Rais Samia asijikite kutumbua Wakuu wa Mikoa na Wilaya pekee. Amulike ufisadi unaofanywa na Mawaziri wake

6 Pack

JF-Expert Member
Apr 17, 2022
1,826
4,074
Niaje waungwana,

Kiukweli mimi sio mwanasiasa, wala mfuatiliaji wa mambo ya siasa hapa JF. Hivyo nimesukumwa tu na uzalendo wangu mwenyewe kuandika haya niliyoandika. Kwa kawaida nchi yetu ina mawaziri zaidi ya ishirini na manaibu wake (hapo sijazungumzia makatibu wakuu na manaibu). Kikawaida na kikatiba kila Waziri ana wizara yake, na lengo la kuteuliwa kwake ni kuisaidia nchi na wananchi kulingana na kanuni na muongozo wa wizara husika.

Sasa cha kushangaza Mawaziri wengi wamekuwa hawafanyi lolote la maana kuisaidia nchi wala wananchi. Unakuta nchi ina wizara mbalimbali, lakini yanayofanyika ndani ya nchi utafikiri labda Raisi bado hajaunda baraza la mawaziri. Wananchi wapo wanaona, bunge lipo linaona na raisi ambae ndio mkuu wa nchi yupo anaona lakini hakuna hatua yoyote anayochukua kuhusiana na uzembe wa baraza lake la mawaziri.

Ufisadi umetamalaki katika wizara nyingi, utendaji wa kazi wa mawaziri hao umekuwa mbovu, wa kusua sua na wa kukatisha tamaa wananchi, miradi mingi ya maendeleo inakwamishwa na wizara hizo, lakini mamlaka ya juu wote kimya wanaangalia tu mambo yanavyokwenda shagala bagala kama vile nchi haina raisi wala viongozi wanaoweza kutoa muongozo kwa mawaziri hao.

Sasa pamoja na uozo wote huo, tunashangaa raisi amekuwa akitumia uozo huo wa Mawaziri wake kuwaadhibu wakuu wa mikoa na wilaya. Hakuna siku tuliwahi kuona raisi anaadhibu mawaziri fulan kwa uzembe, ufujaji wa fedha za serikali, ufisadi nk. Kila siku yeye ana deal na wakuu wa mikoa na watendaji wengine wa chini ambao hawana tija yoyote katika nchi.

Kwangu mimi ukimtoa waziri Dkt Dorothy Gwajima, Silaa na Jafo yule wa enzi za "Tamisemi", waliobakia wote ni mizigo inayotafuna kodi zetu bila kufanya kazi yoyote ya maana katika ofisi zao.

Ushauri ni kwamba raisi asiwe busy tu kuangalia makosa ya wakuu wa mikoa na wilaya bali awe anafuatilia pia na yale yanayofanyika katika baraza lake la mawaziri lililojaa wachumia tumbo wengi uongozini.

Usiku mwema.
 
Niaje waungwana,

Kiukweli mimi sio mwanasiasa, wala mfuatiliaji wa mambo ya siasa hapa JF. Hivyo nimesukumwa tu na uzalendo wangu mwenyewe kuandika haya niliyoandika. Kwa kawaida nchi yetu ina mawaziri zaidi ya ishirini na manaibu wake (hapo sijazungumzia makatibu wakuu na manaibu). Kikawaida na kikatiba kila Waziri ana wizara yake, na lengo la kuteuliwa kwake ni kuisaidia nchi na wananchi kulingana na kanuni na muongozo wa wizara husika.

Sasa cha kushangaza Mawaziri wengi wamekuwa hawafanyi lolote la maana kuisaidia nchi wala wananchi. Unakuta nchi ina wizara mbalimbali, lakini yanayofanyika ndani ya nchi utafikiri labda Raisi bado hajaunda baraza la mawaziri. Wananchi wapo wanaona, bunge lipo linaona na raisi ambae ndio mkuu wa nchi yupo anaona lakini hakuna hatua yoyote anayochukua kuhusiana na uzembe wa baraza lake la mawaziri.

Ufisadi umetamalaki katika wizara nyingi, utendaji wa kazi wa mawaziri hao umekuwa mbovu, wa kusua sua na wa kukatisha tamaa wananchi, miradi mingi ya maendeleo inakwamishwa na wizara hizo, lakini mamlaka ya juu wote kimya wanaangalia tu mambo yanavyokwenda shagala bagala kama vile nchi haina raisi wala viongozi wanaoweza kutoa muongozo kwa mawaziri hao.

Sasa pamoja na uozo wote huo, tunashangaa raisi amekuwa akitumia uozo huo wa Mawaziri wake kuwaadhibu wakuu wa mikoa na wilaya. Hakuna siku tuliwahi kuona raisi anaadhibu mawaziri fulan kwa uzembe, ufujaji wa fedha za serikali, ufisadi nk. Kila siku yeye ana deal na wakuu wa mikoa na watendaji wengine wa chini ambao hawana tija yoyote katika nchi.

Kwangu mimi ukimtoa waziri Dkt Dorothy Gwajima, Silaa na Jafo yule wa enzi za "Tamisemi", waliobakia wote ni mizigo inayotafuna kodi zetu bila kufanya kazi yoyote ya maana katika ofisi zao.

Ushauri ni kwamba raisi asiwe busy tu kuangalia makosa ya wakuu wa mikoa na wilaya bali awe anafuatilia pia na yale yanayofanyika katika baraza lake la mawaziri lililojaa wachumia tumbo wengi uongozini.

Usiku mwema.
Mfano hai wa ufisadi huo ni upi ili tusipoteze muda?
 
Hapo ndipo udhaifu wa wazi wa Samia unapodhihirika, amejisahau kabisa kuwakumbatia mawaziri ambao dhahiri wanaonekana kushindwa kazi, mfano wa hivi karibuni Bashe na mradi wake wa BBT, yule ameshindwa kazi, amepoteza pesa za walipa kodi, ajabu bado yuko ofisini.
 
Kashfa nzito sana hii yaan hadi Angelina Mabula nae Jenista Muhagama wote ni Mizigo?

Nje ya mada

Nilipomsikiliza Daktari akasema kwamba ukifanya mazoezi muda mrefu mfano masaa matatu mfululizo unafanya tu mazoezi unaua Figo unaua Moyo unaua ini unaua kibofu cha mkojo, sitaki tena kusikia mazoezi
 
Niaje waungwana,

Kiukweli mimi sio mwanasiasa, wala mfuatiliaji wa mambo ya siasa hapa JF. Hivyo nimesukumwa tu na uzalendo wangu mwenyewe kuandika haya niliyoandika. Kwa kawaida nchi yetu ina mawaziri zaidi ya ishirini na manaibu wake (hapo sijazungumzia makatibu wakuu na manaibu). Kikawaida na kikatiba kila Waziri ana wizara yake, na lengo la kuteuliwa kwake ni kuisaidia nchi na wananchi kulingana na kanuni na muongozo wa wizara husika.

Sasa cha kushangaza Mawaziri wengi wamekuwa hawafanyi lolote la maana kuisaidia nchi wala wananchi. Unakuta nchi ina wizara mbalimbali, lakini yanayofanyika ndani ya nchi utafikiri labda Raisi bado hajaunda baraza la mawaziri. Wananchi wapo wanaona, bunge lipo linaona na raisi ambae ndio mkuu wa nchi yupo anaona lakini hakuna hatua yoyote anayochukua kuhusiana na uzembe wa baraza lake la mawaziri.

Ufisadi umetamalaki katika wizara nyingi, utendaji wa kazi wa mawaziri hao umekuwa mbovu, wa kusua sua na wa kukatisha tamaa wananchi, miradi mingi ya maendeleo inakwamishwa na wizara hizo, lakini mamlaka ya juu wote kimya wanaangalia tu mambo yanavyokwenda shagala bagala kama vile nchi haina raisi wala viongozi wanaoweza kutoa muongozo kwa mawaziri hao.

Sasa pamoja na uozo wote huo, tunashangaa raisi amekuwa akitumia uozo huo wa Mawaziri wake kuwaadhibu wakuu wa mikoa na wilaya. Hakuna siku tuliwahi kuona raisi anaadhibu mawaziri fulan kwa uzembe, ufujaji wa fedha za serikali, ufisadi nk. Kila siku yeye ana deal na wakuu wa mikoa na watendaji wengine wa chini ambao hawana tija yoyote katika nchi.

Kwangu mimi ukimtoa waziri Dkt Dorothy Gwajima, Silaa na Jafo yule wa enzi za "Tamisemi", waliobakia wote ni mizigo inayotafuna kodi zetu bila kufanya kazi yoyote ya maana katika ofisi zao.

Ushauri ni kwamba raisi asiwe busy tu kuangalia makosa ya wakuu wa mikoa na wilaya bali awe anafuatilia pia na yale yanayofanyika katika baraza lake la mawaziri lililojaa wachumia tumbo wengi uongozini.

Usiku mwema.

View: https://www.instagram.com/reel/C40DpZ6s8Ya/?igsh=M2RxMDBleDRvNnhu

Mwisho Mawaziri sio watendaji mfano anachofanya Jerry Silaa ni kama maigizo ya Kisiasa anatakiwa ahakilishe system inafanya kazi.

Ataweza kwenda Kila mtaa na Kijiji na Kwa Kila mtu mwenye Mgogoro wa Ardhi? Hao watu Walioajiriwa huko kuanzia ngazi ya Wilaya Wana fanya kazi gani?

Ni kufukuza hao watendaji kama Aweso alivyowafanya Mainjinia wa Maji na Sasa hakuna miradi hewa na maji yanatoka.
 
Hapo ndipo udhaifu wa wazi wa Samia unapodhihirika, amejisahau kabisa kuwakumbatia mawaziri ambao dhahiri wanaonekana kushindwa kazi, mfano wa hivi karibuni Bashe na mradi wake wa BBT, yule ameshindwa kazi, amepoteza pesa za walipa kodi, ajabu bado yuko ofisini.
Katika mawaziri ambao walishindwa toka mwanzo wa kuteuliwa kwao. Basi Bashe ni mmoja wao, lakini anaachwa tu mpaka leo, hasira zinaishia kwa wakuu wa wilaya ambao hawajui hili wala lile.
 
Nitofautiane na hoja yako mkuu,kati ya waziri mchapa kazi Mchengerwa ni wa mfano,acha chuki brother
Mchengerwa ni miongoni mwa wachapa kazi wachache, ila waliobakia wanazurura na hakuna wanachofanywa.
 
Kashfa nzito sana hii yaan hadi Angelina Mabula nae Jenista Muhagama wote ni Mizigo?

Nje ya mada

Nilipomsikiliza Daktari akasema kwamba ukifanya mazoezi muda mrefu mfano masaa matatu mfululizo unafanya tu mazoezi unaua Figo unaua Moyo unaua ini unaua kibofu cha mkojo, sitaki tena kusikia mazoezi
Fanya mazoezi mepesi mepesi tu ili kujenga afya yako. Ukizidisha basi ujue ni hasara kwako.
 

View: https://www.instagram.com/reel/C40DpZ6s8Ya/?igsh=M2RxMDBleDRvNnhu

Mwisho Mawaziri sio watendaji mfano anachofanya Jerry Silaa ni kama maigizo ya Kisiasa anatakiwa ahakilishe system inafanya kazi.

Ataweza kwenda Kila mtaa na Kijiji na Kwa Kila mtu mwenye Mgogoro wa Ardhi? Hao watu Walioajiriwa huko kuanzia ngazi ya Wilaya Wana fanya kazi gani?

Ni kufukuza hao watendaji kama Aweso alivyowafanya Mainjinia wa Maji na Sasa hakuna miradi hewa na maji yanatoka.
 
Back
Top Bottom