Sorry madam (Destination of my enemies)

um
Story Za Eddy
SORRY MADAM 71
WRITTER……………………………………….EDDAZARIA
G.MSULWA
www.storyzaeddy.blog.com
UNAWEZA KUJITOLEA KATIKA KUIKUZA KAZI
YANGU HII YA UANDISHI IKIWEMO, KUSAIDIA
UCHAPISHAJI WA KITABU CHANGU CHA MY
MOMMY’S FRIEND SIMI NO 0657072588(Tigo
pesa) AU 0768516188(m-pesa)
ILIPOISHIA
“Nafanya hii, kwa ajili yakulipiza kisasi cha mume
wangu”
“Ngoja kwanza, nipo tayari kufa, ila ninakuomba
usimuue mke wangu”
Nilizungumza kwa ujasiri, nikiwa nipo tayari kwa
kufa, Madam Mery akalinyanyua panga lake juu,
akalishusha kwa kasi kwenye mkono wangu wa
kulia
ENDELEA
Nikatoa ukulele mkali, ulio mfanya madam Mery
kusitisha zoezi lake kuukata mkono wangu, panga
lake likiwa limesimama sentimita chache kutoka
ulipo mkono wangu
“Madam, ninakuomba unisamee”
Nilizungumza huku machozi yakiendelea
kunimwagika usoni mwangu, madam Mery
akanitazama kwa macho ya hasira yaliyo jaa ukatili
mkubwa, akawatazama Victoria na John ambao
macho yao yote yalikuwa kwetu
“Natambua kwamba mimi nimkosaji sana kwako,
ninastahili kufa mbele yako, ila si mbele ya macho
ya mke wangu.Mtazame jinsi alivyo katika hali
yake.Mule ndani amebeba kiumbe kama ulicho
kuwa umekibeba wewe, miezi tisa, na Derick
akakiangamiza mbele yetu.Yule ni mwanamke
mwenzako ambaye anauchungu kama wewe”
Nilizungumza huku machozi yakiendelea
kunimwagilka usoni mwangu, madam Mery kwa
mbali machozi yakaanza kumlenga lenga, macho
yake yamebadilika rangi na kuwa mekundu kiasi
huku sura yake ikiwa imejaa mikunjo kwenye paji
lake la uso akinitazama kwa uchungu sana
“Mery mimi pia ni binadamu, kumbuka ni mambo
mangapi tuliyafanya tukiwa pamoja, vuta
kumbukumbu ni vitu vingapi tulishiriki tukiwa
pamoja, Eheeee, leo hii unataka kuimwaga damu
yangu, leo hii unataka kunisulubu kikatili, le……..”
“Eddy STOP TALKING”(Eddy nyamaza kuzungumza)
Madam Merry alizungumza kwa sauti ya juu, yenye
uchungu ndani yake.Akalitupa chini panga lake
alilokuwa amelishika.Machozi mengi yakaanza
kumbubujika usoni mwake, John na Vivtoria
wakabaki wakimtazama madam Mery, ambaye
taratibu alianza kupiga hatua za kuelekea kwenye
gari lake alilo kuja nalo
“Madam Vipi?”
John alizungumza huku akimwafwata madam Mery
kwa nyuma
“John ninakuomba uniache”
Madam Mery aluzungumza huku akiunyanyua
mkono wake mmoja akimzuia John asimfwae
anapo elekea
“Ila madam haya sio makubaliano yetu”
“John sipo sawa nimekuambia usinifwate”
Madam Mery alizungumza kwa sauti ya ukali, huku
machozi yakiendelea kumchuruzika usoni mwake.
“Sasa Madam tumfanye nini Eddy?”
Madam Mery akageuka kwa hasira, hadi John
akastuka kidogo, akanitazama jinsi machozi
yanavyo nimwagika, akayafumba macho yake kwa
sekunde kadhaa, akionekana akifikiria kitu cha
kufanya juu yangu.
“Kesho nimkute akiwa hai”
Madam Mery alizungumza kwa sauti ya upole,
kisha akaelekea lilipo gari lake, akafunguliwa
mlango na mlinzi wake, akaingia ndani ya gari na
wakaondoka zao.John akalisindikiza magari ya
Madam Merry yanayotoka kwenye geti kubwa la
Godauni, lilipo fungwa taratibu John akanigeukia,
akanitazama kwa macho ya dharau huku Victoria
akiwa amejichokea, kwani ninaamini mipango yao
waliyo kuwa wameipanga dhidi yangu
imeharibika.John akamfwata Victoria sehemu alipo
simama, wakanong’onezana kwa muda kisha
wakamtama Phidaya ambaye muda wote, amejilaza
chini huku machozi yakimwagika kwa uchungu
“Mchukueni huyo Malaya mumrudishe mulipo
mtoa”
John aliwaamrisha watu wake, wakamnyanyua
Phidaya na kumbeba juu juu, japo anajitahidi
kujitoa mikononi mwa watu walio mbeba, huku
aikiliita jina langu kwa sauyti ya juu, ila
hakuifanikiwa kujitoa mikononi mwao
John akapiga hatua hadi katika sehemu nilipo
fungwa, akanitazama kwa muda, huku macho yake
yakiwa yamejaa dharau kubwa, akanitemea mate ya
usoni, akiyasindikiza kwa kofi zito lililo tua kwenye
shavu langu la kushoto
“Mmmmmm Eddy, unajisikiaje?”
John alizungumza huku akivifikisha viganja vyake,
na kuvipuliza taratibu taratibu.Akanishika sikio
langu la upande wakulia, akaanza kulivuta kwa
nguvu zake zote, nikaendelea kuugulia maumivu
ndani kwa ndani, sikutoa sauti yoyote kwenye
kinjwa changu
“Waooo, unajifanya komandoo usikii maumivu
eheeee?”
John alizungumza, huku akiliachia sikio
langu.Akaanza kunitandika vibao mfululizo kwenye
mashavu yangu, hasira ikazidi kumiliki nafisi
yangu.
“John, tumpeleke kisimani, hapo unajisumbua
bure”
Victori alitoa wazo ambalo John alilikubali,
wafanyakazi wao wakanishusha kwenye meza,
majamaa wawili wakanibeba kwenye mabega yao.
kama wawindaji walio beba swala waliye muua
kwenye mawindo yao.Tukaingia kwenye moja ya
ukumbi mkubwa wenye mwanga hafifu, unao pita
kwa kutumia madirisha machache yaliyopo juu
yake.Wakanibwaga chini, na kunifanya nitoe
mguno wa maumivu kutokana na kujiumiza
sehemu ya paja langu, nililo pigwa risasi
Taa kubwa zenye rangi nyeupe zikawaka na
kulifanya eneo zima la ikumbu kuponekana vizuri,
kuna mashimo makubwa mawili, kwa haraka
nikatabua ndio hivyo visima wanavyo vizungumzia,
mabaunsa walio kuwa wamenibeba, wakaufunga
mwili wangu kwa kamba ngumu aina ya manila.
“Eddy utakufa kifo kibaya sana”
John alizungumza huku akiwa ameniinamia
“Usiombe nikatoka, kwenye mikono yeno, utajuta”
Nilizungumza kwa kujiamini sana, John akaanza
kucheka kwa dharau, huku akinipiga piga
mashavuni mwangu
“Eddy huwezi kutoka mikononi mwangu, nakujua
wewe vizuri sana.Huwezi fanya chochote dhidi
yangu.Muda wako umekwisha kaka”
“Angalia wakwako ndio utakuwa umekwisha”
John akaanza kunipiga mateke mfululizo kwenye
mbavu zangu, nikaendelea kutoa sauti ya maumivu
ila John hakunionea huruma zaidi ya kuendelea
kunipiga kwa nguvu zake zote
“Mchukueni na mukamdumbukize kwenye kisima”
John aliwaamrisha watu wake, wakanibeba, kabla
hawajaondoka na mimi, Victoria akawazuia.Akapi
ga hatua hadi sehemu tulipo simama
“Eddy nakupenda kaka yangu, kwaheri”
Victoria alizungumza huku akinibusu shavuni
mwangu, akawarusuhu watu kuonipeleka kwenye
kisima kilichopo kwenye huu ukumbi, kwa jinsi
walivyo nifunga kamba mwili wangu sikuweza
kufanya kitu cha aina yoyote zaidia ya mwili wangu
kunyooka moja kwa moja, mithili ya mtu aliye fariki
dunia.Wakanifunga kwenye kamba nene, tartibu
wakaanza kunishusha kwenda chini, taratibu.Giza
jingi lililo tawala ndani ya shimo hili, likazidi
kuniogopesha na kunifanya nizidi kuchanganyikiwa
.Nikastuykia nikigusa chini, kwenye shimo hili
lenye futi zaida kumi na mbili.
Gafla nikaanza kuhisi vitu vidogo vidogo
vikinitambalia mwilini mwangu, nikastukia mwili
wangu ukianza kupata maumivu maklali yaliyo
tokana kung’atwa na wadudu wadogo ambao
sikujua ni waduudu wa aina gani, jambo lililo
nifanya nitoe ukelele mkali sana
ITAENDELEA
umechanganya mafaili
 
Habari Wana jf
Nilikuwa nimenyuti siku 2 hizi nikiwa nasoma hadithi ya "SORRY MADAM"
Hadithi ni tamu sana ile hongera zako mtunzi
Mimi ni mpenzi mkubwa Wa hizi story za kusisimua na machombezo ya kila aina Naomba mnitajie blogs ambazo naweza kuingia na kusoma hizo hadithi
Samahani kwa usumbufu
 
Ubuyu blog story ya sorry madam orijino ipo huko saiv ipo part two

Ila namlaumu sana huyu anayeiiba hii story na kuileta huku sio vizur anavyofanya kapunguza sana moral ya mtunzi,zaman kwa wiki alikua anaweka mara mbili au tatu siku hizi anaweka mara moja tu.

Kuna blog nyingine ya hadithi na akilimani ipo vizuri.
 
Ubuyu blog story ya sorry madam orijino ipo huko saiv ipo part two

Ila namlaumu sana huyu anayeiiba hii story na kuileta huku sio vizur anavyofanya kapunguza sana moral ya mtunzi,zaman kwa wiki alikua anaweka mara mbili au tatu siku hizi anaweka mara moja tu.

Kuna blog nyingine ya hadithi na akilimani ipo vizuri.
Asante mkuu ngoja nitembelee nikafaidi uhondo
 
Back
Top Bottom