na kuvaa koti la baridi, akajifutamachozi usoni
mwake, wala hakuhitajki tena kuzungumza na
mumewe kwa kitu alicho wahi kukiona. Kwani roho
ya kumchukia mwanume huyo ilianza kumvaa.
Swali ambalo mara kwa mara alijiuliza kichwani
mwake, kwamba yeye ni nani, taratibu alihisi
linaanza kupata jibu.
“Lazima nijijua mimi ni nani”
Phidaya alizungumza peke yake huku akitembea
kwenye kordo ya kuelekea nje ya hospitali.
***
Kwa juhudi za mwana sheria aliye msimamia
Shamsa, kwenye mahojiano kati yake na polisi,
yalizaa matunda, kwani hadi inatimu alfajiri tayari
Shamsa alionekana kwamba hana hatia kutokana
na maelezo yake aliyo yatoa. Uchunguzi ulio
fanywa kwa nesi ambaye aliuawa na Shamsa,
ulionyesha kwamba hakuwa ni nesi wa hospitali
hiyo kutokana na kukutwa na michoro mingi
(tattoo) mwilini mwake.
Pia katika kubanwa kwa waalifu wawili wa kiume
walio kamatwa, walidhibitisha kwamba Shamasa
sio mwenzao, hilo pia lilichangia kwa Shamsa
kuachiliwa huru.
“Inabidi sasa twende nyumbani ukapumzike”
Sa Yoo alizungumza mara baada ya Shamsa
kuachiliwa huru, kwani naye pia alishinda kituoni
hapo kuhakikisha kwamba rafiki yake anaachiwa
huru.
“Hapana nahitaji kwenda hospitali kumuona Black
Shadow ndio niweze kwenda nyumbani’
Kutokana Shamsa ni mtu wa kung’ang’ania
maamuzi yake mwanzo mwisho, Sa Yoo na daktari
hawakuwa na hiyana zaidi ya kuanza safari
kuelekea katika hospitali aliyo lazwa Black
Shadow. Akilini mwa Shamsa hakumfikiria Phidaya
kutoka alihisi labda alimfananisha, isitoshe tayari
walisha mzika mama yeka huyo. Kutokana ni
asubuhi, barabara ilijaa foleni nyingi, kwa hiyo
iliwachukua muda mwingi sana hadi kuweza kufika
katika hospitali hiyo. Wakiwa getini, wakapishana
na gari aina ya Aud A4. Hakuna aliye weza
kuifwatilia sana, haswa Shamsa ambaye muda
wote alimuwaza Black Shadow wake.
Wakaegesha gari walilo jia kwenye maegesho ya
hospitalini hapo, Shamsa akawa wa kwanza
kushuka kwenye gari huku akifwatiwa na Sa Yoo
pamoja na daktari wake.
Kila nesi aliye muona Shamsa, alijikuta
akimuogopa sana, kwani kila mmoja anatambua ni
miongoni mwa majambazi walio sababisha kifo
cha nesi mwezao aliye pigwa risasi jana usiku
akijaribu kuyaokoa maisha yake.
“Daktari mkuu yupo wapi?”
Sa Yoo alimuuliza nesi wa mapokezi, aliye baki
akimtumbulia macho Shamsa asijue ajibu nini.
“Dada nakuuliza daktari mkuu bwana Ranjiti yupo
wapi?”
“Ahahaa ameetoka”
“Una uhakika?”
Shamsa alimuuliza nesi huyo huku akiwa amekazia
jicho.
“Yupo ofisini kwake”
Sa Yoo alijikuta akiangua kicheko, baada ya
kumuona nesi huyo akiwa anababaika babaika,
wote watatu wakamuaga nesi huyo na kuelekea
katika ofisi ya bwana Ranjiti.
***
Gafla Phidaya akajikuta akifunga breki za gari lake,
alihisi kama mtu aliye muona kwenye gari aliyo
pishana nayo getini, hajakosea.
”Ndio yeye”
Alizungumza huku akikunja kona ya haraka na
kunza kurudi hospitalini kwa mwendo wa kasi,
haikumchukua muda tayari akawa amesimama
kwenye geti la kuingilia hospitalini kwake. Askari
wakamfungulia geti hilo kuwa, kwa haraka
akalisimamisha gari lake kwenye maegesho, kisha
akashuka na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea
ndani. Akakuta manesi wa mapokezi wakiwa
wanajadiliana kitu, walipo muona kila mmoja
akajifanya kama anaendelea na kazi zake.
“Kuna nini hapa?”
“Hakuna kitu madam”
“Muna nidanganya eheee?”
“Madama kusema kweli yule jambazi wa kike
amekuja tena, na sasa hivi ameelekea ofisini mwa
mume wako”
“Muna sema kweli?”
“Ndio”
Phidaya akaanza kukimbia kuelekea ofisini mwa
mume wake na kuwaacha manesi hao
wakimshangaa boasi wao, Phidaya bila hata
kubisha hodi akaufungua mlango wa ofisi ya mume
wake, macho yake yakagongana na macho ya
Shamsa, aliye aliye geuka kutazama mtu aliye ingia
ndani ya ofisi ya daktari bila kubisha hodi.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 54 YA SIMUHILI HII.
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Shamsa akajikuta akistuka baada ya kumuona
Phidaya akimfwata katika sehemu alipo shikiliwa
na polisi.
“Hawa ndio majambazi eheee?”
Phidaya alizungumza kwa sauti ya ukali, askari
mmoja akamuitikia, Phidaya bila hata kujiuliza
mara mbili, akamzaba kofi Shamsa, aliye kuwa
akimshangaa, pasipo kuamini kwamba huyo ni
Phidaya au laa, kwa maana wamefanana kila kitu.
Ilibidi baadhi ya askari wamzuie Phidaya
asiendelea kuwashambulia majambazi hao walio
ivamia hospitali yake.
ENDELEA
Shamsa na majambazi wengine watatu
wakaingizwa ndani ya gari tatu tofauti za polisi,
tukio hilo Sa Yoo aliweza kulishuhudia ila hakujau
ni kitu gani kimetokea hadi Shamsa kukamatwa na
askari, isitoshe akiwa katika mavazi ya unesi,
wakati si mavazi ambayo alikuwa nayo.
Gari za polisi zilizo beba wahalifu zikaondoka Sa
Yoo naye akaingia kwenye gari lake na kuzifwatilia
hadi kituoni. Shamsa na waalifu wengine wawili
wakaingizwa mahabusu, kusubiria mahojiano
yatakayo fwanywa dhidi yao.
Akilini mwa Shamsa kumbukumbu za Phidaya,
zilizidi kujirudia kichwani mwake. Hakuelewa ni
jambo gani ambalo limetokea hadi Phidaya kuwa
hai.
“Au sio yeye?”
Alijiuliza mwenyewe, huku akiwa amesimama
kwenye moja ya kona ya mahabusu, huku
mahabusu wezake wengine wakike wakiwa
wamejilaza, kwenye sakafu.
“Kwa usiku huu hautaweza kumuona”
Askari mmoja alimueleza Sa Yoo, ambaye alihitaji
kukutana na rafiki yake ili amuhoji kuhusu jambo
lililo jitokeza muda mchache ulio pita. Sa Yoo kwa
haraka akampigia simu daktari wa Shamsa,
akamueleza kila kitui kilicho tokea, daktri hiyo aliye
kabidhiwa jukumu la kumuangalia Shamsa, kwa
haraka akafika kituo cha polisi akiwa ameongozana
na mwanasheria wake kuhakikisha kwamba
Shamsa anaachiwa huru.
***
Maisha ya madam Mery yalizidi kuwa mazuri kadri
siku zilivyo zidi kwenda, jeraha la risasi aliyo
pigwa na Manka lilisha pona muda mrefu sana.
Maisha yake aliamua kuyahamishia mkoani
Mwanza, ambapo alifanikiwa kufungua mgahawa
mmoja mkubwa wa kisasa, ambao kwa siku una
uwezo wa kuhudumia wateja mia tisa hasi alfu
moja kwa siku.
Umaarufu wa mgahawa wake uliendana moja kwa
moja na jina lake, jumba kubwa la gorofa la
kifahari, lililopo maeneo ya majango mapya.
Aliliwekea ulinzi mkali kutoka katika mashirika
mawili tofauti yanayo jishuhulisha na ulinzi. Uzuri
wake uliwanyima usingizi wanaume wengi wa jijini
Mwanza, umri wa miaka arobaini na moja alio nao,
kwa haraka haraka ukimtazama utahisi ni
msichana mwenye umri wa miaka ishirini na tano.
Kwa siku hiyo, madam Mery alijawa na furaha sana
moyoni mwake, pale alipo toka katioka banki ya
Bacrays, na kukuta kiasi cha miliomi moja dola za
kimarekani zikiwa zimeingizwa kwenye akaunti
yake hiyo.
“Ranjiti nitakutesa hadi kufa kwako”
Madam Mery alizungumza baada ya kupokea risiti
yake inayo onyesha kiasi hicho kikubwa cha pesa
kikiwa kimeingizwa kwenye akaunti yake. Kwa
mwendo wa madaha akaanza kutembea huku
mlinzi wake wa kike akiwa ameibeba pochi lake
kubwa. Wakaingia kwenye gari, walipo muacha
dereva wake.
“Nirudishe nyumbani nahitaji kupumzika kwa sasa”
“Sawa madam”
Safari ya kutoka benk hadi nyumbani kwake
iliwachukua dakika ishirini, geti kubwa linalo
funguliwa na umeme likafunguka. Gari yake aina ya
Hammer, likaingia na dereva akalisimamisha
kwenye maegesho ya magari, ambapo kuna gari
nyingine nne za kifahari zikiwemo, Range rover
sport, Aud Q7, Ferrari spider na BMW X6. Milinzi
wake kwa haraka akashuka na kumfungulia
mlango.
“Lete tu pochi pumzika”
Madam Mery alizungumza huku akiichukua pochi
yake kwa mlinzi wake huyo, akaelekea ndani, alipo
pokelewa na mfanyakazi wake wa ndani.
“Mama utakula nikuandalie chakula?”
Hapana sijisikii kula”
Kwa furaha ambayo madam Mery anayo,
hakutamani siku hiyo kuweza kuingiza kiu
chochote mdoni mwake, kwani utajiri wake unazidi
kuongezeka mara dufu, akaingia chumbani kwake,
ajitupa kwenye tanda lake kubwa linalo nesa nesa.
“Mery sasa hivi mimi ni milionear”
Alizungumza huku akiliachilia tabasamu lake pana,
akakaa kitako, akaichukua rimoti ya Tv yake kubwa
ilipo ukutani, akaiwasha na kuanza kutafuta chaneli
ambayo ina kipindi kizuri cha kutazama. Chaguo la
chaneli likaangukia katika chaneli ya ITV, ambapo
amekuta mwenyekiti wa chama cha upinzani cha
TDPP(Tanzania Democras People Party), bwana
Kibwila, akizungumza na waandishi wa habari.
Masikio na macho ya Madam Mery yote yakaelekea
kwenye Tv yake, mapigo ya moyo yakaanza
kumdunda pale alipo muona Manka akiwa pembeni
ya kiongozi huyo.
“Huyu mtoto amefwata nini kwenye hichi chama?”
Madam Mery aalijiuliza huku akiongeza kidogo
sauti ya Tv hiyo. Mwenyekiti wa chama hicho
bwana Kibwila, akafikia wakati wa kumtangaza
mgombea uraisi wa chama chake.
“Mgombea wetu atakaye ipeperusha bendera ya
chama chetu atakuwa ndugu Godwin, gererali
mstaafu wa jeshi la wananchi Tanzania”
Madama Mery, akahisi kizunguzungu kikali kikitaka
kumchukua, baada ya kulisikia jina la Mzee
Godwin, kwa kudhibitishiwa kwamba mwenyekiti
huyo hajakosea kabisa, akaonyesha picha ya Mzee
Godwin, hapo ndipo furaha yote ya Madam Mery
ikayeyuka kama barafu liwekwapo juani.
***
Taratibu Rahab akamfikia Raisi Praygod kwenye
mlango alipo simama, kwa haraka akamkumbatia,
na kuanza kumwagikwa na machozi jambo lililo
mshangaza raisi Praygod.
“Mume wangu nisamehe”
Rahab alizungumza huku machozi yakimwagika,
raisi Praygod, alizidi kuendelea kushangaa,
kumuona Rahab akiwa amerejea katika hali ya
kawaida. Rahab, hakusita kuanza kuzinyonya lipsi
za mume wake, joto la hisia za kimapenzi likaanza
kupanda katikati yao. Kila mmoja akajikuta akiwa
na hamu ya kupata penzi la mwenzake, ambalo
walilikosa kwa kipindi fulani. Ndani ya dakika
kadhaa wote wawilili wakajikuta wakiwa hawana
nguo katika miili yao.
Kila mmoja alipo hakikisha kwamba amemuandaa
mwenzake vya kutosha, mechi ikaanza, si raisi
wala Rahab aliye onekana kuchoka, kila mmoja
alihakikisha kwamba anampa mwenzake kile kitu
roho inapenda, huku wote wakiwa wamejawa na
furaha mioyoni mwao.
***
Iliwalazimu Black Shadow kuhamishiwa katika
chumba kingine cha siri, kilichopo chini ya ardhi
ndani ya hospitali hiyo. Kazi hiyo ilifanywa na
dokta Ranjiti na wasaidizi wake, usiku huo huo,
baada ya tukio la uvamizi kutokea katika hospitali
yake. Polisi wakatoa tamko kwa watu ambao
walijitokeza kumuombea shujaa huyo, kwamba
warudi majumbani kwao na kuanzia siku hiyo watu
hawata ruhusiwa kuja kujazana katika hospitali
hiyo, hadi pale afya ya Black Shadow itakapo
imarika.
Lilikuwa ni pigo kwa mashabiki wa Black Shadow,
ila hawakuwa na jinsi, ni lazima waweze kutii
tamko hilo la askari. Ulinzi ukazidi kuimarishwa
kwenye hospitali hiyo, hata dhiara ya raisi,
ikakatishwa hadi pale mambo yatakapo kuja kuwa
sawa ndipo raisi aweze kumtembelea mpiganaji
huyo.
Uwepo wa Black Shadow katika chumba cha siri
ulijilukana kwa watu wachache tu akiwemo
Sabogo, ambaye yeye pekee ndiyo alipewa ruhusa
ya kwenda kumuona Black Shadow katika chumba
hicho. Asubuhi na mapema, Sabogo akawa yupo
ndani ya chumba hicho cha siri kilicho jaa taa
nyingi zenye mwanga mweupe.
Sabogo akatoa kinyago kingine kilicho tengenezwa,
kwa ajili ya Black Shadow, akamvua kinyago cha
mwanzo na kumvalishi kingine kipaya lilicho mkaa
vizuri, alipo hakikisha rafiki yake yupo salama,
akatoka ndani ya chumba hicho na kurudi kwa
daktari mkuu wa hospitali bwana Ranjiti.
“Itamchukua muda gani hadi kupata fahamu?”
“Itamchukua kipindi kidogo, ila kutokana bado
tunaendelea kumuangalia kwa usalama mkubwa,
basi tumuombe Mungu, kila jambo litakwenda
sawa”
“Sawa dokta ila hakikisha kwamba hakuna mtu
ambaye atagundua kwamba yupo chumba cha siri”
“Usijali kwa hilo”
Yote yakiwa yanazungumza ndani ya ofisi ya dokta
Ranjiti Phidaya aliweza kuyasikia akiwa nje ya
mlango, moyo wake ulizidi kumsumbua kila alipo
fikiria juu ya donge nono ambalo polisi
walilitangaza kwa mtu ambaye angelisaidia jeshi
hilo kumkamata Eddy.
Phidaya akarudi kwenye ofisi yake akiwa na
mawazo mengi, akilini mwake akaanza kulifikiria
tukio la jana alipo weza kuiona sura ya Black
Shadow, pili akafirikiria jinsi, majambazi walivyo
vamia kwenye hospitali yake, na kutaka kumuua
Black Shadow.
“Ina maana wanamjua kwamab ni Eddy nini?”
Phidaya alizungumza huku akinyanyuka kwenye
kiti chake na kuanza kuzunguka zunguka ndani ya
ofisi yake.
“Ngoja nikamueleze kila kitu mume wangu”
Phidaya alizungumza, kwa haraka akaanza kupiga
hatua hadi mlangoni kwake, akavuta kitasa cha
mlango huo, akaufungua na kuanza kutembea
kuelekea katika ofisi ya mume wake.
***
Baada ya Sabogo kutoka ofisini kwake, dokta
Ranjiti, akawasha Tv yake, moja ya taarifa aliyo
ikuta ni jinsi hospitali yake ilivyo vamiwa. Ila kati
ya majambazi walio kamatwa, mmoja wao
akamstua kidogo. Akajikuta akisimama kabisa na
kwenda kuikodolea macho Tv hiyo. Jina la Shamsa
Eddy, ndio kabisa zikazidi kumpagawisha. Na moja
ya picha ikapita kwenye taarifa hiyo ya habari jinsi
mke wake alivyo mtandika kofi jambazi huyo wa
kike.
‘Mungu wangu siri inakwenda kufichuka’
Dokta Ranjiti alizungumza huku kijasho kikianza
kumpiga na mapigo yake moyo yakizidi kwenda
mbio. Akaanza kujipapasa kuitafuta simu yake ya
mkononi sehemu alipo iweka, kwa bahati nzuri
akaikuta kwenye koti lake, akaichomoa kwa haraka
na kuminya baadhi ya namba kisha akaiweka
sikioni, baada ya muda ikapokelewa upande wa
pili.
“Ehee mkuu habari yako bwana”
‘Salama vipi dokta nikusaidie nini?’
“Naamini hao majambazi walio kuja kuvamia
hospitalini kwangu wapo mikononi mwako”
‘Ndio na wanaendelea kufanyiwa mahojiano, ila
huyu mmoja wa kike hana hatia ndio tumemuachia
mida hii’
“Mungu wangu…….!!!”
‘VVipi kuna tatizo kwani?’
“Aha…ahaaa hapana”
‘Basi kila litakalo kuwa linaendelea nitakujulisha’
“Sawa mkuu”
Dokta Ranjiti baada ya kukata simu alipo maliza
kuzungumza na mkuu wa kituo cha polisi, akili
yake ikaanza kufanya kazi kama compyuta pale
inapo tafuta, majina yaliyo hifadhiwa kwenye
kumbukumbu zake. Kwa haraka mkumbukumbu
zake zikatua kwenye moja ya mtu ambaye kazi
zake ni umafia na huzifanya kazi za matajiri wengi
ndani na nje ya Japani, pasipo kukosea wala
kukamatwa na askari polisi kutokana na
kujibadilisha badilisha sura na yeye huwa mara
nyingi huwa ndio mtu anaye mfanyia upasuaji wa
kumbadilisha sura.
“Ndio Kim upo wapi?’
‘Yokoma, vipi kuna tatizo dokta?’
“Ndio kuna tatizo bwana, kuna binti anaitwa
Shamsa Eddy nahitaji uweze kumuondoa dunia”
‘Amekufanyaje tena dokta?’
“Ni binti ambaye anaitambua siri ya yangu juu ya
mke wangu Phidaya, si unatambua kwamba huyu
Phidaya ni mwanamke niliye mpora waziri mmoja
nchini Tanzania”
‘Yap nalitambua hilo ulisha wahi kuniambia’
“Ndio basi binti huyo ni kati ya wale majambazi
walio kamatwa jana na polisi na yeye anamtambua
vizuri Phidaya kutokana ni mama yake”
Mazungumza ya simu ya dokta Ranjiti yakamfanya
Phidaya kusimama nje ya mlango, aliweza kusikia
kila kitu alicho kizungumza mume wake, ila
hakuweza kusikia mazungumzo na mtu wa pili.
‘Phidaya kutokana ni mama yake’
Maneno hayo yakaanza kujirudia kwa nguvu akilini
mwake, machozi yakaanza kumlanga lenga
Phidaya, hakuona haja ya kuendelea kukaa
mlangoni mwa mume wake kwa haraka akaanza
kutembea kurudi ofisini mwake. Akaufunga mlango
wake kwa ndani, akavuta kiti chake, akawa kama
mtu aliye changanyikiwa mara kadhaa akijiuliza
maswali mengi kuhusiana na kitui alicho kisikia.
“Shamsa Eddy”
‘Ni binti ambaye anaitambua siri yangu juu ya mke
wangu Phidaya’
Phidaya akajikuta akizidi kuyakumbuka maneno ya
mume wake bwana Ranjiti, kiu na hamu ya
kumuona Shamsa, ikaanza kumjaa moyoni mwake,
kwani anatambu ni kati ya majambazi ambao
walikamatwa jana na ni yule aliye mtandika kibao
jana usiku. Kwa haraka Phidaya akavua koti lake
na kuvaa koti la baridi, akajifutamachozi usoni
mwake, wala hakuhitajki tena kuzungumza na
mumewe kwa kitu alicho wahi kukiona. Kwani roho
ya kumchukia mwanume huyo ilianza kumvaa.
Swali ambalo mara kwa mara alijiuliza kichwani
mwake, kwamba yeye ni nani, taratibu alihisi
linaanza kupata jibu.
“Lazima nijijua mimi ni nani”
Phidaya alizungumza peke yake huku akitembea
kwenye kordo ya kuelekea nje ya hospitali.
***
Kwa juhudi za mwana sheria aliye msimamia
Shamsa, kwenye mahojiano kati yake na polisi,
yalizaa matunda, kwani hadi inatimu alfajiri tayari
Shamsa alionekana kwamba hana hatia kutokana
na maelezo yake aliyo yatoa. Uchunguzi ulio
fanywa kwa nesi ambaye aliuawa na Shamsa,
ulionyesha kwamba hakuwa ni nesi wa hospitali
hiyo kutokana na kukutwa na michoro mingi
(tattoo) mwilini mwake.
Pia katika kubanwa kwa waalifu wawili wa kiume
walio kamatwa, walidhibitisha kwamba Shamasa
sio mwenzao, hilo pia lilichangia kwa Shamsa
kuachiliwa huru.
“Inabidi sasa twende nyumbani ukapumzike”
Sa Yoo alizungumza mara baada ya Shamsa
kuachiliwa huru, kwani naye pia alishinda kituoni
hapo kuhakikisha kwamba rafiki yake anaachiwa
huru.
“Hapana nahitaji kwenda hospitali kumuona Black
Shadow ndio niweze kwenda nyumbani’
Kutokana Shamsa ni mtu wa kung’ang’ania
maamuzi yake mwanzo mwisho, Sa Yoo na daktari
hawakuwa na hiyana zaidi ya kuanza safari
kuelekea katika hospitali aliyo lazwa Black
Shadow. Akilini mwa Shamsa hakumfikiria Phidaya
kutoka alihisi labda alimfananisha, isitoshe tayari
walisha mzika mama yeka huyo. Kutokana ni
asubuhi, barabara ilijaa foleni nyingi, kwa hiyo
iliwachukua muda mwingi sana hadi kuweza kufika
katika hospitali hiyo. Wakiwa getini, wakapishana
na gari aina ya Aud A4. Hakuna aliye weza
kuifwatilia sana, haswa Shamsa ambaye muda
wote alimuwaza Black Shadow wake.
Wakaegesha gari walilo jia kwenye maegesho ya
hospitalini hapo, Shamsa akawa wa kwanza
kushuka kwenye gari huku akifwatiwa na Sa Yoo
pamoja na daktari wake.
Kila nesi aliye muona Shamsa, alijikuta
akimuogopa sana, kwani kila mmoja anatambua ni
miongoni mwa majambazi walio sababisha kifo
cha nesi mwezao aliye pigwa risasi jana usiku
akijaribu kuyaokoa maisha yake.
“Daktari mkuu yupo wapi?”
Sa Yoo alimuuliza nesi wa mapokezi, aliye baki
akimtumbulia macho Shamsa asijue ajibu nini.
“Dada nakuuliza daktari mkuu bwana Ranjiti yupo
wapi?”
“Ahahaa ameetoka”
“Una uhakika?”
Shamsa alimuuliza nesi huyo huku akiwa amekazia
jicho.
“Yupo ofisini kwake”
Sa Yoo alijikuta akiangua kicheko, baada ya
kumuona nesi huyo akiwa anababaika babaika,
wote watatu wakamuaga nesi huyo na kuelekea
katika ofisi ya bwana Ranjiti.
***
Gafla Phidaya akajikuta akifunga breki za gari lake,
alihisi kama mtu aliye muona kwenye gari aliyo
pishana nayo getini, hajakosea.
”Ndio yeye”
Alizungumza huku akikunja kona ya haraka na
kunza kurudi hospitalini kwa mwendo wa kasi,
haikumchukua muda tayari akawa amesimama
kwenye geti la kuingilia hospitalini kwake. Askari
wakamfungulia geti hilo kuwa, kwa haraka
akalisimamisha gari lake kwenye maegesho, kisha
akashuka na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea
ndani. Akakuta manesi wa mapokezi wakiwa
wanajadiliana kitu, walipo muona kila mmoja
akajifanya kama anaendelea na kazi zake.
“Kuna nini hapa?”
“Hakuna kitu madam”
“Muna nidanganya eheee?”
“Madama kusema kweli yule jambazi wa kike
amekuja tena, na sasa hivi ameelekea ofisini mwa
mume wako”
“Muna sema kweli?”
“Ndio”
Phidaya akaanza kukimbia kuelekea ofisini mwa
mume wake na kuwaacha manesi hao
wakimshangaa boasi wao, Phidaya bila hata
kubisha hodi akaufungua mlango wa ofisi ya mume
wake, macho yake yakagongana na macho ya
Shamsa, aliye aliye geuka kutazama mtu aliye ingia
ndani ya ofisi ya daktari bila kubisha hodi.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 54 YA SIMUHILI HII.