Sorry madam (Destination of my enemies)

SORRY MADAM (17)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
. Akiwa gorofa ya kwanza kwenda gorofa ya pili,
akakutana na askari wawili wakishiuka chini,
akaishusha kofia yake chini kidogo, akapisha na
askari hao wakimtazama.
“Ngoja kwanza”
Askari mmoja alizungumza baada ya kushuka
ngazi sita kwenda chini, akatoa picha iliyopo
mfukoni mwake.
“Ndio huyu tunaye mtafuta”
Askari mmoja alizungumza na kuanza kupandisha
kwenda ngazi za juu huku akikimbia, kwa bahati
nzuri akafanikiwa kumuona mzee Godwin
akitembea kwenye moja ya kordo.
“Simama polisii”
Askari huyo alizungumza huku bunduki yake akiwa
amemnyooshea mzee Godwin kwa nyuma.
ENDELEA
“Nyoosha mikono yako juu”
Watu walio karibu na eneo alipo simama Mzee
Godwin pamoja na askari hao walipo nyuma yake
mita chache kutoka sehemu alipo, wakabaki
wakishangaa tukio hilo kwani hawakujua ni kwanini
askari hao wamemshikia mtutu mtu huyo. Taratibu
Mzee Godwin akanyoosha mikono yake juu, huku
akiwa bado hajageuka kuwatazama askari hao.
Askari mmoja akamkonyeza mwenzake amfwate
mzee Godwin, kwenda kumfunga piungu.
Kwa umakini mkubwa askari huyo akaanza
kutembea kwa kunyata huku bunduki yake aina ya
SMG akiwa ameishika vizuri mikononi mwake.
Kitendo cha kumfikia Mzee Godwin, ikawa ni moja
ya kosa kubwa sana, mzee Godwin akageuka na
teke la mguu wa kustoto, lililo mchota askari huyo
miguu yake na kujikuta akianguka kama mzingo na
bunduki yake akiitupia pembeni, kwa uharaka wa
hali ya juu, mzee Godwin, akaichomoa bastola
yake iliyo ichomeka kiunoni mwake kwa nyuma.
Hakuhitaji hata kuwa na huruma na askari aliye
mshikia bunduki, akibabaika. Akapimga risasi moja
ya paja askari huyo, akaanguka huku akilia kwa
uchungu na maumivu makali sana.
Mlio wa bastola yake ukawafanya watu
kutawanyika, si madaktari wala wagonjwa walio
jiweza, kila mmoja akaikoa roho yake, hata
kushangaa kwao kukaingia doa. Askari wengine
walio kuwa kwenye maeneo tofauti ya hospitali,
baada ya kusikia mlio huo wakakimbilia katika
jengo hilo la maabara.
Askari aliye anguka chini, baada ya kuona
mwenzie ametandikwa risasi ya paja na
anaendelea kuhangaika hangaika chini, huku akilia,
akajaribu kurusha teke la chini, ambalo
lilimuangusha mzee Godwin. Askari huyo
akanyenyuka, huku akikunja ngumi, mzee Godwin
akasimama huku akitabasamu, kwani akimuangalia
askari huyo, umri wake wapata miaka ishirini na
tatu hadi tano.
Askari akaanza kurusha ngumi zake, zilizo mkosa
Mzee Godwin, kwani aliweza kuzikwepa zote huku
akiendelea kumuonea huruma kijana huyo. Mzee
Godwin akakimbia kwa kasi, askari huyo akanzanza
kumfukuza, mzee Godwin akafika hadi karibu ya
ukuta, kwa uwezo mkubwa alio kuwa nao
akakanyaga ukutani, na kujigeuza kwa kasi, askari
huyo akakutana na teke zito la kichwa lililo
muangusha chini, na kupoteza fahamu hapo hapo.
“Nice job, kijana”
Mzee Godwin alizungumza huku akijiweka sawa
koti lake. Akiwa katika kordo hiyo, askari mmoja
akajitokeza akiwa na bunduki. Askari akaanza
kufyatua risasi kwa mawenge yaliyo muingia baada
ya kumuona wezake wakiwa wamelala chini,
mmoja akiwa ametulia kimya na mwengine
akiendelea kulia huku damu nyingi zikiwa
zimesambaa kwenye sakafu.
Mzee Godwin, akauvamila mlango ulipo mbele
yake, na kuingia ndani ya chumba hicho, alicho
wakuta madaktari wawili wakiwa wamelala chini ya
meza kwa woga. Mzee Godwin akaufunga mlango
kwa ndani kisha akaichomoa bastola yake.
“Simameni”
Aliwaamrisha askari hao, wakatoka chini ya meza
huku kila mmoja akionekana kuwa ni muoga
kupindukia, kwani haja ndogo ilianza kuitotesha
suruali yake.
“Vueni nguo haraka”
Kila walicho ambiwa ndicho ambacho madaktari
hao waliweza kukifanya, Mzee Godwin naye
akaanza kuvua nguo zake na kubakiwa na nguo za
ndani.
“Wewe kikojozi vaa hizi”
Akamrushia daktari nguo zake, kisha yeye
akachukua nguo za daktari mwengine. Alipo maliza
kuvaa mavazi hayo ya kidaktari pamoja na miwani,
akamuamrisha daktari huyo kuvaa, kofia yake aliyo
kuwa ameivaa.
Gari za polisi wa vikosi vya kutuliza ghasia F.F.U,
zikazidi kuongezeka katika hospitali ya muhimbili,
hii ni baada ya kupata habari kwamba, gaidi Mzee
Godwin ameweza kuonekana katika hospitali hiyo
na kuwashambulia askari wawili. Wananchi walipo
katika eneo la hospitali wakawekwa chini ya ulinzi
mkali, hapakuwa na aliye ruhusiwa kuingia ndani
ya hospitali, wala aliye ndani ya hospitali
hakuruhusiwa kuweza kutoka nje. Hii yote ni
kuhakikisha gaidi wao hajichanganyi na wananchi
na kuweza kutoweka katika eneo la hospitali.
***
Nguvu na umahiri wa kikosi cha bwana Rusev
kikazidi kuongezeka siku hadi siku, akazidi
kuchukua vijana mbali mbali katika mataifa ya
kiafrika, akawaingiza katika kikosi chake ili
kuhakikisha mipango yake anayo ipanga
inakwenda vizuri sana.
“Muheshimiwa mipango yako ni nini?”
Mshauri wake wa karibu alimuuliza bwana Rusev
mara baada ya vijana zaidi ya ishirini kutoka nchi
ya Afrika kuweza kuingizwa kwenye kambi yake,
iliyopo chini ya bahari.
“Nahitaji kuifanya dunia nzima kuwa na kiongozi
mmoja tu, ambaye ni mimi”
“Ila muheshimiwa itawezekana kweli, kutokana
mataifa mengi yana nguvu sana”
“Kwa ukimya ambao tumeufanya tangu kifo cha
Pual Hennry Jr, sasa ninakwenda kuitingisha dunia.
Nahitaji ndoto za Adolf Hitler niweze kuzitimiza
mimi”
Bwana Rusev alizungumza huku akitabasamu.
Akiendelea kuwaangalia vijana hao, wakinza
kupatiwa mafunzo maalumu katika ngome yake,
ambayo ni ngumu sana kwa mtu kuweza
kuifahamu.
Simu ya mshauri wake, ikaingia ujumbe wa video
ulio mstua sana, ikabidi amuonyeshe bosi wake
bwana Rusev.
“RUSEV, RUSEV RUSEV, Umenimiss eheee”
Sauti na sura ya Jaquline, vinaoenekana kwenye
simu hiyo. Bwana Rusev akajikuta akiitumbulia
macho video hiyo aliyo tumwa na muda mchache
ulio pita.
“Huyu Malaya yupo hai?”
Bwana Rusev alizungumza kwa hasira huku
akiendelea kuitazama video hiyo.
“Najua utashangaa, kuniona nipo hai.
Hahahaaaaaa, ngoja niende kwenye point muhimu.
Niliapa kwamba nilazima nitakuua, na hii ni moja
ya ahadi nitakayo ifanya siku na muda wowote.”
“Ila kabla ya kufanya hivyo kutana na mgeni rafiki
yako mpendwa”
Video hiyo ikasogezwa pembeni, ambapo bwana
Rusev akaiona sura ya Agnes akitabasamu.
“Umewaacha wezangu wamekwenda jela kwa ajili
yako, sasa tambua kazi ni moja tu. Tutakupeleka
kuzimu mw………”
Bwana Rusev kwa hasira akaizima video hiyo ya
vitisho kutoka kwa mabinti ambao anawatambua
vizuri sana.
“Muheshimiwa ut…..”
Bwana Rusev akamtandika ngumi nzito mshauri
wake huyo, kisha akaondoka kwa hasira na
kuwafanya baadhiya askari wake kushangaa tukio
hilo.
***
Mzee Godwin kuchungulia dirishani, akaona askari
wengi wakiwa wamemiminika katika eneo la
hospitalini, wakiwa na silaha nzito pamoja na
mbwa wakali.
“Shitii”
Mzee Godwin alizungumza huku akijikuna kichwa
chake
“Shika meza huko”
Aliwaamuru madkatari hao kuisukumia meza hiyo
kubwa kwenye mlango, kwani alihisi muda wowote
mlango unaweza kuvunjwa na askari walipo nje.
“Laleni chini”
Mzee Godwin aliendelea kuwaamrisha madaktari
hao walio tii, kwani pasipo kuweza kufanya hivyo
wanaweza kupoteza maisha yao. Katika
kukichunguza chumba, kwa bahati nzuri akaona
sehemu ya juu kuna sehemu inaweza kufunguka.
“Mukinyanya kichwa tu, ninawapasua ubongo”
Mzee Godwin alizungumza huku akipanda juu ya
meza hiyo, akiendelea kutafuta ni jinsi gani
anaweza kuifungua sehemu hiyo yenye mfuniko
mgumu kiasi. Kwa bahati nzuri akafanikiwa
kufungua mfuniko huo, akachungulia juu ya dari,
akakuta uwazi mkubwa ambao unaweza
kumruhusu yeye kuweza kupita pasipo wasiwasi.
“Hivi ni kwanini tusivunje mlango?”
Askari mmoja alishauri, wezake kwani ni muda
umekatika wamekaa nje ya mlango huo
wakishikilizia kitu kinacho endela ndani.
“Humo ndani kuna madaktari tukifanya hivyo
tunaweza kuwapelekea wakauliwa
“Ila mkuu tutaendela kukaa hapa hadi saa ngapi?”
Hapakuwa na jibu lolote alilo litoa mkuu wao huyo,
anaye hofia maisha ya madaktari hao.
Mzee Godwin akaendelea kufwata njia hiyo iliyopo
juu ya dari, akafanikiwa kufika kwenye moja ya
sehemu yenye upenyo mdogo, akatizama chini na
kugundua ni chumba cha kuhifadhia vitu vya
maabara, akapatizama hapakwa na mtu wa aina
yoyote, Kwa kutumia vidole yake akavingiiza
kwenye matundu madogo ya mfuniko huo kisha
akaufungua, na kuusogeza pembeni. Akashusha
kichwa taratibu na kuchungulia chini, alipo
hakikisha kwamba hakuna mtu yoyote, taratibu
akashuka chini, kimya kimya pasipo kutoa
kishindo cha aina yoyote.
“Shitiii pesa zangu?”
Mzee Godwin akajilaumu sana, kwani kiasi kikubwa
cha pesa amekiacha kwenye koti alilo mvalisha
daktari aliye kuwa akijikojolea kwa woga. Hakuwa
na jinsi tena ya kuweza kurudi katika enoeo hilo,
akachungulia dirishani akakuta eneo hilo lipo kinya,
ila kuna umbali wa gorofa moja chini.
“Hapa nashuka”
Mzee Godwin alijisemea kimoyo moyo, taratibu
akaanza kushuka, kwenye ukuta huo, wenye
vishikizo vidogo vidogo. Akafanikiwa kufika chini.
Sehemu aliyo simama imezungukwa na maua
maua mengi. Akanyata taratibu hadi kwenye
sehemu ya lango la gorofa hilo, akakuta askari
wengi wakiwa wanaendeleza ulinzi.
Akaachana na askari hao, na kuanza kutembele
kuelekea kwenye upande wa jengo la kuhifadhia
damu, akafanikiwa kufika nyuma ya jengo hilo
pasipo kuweza kustukiwa. Akiwa katika
kuchungulai chungulia, akastukia akishikwa bega
kwa nyuma
“Dokta unafany……..”
Baada ya kutazamana na mtu anaye msemesha,
askari huyo akanyamaza gafla, baada ya kugundua
huyo anaye muita daktrai ni gaidi. Mzee Godwin
kwa haraka sana, akaizungusha kwa nguvu shingo
ya askari huyo aliye mtumbulia macho na
kuivunja. Kwa haraka akamvua mavazi askari huyo
na kuchukua nguo zake. Alipo maliza kuvaa nguo
za askari huyo, pamoja na kofia lake aina ya
helment. Akaanza kutembea kuelekea getini kwa
kujiamini sana.
“Vipi unaelekea wapi?’
Askari mmoja alimuuliza baada ya kumuona
akihitaji kufungua mlango wa gari hilo.
“Nahitaji kwenda kuchukua askari wengine”
Mzee Godwin alizungumza huku akibadilisha sauti
yake, kutokana huyo aliye muuliza anacheo
kikubwa zaidi ya mavazi aliyo yavaa, ikambidi awe
mpole kidogo kusikilizia jibu la mkubwa wake
huyo, anaye onekena kuchanganykiwa kidogo.
“Nipeleke kwa waziri wa ulinzi”
“Wapi nyumbani kwake?”
“Ndio muheshimiwa ameniiita”
Mzee Godwin akatii, wakaingia kwenye gari hilo
aina ya ‘Landrove defender’ na kuondoka katika
eneo hilo la hospitalini pasipo hata kustukiwa na
askari yoyote, hata aliiye mpakiza hakuweza
kumtambua.
Kutokana na king’ora alicho kiwasha, magari
mengi barabarani yaliwapisha. Haikuwachukua
muda mwingi sana wakafanikiwa kufika katika
jumba la waziri Eddy, mkuu huyo wa polisi
akashuka na kuelekea katika moja ya hema walilo
kaa viongozi wakubwa. Eddy taratibu akiwa
anatoka sebleni kwake pamoja na Rahab. Macho
yake akaitazama gari ya polisi iliyo fika muda si
mrefu. Askari huyo ambaye ni mzee Godwin
aliyomo ndani ya gari hiyo, alipo yageuza macho
yake kutazama nje yakakutana na Eddy stuka na
kuanza kumtilia mashaka.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 18 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (18)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
. Haikuwachukua muda mwingi sana wakafanikiwa
kufika katika jumba la waziri Eddy, mkuu huyo wa
polisi akashuka na kuelekea katika moja ya hema
walilo kaa viongozi wakubwa. Eddy taratibu akiwa
anatoka sebleni kwake pamoja na Rahab. Macho
yake akaitazama gari ya polisi iliyo fika muda si
mrefu. Askari huyo ambaye ni mzee Godwin
aliyomo ndani ya gari hiyo, alipo yageuza macho
yake kutazama nje yakakutana na Eddy aliye stuka
na kuanza kumtilia mashaka.
ENDELEA
Wakiwa katika mtazamano huo, ambao mzee
Godwin hakuhitaji kuweza kuyakwepesha macho
yake, kumtazama Eddy ili asistukiwe. Ving’ora vya
gari za polisi vikaingia ndani ya jumba hilo huku
nyuma kukifwatiwa na msafara mkubwa wa magari
yapatayo nane, ikiashiria raisi anaingia katika
eneohilo.
“Sogeza gari yako pembeni?”
Askari mmoja alimuamuru Mzee Godwin pasipo
kujua ni gaidi wanaye mtafuta. Mzee Godwin
akawasha gari na kuisogeza pembeni na kuzipa
nafasi gari zinazo ingia kukaa ktika eneo ambalo
alikuwa amelisimamisha gari la polisi.
Eddy hakuwa na haja ya kuendelea kumtazama
askari huyo, akiamini kwamba atakuwa
amemfananisha kutokana na mawenge ya
kumfikiria sana mzee Godwin. Akajumuika pamoja
na Rahab kumpokea muheshimiwa Raisi bwan
Praygod Makuya. Moja kwa moja wakaelekea
kwenye mahema ambayo, wapo viongozi wengine
walio weza kufika katika maombolezo hayo.
“Ina maana hata Eddy mwenyewe hajanitambua?”
Mzee Godwin alijiuliza huku, akiiweka sawa gari
hiyo ya polisi kutoka katika geti la jumba la waziri
Eddy. Moja kwa moja akaanza safari ya kuelekea
nje ya jiji la Dar es Salaam ambapo, amemuacha
Tom. Moyoni mwake akajikuta akianza kuingiwa
na uchungu mzito, juu ya kifo cha mke wake.
Baadhi ya matukio yanayo husiana na mke wake
kipindi wakiwa katika mahusiano, zikaanza kumjia
kichwani mwake. Na ukakamavu wake wote
machozi yakaanza kumwagika sana.
Kila jinsi alivyo zidi kukumbuka matukio mema ya
mke wake hadi anamzalia mtoto wa kiume ambaye
ni Eddy, hasira na uchungu ndivyo vilivyo zidi
kuongezeka, akajikuta akizidisha mwendo kasi wa
gari hiyo ya polisi.
Kumbukumbu zake, zikahamia kwenye siku
ambayo dokta wa familia alipo weza kumpa taarifa
kwamba Eddy si mwanae wa kumzaa, ila ni mtoto
wa pacha wake. Uchungu, ukaizidisha hasira yake,
akiamini kwamba kwa makosa aliyo weza
kuyafanya mke wake ndiyo yalipelekea familia yake
iliyo kuwa na faraha na amani kuweza
kupangaranyika, na uhasama mkubwa ukatawala
kati ya baba na mke pamoja na mtoto.
Gafla mzee Godwin akajikuta akifunga breki za
gafla, kwa kadri ya uwezo wake, akajikuta
akiikwepa gari ndogo, iliyo hama na kumfwata
upande wake huku nayo ikiwa katika mwendo kasi.
***
“Nastahili kufaa mimi”
Maneno ya binti mmoja, aliye lewa, alizungumza
huku akizidi kugugumia mafumba ya pombe kali,
hadi watu baadhi walipo ndani ya mgahawa huo
wakaanza kumshangaa.
“Oya cheki yule manzi anavyo kata ulabu”
Kijana mmoja limuambia mwenzake aliye kaa naye
karibu mara baada ya kuweza kumuona msichana
huyo akiwa amesha angusha mizinga miwili ya
whyne, huku akiwa na mzinga wa tatu ukimalizikia
malizikia kuisha.
“Alafu ni bonge la manzi aiseee”
“Yaaa masister duu wengine wanashida kweli
kweli”
“Pale utakuta anakunywa kutokana na mapenzi
yamemuharibu”
“Nikamtokee nini?”
“Hembu kalmia mpododo wako hapa, dada humjui
unataka ukamtokee, kwanza anaonekana ana
mkwaja mrefu”
“Etii ehee”
“Hakuna cha etiii”
Wakaendelea kumshangaa dada huyo aliye umbika
kwa maumbile mazuri pamoja na sura nzuri ya
kuvutia, hadi dada huyo akawastukia kwamba
vijana hao wawili wanamtazama. Akaachia msunyo
wa nguvu, hadi watu wengine ambao hawakuwa na
muda naye ikabidi wamtazame kwa muda.
“Shenzi nyinyi”
Dada huyo alizungumza, kwa dharau kubwa,
taratibu akasimama, huku akiyumba yumba sana.
Akachomoa noti mbili ya dola mia mbili kisha
akamzibandika kwa nguvu mezani, taratibu
akaanza kutembea huku akiyumba sana.
‘Nimeuaaa’
Alijisemea kimoyo moyo huku akizidi kutembea
kwa hatua zakuyumba, akafika kwenye gari yake
aina ya ‘Crown’, akafungua mlango wa upande wa
dereva na kujitupia ndani ya gari. Kila alipo tizama
mbele, akilini mwake, alikumbuka jinsi alivyo weza
kumgonga mtoto mdogo, akiwa na gari yake aina
ya Verosa. Kisha akkimbia kuepuka kukamatwa na
polisi,
“Weee mtoto weweeeeee, poleeeeeeeee”
Alijisemea kwa sauti iliyo legea, akawasha gari
yake, kabla hajaondoka, kioo cha mlango wake
ukagongwa na muhudumu wa mgahawa huo ulipo
maeneo ya bagamoyo.
“Samahani dada, kutokana na kiasi ulicho kunywa
cha pombe, tungependa kukupa dereva
akakupeleka hadi huko unapo elekea”
“Wewe kijana ni kum***** nini, unadhania hii gari ni
ya baba yakooooooo”
Kwa tusi alilo litoa dada huyo, likamfanya
muhudumu huyo kupata kigugumizi hata cha
kuzungumza, dada huyo akafunga koo cha gari
lake, akafunga mkanda, akakanyaga breki pamoja
na mafuta na kuzifanya tairi za nyuma kuanza
kuserereka kwa nguvuu, hadi watu walipo karibu
na eneo hilo wakabakiw ameduwaa. Kisha akaachia
breki na kuifanya gari hiyo kuchomoka kwa kasi
katika eneo la maegesho, kwa bahati nzuri geti la
eneo la kutokea lipo wazi. Kwa mwendo huo huo
wa kasi, akafanikiwa kufika eneo la kuingia
barabara kubwa itokayo mkoani na kuelekea Dar es
Salaam.
“Waoooooooo fast and furious hahahaaaaaaaaaaaa”
Dada huyo alishangilia sana, akijifananisha na
wacheza filamu ya kimarekani ijulikanayo kwa Fast
and Furious. Akazidi kukanyaga mafuta, huku
akihakikisha kila gari lililopo mbele yake analipita
kwa mwendo mkali, huku kwa mara kadhaa akiwa
anawaonyeshea kidole cha katikati madereva anao
wapiti, akiashiria kuwatukana na wao si lolote wa
sichochote mbele ya gari lake hiyo ndogo.
Kwa mbali katika eneo la barabara iliyo nyooka,
akaiona gari ya polisi ikija kwa kasi huku ikiliza
king’ora.
“Ahaaa mumenifwata hadi huku eneeee”
Alizungumza kwa dharau, huku akibenua midomo
yake kwa dharau kubwa, akazdisha mwendo kasi
hadi ikafika spidi mita mia na sabini, akiamini spidi
mita kumi zilizo baki kufika mia na themanini,
atazimalizia pale atakapo weza kulifikia gari hiyo
ya polisi. Mita chache kutoka linapo kuja gari la
polisi, gafla akahama upande wake na kuifwata gari
ya polisi, nakulengana nayo uso kwa uso.
Binti huyo akayafumba macho yake akiamini huo
ndio mwisho wa maisha yake, kwani gari hizo
zitagongana uso kwa uso, ila gafla akastukia gari
yake ikipitiliza, mbele na gari ya polisi ikiwa
imemkwepa, kitendo cha kulishangaa tukio hilo,
akajikuta gari ikimshinda na kuanza kuserereka
kuelekea pembezoni mwa barabara, akajitahidi
kufunga breki, ila tayari alisha chelewa, gari hiyo
ikaenda kugonga mti mkubwa wa mkuyu, na hapo
hapo ikatulia, huku moshi mwingi ukiwa unatoka
maeneo ya mbele, kwenye bonet.
“Pumbavuu”
Mzee Godwin alizungumza huku akisuka kwenye
gari kwa hasira, akachomoa bastola yake, kwa
mwenzo wa haraka akaelekea sehemu gari ndogo
hiyo ilipo elekea, Nia na dhumuni lake ni kwenda
kumshikisha adabu dereva huyo mpumbavu aliye
damiria kuitoa roho yake wakati bado ana kazi
ngumu mbeleni mwake.
Akaifikia gari ndogo hiyo, na kukuta dereva wake
akiwa amezibwa na ftuza kubwa lililo jaa upepo
mwingi. Akiwa katika kumfikiria ampige risasi afe,
moto mdogo ukaanza kuwaka kwenye boneti ya
gari hilo.
‘Wewe natakiwa nikuulie nje’
Mzee Godwin alizungumza huku akianza kumpa
masaada dada huyo, mwenye mwenye nyingi zilizo
mfunika usoni mwake. Akafanikiwa kumtoa ndani
ya gari hilo, ili kuyaokoa maisha yake na dada
huyo, akambeba na kukimbilia naye, kabla
hawajafika mbali, gari hiyo ikalipuka, na
kuchanguka, mzee Godwin akajikuta akianguka
chini huku akiwa amemkumbatia binti huyo.
Mzee Godwin akaanza kuhema sana, huku
akilitazama gari hilo likiteketea kwa moto, ulio toa
moshi mwingi mweusi na unao palia sana, pale
unapo uvuta. Akaanza kumffunua nywele binti huyo
zilizo tanda usoni mwake, Mzee Godwin akastuka
huku akiwa amemtumbulia macho binti huyo.
“MANKAAA……..!!!!”
***
Zoezi la kumkamata Mzee Godwin, likawa gumu
zaidi baada ya askari kugundua muhusia wanaye
muhitaji amesha watoroka muda mwingi, katika ya
hispitali ya muhimbili.
Taarifa zikazidi kusambazwa kwa wananchi kupitia
vyombo vya habari kwamba endapo watamuona
gaidi Mzee Godwin, basi watoe taarifa kituo cha
polisi, kwani mtu huyo ni hatari sana na tayari
amesha weza kuua askari walikuwa wakifanya
msako huo.
Kila mtandao wa kijamii, wananchi wakaendelea
kupashana taarifa na kusambaza picha za Mzee
Godwin akiwa katika mikao tofauto tofauti, kuanzia
alivyo kuwa kijana hadi sasa alivyo kuwa mzee.
Ulinzi ukazidi kuimarisha katika mipaka yote ya
kutoka nchini Tanzania, idadi ya polisi ikazidi
kupelekwa mipakani, ili kuhakikisha kwamba Mzee
Godwin anatiwa nguvuni.
Kwa jinsi jeshi lilivyo mpenda, waziri Eddy, alivyo
wafanyia mabadiliko muda mchache tangu kuingia
kwake madarakani, basi wakajikuta wakifanya kazi
kwa juhudi kuhakikisha wanamfurahisha kiongozi
wao huyo.
***
Makaburi matatu yaliyo chimba katika eneo la
jumba la waziri Eddy, yakaandaliwa kwa kuweza
kuhifadhia miili mitatu ya wapendwa wa Eddy
pamoja na Shamsa. Jinsi Eddy kila alilivyo
yatizama majeneza matatu yaliyopo mbele yake,
machozi ya uchungu yakazidi kumwagika.
Hakuamini mke wa mtoto wake alio pambana kadri
ya uwezo wake leo wamesha poteza pumzi.
Eddy taratibu akapiga magoti kwenye jeneza la
Junio, lililo funguliwa ili aweze kutoa heshima zake
za mwisho kwa mwanaye huyo. Jinsi anavyo
mtazama haamini kama mwanaye leo amekuwa
mfu.
“Junio, Junio, Dady….ni… nipo hapa nimekuletea
zawad…..i mwanangu wake up my boy. Kwa kwaa
nini uondoke wakati hata shule ba….baadoo
hujakwenda”
Eddy alizungumza huku machozi yakimwagika
sana, hakuwa ambaye aliweza kuyazuia machozi
yake pale Eddy alipokuwa akiyazungumza maneno
hayo.
“Junio I love you my son”
Eddy alizungumza kwa uchungu zaidi, huku
akikumbua jinsi alivyo kuwa akicheza na mwanaye,
mpira nchini brazil kwenye fukwe zilizo tulia.
Akakumbuka jinsi Junio alivyo mfunga goli zuri
walipo kuwa wakicheza mpira huo na jinsi alivyo
kuwa akishangilia na wezake.Eddy akaangua kilio
kikubwa zaidi, kilicho wafanya walinzi wake
kumnyanyua na kumuhamishia kwenye jeneza la
Phidaya.
Eddy akakaa kimya huku akimtazama Phidaya mke
wake, mrembo kupita wanawake wote alio wahi
kuwaona dunia, akajikuta akiachia tabasamu lililo
ambatana na machozi mengi ya uchungu. Alicho
kifanya ni kupitisha kiganja chake cha mkono wa
kulia katika shavu la Phidaya, aliye wa baridi sana.
Eddy akajikuta akishindwa kuzungumza chochote
zaidi ya kufuta machozi yake, na kupiga hatua
moja mbele kwenye jeneza la mama yake.
“Mom…….”
Eddy aliita kisha akakaa kimya, akamtizama mama
yake huyo aliye weza kumfundisha mambo mengi.
Kumbukumbu za mama yeke alivyo weza kutekwa
na mee Godwin, Afrika kusini na kupelekwa
kwenye mapango ya utumwa, na jinsi alivyo weza
kumuokoa, Eddy akajikuta akitetemeka kwa hasira
na uchungu mwingi. Machozi yakazifi kumwagika,
huku akiwa ameyang’ata meno yake kwa hasira
kali. Taratibu damu za pua zikaanza kumwagika,
kizunguzungu kikali kikamkata, akayumba mara ya
kwanza ya pili walinzi wake wakamdaka asianguka
chini.
Tukio hilo likamuogopesha sana Shamsa, aliye
simama nyuma yake, kwa mara nyingine nguvu
zikamuishia Shamsa na kujikuta akikaa chini
mwenyewe bila hata kupenda. Roho ya Rahab,
ikazidi kumuuma kwani uwezo wa kutenda msaada
kwa familia ya Eddy, anao ila akifanya msaada wa
kuwafufua, watu wote watamkimbia, na kuamini
kwamba yeye si mwanadamu na itakuwa ni
miongoni mwa kasfa chafu kwa raisi Praygod,
kwamba ameoa jinni.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 19 YA SIMUHILI HII.
 
MADAM (19)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Eddy akajikuta akitetemeka kwa hasira na uchungu
mwingi. Machozi yakazifi kumwagika, huku akiwa
ameyang’ata meno yake kwa hasira kali. Taratibu
damu za pua zikaanza kumwagika, kizunguzungu
kikali kikamkata, akayumba mara ya kwanza ya pili
walinzi wake wakamdaka asianguka chini.
Tukio hilo likamuogopesha sana Shamsa, aliye
simama nyuma yake, kwa mara nyingine nguvu
zikamuishia Shamsa na kujikuta akikaa chini
mwenyewe bila hata kupenda. Roho ya Rahab,
ikazidi kumuuma kwani uwezo wa kutenda msaada
kwa familia ya Eddy, anao ila akifanya msaada wa
kuwafufua, watu wote watamkimbia, na kuamini
kwamba yeye si mwanadamu na itakuwa ni
miongoni mwa kasfa chafu kwa raisi Praygod,
kwamba ameoa jinni.
ENDELEA
Madaktari waliopo katika eneo hilo wakaanza
kumpatia Eddy huduma ya kwanza pamoja na
Shamsa, ikawalazimu kuweza kusimamisha
hudmua za mazishi kwa muda, kusubiria wahusika
wakuu kkukaa katika hali nzuri. Baada ya lisaa,
Eddy na Shamsa wakarejea katika viwanja vya
hapo kwenye jumba lake kuendelea na mazishi ya
familia yake. Rahab hakuwa na jinsi zaidi ya
kuacha mazishi hayo kuweza kufanyika, huku
moyoni mwake akizidi kuumia, akimuhurumia
kijana mdogo Junio, kwani umri unampasa sana
kuweza kuendelea kuishi katika dunia hii.
Viongozi wakubwa wakaanza kuondoka katika
jumba la Eddy, kila mmoja akiamini kwamba kazi
ya Mungu haina makosa na wengine wakiingiwa na
hofu pamoja na mashaka makubwa ya kutaka
kujua ni lini Mzee Godwin anaweza kukamatwa
mikononi mwao.
“Eddy jikaze kaka yangu, tutazidi kuwa pamoja”
Rahab alizungumza maneno ya kumfariji Eddy
huku akiwa amemkumbatia
“Sawa dada Rahab”
“Ina bidi upae mapumziko ya kwenda mbali na
hapa, ili akili yako ikatulie”
“Hapana Rahab, hapa ni nyumbani kwamngu na
ndipo walipo lala wapenzi wangu, siwezi kwenda
popote nitakaa hapa hapa”
“Hapana Eddy, inabidi ukatafute sehemu ya
kwenda kutuliza akili wewe pamoja na Shamsa,
tambua ya kwamba unavyo endelea kukaa na
kutazama hayo makaburi huo weza kusahau
kamwe”
“Ni kweli siwezi kusahau, ila……”
Eddy akastukia akipigwa busu zito la mdomo na
Rahab, jambo lililo mstua sana.
“Madam samahani unafanya nini?”
Eddy alizungumza huku akijitoa mikononi mwa
Rahab
“Unaogopa nini Eddy, tambua hapa tupo chumbani
peke yetu”
“Namuheshimu muheshimiwa”
“Hayupo”
Rahab alizungumza huku akianza kuvua kitenge
alicho jifunga kiunoni mwake na kubakiwa na
skintait, pamoja na tisheti nyeusi alivyo vaa, iliyo
bandikwa picha ya Junio, Phidaya pamoja na
mama Eddy.
***
Mapigo ya moyo ya Mzee Godwin yakaanza
kumuenda mbio, akajaribu kumtingisha Manka
aweze kuamka, ila Manka hakuweza kujibu kitu
chochote zaidi ya kuendelea kukaa kimya. Mzee
Godwin gafla akasikia minong’ono ya watu nyuma
yake, akageuka na kukuta vijana wawili wakiwa
wamesimama huku wakichukua tukio la kuwaka
moto la gari hiyo ndogo.
Walipo muona mzee Godwin wakastuka, kwani nao
ni miongoni mwa watu walio weza kuiona picha
yam zee Godwin kwenye mitandano ya kijamii
akitafutwa kama Rubin na jeshi la polisi la
Tanzania.
“Huyu si ndio yule gaidi”
Mmoja aliropoka huku akiigeuzia simu yake upande
aliopo mzee Godwin ili kumchukua video. Kama
mbogo aliye uliwa mwanaye, mzee Godwin
akanyanyuka kwa kasi ya ajabu na kuwarukia
vijana hao masharo baro. Akaanza kuwatandika
ngumi za kutosha huku akiwatukana matusi ya
uchungu sana. Vijana hao walilia kama watoto
wadogo, wakajutia ni kwanini walisimamisha gari
na kuja kushuhudia ajali hiyo. Mzee Godwin
akachomoa mkanda wa suruali yake na kuandelea
kuwachapa vijana hao kwa hasira kali, hadi
wakapoteza fahamu.
Mzee Godwin akamgeukia Manka, kwa bahati nzuri
akamkuta akitingisha tingisha mkono mmoja, kwa
haraka akamuweka begani na kuanza kukimbia
naye kuelekea alipo simamisha gari la polisi,
akamuingiza Manka ndani na kuondoka naye katika
eneo hilo,
Kila alipo mtazama binti yake huyo, waliye
potezana naye miaka mingi ya nyuma roho yake
ikaingiwa na furaa kubwa sana, moyoni mwake
akaanza kumuomba Mungu ampe binti yake nafasi
nyingine ya kuweza kuishi.
Majira ya saa mbili usiku akafika katika handaki
alilo muacha Tom, kwa haraka akafungua mfuniko
wa kuingilia kwenye handaki hilo kisha
akamshusha Manka ambaye bado fahamu
hazijamrejea.
“Tom fungua mlango wa chumba cha kwanza”
Mzee Godwin alimuamrisha Tom huku akiwa
anahema sana kutokana na kuchoka sana pmoja
na wasiwasi mwingi unao mtawala. Akamlaza
Manka juu ya kitanda.
“Babu huyu naye ni nani?”
“Utamjua hembu tumpe nafasi ya kuweza
kupumzika?”
“Amefanyaje?”
“Heiii Tom sihitaji maswali Mengi”
Mzee Godwin alizungumza kwa hasira na kutoka
nje ya chuma hicho, Toma akamtazama kidogogo
Manka usoni kisha na yeye akatoka.
***
Wasamaria wema walo kuwa wakikatika katika
barabara kuu, yakutokea mikoa ya Tanga na
Arusha, wakasimama kwenye sehemu walipo ona
moshi mwingi ukiendelea kuonekana katika upande
wa pili wa barabara. Abiria waliomo katika basi la
Ngorika, wakashuka kwenda kujaribu kuangalia gari
hilo linalo teketea kwa moto. Wakakuta vijana
wawili wakiwa wamelala pembeni huku
wakionekana kupoteza fahamu na miili yao ikiwa
imajaa makovu ambayo, hakuna ambaye aliweza
kuyatilia mashaka kwani waliamini kwamba ajali
hiyo ya gari ndogo ndio imeweza kusababisha
majeraha hayo.
“Niwazima hawa?”
Jamaa mmoja alizungumza huku akiwatazama.
Kijana mwengine mrefu na mweusi kiasi,
akawatazama vijana hao jinsi walivyo lala chini,
baadhi ya watu wakataka kuwanyanyua.
“Hembu musiwanyanyue mara moja, sogeeni
pembeni”
Alizungumza na kuwafanya watu wengine
kumshangaa, kwani majeruhi hao wanahitaji
msaada wao na si kuwaacha katika eneo hilo.
“Wewe kijana mjinga kweli, hao wangekuwa ni
wadogo zako ungewaacha waendelee kulala hapo
chini?”
Mzee mmoja wa kichaga alimjia juu kijana huyo
anaye onekena ni mstaarabu na mtulivu sana,
mwenye sura ya kipole.
“Mzee wangu nimewaomba na sijataka kutimia
nguvu, hivi munavyo ona hawa wamepata ajali
kweli?”
“Wewe unaonaje?”
Mzee huyo aliendelea kumropokea kijana huyo,
aliye achia tabasamua pana kisha akaendelea
kutazama sehemu walipo lala vijana hao. Kila alipo
zidi kuchunguza kwa umakini eneo hilo, ndipo
alipo gundua kwamba kuna mtu ambaye aliweza
kuwadhuru vijana hao kwa kuweza kuwapiga sana.
Kitu kilicho zidi kumshangaza kwa vijana hao,
shawakuweza kuporwa kitu cha aina yoyote, simu
zao zipo katika eneo la tukio. Akachukua simu za
vijana hao wawili, kwa bhati nzuri moja ya simu
bado ilikuwa inaendelea kurekodi tukio katika eneo
hilo. Akaisave video hiyo kisha akaanza kuitazama,
sauti za vijana hao zikasikika kwenye video hiyo
huku picha ya gari hilo linalo malizikia kuteketea
kwa moto.
Video hiyo ikamuonyesha mzee Godwin, akiwa
amemshikila binti mmoja, ila gafla mshika kamera
ya simu hiyo, akastukia akiangushwa chini na
kuanza kulia kwa uchungu mkali ikiashiria kwamba
mzee huyo aliweza kuwapiga vikali.
“Haya munaweza kuwachukua vijana hao”
Kijana huyo alizungumza huku akizichukua simu
hizo, kisha akaituma video hiyo kwenye simu yake
kisha akaituma makao makuu alipo kuwa ameitwa
kwa ajili ya kazi maalumu
***
Agnes na Jaquline baada ya kufanya tukio la
kuituma video ya vitisho kwa bwana Rusev,
wakaagana na mzee ambaye aliweza kuwafundisha
mbinu nyingi za kupambana kutumia miili yao
pasipo kutumia silaha za moto. Agnes aliweza
kufuzu kwa asilimia mia, katika kujua mbinu hizo
za kupambana. Moja kwa moja wakafunga safari
hadi mjini Mosscow, huku wakiwa wameziweka
nywele zao katika mfumo ambao si rahisi sana
kwa watu kuweza kumstukia Agnes kwamba ni
muuaji aliye weza kuhusika na kifo cha waziri wa
mambo ya nje wa Marekani bwana Paul Henry Jr,
mwaka mmoja ulio pita.
Kwa kutumia hati feki zilizo tengenezwa na
Jaquline mwenye utaalamu mkubwa wa kuweza
kufanya hiyo kazi, wakapanda ndege na moja kwa
moja wakafunga safari hadi nchini Marekani pasipo
mtu wa aina yoyote kuwastukia.
Wakafika salama na moja kwa moja wakaelekea
katika jiji la Chikago, ambapo wakakodi chumba
kwenye moja ya magorofa ambayo hutumiwa na
watu kukodi vyumba pale ambapo mtu anapo hitaji
kufanya kitu na kila kitu kinacho stahili kuwemo
ndani ya chumba kimo ndani ya chumba.
Wakaweka mabegi yao makubwa kwenye moja ya
kabati kisha, Jaquline akafungua laptop yake na
kuanza kufanya moja ya kazi ambayo ni miongoni
mwa mpango ambao wameupanga kuufanya
“Bingoo”
Jaquline alizungumza huku akiwa na furaha sana
“Nini?”
“Nimesha ipata ramani nzima ya whaite house”
Jaquline alizungumza huku akimgeuzia Agnes
ramani hiyo, inayo onekana kwenye laptop.
“Hivi kweli Jack tutafanikiwa kweli kwenye huo
mpango tulio upanga?”
“Agy kwa uwezo tulio nao ni lazima tuiteke whaite
house, tukisha fanikiwa tu, lazima kina Fetty
waweze kuachiwa”
“Ila mimi mwenzio naogopa, kwani hiyo kazi ni
ngumu sana unajua?”
“Agnes usijali kila kitu niachine mimi, lazima
tuishushe whaite house”
Jaquline alizungumza huku akiwa amejiamini sana,
jambo lililo mpa faraja Agnes kupata mpiganaji
ambaye anaweza kumsaidia katika mpango wa
kuwatorosha Fetty, Halima na Anna, ambao wapo
chini ya uangalizi wa serikali ya Marekani katika
gereza la Pentagon lililopo katikati ya bahari
kwenye moja ya kisiwa kinacho lindwa sana kupita
maelezo.
***
Rahab akamsukumia Eddy kwenye sofa lililopo
ndani ya chumba hicho cha kupumzikia alipo kuwa
ameingia Eddy kwa ajili ya mazungumzo maalumu
na Rahab. Rahab akamkalia mapajani Eddy, na
kuendelea kumnyonya midomo yake, kwa haraka
Rahab akashusha ulimi wake kwenye sikio la
upende wa kushoto la Eddy na kuanza kulinyonya,
na kuufanya mwili wa Eddy kuanza kusisimka, kwa
hisia kali za kimapenzi.
“Madam Rahab unafanyaje lakini?”
“Tulia, hii ni zawadi yangu kwako”
Rahab, hakutaka kumpa nafasi Eddy ya kuweza
kufanya kitu chochote, kwani tayari alisha gundua
ni wapi akimgusa Eddy hisia zinamsisimka sana.
Rahab akauchukua mkono wa Eddy na kuuzamisha
kwenye skintaite yake. Gafla mlanngo ukagongwa
kwa nje.
“Nani?”
Eddy aliuliza kwa sauti nzito, iliyo mlegea kiasi
“Mimi”
Sauti ya raisi Praygod ilisikika nje ya mlango na
kumfanya Eddy na Rahab kukurupuka, wote wakiwa
na wasiwasi mkubwa wa kufumaniwa.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 20 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (20)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“Madam Rahab unafanyaje lakini?”
“Tulia, hii ni zawadi yangu kwako”
Rahab, hakutaka kumpa nafasi Eddy ya kuweza
kufanya kitu chochote, kwani tayari alisha gundua
ni wapi akimgusa Eddy hisia zinamsisimka sana.
Rahab akauchukua mkono wa Eddy na kuuzamisha
kwenye skintaite yake. Gafla mlanngo ukagongwa
kwa nje.
“Nani?”
Eddy aliuliza kwa sauti nzito, iliyo mlegea kiasi
“Mimi”
Sauti ya raisi Praygod ilisikika nje ya mlango na
kumfanya Eddy na Rahab kukurupuka, wote wakiwa
na wasiwasi mkubwa wa kufumaniwa.
ENDELEA
Kila mmoja akajiweka sawa mavazi yake kisa Eddy
akakaa kwenye sofa, na kuanza kumwagikwa na
machozi mengi. Rahab akapiga hatua taratibu hadi
mlangoni na kuufungua. Akakutana na mumewe
akiwa katika sura ya kujiuliza maswali ambayo
asinge penda kuyazungumza kwa mdomo wake.
Raisi Praygod akaingia ndani, moja kwa moja
akaelekea kwenye sofa alilo kaa Eddy, kwa jinsi
alivyo mkuta Eddy, wasiwasi wake taratibu
ukapungua, kwani tayari wivu wa mapenzi ulisha
anza kumvaa Raisi Praygod.
“Eddy kwenye maisha ni lazima kuna vitu ambavyo
binadamu wote tutavipitia, iwe ni mchungaji,
shehe, raisi au waziri, sote njia yetu ni moja.
Nilazima tutaondoka duniani”
Raisi Praygod alizungumza kwa sauti ya upole iliyo
jaa hekima ndani yake, mkono wake mmoja akiwa
ameuweka begani mwa Eddy.
“Natambua kwamba, kifo siku zote huwa kina
umiza, ila hatuna budi kujikaza. Kuwa mkakamavu
Eddy wananchi bado wanahitaji msaada wako
katika kuwatumikia. Ukiwa kama kiongozi
ukiyumba basi nao watakosa ukakamau”
Eddy akamtazama raisi Praygod kidogo kisha,
akaendelea kutazama chini, akilini mwake akajutia
ni kwanini ameweza kumpa nafasi Rahab ya
kuushika mwili wake, tena katika siku muhimu
sana kama hii.
“Nitakuandalia ndege uende,nchi yoyote utakayo
ihitaji ukapumzike kwa muda ili mawazo na
unyonge ukuepukie”
“Asante muheshimiwa”
Wakati mazungumzo yanaendelea Rahab, amekaa
pembeni akiwasikiliza kwa umakini, macho ya
Rahab hayakucheza mbali sana na sura ya Eddy.
“Nikutakie mapumziko mema, baby tuondoke sasa”
Raisi Praygod akanyanyuka kwenye sofa, pamoja
na Rahab.
“Eddy jikaze kama nilivyo kuambia wewe ni
mwanaume haya ni mapito tu hutakiwi
kuyachukulia kama ni kitu kisicho isha, hakikisha
unaziongoza hisia zako katika hili”
Rahab alizungumza maneno ya kujiamini, sana.
Wakatoka ndani ya chumba hicho na kumuacha
Eddy akiwa ametawaliwa na mawazo mengi. Muda
haukupita sana Shamsa akaingia akiwa katika hali
ya unyonge, taratibu akafika kwenye sofa alilo keti
Eddy, akajilaza na kichwa chake kukiweka kwenye
mapaja ya Eddy. Uso mzima wa Shamsa
umetawaliwa na machozi mengi, kila alipo jaribu
kuyafumba macho yake kuutafuta usingizi ila
akashindwa kwani sura ya Junio mara nyingi
iliweza kusumbua katika hisia zake.
“Muheshimiwa una mgeni”
Mlimzi mmoja wa Eddy alizungumza akiwa
amesimama mbele ya Eddy. Eddy akatingisha
kichwa kuruhusu mgeni huyo kuweza kuingia
ndani ya chumba. Macho ya Eddy yakagondana na
macho ya Madam Merry aliye simama katikati ya
mlango, akijishauri kuingia ndani ya chumba hicho.
***
“Babu tutaendelea kukaa humu humu ndani ya hili
pango?”
“Kwa nini unauliza hivyo?”
“Kwa maana naona hatuzungumzii swala lolote la
kuweza kutoka ndani ya hili pango”
“Tutato………”
Mzee Godwin akanyamaza na kumtazama Manka
aliye simama kwenye mlango wa chumba walicho
muingiza muda mrefu tangu amuokoe kutoka
kwenye ajali. Manka hakuamini kitu anacho kiona
mbele yake, kwani kukutana na baba yake mzazi ni
swala ambalo hakulitegemea kabisa na jinsi baba
yake anavyo tafutwa basi hakuamini kama atakuja
kumuona akiwa hai.
“Babaaa…!!”
Manka aliita huku akipiga hatua za taratibu
kuelekea sehemu alipo kaa mzee Godwin. Mzee
Godwin akanyanyuka taratibu na kumfwata Manka
sehemu alipo simama, wakakumbatia huku wote
wakimwagikwa na machozi ya furaha
“Baba upo hai?”
“Ndio mwananangu”
“Ehee kumbe ni baba na mwana!!!?”
Baada ya kukumbatiana kwa muda mrefu, kila
mmoja akaketi kwenye kiti ili kuweza kuhojiana
mambo mawili matatu.
“Baba kwa nini unaendelea kutafutwa tena na nchi
nzima”
“Ni story ndefu mwanangu ila yatakwisha pale
nitakapo yatimiza malengo yangu”
“Malengo gani baba”
“Utayafahamu tukiendelea kuwa pamoja. Ila Manka
wangu haujabadilika sana”
“Kwa nini baba?”
“Kila nikikutazama bado ninaiona roho yangu ipo
ndani mwako, natumaini utaungana name katika
hili tunalo kwenda kulifanya”
“Baba, sihitaji kuwa adui tena na familia yako,
hapa nilipo fikia panatosha baba nahitaji kufa”
“Nini? Unacho kizungumza umekifikiria kweli?”
“Ndio baba, sihitaji kuendelea kuishi, niliyo yafanya
ni mengi sana, juzi juzi nimemgpnga mtoto mdogo
amefariki, bado askari wanaendelea kufanya
uchunguzi katika hilo”
“Je wamegundua kwamba ni wewe?”
“Lazima watakuwa wamefwatilia kila rekodi za
usajili wa gari langu. Baba najisikia vibaya, niliahidi
kwa Mungu wangu kwamba sinto ua tena ila
imeshindika baba”
Mankla alizungumza huku machozi yakimwagika,
mzee Godwin akamsogelea Manka hadi kwenye kiti
alicho kaa, akamshikilia mikono yake miwili na
kuinyanyua sura ya Manka kidogo, wakatazamana.
“Manka unatakiwa kuwa mkakamavu, bado
unamiaka mingi yakuishi mwanangu, nahitaji
kuweza kutimiza ndoto zako”
“Ndoto, ndoto gani baba, siwezi kutimiza ndoto
zangu nikiwa ninaandamwa na polisi kwa kosa la
mauaji”
“Huyo kijana uliye mgonga ana umri gani?”
“Kama miaka nane au saba hivi”
Mzee Godwin akajikuta akikuna kichwa chake, kwa
haraka akaka kwenye kiti kinacho tazamana na
moja ya computer, kwa bahati nzuri computer hizo
zimeunganishwa na internet, kwa haraka akaanza
kutafuta kitu alicho hitaji kukitafua kupitia kwenye
mtandao wa jeshi la polisi, kutokana yeye alikuwa
ni kiongozi wa jeshi, ni mambo mengi na siri
nyingi za nchi ya Tanzania anazifahamu.
Akaingiza namba za siri ambazo hutumika
kufungulia mtandao huo wa polisi unao husika
katika maswala ya upelelezi. Akakutana na namba
taarifa nyingi kati ya taarifa hizo ni moja ya video,
aliyo onekana akiwapiga vijana alio taka kumpiga
picha
“Fuc***”
Mzee Godwin alizungumza kwa hasira hadi Tom
na Manka wakastuka
“Nini tena babu?”
“Hakuna kitu”
Mzee Godwin akaachana na taarifa hiyo, akatafuta
taarifa ambayo inahusiana na ajali ya Junio Eddy.
Akafanikiwa kuipata pamoja na maelezo yake.
“Manka”
“Bee”
“Njoo uone”
Manka akasimama pembeni ya mzee Godwin.
Manka hakuamini macho yake kwani, picha ya
kijana aliye mgonga chini ya picha hiyo kuna jina
la kijana huyo ambaye ni Junio Eddy Godwin
’Ina maana ni mtoto wa Eddy!!?”
“Ndio”
“Mungu wangu!!!”
Manka akahisi kuchanganyikiwa, kila alipo fikiria
matukio ambayo alimfanyia Eddy kipindi akiwa
anasoma mkoani Arusha, ajahisi kichwa kinaweza
kumpasuka kwa mawazo mabaya
“Piga picha Eddy akifahamu wewe ndio
msababishaji wa kifo cha mwanae atakuacha
kweli?”
Swali la Mzee Godwin likawa kama msumari wa
mato ulio tua kwenye moyo wa Manka na
kusabisha maumivu makali kupita maelezo.
***
“Unaendeleaje?”
Eddy alimuuliza madam Merry mara baada ya
kuingia ndani ya chumba hicho
“Nina unafuu kidogo, japo nina maumivu kwa
mbali”
“Utapona usijali”
“Asante. Pole sana kwa yale yaliyo tokea”
Eddy akashusha pumzi nyingi na kumtazama
Madam Merry aliye nyongea sura yake kutokana na
kuumwa, kisha akamjibu kiunyonge.
“Asante”
“Tunaweza kuzungumza sisi wawili tu?”
Madam Merry alizungumza huku akimtupia macho
Shamsa aliye lala kwenye mapaja ya Eddy. Eddy
akamuamsha Shamsa, akamuomba aelekee
sebleni, Shamsa akatii.
“Natambua kwamba upo katika hali ngumu sana,
ila nimeona wewe ndio mtu sahihi ambaye
ninaweza kukupa taarifa hii, kabla hayajatokea
yakutokea”
“Una maana gani kusema hivyo?”
Madam Merry akaka kimya kwa muda kidogo huku
akiwa ametazama pembeni akionekana kuwa ni
mtu mwenye mawazo mengi sana kisha
akamtazama Eddy usoni.
“Mimi na baba…… baba yako tu tulikuwa
tunashirikiana?”
“WHAT ARE YOU SAY………!!!??”(UNASEMA
NINI………!!!??)
Eddy alizungumza huku akiwa amemkazia macho
Madam Merry aliye anza kutetemeka kiasi.
“Ndio, leo nimekuja kukiri kilakitu kwako, sihitaji
kufa pasipo kuweza kuikiri dhambi hii. Miaka
kadhaa ya nyuma niliweza kuungana na baba
yako. Alitokea sana kunipenda Godwin, nikajikuta
nikizama kwenye dimbwi la mapenzi yake……”
Madam Merry alizungumza kwa uchungu huku
machozi yakianza kumwagika usoni mwake
“Lengo kubwa lilikuwa niweze kupata nguvu ya
kulipiza kisasi cha mume wangu Derick, uliye
muua kwa kumkata kata vipande kama mnyama
pori.”
“Iliniuma sana Eddy lile tukio, halikufutika moyoni
mwangu kiurahisi kama ulivyo dhani. Hii ni
kutokana na Derick kuwa ndio mwanaume wangu
wa kwanza kunivua usichana wangu”
“Eddy roho yangu ilijaa unyama kama unyama
ambao ulinitendea kwa mume wangu, hata kama
naye aliweza kukuulia mwanao. Nilimuingiza John
rafiki yako kipenzi kwenye kikosi cha Mzee
Godwin, kutokana pia nilikuwa na mahusiano ya
kimapenzi na Johm.”
Machozi yakaanza kumlenga lenga Eddy usoni
mwake
“Nilimtumia John kuweza kukupata wewe, akutese
akunyanyase ili adhima ya moyo wangu iweze
kukamilika. John alikupenda sana, tena sana. Ila
kutokana na ushetani wangu na nguvu ya mapenzi
kati yetu, iliweza kumbadilisha na kuwa adui yako
namba moja”
“Madam Stop, I don’t want hear anymore”(Madam
acha, sihitaji kusikia zaidi)
Eddy alizungumza huku machozi yakimwagika,
matukio ya kikatili aliyo weza kufanyiwa na rafiki
yake John yakaanza kumjia kichwani mwake,
akakumbuka jinsi alivyo weza kumuua John na
Sheila uchungu ndivyo ukazidi kuongezeka moyoni
mwake
“Eddy yoyote katika yote mimi ndio msababishaji
wa maisha yako kuingia uhasama na wote, hii
nikutokana na wivu wa mapenzi nilio kuwa nao juu
yako”
“Wivu, eheheeee, wivu kivipi?”
Madam Mery akaka kimya kidodogo huku
akimtazama Eddy aliye simama akizunguka
zunguka ndani ya chumba hicho akionekana
kuchanganyikiwa kiasi.
“Kipindi tukiwa kwenye mahusiano, niligundua
kwamba upo katika mahusiano na Salome, iliniuma
sana, kwani nilipo gundua Salome ametembea na
wewe, kisha akatembea na mkuu wa shule ambaye
alikuwa ni muadhirika, iliniuma sana. Nikajiapiza
kuhakikisha ninafanya kitu utakacho jutia maisha
yako yote.”
Madam Mery alizungumza huku akiendelea
kumwagikwa na machozi mengi, taratibu akapiga
magoti chini huku akiendelea kulia kwa uchungu
mwingi.
“Ila mimi nilitembea na Salome kabla hajaadhirika,
na hata hapa ukinipima sina HVI”
“Nalitambua hilo Eddy”
Shamsa akiwa sebleni amejilaza kwenye sofa, kwa
haraka akurupuka na kusimama hadi walinzi
walipo sebleni wakamshangaa. Akili yake kwa
haraka ikamkumbuka Madam Mery ni mke wa
waziri wa fedha nchini Somali, na ndio huyo huyo
ambaye siku walipo kuwa Somalia na Eddy, alikuja
kwenye hoteli yao na kulala na Eddy, jambo
ambalo lilianza kumpa mashaka Shamsa. Akaanza
kutembea kwa haraka hadi kwenye mlango wa
chumba alipo Eddy, akataka kuingia ila akasita,
akisikia miguno ya mtu kulia, ikambidi atege siko
lake vizuri kwenye mlango.
“Muheshimiwa yupo ndani?”
Shamsa akastushwa na sauti ya askari mmoja
aliye simama nyuma yake
“Ndio yupo ndani, ila anamazungumza”
“Basi kuna ili faili ningependa mpatie pale atakapo
maliza mazungumzo”
“Linausiana na nini?”
“Na kesi ya mtu aliye sababisha kifo cha junio”
Kwa haraka Shamsa akalichukua faili na kulifungua
mbele ya askari huyo hata kabla hajaondoka.
Shamsa akastuka kukuta picha ya msichana
ambaye alisha wahi kumuona sehemu ila
kumbukumbu zake hazikumbuki ni sehemu gani
ambayo aliweza kumuona. Shamsa akajikuta
akiusukuma mlango na kuingia dani ya chumba
hicho. Akamkuta Madam Mery akiwa amepiga
magoti, wote wakamtazama Shamsa ambaye
ameingia gafla,
“Dady huyu ndio aliye muua Junio”
Eddy kusikia taarifa hiyo, akastuka, kwa haraka
akalichukua faili hilo na kulifunua, kitu alicho kiona
picha ya Manka pamoja na jina lake pembeni.
“MANKA……..!!!! MANKA SI ALIKUFA…….??.”
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 21 YA SIMUHILI HII.
 
Story Za Eddy
SORRY MADAM (21)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Kwa haraka Shamsa akalichukua faili na kulifungua
mbele ya askari huyo hata kabla hajaondoka.
Shamsa akastuka kukuta picha ya msichana
ambaye alisha wahi kumuona sehemu ila
kumbukumbu zake hazikumbuki ni sehemu gani
ambayo aliweza kumuona. Shamsa akajikuta
akiusukuma mlango na kuingia dani ya chumba
hicho. Akamkuta Madam Mery akiwa amepiga
magoti, wote wakamtazama Shamsa ambaye
ameingia gafla,
“Dady huyu ndio aliye muua Junio”
Eddy kusikia taarifa hiyo, akastuka, kwa haraka
akalichukua faili hilo na kulifunua, kitu alicho kiona
picha ya Manka pamoja na jina lake pembeni.
“MANKA……..!!!! MANKA SI ALIKUFA…….??.”
ENDELEA
“Manka………!!!”
Madam Mery alizungumza huku akinyanyanyuka,
Eddy na Shamsa wote wakamgeukia na
kumshangaa.
“Hembu nione”
Madam Mery akachukua faili alilo lishika Eddy,
macho yakamzidi kumtoka huku akimtazama
Manka kwenye picha,
“Unamfahamu huyo?”
Eddy aliuliza huku akimtazama Madam Mery
ambaye anaonekana kuwa na wasiwasi mkubwa
sana. Madam Merya akajibu kwa kutingissha
kichwa akionekana kumfahamu Manka.
“Hakufa”
Madam Mery alizungumza huku akimtazama Eddy
usuoni kwa macho ya wasiwasi mwingi.
“Una maana gani?”
***
“Ila Eddy ni chanzo cha mume mume wangu kufa”
Manka alizungumza huku akimtazama Mzee
Godwin.
“Kwani, kwani uliolewa?”
“Hapana baba, ila nilikuwa na mwanaume ambaye
nilimpenda sana, na alikuwa anafanana sana na
Eddy”
“Nilimpenda sana yule mwanume, nakumbuka
Eddy aliamua kumpa mume wangu kazi ya kwenda
kumuoa Sheila aliye kuwa ni mpenzi wake, ila
haikuwa hivyo kwani siku ya harusi yao ndipo
walipo vamiwa na mume wangu kutekwa na
kuuawa”
Maneno ya Manka yakamkumbusha Mzee Godwin,
tukio ambalo yeye ndio alikuwa ni muhusika mkuu
katika kupanga mpango mzima wa kuweza
kumteka Eddy kwenye harusi yake yeye pamoja na
mke wake. Huku akimtumia John kuweza
kukamilisha mipango yote hiyo. Ila kitu ambacho
kilimchanganya Mzee Godwin ni siku alipo gundua
kwamba mtu waliye weza kumuu si Eddy, ila swali
lililo muumiza sana kichwani mwake kijana huyo ni
nani, na ametoka wapi. Leo ndio anapata jibu
kamili kwamba yeye ndio muhusika mkuu wa kifo
cha mpenzi wa mwanae kipenzi Manka.
Mzee Godwin taratibu akamvuta Manka hadi kifuani
mwake na kumkumbatia taratibu, akaanza
kumbembeleza ili asimwagikwe na machozi.
“Hatuna jinsi ya kufanya mwangu, tambua
ninatafutwa ina bidi niweze kurudi makao makuu
haraka iwezekanavyo”
“Makao makuu?”
“Ndio makao makuu ya kikosi changu cha DFE
(Destination of my enemies)”
“Sawa, ila kuna Madam Mery yupo wapi?”
Mzee Godwin akamtazama Tom, kisha akamgeukia
Manka. Kwa jinsi macho yam zee Godwin yanavyo
oenekana Manka tayari akagundua kuna kitu cha
tofauti kinacho endelea baina ya Mzee Godwin na
Madam Mery, ambaye alisha tambulishwa na baba
yake kama mama yake mdogo.
“Kuna kazi nahitaji nikupe kabla hatujaondoka”
“Sawa baba”
“Tom, huyu ni Manka ni dada yako, kuanzia hivi
sasa. Jiandaeni kwa kuondoka”
Tom na Mzee Godwin wakaingia kwenye chumba
amacho kimehifadhiwa pesa nyingi, wakaanza
kuvikusanya vibunda vya pesa na kuviweka
kwenye mabegi yaliyo kuwa na nguo. Manka
akaanza kupitia pitai vitu ambayo vipo kwenye
computer ambayo baba yake alikuwa anafwatilia
baadhi ya kesi ikiwemo ya kwake, hapo ndipo
akakutana na sura ya binti ambaye, anakumbuka
alisha wahi kuwa rafiki yake enzi za utoto.
“Huyu si Fetty?”
Manka alijiuliza huku akiendelea kuiangali picha ya
Fetty, akasoma maelezo ya msichana huyo na
kukuta habari ambayo ilimshangaza sana.
“Fetty ni gaidi?”
Mzee Godwin na Tom wakamaliza kukusanya pesa
hizo, kisha wakaanza kuchukua baadhi ya silaha
ambazo Tom hakujua kazi yake ni nini.
“Babu hizi za kazi gani?”
“Ni kwaajili ya kujilinda unaweza kutumia?”
“Hapana, nimezoea kuona kwenye video, wakina
Van dame, kina Rambo wakizitumia”
“Je unahitaji kujua kuzitumia?”
“Ndio”
Tom alijibu kwa shahuku kubwa akionekana
anahitaji kufahamu kutumia bunduki, jambo lililo
mfanya mzee Godwin kuachia tabasam pana.
Wakatoka na kumkuta Manka akiendelea kuwa bize
akisoma historia ya wasichana waliopo kundi moja
na Fetty wanao sadikika kuwa chini ya mikono ya
serikali ya kimarekani.
**
Ni usiku ulio tawala shamra shamra nyingi katika
ikulu ya Marekani ijulikana Whaite house, ulinzi
mkali umeimarishwa kwenye kila kona ya eneo
zima la ikulu. Wageni rasmi kutoka maeneo mbali
mbali ya nchi ya Marekani na hata nje ya nchi ya
Marekani wameudhuria, katika sherehe ya kuzaliwa
kwa raisi Markn Tosh.
“Nimefika”
Sauti ya Jaquline ilisikika kwenye sikio la Agnes
kupitia kifaa, maalumu alicho kifaa kwenye sikio
lake, Agnes kwa kutumia mitambo maalumu ya
Satelaite, anaweza kumuona Jaquline kila sehemu
anapo pita, akitumia gari ndogo ya kifahari anai ya
Ferrari Spider. Kwa kutumia kadi maalumu ya
mualiko waliyo ipata kwa binti mmoja anaye fanya
kazi ndani ya ikulu hiyo, aliweza kuionyesha kwa
walinzi wanao kagua kadi ya kila mmoja anaye
katika katika eneo hilo.
Wakamtazama Jaquline kwenye computer kama ni
miongoni mwa waalikwa, kwa bahati nzuri
wakamkuta ni mualikwa mmoja wapo.
“Welcome miss”
“Thank you”
Baada ya kumkagua, taratibu Jaquline akanza
kupiga hatua kuelekea ndani ya ukumbi, wa ikulu.
Macho ya Jaquline yakakutana na macho ya Lidya,
binti aliye weza kuwasaidia katika kuingia katika
sherehe hiyo, huku wakiwa wamemshirikisha katika
mpango wao mzima wa kumteka raisi. Lidya ni
binti wa kikorea aliye kulia Marekani tangu akiwa
na umri wa miaka sita, baba yake Mr Jang Woo,
aliweza kuhamishiwa kikazi nchini Marekani, kama
mpelelezi kwenye kitengo cha CIA. Jambo lililo
mlazimu kuweza kuhamia na binti yake Lidya, aliye
mbadili jina kutoka katika Jang Woo hadi Lidya, hii
ni kutokana na sababu za kimsingi alizo weza
kuziona ni muhimu kwa yeye kufanya hivyo ili binti
yake kuweza kuwa salama.
Lidya akiwa katika umri wa miaka kumi na mbili,
baba yake aliweza kupoteza maisha kwenye
shambulizi la kigaidi la kulipuliwa kwa magorofa
ya kiuchumi ya Marekani yaitwayo Twin Tower, na
gaidi la kimataifa Osama bin Laden. Kuanzia hapo,
Lidya akaanza kulelewa chini ya uangalizi wa
serikali ya kimarekani katika kikosi cha CIA(Central
Intrligrnce Agency).
Katika kukua kwake, wakiwa katika mafunzo ya
ujasusi nchini Russia ndipo, alipo weza kukutana
na Jaquline aliye muokoa kwenye ajali ya bomu
lililo tegwa kwenye gari lao na magaidi walio
tumwa na bwana Rusev, Jaquline akiwa ni
miongoni mwa magaidi hao, ila aliweza kufanya
hivyo kutokana na kutokea kumuoenea hurua binti
huyo mdogo kuangamia katika kifo hicho. Kuanzia
hapo Lidya akatokea kumpenda sana Jaquline na
kumuheshimu kama dada yake.
Jaquline akajichanganya na wageni wengine, huku
akifwata maelekezo kutoka kwa Agnes, aliye
muacha hotelini akitumia laptop yake kuweza
kuona kamera zote za ikulu hiyo zinavyo fanya
kazi, hii ni baada ya kupewa namba maalumu
(Code) na Lidya zinazo tumia na askari walipo
chumba maalimu cha ulinzi.
“Jiweke karibu na raisi”
Agnes alimpa maelekezo Jaquline naye akafanya
hivyo, muda wote watu wakiwa wanaendelea
kupiga stori za hapa na pale, ndivyo jinsi Jaquline
alivyo zidi kuendelea kuwasoma walinzi wote
walipo kwenye ukumbi huo.
Wakati huo huo, askari mmoja akaanza kumtilia
mashaka Jaquline, kwani muda wote Jaquline yupo
peke yake, hana mtu wa kuzungumza naye. Askari
huyo ambaye ni miongoni mwa askari wanao
mlinda raisi moja kwa moja akaelekea chumba cha
ulinzi, ili kufwatilia taafa muhimu za binti huyo
kwani kila mgeni aliye ingia ndani ya ukumbi huo
ana taarifa muhimu zinazo julikana na ikulu, na
endapo kutajitokeza tatizo lolote basi, kukamatwa
kwake ni rahisi.
“Mvute karibu huyo binti”
Askari huyo alimuamuru mmoja wa mafundi
mitambo waliomo kwenye chumba hicho cha ulinzi
kilicho jaa computer nyingi, za kisasa na zenye
uwezo wa hali ya juu katika matumizi yake.
“Tafuta taarifa muhimu za huyu binti”
Kijana huyo mwenye utaalamu wa mkubwa katika
maswala ya coputer, akaanza kufanya kazi aliyo
agizwa. Kila kilicho anza kufanyika, Agnes aliweza
kukiona, kwenye laptop yake, jinsi askari huyo
wanavyo jaribu kutafuta taarifa za Jaquline.
“Jina lake ni Livna Livba, uraia ni Senegal, ni
mfanya biashara mkubwa”
Kija huyo alimjibu askari huyo, kwani Lidya yeye
ndiye aliye weza kuandika taarifa hizo za uaongo
na kuzituma kwenye mtandao, na endapo
kutatokea kitu chochote kuhusiana na Jaquline
basi iwe ni rahisi kwa yeye kuto weza kujulikana
uhalisia wake halisi zaidi ya sura yake tu.
“Kuna mgeni yoyote kutoka Afrika?”
“Ngoja nicheki orodha ya wageni”
Kijana huyo anaendelea kufanya alicho agizwa.
Kwa bahati nzuri akakuta jina la Livba Livna katika
orodha ya wageni walio weza kuhuzuria katika
sherehe hiyo”
Agnes akajikuta akishusha pumzi nyingi, baada ya
kuona tukio hilo, limeweza kutatulika.
“Muheshimiwa kuna tatizo”
Kijana mwengine alimwambia askari huyo, aliye
kimbilia moja kwa moja kwenye sehemu alipo kaa
kijana huyo na computer yake, hapo ndipo alipo
weza kuiona sura ya Agnes na akionekana yupo
kwenye moja ya hoteli kubwa iliyopo karibu na
ikulu hiyo.
“Securty code zimeibwa, narudia tena Securty
code zimeibwa, number 99902, kuna tatizo narudia
tena kuna tatizo”
Askari huyo alitoa taarifwa kwa walinzi wote
waliopo katika eneo la ikulu, huku akitoka kwenye
chumba hicho, kwa haraka sana.
“Kuwa makini naona kama kuna jambo linalo
endelea”
Agnes alimuambia Jaquline aliye endelea
kuwatazama askari waliopo katika ukumbi,
akagundua baadhi ya askri wanaondoka katika
ukumbi huo wakieelekea nje. Agnes
akawashuhudia askari baadhi wakiingia kwenye
magari na kuondoka ikulu.
“Wanakwenda wapi hawa”
Agnes alijiuliza mwenyewe pasipo kugundua
kwamba tayari amesha stukiwa kwamba yupo
kwenye hoteli moja iliyopo karibu na ikulu, na
amejulikana kwamba yeye ndio aliye husika na
mauaji ya kiongozi wao bwana Paul Henry Jr.
***
“Maana yangu huyu binti yupo hai”
Eddy akamtizama Madam Mery huku akiwa
amemkazia macho makali, Eddy akakumbuka siku
ambayo alirudi katika kazi ya kuwaokoa Phidaya,
alipo rudia nyumbani kwa Amina, rafiki wa Manka
aliye kwenda kufanya naye kazi ya kuikomba
familia yake, alikuta nyumbani kwa Amina
kumetulia sana, akakumbuka jinsi alivyo weza
kushuka na masanduku ya pesa na kuingia nayo
ndani, ndipo alipo weza kukuta michirizi mingi ya
damu kwenye sakafu pamoja na ukutani, ila kabla
hajagundua lolote ndipo alipo weza kuvamiwa na
kikundi cha kigaidia huku, Shamsa akiwa ni
miongoni mwa magaidi hao.
Eddy akamgeukia Shamsa na kumtazama kwa
macho makali, akihisi hili jambo anaweza
kuligundua, ila Shamsa hakuonyesha dalili yoyote
ya kufahamu kitu kinacho zungumzwa hapo.
“Mimi ndio niliye weza kumchukua Manka”
Madam Mery alizungumza na kumfanya Eddy
kumtazama vizuri Madam Mery
“Tuligundua uwepo wako nchini Somalia,
tulifwatilia hadi sehemu ambayo ulifikizia, hadi
siku unatoa na yule binti….”
“Binti, binti gani?”
“Uliye ongozana naye kwenye kazi ya kwenda
kuvamia kundi lilolo mteka mke wako”
Eddy akakumbuka vizuri kwamba binti huyo
alikuwa ni Amina.
“Ndipo nilipo weza kuvamia huku nyuma na
kumchukua Manka na kuondoka naye, ila niliacha
vijana wawili wawasubiri hadi murudi,
wawaangamize”
Mapigo ya moyo yakaanza kumuenda mbiao Eddy,
kwani anayo yazungumza Madam Mery ni mambo
ambayo yanazidi kuumiza moyo wake.
“Vijana wangu waliweza kumuona binti huyo
akirejea peke yake ndipo walipo weza kumvamia,
na kumuua, ila waliondoka naye. Asubuhi yake
wakamtupa barabarani”
Shamsa akastuka na kufumba mdomo wake kwa
mshangao mkubwa, kwani tukio la wao kuelekea
kwenye kambi ya wakimbizi majira ya asubuhi,
waliweza kuuona mwili wa dada mmoja ukiwa
umelazwa katikati ya barabara huku macho yake
yakiwa yametobolewa,
Eddy kwa hasira akamsukuma Madam Mery
kwenye sofa na kuiwahi shingo yake na kuanza
kuiokaba, huku machozi yakimwagika, mwili mzima
ukimtetemeka.
“Eddy usimuuee”
Shamsa alizungumza huku akiushikilia mkono wa
Eddy ulio ishika shingo ya madam Mery, aliye anza
kutepa tapa huku akijaribu kuzungumza kitu
“Ed…dy un…iniu…a hu…toj..ua siri za DFE”
“DEF, NDIO NINI WEWE MALAYAAAAAAAAAAAAAA”
Eddy alizungumza kwa hasira kali hadi Shamsa
akasogea pembeni, kwani hakuwahi kumuona Eddy
akiwa amekasirika kwa kiasi kikubwa kama hicho.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 22 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (22)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“Eddy usimuuee”
Shamsa alizungumza huku akiushikilia mkono wa
Eddy ulio ishika shingo ya madam Mery, aliye anza
kutepa tapa huku akijaribu kuzungumza kitu
“Ed…dy un…iniu…a hu…toj..ua siri za DFE”
“DEF, NDIO NINI WEWE MALAYAAAAAAAAAAAAAA”
Eddy alizungumza kwa hasira kali hadi Shamsa
akasogea pembeni, kwani hakuwahi kumuona Eddy
akiwa amekasirika kwa kiasi kikubwa kama hicho.
ENDELEA
Eddy akaendelea kuliminya koo la madam Mery.
Kiasi cha kumfanya aanze kufurukuta kama mtu
anaye kata roho.
“Babab unamuuaaaaaa”
Shamsa alizungumza kwa sauti ya juu na yenye
uklali sana, Eddy akaigeuza sura yake na
kumtazama Shamsa, akamkuta akimwagikwa na
machozi mengi usoni mwake. Eddy akamuachia
Madam Mery, akakamata moja ya kiti kilichomo
ndani ya chumba hicho na kukitupa chini kwa
nguvu hadi kikakatika.
“Fu***”
Eddy alizungumza huku akijishika kichwa cheke
akijaribu kuituliza hasira yake iliyo pitiliza, walinzi
wake wapatao wanne wakaingia ndani ya chumba
baada ya kusikia kishindo kizito cha kiti hicho.
huku wakiwa na bastola zao mikononi.
“Bosi vipi?”
Mkuu wao alimuuliza ila Eddy hakujibu chochote
zaidi ya kuyang’ata meno yake kwa hasira,
Shamsa akatingisha kichwa akiwaashiria kwamba
wamuche na watoke nje, wasi[o ubishi wowote
wakatii na kutoka nje. Sauti ya meno ya Eddy jinsi
anavvyo yatafuna kwa nguvu na kwa hasira,
ikatawala ndani ya chumba, kila mmoja akawa
kimya kabisa hususani madam Mery ambaye
hakudhubutu hata kuutingisha mguu wake
akiogopa kitendo kilicho jitokeza muda mchache
ulio pita kinaweza kujirudia. Isitoshe anamfahamu
vizuri Eddy akiwa kwenye hasira kali anaweza hata
kuua.
“Am sorry”
Eddy alizungumza huku akikaa kwenye sofa,
akiendelea kuhema kwa hasira kama simba dume
lililo kosa mawindo yake aliyo kuwa akiyasubiria
kwa muda mrefu. Samahani ya Eddy hapakuwa na
aliye ijibu si Shamsa wala madam Mery kila mmoja
akawa kimya kama vile hayupo ndani ya chumba
hicho.
“Shamsa kalete vinywaji”
Shamsa akamtazama Madam Mery aliye kaa
kiunyonge kwenye sofa, akamtazama Eddy ila
akakutana na macho makali yaliyo mfanya atoke
ndani ya chumba pasipo kumuaga yoyote. Ukimya
ukaendelea kutawala hadi alipo rejea shamsa
akiwa na glasi tatu za juisi. Akampa kila moja glasi
yake na yeye akabakiwa na glasi yake.
“Ed…….”
Eddy akamkatihs Shamsa kwa kunyanyua mkono
wake wa kulia, ili Shamsa asiendelee na anacho
hitaji kukizungumza kwa wakati huo.
“Kalaleni tutazungumza asubuhi”
Kwa sauti nzito aliyo itumia Eddy. Madam Mery
akawa wa kwanza kunyanyuka kwenye sofa,
Shamsa akafwatia wote wakatoka ndani ya chumba
hicho na kumuacha Eddy peke yake wakiwa hatua
kadhaa kutoka kwenye mlango wa chumba hicho
wakasikia mlio waglasi ukipasukua. Shamsa
akataka kurudi ila madam Mery akamshika mkono
akimuomba asifanye hivyo.
“Muache atakuwa salama”
Madam Mery alizungumza kiunyonge huku akiwa
amemshika mkono Shamsa, taratibu wakaondoka.
Wakapandisha gorofani kwenye vyumbavya kuiala.
Machozi mengi yakaanza kumwagika Eddy, kila
alipo ikumbuka sura ya mwanae, machozi
yakaendelkea kumwagika, akijiona ni baba ambaye
hana thamani tena kwenye haya maisha kwani
ameshindwa kumlinda mwanae kuepuka ajali
ambayo ilitokea. Akalishika faili lenye picha ya
Manka, kwa hasira akaitoa kwenye faili hilo na
kuiminya minya, kwa nguvu.
“Wewe na baba yako ni lazima niwaue”
***
“Ni m,uda wa kuonndoka sasa”
Mzee Godwin alimuambia Manka anaye onekana
kuwa bize sana na kufwatilia taarifa za Fetty
pamoja na wezake kwenye mtandao.
“Ni muda wa kuondoka sasa”
Mzee Godwin alizuingumza baada ya kila kitu
kukiweka sawa, akishirikiana na Tom ambaye hadi
sasa havi aelewi kitu cha aina yoyote
“Babu kwahiyo tunarudi kijijini?”
“Hapana Tom, tunakwenda nje ya nchi ya
Tanzania. Tuna pesa ya kutosha ni muda sasa wa
sisi kuondoka”
Tom ikamlazimu kukubali hivyo hivyo kwani
anayaelewa maisha ya kijijini mwao kwamba ni
magumu sana kupindukia. Wakasaidiana kubeba
mabegi yenye fedha ya kutosha pamoja na silaha
baadhi, wakatoka kwenye handaki hili lililopo chini
ya ardhi. Wakaingiza mizigo yot e kwenye gari.
“Ila kabla hatujaondoka, Manka nahitaji uifanye kazi
moja”
“Kazi gani baba?”
Mzee Godwina akamvuta pembeni Manka
kumuambia hiyo kazi, ambayo Tom hakupaswa
kuweza kuisikia, wakarudi na kuingia ndani ya gari
na safari ikaanza. Ukimya mwingi ukatawala ndani
ya gari, kila kinacho endelea kwernye maisha yake
Tom alihisi ni kama muujiza kwani hakutarajia ipo
siku atakuja kukutana na pesa nyingi kama waliyo
iweka kwenye babegi yao. Usiku mzima
wakautumia katika kusafiri barabarani hadi
wakafika mkoani Arusha, pasipo kukamatwa na
askarti, hii ni kutokana na gari waliyo itumia ni gari
ya polisi. Majira ya saa kumi alfajiri wakawa
wamewasilia mkoani Arusha, wakamshusha Manka
na kumkabidhi kiasi cha kutosha cha pesa, pamoja
na silaha ambazo Manka alihitaji kuweza kuzitumia
katika kazi yake iliyop[o mbeleni mwake. Mzee
Godwin na Tom wao wakaendelea na safari yao
kuelekea nchini Kenye.
“Arusha nimerudi tena”
Manka alizungumza mara baada ya kuingia kwenye
moja ya mgahawa ulio funguliwa, alfajiri na
mapema, akapata supu nzito kwa ni tangu jana
hakuweza kupata chochote mdomoni mwake, alipo
jiweka sawa akaelekea kwenye moja ya nyumba
ambayo anaimiliki, ili kujipanga vizuri kwa kazi
ambayo anakwenda kuiendea
***
Agnes machale yakanza kumcheza akasimam kwa
haraka na kuelekea dirishani, akafungua pazia, na
kutazama nje, akaona gari kadhaa nyeusi
zikisimama chini ya hoteli hiyo, wakashuka watui
wapatao nane walio valia suti nyeusi na kuingia
kwenye hoteli yao.
“Shit”
Agenes akarudi kwa haraka kwenye laptop yake,
akaizima kwa haraka na kuiweka kwenye begi lake,
jambo lililo poteza mawasiliano na chumba cha
mawasiliano Ikulu.
“Jaquline mambo yameharibika fanya utoke huko,
wamenifwata huku”
Taarifa aliyo itoa Agnes ikampa waswasi mwingi
Jaquline aliyomo kwenye ukumbi wa sherehe ndani
ya ikula ya Marekani. Agnes kila kitu muihimu
ndani ya begi lake la mgongoni, akaitoa bastola
yake, akachomoa magazine, akakuta risasi za
kutosha. Akaifunga kiwambo cha kuzuia sauti,
kisha akatoka ndani ya chumba alichopo.
Akaangalia kordo ndefu yenye milango mingi
kwenye kila upande, akashusha pumzi nyingi,
akaziweka vizuri nyele zake ndefu na kuanza
kutembea kwenye kordo hiyo akiwa tayari kwa
lolote litakalo jitokeza kwemye kordo hiyo kwani
anatambua ni lazima askari hawa watatumia lifti
kuweza kufika kwenye gorofa aliyo kuwepo yeye.
Akafika kwenye milango miine ya lifti iliyopo
kwenye kordo hiyo, Kila lifti ikawa inamuonyesha
inakuja juu, huku namba za jinsi lifti inavyo soma,
pale zinapo pita kila gorofa, ikionekana pembeni.
“Wapop gorofa ya sita eheee”
Agnes alijisemea huku akiendelea kuzihesabu
namba hizo kwani yeye yupo gorofa ya tisa.
Akataka kuondoka ila akasita, akachomoa bastola
yake na kusimama kwenye moja ya lifti ya upande
wa kushoto kwake. Lifti hiyo ilipo fika gorofa ya
tisa mlango wake ukafunguka, macho ya askari
wawili waliomo kwenye lifti hiyo yakakutana na
macho ya Agnes aliye shika basatola a;iyo
waelekezea. Agnes akatingisha kichwa akiwaashiria
wasifanye chochote na bastola zao walizo zishika,
kwa haraka akaingia ndani ya lifti hiyo na kuifunga.
“Wekeni chini silaha zenu”
Askari hao wakafanya kama walivyo agizwa
kufanya, askari walio kuwa kwenye lifti nyingine
wakaelekea kwenye chumba walicho elekezwa na
wahudumu kwamba ndipo alipo binti wanaye
mtafuta, pasipo kugundua kwamba wezao
wamewekwa chini ya ulizni mkali wa bnti huyo
huyo wanaye mtafuta..
“Upo salama Agy”
“Yap”
“Upo wapi sasa hivi?”
“Kwqenye lifti na maboya wawili nimewaweka chini
ya ulinzi”
“Ok hakikisha kwamba huwaui kwani itakuwa ni
hali nyingi mbaya kwetu sote”
“Poa dada Jaqie
Agnes alizungumza kiswahili akiamini kwamba
askari hao kutoka ikilu hawaelewi chochote
kinacho endelea katika mazungumza hayo, lifti
hiyo ikaelekea hadi gorofa ya mwisho ya ishirini.
Agnes akawaamuru askari hao kutoka ndani ya lifti,
wakapandisha ngazi hadi juu kabisa ya gorofa hilo.
Askari wengine, wakafika kwenye chumba ambacho
walielekezwa, hawakukuta mtu yoyote zaidi ya vitu
vilivyo changuliwa changuliao ikionekana
muhusika alitoroka muda mchache ulio pita.
“Where is team C”(Ipo wapi timu C)
Mkuu wao aliuliza baada ya kuona vijana wake
wawili hawapo, ikawabidi kuanza kufanya
mawasiliano na vijana hao kupitia vifaa maalumu
vya vinasa sauti walivyo vivaa kwenye masikio
yao.
Kwa tukio la kuwashutkiza, Agnes akawapiga askari
hao nyuma ya shingo zao, na wote wakapoteza
fahamu na kuanguka chini. Vishindo hivyo
vikawastua wezao ambao wahawakujua ni wapi
walipo. Agnes akatazama eneo lote la juu ya
gorofa hiyo, akagundua kuna moja ya gorofa ipo
karibu sana na gorofa hiyo, ambayo hiyo kidogo
ipo chini kidogo.
“Hapa naruka”
Askari wakaanza kupata mashaka na kurudi kwa
haraka kwenye lifti zao, na kupandisha juu kabisa
ya gorofa hiyo wakiamini ndipo walipo wezao.
Wakafika gorofa ya ishirini wakapandisha kwenye
gazi ambazo zinaelekea moja kwa moja juu kabisa
ya gorofa hiyo, kitendo cha wao kufika tu
wakashuhudia binti wanaye mtafuta akiruka kwenye
gorofa nyingioni ya jirani.
“Mfwateni huyo”
Mkuu wao alitoa agizo ambalo vijana wake wawili
wakaanza kutimua kasi, kujaribu kwenda kuruka
kama alivyo fanya binti huyo anaye onekena kuwa
na utaalamu wa kipekee wa kuruka sana kutoka
sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Agnes
akasimama huku akiliweka vizuri begi lake la
mgongoni, akachomo bastola yake na kuwatazama
vijana wawili wanao jiandaa kuruka kumfwata, wa
kwanza akajitahidi kuruka, akiwa hewani katikati ya
gofa hilo kwenda jengine, akakutana na risasi mbili
za miguu zilizo mfanya kupoteza muelekeo badala
ya kwenda mbele akajikuta akianza kwenda chini
kwa kasi, jambo lililo mstua mwenzake akasita
kufanya alicho fanya mwenzake huyo aliye
mshuhudia akiangukia kwenye gari lililo egeshwa
chini pembeni ya gorofa hizo.
“LUKASSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS
SSSSSSSSS…………………………………………..!!!!”
Askari huyo alipiga ukelele wa maumivu na
uchungu baada ya kumshudia mwenzake huyo
akikata roho, yeye akiwa gorofani, kelele hizo
zikawafanya askari wangine walio kuwa wakiwa
huduma ya kwanza wezo kukimbilia alipo
mwenzao. Agnes akatabasamu kwa dharau kisha
akamnyooshea kidole cha kati askari huyo anaye
lia kwa uchungu kisha akaondoka zake kwa
kujiamini sana.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 23 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (23)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“LUKASSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS
SSSSSSSSS…………………………………………..!!!!”
Askari huyo alipiga ukelele wa maumivu na
uchungu baada ya kumshudia mwenzake huyo
akikata roho, yeye akiwa gorofani, kelele hizo
zikawafanya askari wangine walio kuwa wakiwa
huduma ya kwanza wezo kukimbilia alipo
mwenzao. Agnes akatabasamu kwa dharau kisha
akamnyooshea kidole cha kati askari huyo anaye
lia kwa uchungu kisha akaondoka zake kwa
kujiamini sana.
ENDELEA
Agnes akaanza kushuka chini kwa kutumia ngazi
katioka gorofa aliyo ingia huku mara kwa mara
akifanya mawasiliano na Jaquline ambaye aliamua
kusitisha zoaezi la kumteka raisi, akatoka nje, gari
aliyo kuja nayo ikamchukua na moja kwa moja
akaelekea sehemu ambayo Agnes alimuelekeza
***
Hadi kuna pambazuka Eddy, hakuweza kupata hata
lepe la usingizi, akanyanyuka kwenye kiti alicho
kuwa amekaa usiku kucha, akatoka nje na moja
kwa moja akaelekea kwenye makaburi ya familia
yeka. Akasimama kwa dakika kadhaa akiyatazama
makaburi hayo, hakuamini kwamba ni kweli familia
yake imeweza kupotea gafla na kubaki akiwa peke
yake, kila alipo mfikiria mzee Godwin machozi ya
hasira na uchungu ndivyo yalivyo zidi kumwagika.
Akastukia akishikwa mkono wake wa kushoto
taratibu akaigeuza shingo yake na kumkuta
Shamsa akiwa amesimama pembeni yake huku
naye akionekana kuwa na huzuni nyingi sana
usoni mwake.
“Madam Mery ameondoka”
Shamsa alizungumza kwa sauti ya unyonge huku
macho yake akiwa ameyaelekezea kwenye
makaburi hayo matatu
“Amekwenda wapi?”
“Hakuniambia ni wapi alipo kwenda”
“Achana naye”
“Ila baba, kuna mambo mengi muhimu
amaniambia nikuambia”
“Mambo gani?”
Eddy alizungumza huku akimtazama Shamsa usoni
aliye onekena kusita kwa kile ambacho anahitaji
kwenda kukizungumza mbele ya Eddy anaye
mchukulia kama baba yake mlezi.
“Mbona umekaa kimya huwezi kuzungumza?”
“Ni ni kuhusiana na baba yako?”
“Baba yangu……!!”
“Ndio mzee Godwin”
Eddy akatazama kila kona, akamshika mkono
Shamsa, wakatafuta sehemu iliyo tulia kwenye
moja ya bustani zilizopo ndani ya njumba lake la
kifahari.
“Alikuambia kuhusiana na nini?”
“Jana usikua alinieleza kila kitu kuhusiana na
kikundi cha D.F.E. Hicho ni kikundi ambacho
kimeanzishwa na mzee Godwin mwenyewe, kazi
yake kubwa ni kuhakikisha kwamba wanalipiza
visasi kwa wale wote ambao waliweza
kuwatemndea ubaya katika maisha yao.”
“Aliniambia kwamba hicho ni kikundi kikubwa sana
na kina wafuasi wengi ambao wengine wamo ndani
ya serikali yetu ya Tanzania, na anashirikiana nao”
“Amekutajia majina?”
“Hapana hajanitajia majina. Ila anadai wafuasi hao
ni watu wakubwa sana serikalini, si Tanzania pekee
bali nchi nyingi za Afrika pamoja na nchi za
Amerika, ikiwemo Marekani”
Shamsa akanyamaza kimya kidogo kisha
akaendelea kuzungumza kwa umakini kile alicho
ambiwa kukizungumza kutoka kwa madam Mery
ambaye alihofia kufanya hilo.
“Watu hao wana chata ndogo kwenye sehemu za
miili yao, yenye maandishia meusi D.F.E.
Ameneniambia kwamba msaidizi wa mambo yote
ya kikundi hicho ni mtu ambaye anakujua vizuri
kuanzia A hadi Z, ukimuachilia kiongozoi wao
mzee Godwin”
“Ni nani huyo?”
“Alinitajia kwa jina moja tu……..JONH”
Eddy akatumbua macho yake huku akimtzama
Shamsa, akiwa haamini kitui alicho kizungumza
kwani kumbukumbu ya mwisho anakumbuka jinsi
alivyo vikata viungo vya John kwa kulipiza kisasi
cha mambo yote aliyo mfanyia.
“JOHN…..JOHN…….!!!”
“Ndio huyo huyo John, pia ameniambia mtu wa
kwanza kuweza kulengwa katika mikakati yao ni
wewe, wanataka kukuangusha chini, ten echini
kabisa ya aridhi”
Eddy akajikuta akishusha pumzi nyingi, woga wa
gafla ukamuingia moyoni mwake, kajasho
kembamba kakaanza kumwagika kwani hakujua ni
jinsi gani ambavyo wanaweza kumuangusha.
“Ahaa….aaaa aahaame ame kwenda wapi Madam
Mery?”
“Hakuaniambia ni wapi anapo elekea kwa sasa, ila
kitu kingine cha mwisho alicho niambia nikuambia
ni kwamba, ujiudhuru nafasi yako hiyo ya uongozi
kwani ni rahisi kwa wao kuweza kukupata, pili kati
ya watu ambao unafanya nao kazi serikalini wana
kisasi na wewe, ikiwemo wale ambao uliwaharibia
biashara zao kipindi ambapo iliingia madarakani,
wana uchungu na kisasi kikubwa juu yako”
Eddy akahisi kichwa chake kinapasuka kwa
maumivu makali ambayo anayapata kwa taarifa
hiyo ambayo si nzuri kwa upande wake. Taratibu
akanyanyuka kwenye kiti alicho kaa na moja kwa
moja akaelekea ndani kwake. Akafungua kabati lake
lenye baadhi ya vitu muhimu, akatoa kikopo kidogo
chenye dawa za kutuliza mawazo, akatoa vidogo
kadhaa na kuvimeza, pasipo kutumia maji, kisha
akajitupa kitandani.
“Kwa nini kila kitu kinanitokea mimi
tuuuuuuuuuuuuu”
Eddy alizungumza kwa sauti ya ukali iliyo jaaa
jasira na uchungu ndani yake, akiwa katika
kuhangaika hangaika kitandani kujaribu kuutafuta
japo usingizi, mlango wake ukagongwa mara mbili.
“Nani?”
Mlango ukafunguliwa pasipo mtu huyo kujibu,
Eddy akamkuta Rahab akiwa amesimama mlangoni
peke yake, Rahab akapiga hatua moja mbela na
kuufunga mlango kwa ndani.
“Umefwata nini huku ndani?”
Eddy alizungumza huku akishuka kitandani
“Nimekuja nahitaji kuzungumza na wewe?”
Rahab alizungumza huku akipiga hatua kadhaa
kumfwata Eddy kitandani
“Twende tukazungumzie nje ila si ndani ya
chumba ninacho lala na mke wangu”
Eddy alizungumza kwa ukali kidogo, hakujali Rahab
ni mke wa raisi au laa, kabla Eddy hajafika
mlangoni Rahab akamuita na kumfanya Eddy
kugeuka na kutazama ni kitu gani ambacho Rahab
anamuitia.
“Eddy ninakupenda?”
“Upo sawa wewe?”
“Ndio nipo sawa, na ninacho kizungumza ni kitu
kitokacho moyoni mwangu”
Rahaba akapiga hatua kadhaa hadi alipo simama,
wakatazama kwa muda, kitendo ambacho kikaanza
kumfan ya Rahab kumwagikwa na machozi.
“Eddy nipo tayari kuacha kila kitu kwenye maisha
yangu, ili niwe na wewe. Wewe ni mwanaume wa
kwanza katika haya maisha yangu kukupenda, ni
mwauaume abaye umeweza kuziteka hisia zangu
tangu siku ya kwanza nilipo kuona picha yake
nyumbani kwa mama yako”
“Eddy nimekuwa mtumwa kuanzia siku hiyo
nimekuwa ni mtu wa kuishi na majuto ya kwanini
niliamua kuolewa na Praygod, ambaye si chagua la
moyo wangu”
***
Wasiwasi mwingi ukaanza kumtawala Raisi
Praygod, kila alipo jaribu kuipiga simu ya mke
wake, inaita hadi kukata, akamuita mlinzi wake
mmoja anaye muamini sana.
“Mama yupo wapi?”
“Ametoka kama dakika kumi zilizo pita hivi”
“Ameenda wapi?”
“Hakuniambia, ila ngoja kwanza nimpigie dereva
wake”
Kijana huyo akatoa simu yake mfukoni na kumpigia
dereva wa madam Rahab, simu ikaita baada ya
muda ikapokelewa
“Upo wapi?”
“Nipo nyumbani kwa muheshimiwa Eddy”
“Upo na madam?”
“Ndio, ameingia ndani?”
“Mlinzi wake yupo wapi?”
“Yupo nje ya gari, kwani vipi?”
“Ahahaa hakuna kitu”
Kijana huyo akakata simu, na kumtazama raisi
Praygod anaye onekena kujawa na wasiwasi kwani
si kawaidia ya mke wake kuto kupoke simu kwa
kipindi kirefu.
“Yupo kwa waziri wa ulinzi bwana Eddy Godwin”
‘Eddy Eddy’
Wivu wa mapenzi ukaanza kuusumbua moyo wa
raisi Praygod, kila alipo jaribu kuvuta baadhi ya
kumbukumbu, siku jinsi alivyo wakuta Eddy na
mke wake kwenye chumba cha waziri huyo kijana
mdogo, alihisi kitu kilicho kuwa kikiendelea ila
hakuweza kukiweka kichwani mwake akiamini
kwamba ni jambo la kawaida.
‘Kwanini leo tena aende kama walisha maliza
kuzungumza jana?’
Raisi Pryagod alijiuliza tena kichwani mwake swali
ambali jibu lake likajaa wasiwasi mwingi,
akakumbuka kitu kimoja kilicho mstua, wakati
Rahab anamueleza anakwenda kuonana na Eddy
kwenye chumba chake, rangi ya mdomoni mwake,
ilikuwa imekolea vizuri tu. Ila alipo ingia na
kuwakuta rangi hiyo ya mdomoni haikuwa kama
vile alivyo ingia nayo.
‘Au alimkiss mke wangu kilazima?’
Hapo ndipo raisi Praygod akahisi kuna kitu
ambacho kinaendelea kwa watu wawili hao, asira
na uchungu mkali ukampanda moyoni mwake.
“Andaa ndege nahitaji Eddy na mwanae aliye baki
wapelekwe mbali na Tanzania”
“Sawa muheshima na tuwapeleke wapi?”
“Popote ila mbali na Tanzania, na hii taarifa
umpelekee baada ya kila kitu kuwa sawa”
“Sawa muheshimiwa”
“Ila Lube, hakikisha kwamba hili jambo umuelezi
mke wangu, iwe siri yako mimi na wewe”
“Sawa muheshimiwa”
“Pia hakikisha unawafwatilia hatua moja hadi
nyingine, na kila kinacho endelea hakikisha
kwamba unaniambia”
Raisi Praygod akajikuta akiachia tusi zito, lililo jaa
hasira, akihisi hali ya mahusiano kati ya Eddy na
Rahab
“Nitakuuaa wewe mshezi Eddy”
***
Madam Mery akiwa ndani ya basi la Ngorika
liendalo mkoani Arusha, mawazo mengi
yakamtawala moyoni mwake, kila alipo jaribu
kufikiria mambo aliyo mfanyia Eddy, roho yake
ilizidi kumuuma sana hadi wakati wingine
akatamani kufa kwani hastahili kabisa kuwa
binadamu anaye paswa kusamehewa.
Akaanza kukumbuka jinsi mahusiano mazuri yaliyo
kuwepo kati yake na Mzee Godwin, kipindi alipo
mleta Eddy shuleni kwake kumuanzisha kidato cha
tano. Ni siku ambayo mzee Godwin aliweza
kumkabidhi Eddy kwake awe anamtzama kwa kila
kitu na hata baadhi ya pesa ya matumizi ya Eddy
aliweza kumuachia endapo Eddy ataishiwa na pesa
iwe rahisi kumsaidia. Uchshi, ukaribu na uzuri wa
Eddy, ndivyo vitu ambavyo vilimkosesha ujasiri na
ustahimilivu wa kuzuia hisia zake za mapenzi juu
ya Eddy. Kitu kilicho muumiza akili ni jinsi gani
ambavyo angeweza kumuanza Eddy katika swala
zima la mahusiano isitoshe yeye alikuwa ni
mwalimu wake.
Siku ambayo aliweza kumkuta Eddy chumbani
kwake akiwa ameshika mdoli wake ulio kaa kama
jinsia ya mwaume, alio kuwa akiutumia katika
kujichua pale hamu, zinapo mzidi, ndipo ikawa
nafasi yake ya kuweza kufanya kila kitu kwa ajili ya
kumpata kijana huyo aliye tokea kuutesa moyo
wake.
‘Mapenzi yalinifanya niwe mjinga’
Madam Mery alijisemea kimoyo moyo huku
akiachia tabasamu dogo, kila alipo kumbuka
mambo ambayo walifanya kitandani na Eddy,
akajikuta akizidi kuumia sana moyoni mwake
‘Eddy am sorry again’
Hapo machozi yakamwagika madam Mery hata
kijana aliye kaa naye pembeni ya siti akashnagaa
ni kwanini mama huyu anamwagikwa na machozi.
***
Rahab akaikamata shingo ya Eddy, kwa haraka
akaupeleka mdomo wake, kwenye lipsi za Eddy,
safari hiii akatuma kila aina ya mbinu kuhakikisha
anapata penzi la Eddy, ambaye mwanzoni alikuwa
ni mgumu sana kuweza kumruhusu Rahab kuweza
kufanya hivyo. Ila Rahab akafanikiwa kupeleka
mikono yake sehemu ambayo, hisia za kimapenzi
za Eddy ndipo zilipo. Wakiwa kama watu wanao
kimbizwa wakajikuta wote wakivua nguo zao na
kubaki kama walivyo zaliwa, Eddy akambeba Rahab
hadi kwenye kitanda na kuanza kuonyesha ujuzi
wake kwenye kitengo hicho cha kitandani ambacho
hakina cheo maalumu kwa mtu yoyote. Kwa raha
ambazo Rahab alianza kuzisikia akajikuta akipiga
makelele kama mtoto mdogo, kwa mara kadhaa
akajikuta akilitaja jina la Eddy.
“Madam yupo wapi?”
Lube alimuuliza mlinzi wa kike wa Rahab, mara
baada ya kufika nyumbani kwa waziri Eddy.
“Yupo ndani, anamazungumza muhimu
anazungumza na muheshimiwa”
“Nina ujumbe wake nahitaji kwenda kumuona”
“Sawa”
Latifa hakuwa na wasiwasi wowote kwani Lube ni
miongoni mwa walinzi wanao walinda raisi
Praygod pamoja mke wake. Lube akaingia hadi
sebleni hakumkuta mtu yoyote, baada ya kutaza
maeneo yote ya vyumba vya chini, pasipo
kuwaona Eddy na Rahab. Ikambidi kupandisha
gorofani kutazama seble nyingine ambayo alihisi
kwamba wanaweza kuwemo humo, ila cha
kushangaza hakuweza kuwaona. Akiwa
amesimama sebleni akautazama mmoja wa
mlango, ambao akahisi kitakuwa ni chumba cha
kulala cha waziri Eddy, akatembea kwa hatua za
kunyata hadi kwenye mlango huo.
Lube hakuamini kusikia miguno ya kimahaba, huku
sauti ya mke wa raisi, ikiwa imeizidi sauti ya waziri
Eddy.
“Eddy nipo tayari kumuacha mume wangu, niende
popote na wewe”
Maneno hayo ya Rahaba yakamstua sana Lube.
Lube akakumbuka maneno ya raisi Praygod aliyo
toka kumumbia muda mchache ulio pita kwamba
awafwatilie watu hao hatu kwa hatua na chochote
ambacho kitaendelea ajulishwe. Kwa haraka Lube
akatoa simu yake mfukoni, akaingia upande wa
kurekodi sauti, na kuanza kurekodi sauti hizo za
mahaba zilizo jaa ahadi nyingi za kimapenzi,
ikiwemo sifa kedekede ambazo Rahab anamwagia
Eddy. Lube akiwa anaendelea kurekodi tukio hilo
kwa sauti, Shamsa akasimama nyuma yake na
kushuhudia kila kitu ambacho Lube anakifanya nje
ya mlango wa baba yake, kitu kilicho mchukiza
sana Shamsa, na kujikuta akimshika bega Lube,
kwa ajili ya kujmshambulia kuzuia sirihiyo kuweza
kuvuja
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 24 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (24)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Kwa haraka Lube akatoa simu yake mfukoni,
akaingia upande wa kurekodi sauti, na kuanza
kurekodi sauti hizo za mahaba zilizo jaa ahadi
nyingi za kimapenzi, ikiwemo sifa kedekede
ambazo Rahab anamwagia Eddy. Lube akiwa
anaendelea kurekodi tukio hilo la sauti, Shamsa
akasimama nyuma yake na kushuhudia kila kitu
ambacho Lube anakifanya nje ya mlango wa baba
yake, kitu kilicho mchukiza sana Shamsa, na
kujikuta akimshika bega Lube, kwa ajili ya
kujiandaa kumshambulia kuzuia siri hiyo kuweza
kuvuja.
ENDELEA
Kitendo cha Lube, kugeuka akakutana na kofi zito
la uso lililo mfanya kufumba na kumfumbua macho
yake mara kadhaa na kigiza kikali kikapita kwenye
usawa wa macho yake asitambue kofi hilo
amepigwa na nani, kabla hajajiweka sawa, ngumi
nzito, ikatua tumboni mwake na kujikuta akijikunja,
huku akigugumia mguno mkali wa maumivu, kigoti
kikatua kwenye kidevu chake na kumfanya
anyanyuke juu pasipo kupenda, huku baadhi ya
meno yake yakigongana gongana kinywani mwake.
Shamsa kwa haraka akamdaka shingo Lube na
kumpokonya simu ailiyo ishika na kuidumbukiza
mfukoni mwa suruali aliyo vaa, kisha kwa haraka
akaupitisha mkono wake mmoja kwenye kiuno cha
Lube na kuikuta bastola ikiwa imechomekwa
nyuma ya kiuono chake, akaichomoa na kuishika
mkononi mwake na kuendelea kumgandamiza
Lube ukutani.
“Nani amekutuma?”
Shamsa alimuuliza Lube kwa sauti ndogo ambayo
si rahisi kwa watu waliomo ndani kuweza kumsikia,
Lube akabaki akiwa katika kushangaa shanga,
kwani hakuamini mtu anaye mshushia shambulio
hilo ni binti ambaye mara nyingi anamuona ni
mpole na mnyonge sana. Gafla akastukia kichwa
kizito kikitua kwenye pua yake na kumfanya atoe
ukelele mkali hadi Eddy na Rahab wakastuka,
wakiwa katikati ya mchezo wao.
“Kuna nini huko nje?”
Eddy alizungumza huku akiutazama mlango wa
kuingilia chumbani kwake, kwani sauti hiyo
inaonekana kutokea nje ya mlango wake.
“Mmmm hata sijui”
“Ngoja nitazame”
“Bwana acha, tumalizie raha yetu”
Rahab akamshinda Eddy kwenye maamuzi na
kuamua waendelee na kitendo chao, kinacho
wafurahisha sana. Shamsa, alipo muona Lube
amelegea kwa pigo hilo akamvu na kumuingiza
ndani ya chumba chake na kumsukumia kwenye
sofa.
“Wewe ni nani?”
“Ehehehheee……………..!!!”
“Nakuuliza wewe ni nani?”
Shamsa alizunngumza kwa sauti ya ukali hadi
Lube akaanza kutetemeka kwa owga, Lube akatoa
kitambulisho chake na kumuonyesha Shamsa
kwamba yeye ni miongoni mwa wafanyakazi wa
ikulu na nimlinzi wa kiongozi wa nchi raisi
Praygod Makuya.
“Nani amekutuma?”
Likawa ni swali jengine lililo mfanya Lube kuwaza
meneno ambayo raisi alimuambia masaa
machache nyumba kwamba iwe siri kati yao na
asimuambie mtu wa aina yoyote.
“Hakuna aliye nituma”
Luba akajibu kwa dharau huku akiikunja midomo
yake, akijiona amekuwaje kupigwa na kabinti
kadogo ambacho alikachukulia kama kimdoli
“Ahaa hakuna eneee……….!!”
Bila ya hata huruma, Shamsa akamtandika Lube
teke lililo tua kwenye sehemu zake za siri na
kumfanya Lube kujikunja na kugugumia kwa
maumivu makali ambayo hakuwahi kuyapata tangu
kuzaliwa kwake. Shamsa akaikoki bastola ya Lube
na kumuelekezea, akionekana hana masihara hata
kidogo na endepo Lube ataleta ujinga basi risasi
zilizomo kwenye bastola hiyo zitaishilia mwilini
mwake. Shamsa akarudi nyuma nyuma hadi
kabati. akafungua kabati lake la nguo, akatoa moja
ya mkanda wa suaruali, akamvuta Lube kutoka
kwenye sofa aliyo kaa na kumuangusha chini.
Luba akajigeuka kwa kasi ya ajabu na kuichota
miguu ya Shamsa na kumuangusha chini na
kuifanya bastola aliyo ishika kuangukia pembeni.
Wote wakajikuta wakinyanyuka kwa pamoja na
kukunja ngumi za mikono yao. Lube akatema
kwanza fumba la mate lililo jaa damu. zilizo tokana
na kichwa alicho tandikwa nje, Shamsa
akauzungusha mkanda mara mbili mkononi mwake
kuhakikisha kwamba mkando huo hauwezi
kumponyoka.
Lube akarusha la hewani, Shamsa aliweza kuliona
mapema, kwa kasi ya ajabu akabonye chini,
akanyanyuka kwa ngumi nzito iliyo tua sikioni mwa
Lube na kumfanya ahisi ukelele mkali, kwenye
sikio hilo. Akatingisha kichwa chake mara kadhaa
akijitahidi kuyaondoa maumivu hayo makali.
“Umeniotea eheeeee”
Lube alizungumza huku akifungua vifungo vya
shati lake, akakunja mikono ya shati hilo iliyo
mirefu, akajinyoosha viungo vyake kiasi na
kujiweka sawa. Shamsa akamtazama jinsi Lube
alivyo jiweka kwa haraka akakimbia kwenye pembe
ya kitanda, akakanyaga na mguu wa kushoto,
ukaupa fursa mguu wa kulia kugeuka na teke zito
lililo yua shingoni mwa Lube aliye kuwa akimfwata
kwa nyuma pasipo kujua lengo la Shamsa ni nini
kwake. Teke hilo zito likamfanya Lube, kuanguka
mzima mzima pasipo hata kujitingisha, akiashiria
amepoteza fahamu. Kwa haraka Shamsa akamlaza
Lube kifudifudi na kuifunga mikono yake kwa
nyuma kwa kutumia mkanda alio ushika.
Shamsa akamtazama kwa muda Lube aliye lala
chini, akatoka chumbani kwake, akelekea jikoni
akachukua jagi na kuweka maji ya baridi yenye
vibarafu vidogo vidogo, akarudi chumbani kwake,
kwa kutumia maji hayo akamwagia Lube ya
kichwani na kumfanya akurupuke kwa haraka huku
akihema kwa nguvu
“Naona umerudi kutoka kuzimu si ndio”
Shamsa alizungumza huku akiwa amekaa kwenye
sofa na bastola akiwa ameielekezea kwa Lube aliye
lala chini.
“Swali langu ni lile lile, ni nani aliye kutuma?”
Luba hakujibu chochote zaidi ya kukaa kimya na
kumtazama Shamsa kwa hasira kali
“Nahesaba hadi tatu baada ya hapo tutaonana
ahera madukani sawa bwana kaka?”
“No nakuomba usiniue nipo tayari kukueleza kila
kitu ambacho utaniambia nikueleze”
“Unauhakika?”
“Ndio nipo tayari”
Lube alizungumza kwa woga hadi akahisi haja
ndogo ikiwa inataka kumwagika
***
Mzee Godwin na Tom wakafika kwenye moja ya
mji, wakatekeza gari ya polisi wanayo itumia, kwa
pesa walizo nazo wakanunua mavazi ambayo si
rahisi kwa mzee Godwin kujulikana kwamba yeye
ni muhalifu, anaye tafutwa kila kona ya Tanzania.
“Babu hapa ni wapi?”
“Hapa kunaitwa Namanga ni mpakani kati ya
Tanzania na Kenya”
“Ahahaaa ila kuna baridi?”
“Ndio mana tukanunua makoti ili kuweza kujikinga
na baridi hii, huku sio kama kule pwani ni upepo
tu wabahari ndio unawanya muoene baridi”
Kutokana ni majira ya mchana, ikawabidi wakae
kwenye moja ya kimgahawa kidogo kujipatia
chakula, wakivu vuta muda wakisubiria Manka
kutekeleza kazi ambayo amempatia, ili waondoke
naye.
“Babu napenda sana siku moja niwe kama wewe”
“Kama mimi kivipi?”
“Nahitaji kuwa mmoja wa watu wako, nahitaji
kulipiza kisasi na mimi?”
“Ahahaaa, Tom unajua nini maana ya kisasi?”
“Kisasi kwa uwelewa wangu, ni kulipiza baya kwa
aliye weza kukufanyia mabaya.”
“Sasa unahitaji kulipiza kisasi cha nani?”
“Kwa mtu aliye weza kuniulia kaka yangu na
kusababisha pia mama na baba kufariki kwa
mstuko babaada ya kusikia kifo chake”
“Kaka yako, alikuwa ni nani?”
Tom akamatazama Mzee Godwin usoni kisha
akaachia tabasamu pana kidogo, akachukua glasi
iliyo jaa juisi na kuinywa taratibu kulisuuuza koo
lake.
“Anaitwa DERICK”
“Derick……..!!! Ahaa sawa usijali kila kitu kitakuwa
sawa”
Jina la Derick halikuwa geni kichwani mwa mzee
Godwin, akamtazama Tom kwa macho ya
kumchunguza, akagundua ukweli na uchungu ulio
mtawala Tom.
***
Majira ya saa kumi na moja jioni madam Mery
akafika mkoani Arusha moja kwa moja akaelekea
nyumbani kwake alipo paacha miaka mitano iliyo
pita pasipo kupakanyaga. Ukimya wa nyumbani
kwake halikuwa jambo la kumuogopesha sana
kwani hakuacha mtu yoyote aliye weza kuitunza
hiyo nymba yake aliyo inunua miaka sita iliyo pita,
nyasi ndevu zilizo izunguka nyumba yake,
ziliashiria kwamba hapakuwa na mtu ambaye
Alisha wahi kufika hapo kabla yake kwani geti lake
hakulifunga kabisa zaidi ya kulitegesha na
kuonekana kama limefungwa. Akazunguka nyuma
ya nyumba kwenye vyungu vikubwa ambavyo
ameoteshea maua, akasimama kwenye moja ya
chungu na kuchukua funguo ya mlango wa kuingia
katika mlango wa mbele wa nyumba yake. Sehemu
alipo icha funguo hiyo ndipo sehemu aliiweka
kipindi anaondoka kuelekea nchini Somali kwa kazi
maalumu aliyo pewa na Mzee Godwin kuwa kama
mfanyakazi wa bamnk ya Bacrayce nchini humo.
Akarudi upande wa pili wa nyumba na kufungua
mlango wake, akakutana na vumbi jingi lililo tanda
ndani ya sebule yake likiambatana na mitando
mingi ya buibui.
“Ahaaaaa”
Akashusha pumzi nyingi akitazama uchafu mwingi
uliomo ndani ya nyumba yake hiyo, akaaza
kufungua mlango mmoja baada ya mwingine iliyo
kuwemo kwenye nyumba ytake kuchunguza kama
kuna usalama wowote.
‘Kwa leo siwezi kulala humu’
Madan Mery akafunga nyumba yake na kutoka
getini, akatazama kila kona ya mtaa wake ano ishi,
hapakuwa na mabadiliko makubwa sana ya eneo
hilo, akaita usafiri wa pikipiki, akamuomba dereva
ampeleke kwenye moja ya hoteli ambayo mara
nyingi huitumia katikia kupumzika. Wakati, akiwa
njiani kuelekea katika hoteli hiyo, Manka hakuwa
mbali naye, kuanzia anaingia nyumbani kwake,
Manka aliweza kumuona na kuhakikisha ana
mfwatilia kwa ukaribu wa hali ya juu, kama alivyo
pewa maagizo na baba yake mzee Godwin. Taarifa
za madam Mery kuelekea mkoani Arusha zilitolewa
na miongoni mwa walinzi wa Eddy, walio wekwa
na serikali kumlinda kiongozi huyo mara baada ya
mauaji ya familia yake kutokea, huku mlinzi huyo
Brian anashirikiana fika na mzee Godwin na
nimiongoni mwa wanachama wa kundi la D.F.E
Pasipo Madam Mery kutambua anafwatiliwa, kipindi
alipo kuwa akitoka nyumbani kwa Eddy, mlinzi
huyo aliweza kumfwatilia hadi alipo fika stendi ya
mabasi ubungo, na kupanda basi la kuelekea
mkoani Arusha, ndipo akampa taarifa bosi wake
mzee Godwin, na kwabahati nzuri tayari Mzee
Godwin alisha fika mkoani Arusha akiwa katika
harakati za kuondoka ndani ya nchi ya Tanzania.
Kikubwa ambacho ni cha hatari zaidi ni kwamba
Madam Mery alisha toa siri zao zote kwa binti
mdogo Shamsa, hadi makao makuu yao yanapo
patikana.
Jukumu alilopewa Brian ni kuweza kumfwatilia
Shamsa na kuhakikisha kwamba anamuondoa
dunia, na akipata nafasi aweze kumteka Eddy na
kuwa mikononi mwake.
Madam Mery kufika Hotelini, Manka naye akawa
amesha wasili, kwa kutumia usafiri wa taksi,
akamlipa dereva wa taski na kushuka kuelekea
ndani alipo elekea madam Mery. Akamshuhudia
Madam Mery akielekea kwenye lifti iliyo mpeleka
gorofa ya tano kwenye hoteli hiyo. Naye akaingia
kwenye lifti ya pembeni iliyo mpeleka kwenye
gorofa aliyo eleke madam Mery, ndani ya dakika
moja akawa amesha fika kwenye gorofa hiyo
akamshuhudia madam Mery akiingia kwenye moja
ya chumba namba 1220. Baada ya Madama Mery
kuingia ndani ya chumba hicho akachomoa bastola
yake na kuifunga kiwambo cha kuzuia sauti na
kuanza kutembea kwa mwendo wa kasi katika
kordo hiyo akielekea kwenye chumba alicho ingia
Madam Mery
***
“Raisi Pray ndio ameniagiza……………..”
Lube alizungumza huku akihema sana, akisikilizia
maumivu ya viungo aliyo weza kupewa na
Shamsa, ikiwemo shingo yake aliyo shindwa
kuigeuza kwa muda sasa
“Amekutuma nini?”
“Ameniambia kwamba niweze kumfwatilia
muheshimiwa na madam Rahab”
“Baada ya kuwafwatilia?”
“Ameniambia wewe na muheshimiwa niweze
kuwatafutia sehemu ya mbali na Tanzania
muondoke mukaishi huko hapa haitaji kuwaona”
“Una uhakika kwa uliyo yazungumza?”
“Ndio ninauhakika dada yangu, ila ninakuomba
usimwambiea muheshimiwa tafadhali”
Shamsa akamtazama Lube jinsi anavyo zungumza
kwa woga mwingi ulio mtawala huku machozi
yakimwagika usoni mwake, akamnyanyua na
kumkalisha kitandani huku akiwa emendeleea
kumuelekezea bastola yake.
“Sina haja ya kuweza kukuua ila ninauwezo huo
wa kukua endapo utafungua hilo bakuli lako
kuweza kumueleza huyo raisi wako kwa kitu ulicho
weza kukisikia”
“Sawa”
“Poteee na nisikuone ukirudi tena hapa”
Shamsa alizungumza huku akimfungua Lube
mkanda alio mfunga kwenye mikono, taratibu Lube
akatoka ndani ya chumba cha Shamsa huku macho
yake yakiitzama bastola yake asiamini kwamba
binti huyo ameweza kumzibiti vya kutosha.
“Ohhhhhhhh Eddy wewe ni noma”
Rahaba alizungumza huku akilala pembeni ya Eddy
mara baada ya kumaliza mechi iliyokuwa na
ushindani wa hali ya juu.
“Kwa nini?”
“Mmmmm sijapata ona, mwanaume mwenye kasi
kama wewe aiseee ahahaa hapana yaani
mmmmm…..”
“Hakuna kitu”
“Mmmmm natamani niendelee kufanya siku nzima
ila yule bwege ananisubiri huko ikulu kwake”
“Hivi ni kwanini umeweza kumsaliti mume wako?”
“Kuna sababu nyingi sana, ila moja wapo
simpendi”
“Ilikuwaje ukakuoa?”
“Ilikuwa ni kama bahati mbaya kuokota embe dodo
chini ya mpapai, ila pia nipo kwa ajili ya
kuhakikisha wezangu ninaweza kuwakomboa”
Rahab alizungumza huku akikaa kitako, taratibu
akamgeukia Eddy na kuanza kumchezea kifua
chake kipana, kilicho weza kujazia vizuri kwa
mazoezi.
“Eddy nina historia ndefu sana kwenye maisha
yangu, hadi leo nimefanikiwa kufika hapa kusema
kweli ni kazi kubwa sana, ila kuna siri nitakueleza
tukiendelea kuwa pamoja”
“Siri, siri gani………..!!?”
“Kuhusiana na maisha yangu ila kwa leo tuishie
hapa”
Rahaba akanyanyuka kitandani na kuelekea bafuni
na kumucha Eddy akiwa katika alama ya mshangao
kwani hakujua ni siri gani ambayo Rahab anahitaji
kumueleza, Rahab akatoka bafuni, akajifuta maji
mwili mzima kwa kutumia taulo, akavaa nguo zake
na kujiweka sawa kama alivyo ingia, muda wote
Eddy akiwa kitandani akimtazama jinsi anavyo
jiremba, hapo ndipo Eddy akautambua uzuri wa
Rahab kuanzia chini hadi juu.
“Eddy nahitaji unioe”
“Niku…….”
Rahab akamziba kwa kidole kimoja mdomoni,
taratibu akaushusha mdomo wake na kumpiga
busu zito la mdomo Eddy na kuzidi kumpagawisha
“Tutaonana siku nyingine”
Rahab akanyanyuka kitandani na kuondoka,
akamuachia maswali mengi Eddy, dakika hata mbili
hazikupita Shamsa akaingia chumbani kwa Eddy
bila hata ya kubisha hodi, mkononi akiwa
ameshika bastola huku mkono mwingine akiwa
ameishika simu ya Lube, huku akiwa ameiweka
sauti iliyo rekodiwa, sura yake akiwa ameikunja
kwa hasira akichefuliwa na tukio alilo lifanya Eddy
pamoja na mke wa raisia, kwa bahati mbaya
akamkuta Eddy ndio ananyanyuka kitandani akiwa
kama alivyo zaliwa na wote wakabakiwa wakiwa
wametazamana.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 25 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (25)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Rahab akanyanyuka kitandani na kuondoka,
akamuachia maswali mengi Eddy, dakika hata mbili
hazikupita Shamsa akaingia chumbani kwa Eddy
bila hata ya kubisha hodi, mkononi akiwa
ameshika bastola huku mkono mwingine akiwa
ameishika simu ya Lube, huku akiwa ameiweka
sauti iliyo rekodiwa, sura yake akiwa ameikunja
kwa hasira akichefuliwa na tukio alilo lifanya Eddy
pamoja na mke wa raisia, kwa bahati mbaya
akamkuta Eddy ndio ananyanyuka kitandani akiwa
kama alivyo zaliwa na wote wakabakiwa wakiwa
wametazamana.
ENDELEA
“SHAMSAAAAAAA…………………..”
Eddy alijikuta akipiga kelele huku akimtazama
shamsa aliye ingia, Shamsa akageuka na kumpa
Eddy mgongo, akimuashiria ajisitiri kwa chohote,
haraka haraka, Eddy akajifunga taulo alilo jifutia mji
Rahab kisha akaguna, Shamsa akageuka akiwa na
sura ya kukasirika aliyo ingia nayo ndani humo.
‘Eddy huu ndio ujinga gani unaufanya, hata wiki
haijaishi ta mazishi ya mama leo hii unakuja kulala
na mke wa raisi hivi akili yako ina akili kweli
wewe”
“Nena haitoshi umeamua kufanya nae huo ushenzi
ndani ya chumba alicho kuwa ana lala mke wako
kipenzi, juu ya kitanda chake hivi ni haki kweli
eheeee?”
Maswali yote ya Shamsa hapakuwa na jibu lolote
kutoka kwa Eddy, kichwa alikiinamisha chini kwa
aibu ambayo ameipata kutoka kwa binti huyo
anaye mchukulia kama mwanae.
“Sikiliza ujinga wenu huu na umesha tumwa kwa
raisi sasa wewe angalia ni kipi ambacho kitatokea
muda wowote kuanzia sasa hivi”
Shamsa akamrushia Eddy simu iliyo rekodiwa sauti
zao wakiwa kitandani, Eddy akazisikiliza kwa
umakini, mapigo ya moyo yakaanza kumuenda
mbia kiasi kwamba akatamani ardhi ipasuke ili
aingie na kujichimbia humo. Ila haikuwa hivyo,
akarudia tena kuisikiliza akihisi kama sauti sio zao
ila sauti ya Rahab na yake zilisikika vizuri kutoka
kwenye simu hiyo.
“Haya ona sasa, sura yako utaiweka wapi Eddy,
Sura zetu tutaziweka wapi, hivi hiyo zipu yako
huwezi kuifunga unapo ona ku** za wanawake
eheeee?”
Shamsa alizungumza kwa hasira kali hukuy
machozi yakimwgika kwa uchungu.
“Hembu tazama jinsi jamii inavyo kuchukulia,
halijaisha tatizo moja umezua jengine kweli, kweli
Eddy huu ndio uwaziri wako jinsi unavyo kutuma
kufanya. Unadhani kifo chako kipo mbali kwenye
hii dunia?”
“Nilitegemea kuwa na kiongozi bora mwenye
kuipenda na kuiheshimu thamani yake ila wewe,
sijui humo akilini mwako unategemea nini”
Eddy taratibu akanyanyuka kitandani na kuanza
kupiga hatua za kumfwata Shamsa sehemu alipo
simama, ila kambla hajamkaribia, akajikuta
akitazamana na mdomo wa bastola aliyop ishika
Shamsa.
“Ukinisogelea Eddy ninakumwaga ubongo”
Shamsa alizungumza huku akiikoki vizuri bunduki
yake tayari kwa kufyatua risasi
***
Jaclline akampitia Agnes kwenye sehemu aliyo
muambia wakutane na safari ya kuondoka katika
eneo la karibu na ikulu ikaanza.
“Ilikuwaje kuwaje hadi wakakufahamu?”
“Hata mimi mwenyewe sifahamu”
“Muda mwengine tuwe makini Agy hii nchi ulinzi
wake ni mkali kama tumeamua kufanya tukio kama
hilo tunatrakiwa kuwa makini, hapa kama walisha
weza kuidaka sura yako basi watatufwatiliwa kwa
satelait kujua ni wapi tulipo”
“Sasa itkuwaje?”
“Hapa ni lazima tuondoke ndani ya Marekani
hatuna jinsi tena”
Wakiwa barabarani gafla mwanga mkali kutoka juu
ukalimulika gari lao linalo kwenda kwa kasi kubwa.
Kila mmoja wao akatambua tayari mambo yamesha
haribika na hapo wanafwatiliwa na helcoptar ya
polisi.
Jaquline akazidi kuongeza mwendo kasi wa gari
hiyo ndogo aina ya Ferrari Spide yenye spidi mita
zaidi ya mia tatu. Risasi kutoka juu zikaanza
kuilenga gari yao, jambo lililo mfanya Jaquline
kuiendesha gari hiyo kwa kuiyuimbisha yumbisha
ili mradi risasi zisije kuingia kwenye gari yao.
Askari mji mzima wakap[ewa taarifa juu ya magaidi
wawili wanawake walio kuwa wamejipanga katika
kuishambulia ikulu ya Marekani, kile eneo la mji
vikosi vyote vya ulinzi vikajiweka sawa,
kuhakikisha magaidi hao hawatoke ndani ya mji
huo
“Ndio bosi”
Sauti nzito ya mwanaume ilisikika baada ya
kupokea simu kutoka kwa bosi wao wanaye
muheshimu sana.
“Hakikisheni hao magaidi wanao fukuzwa hawaingii
mikononi mwa askari, wachukueni na
kuwatorosha”
“Sawa mkuu”
Bosi wao akakata simu huku macho yake
akiyatupia kwenye luninga yake kubwa akitazama
taarifa ya moja kwa moja kwenye kituo cha CNN,
wakionyesha jinsi askari wanavyo ikimbiza gari
ndogo ya magaidi hao wanao sadikika ni
wanawake.
Gari za polisi zinazo wafukuzia, kwa nyuma
zikazidi kuwachanganya Agnes na Jaquline, kila
jinsi wanavyo zidi kwenda ndivyo jinsi gari hizo
zilivyo zidi kuongezaka na kuja kwa mwendo wa
kasi, huku baadhi ya helcoptar za polisi zikizidi
kuwaandama.
Katika daraja refu, wanalo pita, linalo unganisha
mji mmoja na mji mwingine chini yake kukiwa na
maji ya bahari, umbali wa kilomota mbili mbele,
askari wengi wenye silaha tayari walisha iziba njia,
wakiwa tayari kwa kuisubiria gari hiyo inayo
endelea kuandamwa vikali na gari nyingine za
polisi pamoja na kikosi cha FBI. Ukimya ndani ya
gari ukatawala, Jaquline kazi yake ikawa ni
kijitahidi kuhakikisha anaiendesha gari hiyo kwa
kasi jinsi awezavyo kulipita daraja hilo pasipo
kujua kama mbele kuna kizuizi kikubwa cha
askari. Agnes kazi yake ikawa ni kumuomba
Mungu kuwafanyia muujiza wowote ili mradi
waweze kuitoroka mikono hiyo ya askari tena
wakimarekani. Askari wa gari za nyuma hawakusita
kufyatulia gari la kina Jaquline risasi kila walipo
pata nafasi ya kufanya hivyo, Agnes akakoki
bastola yake na kushusha kioo
“Unataka kufanya nini?”
“Nahitaji kujibu mashambulizi hawawezi kutuonea
kiasi hichi”
Agnes akatizama kioo cha pembeni upande wake,
akazihesabu gari hizo zinavyo kuja kwa kasi, kwa
haraka akachomo mkono wake kwa kupita kioo
hicho kwa kutazamia juma, akafyatua risasi kadhaa
zilizo piga kwenye kioo cha mbele kwenye moja ya
gari ya polisi. Ikampata dereva na kuifanya gari
hiyo kuyumba baadhi ya gari za nyuma zikajikuta
zikiigonga gari hiyo na kusababisha ajali mbaya
sana, iliyo ambatana na mlipuko mkubwa.
“Yes”
Agnes akajipongeza huku akifunga kioo cha gari
yake akitazama jinsi baadhi ya gari zikianguka
vibaya sana.
“Nice shoot”
“Thank you”
Wote wakatabasamu, nakazi ya Jaquline ikaendele
kuliendesha gari hiyo kwa spidi kadri ya uwezo
wake. Gafla kwa mbali kidogo wakaona kizuizi cha
askari wakiwa na magari yao pamoja na bunduki
na mbaya azidi kwenye daraja hilo refu hakuna
sehemu ya kukimbilia zaidi ya kujitosa kwenye
maji ya bahari ambapo ni mbali sana kutoka juu
sehmu walipo
***
Kitendo cha mlango kugongwa kikamfanya Madam
Mery kusimama kwa muda huku akiutizama kwa
wasiwasi kwani ni muda mchache tangu alipo ingia
ndani ya chumba hicho na hapakuwa na agizo
lolote alilo litoa kwa wahudumu wa hoteli hiyo.
Madam Mery akataka kuzuuliza ni nani ila akasita
kutokana na mlango kugongwa tena, ikambidi
apige hatua za taratibu hadi kwenye mlango
taratibu akaishia funguo, akaizungusha mara mbili,
akishika kitasa na kuufungua mlango, teke kali lililo
tua kwenye kifua chake likamfanya arudi ndani
huku akianguka chini. Manka akaufunga mlango
kwa haraka na kumtazama Madam Mery anaye
gugumia kwa maumivu makali akijaribu
kunyanyuka kutoka chini.
“MANKA…….!!!”
“Jina langu”
Manka alizungumza huku akiishikilia bastola yake
vizuri akiwa amemuelekezea madam Mry
“Natambua kwamba baba yako ndio amekutuma
kuja kuniua si ndio?”
“Hiyo siyo kazi yako kujua kwamba ni nani aliye
nituma kuja kwako, ila ni kwanini umetusaliti?”
“Manka siwezi kuendelea tena kwenye umoja wa
baba yako, huku nikiwa ninataka kuwahukumu
watu ambao hawana hatia kwenye maisha
yao,tazama jinsi baba yako alivyo iteketeza familia
ya mdogo wako Eddy”
“Ishia hapo hapo Eddy si mdogo wangu, si damu
yetu”
Manka alizungumza kwa hasira kiasi cha kumfanya
Madam Mery kutetemeka kiasi.
“Manka, Manka utaendelea kutumikishwa hadi lini
mdogo wangu. Ni lini ambapo utaamua kuwa na
familia yako, kuwa mama wa wanao. Umeona vizuri
jinsi mtoto mdogo wa mdogo wako alivyo uliwa si
ndio”
Madam Mery alizungumza huku machozi
yakimwagika.
“Machozi yako hayata nizuia mimi kufanya nilicho
agizwa kukifanya kwako sawa wewe Malaya…..”
Madam Mery hakuzungumza chochote zaidi ya
kumwagikwa na machozi mengi. Manka hakuwa na
huruma kwa mwanamke mwenzake huyo, akavuta
triga iliyo ruhusu risasi moja kuchomoka kwa kasi
na kutua kwenye paja la madam Mery na kumfanya
adondoke chini huku akitokwa na ukunga mkali wa
maumivu.
“Shiiiiiii……….. Leo sinto kuua ila hakikisha
unajificha maisha yako yote hadi kufa kwako na
enndapo utajitokeza tena mbele ya macho ya baba
yangu nitakuua sawa”
Madam Mery akatingisha kichwa akikubaliana na
agizo la Manka, aliye toka ndani ya chumba hicho
pasipo kuaga.Madama Mery akajikongoja hadi
kwenye meza yenye simu akachukua mkonga wa
simu hiyo na kuminya namba ya kuomba msaada
kwa wahudumu wa hoteli hiyo.
***
Jaquline akafanga breki za gafla hadi gari tairi
zikaserereka na kuifanya gari hiyop kuyumba kiasi
ila kajitahidi hadi ikakaa sawa.
“Shiti…….”
“Tunafanyaje Jack”
Agnes alizungumza kwa kubabaika, kila mmoja
wasiwasi mwingi ukamtawala kwenye moyo wake,
si mbele wala nyuma waliweza kuzingirwa na gari
za polisi, isitoshe juu angani kuna helcoptar za
polisi zinao wamulika kwa mwanga mkali mweupe.
“Kuna umbali mrefu kutoka chini kwenye hili
daraja la Golden gate’
Jaquline alizungumza huku mapigo ya moyo
yakimwenda mbio, gari za polisi zinazo wafukuzia
zikazidi kuwasogelea kwa ukaribu zaidi. Gafla
helecoptar mbili za polisi zikaalipuka na kuangukia
kwenye kwenye bahari, Helcoptar moja kubwa ya
kivita iitwayo AH-64AVD APACHE, ikaanza
kushambulia garo za polisi zote zilizo kuwa
zikiwasogelea Agnes na Jaquline. Polisi
wakachanganyikiwa kwa shambulizi hilo kwani
Helcoptar nyingine aina hiyo hiyo ya AH-64AVD
APACHE, ikawashambulia askari wote ambao
waliweka kizuia, hadi Agnes na Jaquline wakabaki
wakishangazwa na tukio hilo
“Ni kina nani hao?”
Agnes alizungumza akizitazama Helcoptar hizo
zifanya kazi yake. Helcoptar moja nyingine ya tatu
aina ya UH-72A LAKOTA LIGHT, ikasimama juu
usawa wa gari la kija Jaquline wakashuka vijana
wawili kwa kutumia kamba maalumu huku wakiwa
wamevalia nguo nyeusi pamoja na vinyago vinavyo
waonyesha macho tu. Kila mmoja akapita pande
wake akiwa wa gari, wakiwa na bunduki mikononi,
wakavunja vioo vya gari ya kina Jaquline.
“Tokeni nje, tumekuja kuwachukua”
Mmoja wao alizungumza na kuwafanya Agnes na
Jaquline kutoka nje ya gazi yao, hapakuwa na aliye
hitaji kuuliza swali, kwani tayari walisha anaza
kuwaamini watu hao kutokana na msaada walio
wafanyia na fika wanaonekana si watu wa serikali.
Kila kijana mmoja akamkumbatia Agnes na
kujifunga kamba waliyo shuka nayo, huku
mwingne akimkumbatia Jaquline na kufanya kama
alivyo fanya mwenzake. Kamba hizo zikaanza
kuvutwa kwenda juuu, wakaingia kwenye helcoptar
hiyo na kuondoka katika eneo la tukio na
kuwaachia msiba mzito ndugu wa askari hao walio
kuwa wakijaribu kuwazuia magaidi hao.
Jaquline na Agnes wakavishwa vigunia vyeusi
kichwani wasijue ni wapi wanapo pelekwa na watu
hao wasio wafahamu, Safari yao ikachuku lisaa
moja wakafika katika kambi moja yenye ulinzi
mkali. Wakashushwa kwenye helcoptar na moja
kwa moja wakapelekwa kwa mkuu wa eneo hilo,
huku wakiwa wamevalishwa vigunia hivyo.
“Mkuu hawa hapa”
Mmoja wao alizungumza, Agnes na Jaquline
wakavuliwa vigunia vyao macho yao yakakutana na
mtu mmoja aliye kalia kwenye kiti kidogo cha
matairi cha kusukuma, pembeni yake kukiwa na
mijitu mikubwa miwili iliyo panda hewani na
kujazia vifua vyao. Mtu huyo aliye kaa kwenye kiti
hicho akageuzwa na baunsa mmoja, sura ya mtu
huyo haikuwa nzuri sana kwani upande mmoja upo
kama umeuguzwa na kitu, huku katika eneo la
miguuni akiwa amefunikwa na kitambara
chekundu, mikono yake akiwa amevaa gloves
yeusi.
Mtu huyo akawatizama wasichana hao, kisha
akaachia tabasamu pana, akionekana kufurahishwa
na vijana wake kwa kazi waliyo ifanya.
“Karibuni sana katika makao makuu ya D.F.E, jina
langu ninaitwa JOHN”
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 26 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (26)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“Mkuu hawa hapa”
Mmoja wao alizungumza, Agnes na Jaquline
wakavuliwa vigunia vyao macho yao yakakutana na
mtu mmoja aliye kalia kwenye kiti kidogo cha
matairi cha kusukuma, pembeni yake kukiwa na
mijitu mikubwa miwili iliyo panda hewani na
kujazia vifua vyao. Mtu huyo aliye kaa kwenye kiti
hicho akageuzwa na baunsa mmoja, sura ya mtu
huyo haikuwa nzuri sana kwani upande mmoja upo
kama umeuguzwa na kitu, huku katika eneo la
miguuni akiwa amefunikwa na kitambara
chekundu, mikono yake akiwa amevaa gloves
yeusi.
Mtu huyo akawatizama wasichana hao, kisha
akaachia tabasamu pana, akionekana kufurahishwa
na vijana wake kwa kazi waliyo ifanya.
“Karibuni sana katika makao makuu ya D.F.E, jina
langu ninaitwa JOHN”
ENDELEA
“Niliagiza vijana wangu kuweza kuwakokomboa
kwa lengo moja tu nahitaji muwe huru na kufanya
kazi chini yangu kama hamto jali”
“Hatuhitaji kufanya kazi chini ya mtu yoyote”
Jaquline akajibu kwa kujiamini huku akimtazama
John machoni mwake.
“Nambueni kwamba hadi sasa hivi umesha kuwa
wakimbizi, munatafutwa kila mahali je mupoo
tayari kwenda gerezani kama walivyo wezenu”
Maneno ya John yakamstua Agnes, akamkazia
macho vizuri John, kisha akamgeukia Jaquline
ambaye ajajiuliza juu ya hao wezao, John
amaewajuaje.
“Musishangae kuona ninawafahamu Fatuma,
Halima, na Anna, wote hawa walikwenda jela kwa
ajili yako wewe unaye nitumbulia macho kwa
kushangaa”
John alizungumza kwa dharau huku akiachia
tabasamu pana usoni mwake na kuifanya sura
yake kuzidi kuwa mbaya. John akamnong’oneza
mlizi wake mmoja sikioni kisha, mlizi huyo
akaondosha na John akawageukia Agnes na
Jaquline walio kaa kimya wakimtafakari huyu nimtu
wa aina gani.
Mlinzi wake aliye mnongoneza, baada ya muda
kidogo akarejea akiwa na laptop, John kwa ishara
akamuomba aifungue, mlinzi wake huyo
akaimiminya minya kwa muda kisha John
akamuamuru kuwapa Agnes watazame kilichomo
ndani ya Laptop hiyo.
***
Eddy akazidi kupiga hatua za kumfwata Shamsa
aliye mshikia bastola, Shamsa akazidi kumwagikwa
na machozi akimuomba Eddy asimama katika
sehemu aliyo muamuru kusimama ila Eddy
hakulifanya hilo hadi alipo mfikia, akaishika bastola
na kuigandamiza kifuani mwake kwa uchungu.
“Niuea”
Eddy alizungumza kwa sauti ya utaratibu na
kumfanya Shamza aanguae kilio kikubwa na
kuitupa bastola chini na kumkumbatia kwa nguvu
Eddy. Dakika tatu nzima zikapita huku wote
wakiwa wanamwagikwa na machozi mengi.
“Shamsa samahani sana mwanangu sinto weza
kufanya ujinga kama nilio ufanya awali”
“Kweli baba?”
“Ndio mwanangu”
Shamsa akazidi kumkumbatia Eddy kwa nguvu,
akijaribu jaribu kuyafuta machozi yake. Shamsa
akatoka ndani ya chumba cha Eddy akiwa na
furaha na amani moyoni mwake, akiamini baba
yake hato fanya ujinga kama alio weza kuufanya.
Moja kwa moja akaelekea kwenye bustani moja
kubwa iliyomo ndani ya jumba lao na nipembezini
kabisa kwa fensi inayo elekea kwenye ufukwe wa
bahari. Akiwa katika dimbwi la mawazo sauti nzito
ikamstua nyuma yake.
“Unamuwaza nani?”
Kitendo cha Shamsa kugeuka akakutana na ngumi
nzito ya uso iliyo mpotezea muelekeo, gafla
kitambaa chenye hewa nzito kikatua puani mwake
ndani ya dakika kadhaa akapoteza fahamu. Brian
akatazama pande zote za bustani hapakuwa na
mtu aliye weza kumuona akifanya tukio hilo,
akamnyanyua Shamsa na kumuweka bgegani,
akavuka naye kwenye fensi na kwenda kumuweka
kwenye moja jabali lililopo pembezoni mwa bahari
akisubiria giza litawale anga aweze kuondoka na
binti huyo. Brian akarudi kwenye jumba la
Eddy,kujua ni nini kinacho endelea, hapakuwa na
mlinzi aliye weza kustuka kwamba Shamsa hayupo
katika eneo hilo, akaingia ndani ya gari lake na
kuondoka, akaenda kulisimamisha mbali kidogo na
jumba la Eddy, ila ni pembezoni mwa ufukwe wa
bahari, akarudi hadi sehemu alipo mlaza Shamsa
na kumkuta hayupo jambo lililo mchanganya sana
Brian.
***
Majira ya saa nne usiku Manka akafika katika kijiji
cha Namanga akitokea katika kazi aliyo pewa na
baba yake. Akawakuta Mzee Godwin na Tom,
wakiwa wanamsubiria.
“Umekamilisha?”
“Ndio baba kila kitu kimekwenda sawa”
“Kazi nzuri usafiri upo tayari unatusubiria”
“Sawa”
Wakaondoka na kuingia kwenye roli moja kubwa,
lilio andikwa AU, linalo milikiwa na jeshi la umoja
wa mataifa, huku mzee Godwin akiwa na watu
wake katika jeshi hilo wanao muheshimu na
kumtumikia, kwa lolote lile atakalo waeleza kuweza
kukifanya. Safari ikazidi kusonga mbele huku
wakipita katika baadhi ya vituo vya ukaduzi vya
kijeshi, pasipo kustukiwa na mavazi yao ya kijeshi
waliyo weza kuyavaa, wakawa wanapita salama
hadi wanaingia nchini Somali, wakitokea Tanzania
kisha Kenya na kutua kwenye ardhi hiyo, aliyo
jiwekea kikosi kikubwa cha magaidi anacho
kihudumia kwa pesa pamoja na silaha.
Wakapokelewa na mkuu wa kikosi hicho cha
kigaidi cha Al-Shabab, bwana Abdulah Mohamed.
Mzee Godwin akawatambulisha John na Manka
kwa kiongozi huyo aliye waandalia sherehe ndogo
ya kuwakaribisha katika ngome hiyo inayo lindwa
kwa ulinzi mkali sana.
“Naona D.F.E, inazidi kukua siku hadi siku
kiongozi”
Bwana Abdulah Mohamed alizungumza huku
akishushia bkinywaji alicho kishika kwenye mkono
wake
“Ndio kila siku tunahakikisha tunatengeneza umoja
wa siri ambao utadumu miaka na miaka katika
vizazi na vizazi”
“Kweli, hivi bado Tanzania, haijastukia juu ya kikosi
chako hicho?”
“Hapana hakuna aliye weza kustuka, kwani hata
ndani ya ikulu nina watu ambao wapo mikononi
mwangu na siku ya siku ikifika, wewe mwenyewe
utashuhudia kitakacho tokea”
“Usijali Generali Godwin, nitakusaidia kwa lolote
ambalo utaliomba nikusaidie katika kukamilisha
mipango yako”
“Nitashukuru sana”
Usiku huo mzima ukawa ni stori za hapa na pele
kwa viongozi hao wawili wanao pendana sana na
kuheshimiana. Tom na Manka kila mmojaa
alikabidhiwa chumba chake cha kujipumzisha
ndani ya ngome hiyo, wakisubiria kuendelea na
safari katika siku ya pili inayo fwata.
***
“Nini?”
“Ndio mueheshimiwa tumemtafuta eneo zima la
hapa nyumbani hatujamuona”
Mlinzi mmoja wa Eddy alizungumza huku mikono
yake akiwa ameiweka nyuma akimtazama Eddy
usoni anaye onekena kuchanganyikiwa kwa taarifa
ya Shamsa kuto kuonekana hadi mida hii ya saa
tano usiku. Eddy akayafumba macho yake kila
anacho kifikiria akaishi kichwa kinampasuka, kwani
amesha poteza, mama, mke na mtoto, ila Shamsa
ampoteze pia. Likawa ni jambo gumu sana kuweza
kuliruhusu kuingia katika ubongo wake.
Wazo la kwanza kumjia kichwani mwake ni mtu
gani ambaye anaweza kulifanya tukio la kumfanya
Shamsa kupotea, moja kwa moja mawazo yake
yakaangukia kwa Mzee Godwin.
‘Godwin Godwin, mmmmmmm’
Alisemea kimoyo moyo huku nafsi yake moja
ikimkatalia kwa nguvu zote kwamba Mzee Godwin
hausiki katika tukio hilo la Shamsa kupotea. Wazo
la pili ni simu ambayo Shamsa alimletea chumbani
majira ya mchana. Kwa haraka akafumbua macho
yake na kuanza kupandisha ngazi kwenda gorofani
na kuwaacha walinzi wake wakishangaa kwa nini
bosi wao amekurupuka na kukimbilia juu gorofani
mmoja wao akataka kwenda ila mkuu wake
akamzuia asimfwata, cha msingi watawanyike
kwenda kumtafuta Shamsa, hata maeneo ya nje ya
jumba hilo.
Eddy akaichukua simu aliyo pewa na Shamsa
akaanza kupekua upande wa picha, katika simu
hiyo na kuioa sura ya Lube mmoja wa walinzi wa
Raisi Praygod Makuya. Hapo ndipo picha ikaanza
kumjia kichwani mwake, akaanza kujaribu
kutengeneza matukio ya jinsi Shamsa alivyo weza
kuichuku simu hiyo, jibu likamjia aliichukua kwa
nguvu na si kwakuomba. Kumbu kumbu ya mguno
wa mtu kama kupigwa ukamjia kwenye mfumo wa
akili zake. Kwa haraka akatoka nje na kusimama
mlangoni kwake, akalitazama eneo hilo kwa
umakini akaona baadhi ya mikwaruzo kwenye
ukuta.
Macho yake akayatupia tena kwenye mlango wa
kuingilia chumbani kwa Shamsa, taratibu akapiga
hatua hadi ndani ya chumba hicho. Akakuta jinsi
vitu vilivyo changuka, ikionekana Lube
alibananishwa kwenye chumba hicho.
‘Alimuachia’
Eddy alijisemea, huku akiutazama mlango wa
Shamsa, kwani hapakuwa na tone lolote la damu
ndani ya chumba hicho akiamoni kwamba Lube
hakuweza kujeruhiwa na Shamsa.
“Huyu ndio atanieleza mwanangu yupo wapi?”
Eddy akatoka na kurudi chumbani kwake,
akachukua moja ya funguo ya gari lake, kabla
hajatoka akaiona bastola aliyo kuwa ameishia
Shamsa, akaiikota chini, akaitazama na kukuta
risasi za kutosha. Akashuka hadi sebleni ila
hakukuta mlizi hata mmoja. Moja kwa moja
akaelekea kwenye maegesho ya magari yake,
akaingia kwenye gari yake aina ya Verosa na
kuondoka nyumbani kwake akidhamiria kwenda
Ikulu kumbananisha raisi ili azungumze ni wapi
alipo mficha Shamsa wake.
***
Kwa usiri mkubwa raisi Praygod akapanga kikosi
cha walinzi wake wanne anao waamini, akiwemo
Lube, wahakikishe wanamtia nguvuni waziri Eddy.
Ambaye tayari amesha anaza kumlia utamu wake
wa kitandani(Rahab). Kazi hiyo raisi Praygod
aliwaagiza vijana wake wafanya chochote wawezalo
ila sura zazo, zisiweze kuonekana kwani itakuwa ni
kasfa mbaya kwa wananchi, ambao wanajiandaa
kwenda kwenye uchaguzi wa awamu yake ya pili.
“Kuna kitu kama sikielewi kwa meheshimiwa”
Samson alizungumza baada ya kukutana na Rahab
kwenye moja ya bustani iliyomo ndani ya ikulu
“Mbona unazungumza hivyo?”
“Kuna watu amewaagiza kwa Eddy, sasa sijajua
kama dhamira yao ni nzuri au mbaya”
Maneno ya Samson yakamstua sana Rahab,
akajaribu kuvuta hisia zake, akawaona Eddy akiwa
barabarani akija katika eneo la ikulu, huku
akioenekana akiwa katika hali ya kukasirika sana.
“Samson chukua gari uwafwatilie hao vijana na kila
kitakacho endelea ninakuomba unifahamishe”
“Sawa Madam”
Samson akachukua gari na kuondoka eneo la ikulu
akifwata amri ya Rahab. Lube akiwa barabarani na
wezake, wakapishana na gari aina ya Verosa na
macho yake yakamshuhudia ni Eddy ndio aliyomo
ndani ya gari hiyo.
”Geuza geuza mshenzi tumepishana naye”
Lube aliumuamrisha dereva, akafunga breki za
gafla huku akiigeuza gari hiyo kwa utaalamu
mkubwa, hadi wezake ndani ya gari hiyo
wakashangaa. Kwa uwezo wa gari yao kubwa aina
ya VX V8, ikawa ni rahisi kuweza kuifukuzia gari
hiyo ya Eddy. Waliyo ipita kwa kasi na kuikatizia
kwa mbele na kumfanya Eddy kufunga breki za
gafla na kusimama.
Lube na wezake wakavaa vinyago vyao vilivyo
wabakisha macho tu, wakashuka kwenye gari yao,
huku wakimtazama Eddy aliyomo ndani ya gari
akijishauri nini cha kufanya.
‘Hawanijui hawa’
Eddy alizungumza huku akishuka kwenye gari
bastola yake akiwa ameichomeka kwa nyuma.
“Nyinyi ni wakina nani?”
Eddy aliwauliza huku akijiweka sawa kwa lolote
litakao kwenda kujitokeza, ukimya wa barabara
hiyo inayo elekea ikulu na majira haya ya usiku
iliwafanya Lube na wezake kuweza kuilisikia swali
hilo walilo ulizwa. Hapakuwa na aliye jibu zaidi ya
wao kuanza kujitawanya na kumzingira Eddy na
kumuweka kati tayari kwa kumshambulia.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 27 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (27)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
‘Hawanijui hawa’
Eddy alizungumza huku akishuka kwenye gari
bastola yake akiwa ameichomeka kwa nyuma.
“Nyinyi ni wakina nani?”
Eddy aliwauliza huku akijiweka sawa kwa lolote
litakao kwenda kujitokeza, ukimya wa barabara
hiyo inayo elekea ikulu na majira haya ya usiku
iliwafanya Lube na wezake kuweza kuilisikia swali
hilo walilo ulizwa. Hapakuwa na aliye jibu zaidi ya
wao kuanza kujitawanya na kumzingira Eddy na
kumuweka kati tayari kwa kumshambulia.
ENDELEA
Eddy akawatazama kwa huku akiwahesabu jinsi
walivyo kaa, taratibu akalivua shati lake na kubaki
tumbo wazi, Lube akamuamrisha mwenzake
mmoja kufanya shambulizi kwa Eddy anaye
onekana kujiamini sana. Kitendo cha jamaa
kumfikia Eddy, akakutana na teke zito lilotua
kifuani kwake na kumuangusha chini kama mzigo.
Ikawabidi wengine kushanga kwani kila mmoja
hakuamini kama kiongozi huyo anaweza kufanya
tukio la aina hiyo.
Wote watatu walio bakia wakamvamia Eddy kwa
kasi, kila mmoja akijaribu kupiga sehemu yake
anayo iweza kupiga katika mwili wa Eddy, ila kila
walivyo jaribu kupambana, ndivyo jinsi walivyo
weza kukutana na mapigo makali yaliyo
wachanganya kiasi cha kuwafanya kila mmoja
kujikuta akiwa na maumivu upande wake. Lube
alipo gundua Eddy amewazidi kila jambo. Kwa
bahati nzuri akaona gongo moja pembezoni mwa
barabara. Akarudi nalo hadi sehemu wanapo
endelea kupambana wezake, huku gongo hilo
akiwa amelificha nyuma ya mgongo wake.
“EDDYYYYYYYYY……..”
Lube akamuita Eddy kwa sauti ya juu na kumfanya
Eddy ageuke kutazama mtu anaye muita, ila gafla
gongo zito likatua, kichwani mwake na kumfanya
Eddy kuyumba, kijana mmoja akamsindikiza na
teke zito lililo muangusha Eddy chini na kupoteza
fahamu.
“Mbebeni haraka haraka”
Lube alizungumza, kabla hata hawajamnyanyua
mwanga mkali wa gari ukawamulika, na kuwafanya
wasimama kulitizama gari hilo ni la nani majira
hayo ya usiku. Gari hiyo ikafunga breki na
kusimama, akashuka mtu ambaye wote
wanamfahamu.
“Huyu Samson amefwata nini hapa”
Mmoja wao alizungumza kwa sauti ya chini huku
wakimtazama Samson akitembea na kuwafwata
sehemu walipo.
“Bosi tufanyaje?”
Mmoja wao aliuliza huku kila mmoja akijiweka
sawa. Samson akawatazama kisha akawakazia
macho, wote wakajikuta wakishikwa na woga mkali
kwani macho ya Samson yalibadilika na kutisha
sana
***
Agnes na Jaquline wakashuhudia jinsi Halima na
wezake wanavyo pata mateso gerezani. Video hizo
zikawamfanya Agnes kumwagikwa na machozi ya
uchungu, uzuri wa wezao hao wote umepotea,
alama nyingi za makovu zimetawala kwenye miili
yao.
“Munaweza kuamua sasa, kufanya kazi na sisi au
wezenu waendelee kupata mateso na mwisho wa
siku hukumu ya kuuawa itakuwa dhidi yao”
Kabla hawajajibu mlio wa simu ukalia kutoka
kwenye mfuko wa mmoja wa walinzi, akaitoa simu
hiyo na kuipokea kisha akaiweka sikioni mwa John
“Ndio mkuu”
“Leo ninakuja mako makuu kila kitu ukiweke sawa”
“Sawa mkuu”
Simu ikakatwa John akashusha punzi kidogo, kwa
taarifa aliyo weza kuipata kwa mkuu wake Mzee
Godwin. Akaagiza ulinzi uzidi kuimarishwa na
vijana waweze kujiandaa kumpokea mkubwa wao
huyo anaye tokea barani Afrika.
“Tumekubali, ila kwa sharti moja”
Jaquline alizungumza huku akimtazama John
machoni huku akiwa amemkazia macho, John
akatingisha kichwa chake kumruhusu Jaquline
kuendelea kuzungumza.
“Hatuta weza kufanya kazi yoyote na nyinyi hadi
pale tutakaopo waokoa wezetu”
“Mmmmmmm, nitarifikiria”
“Waandalieni sehemu inayo stahili wao kuwepo”
John akatoa agizo lake kwa vijana wake,
wakawachukua Jaqulne na Agnes na kuwapeleka
kwenye moja ya chumba kilicho na huduma za kila
kitu wakisubiria juu ya jibu watakalo pewa na
John.
Mzee Godwin akaagana na bwana Abdulah
Mohamed mkuu wa kikosi cha kigaidi cha Al-
Shabab, wakaingia kwenye ndege ya kifahari aina
ya Jet inayo ingia abiria watano pamoja na
marubani wawili. Tom na Manka tayari walisha
ingia kwenye ndege hiyo wakimsubiria baba yao
aliye kuwa akipiga stori za hapa na pale na
kiongozi huyo waliye aihidiana kupanga baadhi ya
mipango takayo kuwa kabambe katika kutawala
baadhi ya maeneo kwa kutumia nguvu.
“Mumemechoka ehee”
Mzee Godwin aliwauliza wanae hao huku akijiweka
vizuri katika siti aliyo kaa
“Ahaa kidogo tu”
Tom alijibu
“Mmmm mimi nimechoka sana tu baba, hapa
natamani tufike huko tunapo kwenda”
“Musijali haita chukua masaa mengi tutakuwa
tumefika”
***
Mihemo mizito pamoja na mingurumo anayo itoa
Samson ikawafanya Lube na wezake kuzidi
kutetemeka, mmoja wao akachomoa bastola yake
na kumfyatuia baadhi ya risasi kwa Samson, ila
jambo la kushangaza risasi hizo ziliingia mwilini
mwa Samson ila katika sehemu zilipo ingia jeraha
lake likapona ndani ya sekunde chache. Kwa kasi
ya ajabu Samson akamkimbilia jamaa aliye mpiga
risasi, akamkamata shingo, kwa mkono mmoja
akamnyanyua juu, huku akizidi kukoroma na
macho yake yakiwa yamebadilika na kuwa kama
simba aliye na hasira kali.
“Ondokeni hapaaa”
Samson alizungumza kwa sauti nzito, huku
akimuachia aliye mpiga risasi hakuhitaji kumdhuru
na kuwafanya Lubne na wezake wote kuondoka
katika eneo hilo, wakaingia ndani ya gari lao na
kuondoka kwa mwendo wa kasi kila mmoja akiwa
haamini alicho weza kukiona kwa binadamu huyo
wanaye mtambua kama Samson.
Samson akambeba Eddy begani na kumuingiza
kwenye gari lake na kuondoka naye.
“Madam nimempata”
John alizungumza kupitia simu yake huku akiwa
amesimamisha gari lake pembezoni mwa barabara
huku Eddy akiwa amemlaza siti ya nyuma.
“Safi sasa hakikisha unampeleka kwenye eneo
ambalo si rahisi kwa mtu kuweza kutambua”
“Sawa madam”
Samson akakata simu na kuendelea na safari,
Samson kitu alicho weza kukumbuka ni moja ya
handaki ambalo Rahab alimueleza kwamba
yalikuwa ni maficho yao kipindi walipo weza
kukutana kwa mara ya kwanza, na handaki hilo
lipo nje ya mji. Usiku huo huo akafunga safari hadi
nje ya jiji la Dar es Salaam, akifwatisha maelekezo
anayo tumiwa kwa njia ya meseji na Rahab aliyopo
ndani ya ikulu
“Mke wangu leo unachati sana”
Raisi Praygod alimuuliza Rahab, mara baada ya
kuingia ndani ya chumba chao dakika kadhaa zilizo
pita, ila mapokezi ya leo yapo tofauti sana na siku
nyingine za nyuma, kwani alisha zoea kufanyi
mapokezi ya mabusu motomoto.
“Kuna taarifa ninaisoma hapa”
“Taarifa gani ambayo raisi siifahamu?”
“Aihusiani na Tanzania”
“Mmmm saw………..”
Raisi Praygod hakuimalizia sentesi yake simu yake
ikaita, akaitoa kwenye mfuko wa koti lake la suti na
kukuta Lube ndio anaye mpigia, akamtazama
Rahab kwa macho ya kuiba kisha akaipokea.
“Mmmmmm”
“Mkuu tumeshindwa Samson sio binadamu”
Raisi Praygod akashindwa kuzungumza chochote
zaidi ya kutoka ndani ya chumba chake cha kulala
na kwenda kuzungumzia sebleni, na kumpa nafasi
Rahab ya kumpigia simu Samson.
“Sio binadamu kivipi?”
“Yaaani yaani macho yake yamekuwa kama,
samba”
“Ahahaa Lube hembu pangilia sentesi zako
nikuelewe”
“Yaani Samson ni jinni”
“Jini, mupo wapi?”
“Ndio tunaingia hapa getini”
“Basi njooni ofisini kwangu”
Raisi Praygod akakata simu na kujikuta uchovu
wote alio kuwa nao ukimuishia na kuanza
kutembea hatua za haraka kuelekea ofisini kwake.
“Samson imekuwaje ukaonyesha uhakisia wako”
“Samahani madam”
“Siku nyingine hakikisha kwamba uhalisia wako
unapo uonyesha kwa mtu yoyote, usiye muamini
hakikisha kwamba unaitoa roho yake”
“Sawa madam”
“Mumesha fika”
“Ndio tunafika”
“Kesho nitakuja hakikisha kwamba humuachi peke
yake”
Samson akasimamisha gari lake pembezoni mwa
handaki alilo elekezwa akashuka na kufungua
mfuniko wa chuma ambao pembezoni mwake
akakuta jiwe kubwa. Mazingira ya eneo hilo
yanaonyesha kuna watu wametoka katika eneo hilo
siku chache zilizo pita. Akaingia ndani ya handaki
hilo akiwa peke yake, akalichunguza handaki hilo
kwa umakini, alipo hakikisha usalama upo akarudi
kwenye gari akambeba Eddy na kumpeleka
kwenyemoja ya chumba chenye kitanda, akamlaza
vizuri kisha yeye akatoka na kukaa kwenye moja ya
kiti kilichopo kwenye seble kubwa ndani ya
handaki hilo
Raisi Praygod akajikuta akishusha pumnzi nyingi
baada ya kuambiwa mambo yaliyo tokea, kichwani
kwake akajikuta akimuwa Eddy na Samson.
‘Rahab’
Raisi Praygod akakumbuka kwamba mtu aliye weza
kuurudisha uhadi wa Samson ni Rahab, kwa haraka
akanyanyuka na kuwaacha vijana wake ndani ya
ofisi hiyo na moja kwa moja akaelekea chumbani
kwake na kumkuta Rahab akiwa amelala. Jinsi
anavyo zidi kumtazama ndivyo jinsi uchungu na
wivu unavyo zidi kumtawala kila akimkimbuka
Eddy na kuvuta baadhi ya kumbukumbu jinsi Eddy
alivyo mfanya mke kitandani hasira kali ikazidi
kumpanda hadi akahisi kifua chake kumpasuka.
Akavua nguo zake zote na kubaki kama alivyo
zaliwa, akalifunua shuka alilo jifunika Rahab na
kumkuta akiwa kama alivyo zaliwa, kwa papara
akajikuta akianza kumpapasa kila eneo la mwili wa
Rahab ila kitu kilicho mshangaza siku ya leo, jogoo
wake halikuweza kusimama kitu kilicho mfanya
Rahab kuyafumbua macho yake na kumtazama
mumewe kisha akatabasamu kwa dharau
“Endelea kufanya unacho kifanya”
Maneno ya Rahab yakamfanya raisi Praygod
mapigo yake ya moyo kumuenda mbio kiasi cha
kujikuta jasho likimwagika mwili mzima na kujikuta
akijilaza pembezoni mwa Rahab ikiashiria kwamba
ameshindwa jogoo wake ameshindwa kuwika
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 28 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (28)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Akavua nguo zake zote na kubaki kama alivyo
zaliwa, akalifunua shuka alilo jifunika Rahab na
kumkuta akiwa kama alivyo zaliwa, kwa papara
akajikuta akianza kumpapasa kila eneo la mwili wa
Rahab ila kitu kilicho mshangaza siku ya leo, jogoo
wake halikuweza kusimama kitu kilicho mfanya
Rahab kuyafumbua macho yake na kumtazama
mumewe kisha akatabasamu kwa dharau
“Endelea kufanya unacho kifanya”
Maneno ya Rahab yakamfanya raisi Praygod
mapigo yake ya moyo kumuenda mbio kiasi cha
kujikuta jasho likimwagika mwili mzima na kujikuta
akijilaza pembezoni mwa Rahab ikiashiria kwamba
ameshindwa jogoo wake ameshindwa kuwika
ENDELEA
“Mke wangu kweli unanipenda?”
Raisi Praygod alimuuliza Rahab kwa sauti ya upole
sana hadi Rahab akajisikia huruma ndani ya moyo
wake, taratibu akajinyanyua kitandani akamtazama
mume wake usoni jinsi anavyo onekana
kufedheheshwa na kitendo kilicho weza kutokea
muda mchacha ulio pita.
“Nakupenda sana Pray”
“Kwa nini………”
Raisi Praygod akajikuta akiikatisha sentesi yake,
kwani hakuhitaji kumfanya mke wake kuweza
kugundua kwamba amesha wastukia mahusiano
yake na Eddy. Rahabu taratibu akaushusha mkono
wake hadi kwenye jogoo wa raisi Praygod na
kuanza kuishika taratibu, msisismko mkubwa
ukauvaa mwili wa raisi Praygod na kumfanya jogoo
wake kusimama haraka sana hadi mwenye
akajishangaa ni kitu gani ambacho ameweza
kukifanya mke wake, kwa haraka akajikuta
akijigeuza na kumlaza Rahab chali, kisha
akampanua miguu yake na mkono wake wa kulia
akaupeleka kwenye kitumbua cha Rahab na kuanza
kukichezea kwa haraka, akiwa na wasiwasi jogoo
wake anaweza kulala tena ikawa fedheha.
***
Alfajiri na mapema Eddy akanyanyuka kitandani
huku akiwa amechoka na kichwani kwake maumivu
makali akiyahisi kama kuna vyuma vinagongana
ndani ya kichwa chake. Akajitahidi kutazama kila
kona ya chumba hicho, hakujua ni wapi ambapo
yupo. Akakumbuka tukio la mwisho jana, ni watu
wanne walio mzingira na kupigana naye, hakuweza
kuwafahamu kwani watu hao walizifunika sura zao
na walionekana macho yao tu. Akajinyoosha
kidogo kisha akasimama, mlango wa chumba hicho
umerudishiwa kidogo na haujafungwa moja kwa
moja. Akapiga hatua na kutoka nje ya chumba
hicho, akamkuta Samson akiwa amekaa kwenye
kiti ambacho mbele yake kuna computure kadhaa
akionekana kuwa bize akisoma soma mambo
yaliyomo ndani ya computer hiyo.
“Umeamka”
Samson alianza kuzungumza mara baada ya
kumuona Eddy amesimama nje ya mlango huo
akimtazama pasipo kuzungumza kitu chochote.
“Ndio, hapa ni wapi?”
“Hapa ni makazi mengine mapya, yenye usalama
kwako”
“Kwa nini nipo hapa?”
Samson akanyanyuka kwenye kiti hicho,
akamsogelea Eddy, kwa sauti ya upole
akamuelezea tukio la mwisho la jinsi yeye alivyo
weza kumuokoa kutoka mikononi mwa watu wa
raisi Praygod Makuya.
“Ina maana raisi yeye ndio aliye watuma”
“Ndio yeye ndio yupo nyuma ya hili, ila Madam
amaeniambia kwamba nikuweke hapa hadi atakapo
kuja”
“Na yeye anafahamu juu ya hao watu?”
“Hapana ila mimi ndio niliye weza kumuambia
kwamba kuna watu walityuma kuja kukudhuru”
Eddy akashusha pumzi nyingi huku akishika
maeneo ya nyuma ya kichwa chake akionekana
maumivu yakiendelea kumuumiza sana.
“Shamsa Shamsa yupo wapi?”
Eddy alimuuliza Samson huku akiwa
amemtumbulia macho. Kwa muonekanano wa
Samson anaonekana kuto kujua Shamsa aneye
mzungumzia Eddy, hatambua ni wapi alipo.
“Ohhh Mungu wangu, Samson nitafutie mwanangu
tafahali nakuomba, mwanangu amechukuliwa na
huyo mwanaharamu Makuya”
“Sawa nitalifwatilio hilo”
Eddy katika kutazama tazama kwenye chumba
hicho akaona kamera moja ikiwa juu ya meza
zenye computure hizo, akapiga hatua na kuifwata,
akaichukua na kuiwasha.
“Hii ni yakwako?”
“Ndio, nilikuwa nayo kwenye gari”
“Ile miguu yake ya kusimamia ipo wapi?”
“Nimeicha ndani ya gari”
“Naomba ukaniletee tefadhali”
Samson hakupingana na Eddy akatoka ndani ya
handaki hilo, akafungua mlango wa nyuma wa gari
lake na kuchukua miguu maalumu ya
kusimamishia kamera, ambayo mara nyingi kuwa
ni mitatu ila ipo katika sehemu moja. Samson
akamkabidhi Eddy miguu hiyo, Eddy akaichanua
kwa haraka, akaifunga kamera hiyo aina ya Canoon
7D, alipo hakikisha kwamba ipo katika sehemu
ambayo inafaa. Akachukua moja ya kiti na kukaa.
“Hapo unanipata vizuri?”
Eddy alimuuliza Samson, ambaye alitingisha
kichwa akiashiria kwamba amejaa vizuri kwenye
frame ya kamera hiyo. Eddy akaanza kuzungumza
maneno ambayo hata Samson akajikuta akiwa
anashangaa kwani hakujua ni kwanini Eddy
ameamua kuzungumza maneno hayo.
“Zima kamera”
Eddy alimuamuru Samson, naye akafanya hivyo.
Eddy akaichukua kamera hiyo, akasogea hadi
kwenye moja ya computer, akachukua waya aina
ya USB, unaotokea kwenye moja ya CPU ya
computer moja, akauchomeka kwenye kamera hiyo
na kuanza kunakilini video aliyo zungumza na
kuiingiza kwenye computer alipo hakikisha
amemaliza, akaanza kuifanyia uhakiki. Yote yakiwa
yanaendelea Samson hakuhitaji kuzungumza kitu
cha aina yoyote kwani hakujua ni nini haswa
mpango wa Eddy.
Eddy alipo hakikisha ameimaliza kazi hiyo,
akaingia kwenye moja ya mtandao kwa kupitia
enternet akaiba freguency za chanel zote za
telvishion nchini Tanzania. Pasipo kuomba ushauri
wa mtu yoyote akaituma video hiyo kwenye chanel
zote za televishion, na kila jambo lililo kuwa
likitizamwa kwa wakati huo kwa kila chanel,
likasimama na kuingia video aliyo ituma Eddy kwa
Watanzania wote.
***
“Ndugu Watanzania wezangu, nimatumini yangu
muwazima wa Afya. Nina imani kwamba
mumeshangaza sana na kuona hii video kujitokeza
kwa muda kama huu, huku baadhi yenu nikiwa
nimewakatishia kile mulicho kuwa mukikitazama.”
Sauti inayo toka kwenye luninga ya moja iliyomo
ndani ya chumba kimoja, ikaanza kupenya taratibu
kwenye masikio ya binti ambaye ni siku ya pili
sasa amelala pasipo kujitambua.
“Nichukue nafasi hii kuwashukuru wale wote
ambao mumeweza kunitumia rambirambi na
kuguswa na msiba wa familia yangu, kusema kweli
nimefarijika na kuamini kwamba watanzania ni
watu wakarimu wenye upendo katika mioyo yao
japo si wote.”
“Katika kuzungumza hayo yote niende kwenye
pointi yangu ya msingi iliyo nifanya kuituma video
hii kwa uma.Kuanzi tarehe hii ya leo, nimeamua
kujivua rasmi uwaziri wa Ulinzi wa nchini Tanzania.
Najua kwa upande mmoja itakuwa ni huzuni kwa
wale ambao nimesha wahi kuwafanyia wema na
kuzitetea haki zao, ila pia itakuwa ni sherehe na
furaha kwa wale ambao wanakwenda kinyume na
sheria za nchi hii.”
“Hivyo basi, mali ulinzi ambavyo vyote nilipatiwa
na serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania,
ninavirudisha kwao. Nitabaki kuwa Eddy, EDDY
GODWIN. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki
Tanzania asanteni kwa kunisikiliza.”
Video hiyo ikaisha na vitu vilivyo kuwa vikiendelea
kwenye chanel mbalimbali vikaendelea kama
kawaidia.
“Haaa huyu jamaa ana maana gani sasa”
Kijana aliyo ndani ya chumba hicho alizungumza
akiwa ameitumbulia macho Tv yake, akiwa katika
mshangao huo, binti aliye mlaza kitandani kwake
taratibu akanyanyuka akionekaa kuchoka sana.
“Hapa nipo wapi?”
“Ahaa hapa upo ndani kwangu”
Kijana huyo alizungumza huku akitabasamu sana,
kwa haraka akanyanyuka kwenye sofa moja alilo
kaa nakwenda kitandani kumfwata binti huyo.
“Wewe ni nani?”
“Mimi naitwa Dulla, wewe je unaitwa nani?”
Binti huyo badala ya kujibu kitu chochote,
akajitazama mwili mzima, hapakuwa na alama
yoyote ya yeye kuumia. Mavazi yake aliyo yavaa
siku ya mwisho kabla hajatekwa na mtu asiye
mjua ndio hayo hayo aliyo yavaa.
“Nahitaji kwenda nyumbani”
Binti huyo alizungumza huku akijaribu kushuka
kitandani ila Dulla akamzuia kwa kumshika kwenye
paja la mguu wa kushoto, kwa kitendo cha haraka
Dulla akajikuta sura yake ikiwa imekandamizwa
kwenye godoro huku mkono wake alio kuwa
umeshika paja la binti huyo mrembo sana, ukiwa
menyongorotwa kwa nyuma na kumfanya kutoa
mlio wa maumivu makali, ila haukusikika sana
kwani sauti yote iliishia kwenye godoro hilo.
“Wewe ni nani?”
Binti huyo alizungumza kwa sauti ya ukali, huku
akiwa amekaa juu ya kiuno cha Dulla na kuzidi
kuunyongorota mkono huo kwa kuurudisha nyuma
kwa nguvu.
“Mimi ni Dullaaaaaaa”
Kijana huyo alizungumza huku akilia kwa maumivu
makali
“Wewe ndio uliniteka eheee?”
“Hapana nilikusaidia tu mimi”
Kwa maumivu makali anayo yapata Dulla
yakamfanya sautio yake kuwa yakilio jambo lililo
mfanya binti huyo kidogo kumuamini Dulla sio mtu
mbaya kwake. Akamuachia na kushuka kitandani,
akakitazama chumba vizuri na kugundua ni
chumba cha mtu ambaye anaanza maisha hivi
karibuni.
Dulla akanyanyuka taratibu huku wasiwasi mwingi
ukiwa umemjaa moyoni mwake, woga wa
kumuogopa binti huyo ukazidi kumvaa na kujikuta
akikaa kimya, akiwa anamtazama binti huyo kwa
macho ya woga.
“Samahani”
Dull hakuamini kama msichana huyo anaweza
kumuomba msamaha kwa tukio alilo weza
kulifanya, Dull akatingisha kichwa chake kukubali
msamjaha huo hii ni baada ya kinya chake
kushindwa kuzungumza kwa kigugumizi.
“Umenifikishaje hapa?”
“Hapa nilikueleta ukiwa hujitambu, majuzi nilikuwa
nipo pembezoni mwa fukwe za bahari, nikifanya
fanya mazoezi. Ila kwa bahati nzuri niliweza
kukuona ukiwa umesimama kwenye moja ya
bustani katika jumba la kifahari. Ila ulipo kuwa
pale, nyuma yako nikamuona mtu aliye valia suti
nyeusi pamoja na shati jeupe.”
“Sikusikia mtu huyo alicho kizungumza, ila ulipo
geuka nikashangaa akikupiga ngumi, kisha
akakubana na kitambaa cheupe puani mwako,
nilijificha baada ya kumuona mtu huyo akija
upande wa ufukweni karibu sana na nilipo mimi.”
“Yule jamaa alikuingiza kwenye moja ya jiwe
kubwa kama mwamba lenye tobo kubwa ambapo
mtu ukiingia humu si rahisi kwa watu kuweza
kukuona.”
Dulla alizungumza kwa sauti ya upole huku
akimeza mafumba ya mate ya hapa na pele, kisha
akaendelea kuzungumza.
“Yule jama baada ya kuondoka, mimi
nikakuchukua na kukuingiza kwenye kigari change
nilicho kuwa nimekiweka pembezoni mwa barabara
na kukuleta hapa nyumbani kwangu.”
“Haya ni maeneo gani?”
“Mbezi mwisho”
Binti huyo akapiga hatua hadi dirishani akafungua
dirisha na kuchungulia nje ambapo akaona ukuta
tu ukiwa umepita katika eneo hilo. Akalirudishia
pazia kama alivyo likuta na kumtazama kijana
huyo anaye onekana mpole, akamchunguza vizuiri
akajiridhisha moyoni mwake anaweza kummudu
kama atamletea fujo yoyote.
“Nikuandalie chai?”
Dulla alizungumza binti huyo hakujibu kitu cha
aina yoyote, likawa ni jibu tosha kwa Dulla kwamba
anaweza kuandaa chochote kitu kwani tangu
amuokoe binti huyo hakuna kitu alicho weza
kukiingiza tumboni mwake. Dulla akaandaa
kifungua kinywa kwa binti huyo na kukiweka
mezani, binti huyo taratibu akaanza kufakamia
soseji na mayai yaliyo andaliwa vizuri na kijana
huyo huhu akishushia na mafumba ya chai.
“Umejitahidi katika kupika”
“Ahaa asante sana”
Dulla akajibu kwa kufurahi sana kwani aliweza
kulishuhudia tabasamu la binti huyo anaye
onekana ni mkali sana na nimtu asiye penda
uzembe wa aina yoyote.
“Hapa unaishi na nani?”
“Peke yangu, leo nipo mapumziko, mimi ni daktari.
Nina mwaka mmoja kazini”
“Ahaaa sawa, naomba maji ya kunywa”
Dulla akanyanyuka na kulisogelea friji lake dogo,
akafungua na kutoa jagi lililo jaa maji,
akayamimina kwenye glasi moja kubwa kiasi kisha
akamkabidhi binti huyo ambaye hadi wakati huu
hakulitambua jina lake anaitwa nani. Binti huyo
akayagugumia maji hayo kwa mfululizo, kisha
akaiweka glasi hiyo juu ya meza na kumtazama
Dulla
“Asante kwa chakula chako, nahitaji kurudi
nyumbani”
“Ahaa mbona mapema sana?”
“Nimekuambia nahitaji kurudi nyumbani sawa”
Sauti ya ukali ya binti huyo ikamfanya Dulla
kustuka na kujikuta akinyanyuka na kuanza
kuitafuta funguo ya gari lake ni wapi ilipo, alipo
hakikisha ameiipata akamgeukia binti huyo aliye
simama karibu na mlangoni tayari kwa kuondoka.
“Tunaweza kwenda”
Dulla alizungumza kwa sauti ya upole huku
akishika kitasa cha mlamgo wa kutokea tayari kwa
kuondoka.
***
“Maana yake ni nini kufanya hivi?”
Raisi Praygod aliwauliza baadhi ya washauri wake
alio waita ofisini kwake mara baada ya kuiona
video ya waziri wa ulinzi bwana Eddy Godwin.
“Labda atakuwa ameungana na baba yake”
Mshauri wake mmoja alizungumza nakumfanya
mwengine kuongezea neon
“Kweli damu ni nzito kulilo maji na mototo wa chui
ni chui tu hawezi kuwa paka”
“Sasa tumfanye nini?”
“Kikubwa huyo ni kumkamata na kuhakikisha
kwamba anataja ni wapi alipo baba yake”
Mshauri huyo, kazi yake ni kuwasoma wezake
kwani ni miongoni mwa wanachama wa D.F.E, na
yeye ndio mvujishaji wa siri zote za ikulu kwa
Mzee Godwin.
“Au muheshimiwa unaonaje ukamtangaza kama
most wanted”
“Most wanted ni lazima kuwe na kidhibitisho cha
kumfanya yeye kuwa ni mmoja wa watu wanao
tafutwa”
“Muheshimiwa kama ni ushahidi basi hiyo kazi
niachie mimi, nitahakikisha nay eye tunamfanya
kama tulivyo mfanya baba yake”
Wote watano akiwemo raisi Praygod wakajikuta
wakitabasamu wakiamini mpango wao umekwenda
sawa sawa, lakini yote yaliyo kuwa yakiendelea
ndani ya ofisi hiyo Rahab aliweza kuyasikia, hii ni
baada ya kuingiza kinasa sauti kwenye suti ya
mumewe pasipo yeye kujijua wakati akiwa
anamuandaa wakati wa asubihi akielekea kwenye
kikao hicho na washauri wake. Rahab akatabasamu
huku akiitazama simu yake aliyo iunganisha moja
kwa moja na kinasa sauti hicho. Akaachia
tabasamu na kujiapiza washauri wote wa ofisi ya
mume wake ni lazima wafe kwani wanataka
kuipoteza furaha yake ambayo ni Eddy Godwin.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 29 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (29)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“Muheshimiwa kama ni ushahidi basi hiyo kazi
niachie mimi, nitahakikisha nay eye tunamfanya
kama tulivyo mfanya baba yake”
Wote watano akiwemo raisi Praygod wakajikuta
wakitabasamu wakiamini mpango wao umekwenda
sawa sawa, lakini yote yaliyo kuwa yakiendelea
ndani ya ofisi hiyo Rahab aliweza kuyasikia, hii ni
baada ya kuingiza kinasa sauti kwenye suti ya
mumewe pasipo yeye kujijua wakati akiwa
anamuandaa wakati wa asubihi akielekea kwenye
kikao hicho na washauri wake. Rahab akatabasamu
huku akiitazama simu yake aliyo iunganisha moja
kwa moja na kinasa sauti hicho. Akaachia
tabasamu na kujiapiza washauri wote wa ofisi ya
mume wake ni lazima wafe kwani wanataka
kuipoteza furaha yake ambayo ni Eddy Godwin.
ENDELEA
***
Taarifa ya Eddy kujiuluzu katika nafasi yake ya
uwaziri wa ulinzi, iliwashangaza sana wananchi
wengi wa Tanzania, kila kona ya Tanzania watu
walizungumza maneno yao, wengine wakimlaumu
ni kwanini amefanya hivyo. Baadhi ya watumishi
katika jeshi, wakajikuta wakiumia mioyo yao kwa
kiongozi huyo waliye tokea kumpenda kutokana na
utendaji wake wa kazi na kutetea masilahi yao
ambayo mara nyingi huwa yanacheleweshwa sana
katika kuyapata.
Simu ya mzee Godwin ikaingia ujube wa video,
kwa haraka akaifungua video hiyo, akaanza
kuitazama jinsi Eddy anavyo jiudhuru katika nafasi
ya uwaziri jambo lililo mstua sana.
“Baba ni nini?”
Manka alimuuliza, huku akimtazama usoni mzee
Godwin
“Eddy amejiudhuru uwaziri”
“Ana maana gani ya kujiudhuru”
“Hakuna anaye fahamu”
Safari yao ikachuku masaa kadhaa hadi wakafika
katika nchi ya Mexco kwenye makao makuu ya
kambi yake. Wakapokelewa na John akliwa na
wapambe wengine. Kama kawaida wakampa
heshima Mzee Godwin ambaye ndio mmiliki wa
ngome nzima.
“Muheshimiwa kila kitu kipo sawa”
“Kazi nzuri nahitaji uitishe kikao sasa hivi”
“Sawa muheshimiwa”
Wote wakaingia kwenye magari ya kifahari, yaliyo
wapeleka mpaka kwenye jumba kubwa la kifahari
waitokea kwenye uwanja wa ndege mdigo ulipo
kwenye ngome hiyo. Kikao cha dharura
kikaitishwa, mzee Godwin akakutana na wanajeshi
wake wengi wakiwa ni waasi katika nchi zao walizo
toka, ambao idandi yao ni sawa na watu elfu
hamsini.
Nacho ya Mzee Godwin kila anavyo watazama
wanajeshi wake hao walio jipanga mitsari iliyo
nyooka, moyoni mwake akajihisi nguvu ya ajabu,
kwani taratibu malengo yake yanazidi kuongezeka
siku hadi siku. Agnes na Jaquline nao ni miongoni
mwa wanajeshi walio panga mtari katika kundi la
wanajeshi wa kike katika kiwanja kikubwa ambacho
mara kwa mara hutumika kama makutano ya wote
pale kiongozi wao mkubwa anapo hitaji
kuzungumza nao.
“Destinatio of our enemies oyeeeeeeeeeeeeee”
Mzee Godwin alizungumza kwa sauti kubwa na
yenye ukakamavu wa hli ya juu, wanajeshi wake
wote wakitikia kwa sauti ya juu huku, wakinyoosha
mikono yao ya kushoto juu huku ikiwa na kofia
wanazo zivaa. Mzee Godwin akarudia tena salamu
hiyo, na wanajeshi wake wakajibu kama walivyo
jibu mara ya kwanza kwa sauti za juu.
“Nimerudi, sasa ni mwendo wa kuhakikisha
kwamba kikosi chetu kinakua zaidi ya hapa”
“Mishahara ya kila mmoja wenu kuanzia mwezi
huu, itaongezeka mara mbili ya jinsi anavyo lipwa”
“Sinto hitaji uzembe kati kazi yoyote ambayo
itapangwa, umakini uskivu na uwajibikiaji ndio
ngao yetu”
“Kiongozi wenu nipo salama kama mulivyo sikia
kwamba ninatafutwa inchioni Tanzania, ila kwa
uwezo wangu ninamshukuru Mungu nipo salama”
Mzee Godwin akanyamaza kidogop huku
akiwatazama wanajeshi wake jinsi walivyo simama
kwa uimara wa hali ya juu.
“Munaweza kutawanyika na kurudi kwenye shuhuli
zenu”
Wanajeshi hao wakatawanyika kila mmoja
akaendelea na majukumu yake ambayo
wanayafanya katiaka ngome hiyo, huku wengine
wakijihusiha na utengenezaji wa madawa ya
kulevya aina ya Cocein, jambo linalo ifanya ngome
hiyo kuzidi kutajirika siku hadi siku, wengine kazi
yao ni kufanya kazi za uhalifu, kuvamia watu
matajiri, mabenki makubwa, yote ni kujitahidi
kuweza kuingiza kiasi kikubwa cha pesa ili
huduma zao ziweze kusonga mbele. Wengine kazi
zao ni kutengeneza silaha za kivita zenye ubora wa
hali ya juu. Wengine kutengeneza ndege za kivita
pamoja na magari ambayo yana uhimara mkubwa
sana katika swala zima la kupambana. Kusema
ukweli kambi ya D.F.E imakamilika kila idara, kila
mmoja aliutumia ujuzi wake katika kuhakikisha
kwamba maisha yake ndani ya ngome hiyo
yanakuwa ni bora zaidi ya mwanzo alipo tokea.
“General kuna wageni wawili ambao tuliweza
kuwaongeza kipindi haupo”
John alizungumza mara baada ya kufika katika
ofisi ya mzee Godwin
“Kina nani?”
John akamnong’oneza mpambe wake aende
akawaite Agnes na Jaquline, akafanya hivyo. Mzee
Godwin akatumia fursa hiyo kuwatambulisha Tom
na Manka kwa John. Baada ya dakika chache
mpambe waka akarudi akiwa ameongozana na
Agnes pamoja na Jaquline. Wasimama kwa
heshima mbele ya Mzee Godwin huku mikono yao
ikiwa nyuma. John akaanza kuwatambulisha kisha
akaanza kutoa maelezo ya jinsi walivyo weza
kuwapata wasichana hao, ambao wanatafutwa na
serikali ya nchini Marekani.
“Jisikieni huru mabinti, hapa ni kama nyumbani
kwenu, chochote mutakacho kihitaji basi musisite
kuzungumza nasi, mimi au huyo bwana mdogo”
“Asante general”
Walijibu kwa pamoja, kwa heshima kubwa pamoja
na unyenyekevu, kwani tayari walisha anza
kuyazoea maisha ya humu ndani.
“Mimi nina ombi”
Jaqulie alizungumza kabla Mzee Godwin
hajafungua kinywa chake
“Ombi gani?”
“Ili kuweza kuimarisha ngome hii, nimejaribu
kutazama mafunzoi yanayo tolewa kila siku, ila
kuna mafunzo ya uninja ambao sote wawili tunayo,
hapa hayafundishwi, naoana ni vyema tukanza
kuyafundisha”
“Ahaa hilo tu nawapeni ruhusa, tena itakuwa vizuri
mukianza na huyu mjukuu wangu Tom”
“Hata mimi baba nahitaji”
Manka alizungumza huku akitabasamu
“Sawa tena huyu munatakiwa kumpa tizi la uhakika
kwa maana amekuwa mzembe sana”
“Asante muheshimiwa kwa kukubali kwako”
“Musijali munaweza kwenda”
Watu wote wakatoka ofisini na kuwaacha John na
mzee Godwin kuzungumza mambo mengine ya
muhimu wanayo yafahamu wao wenyewe.
“General madam Mery yupo wapi mbona hujarudi
naye?”
“Ameungana na Eddy”
Jibu la Mzee Godwin likamstua sana Joihn na
kujikuta akimtumbulia macho mzee huyo kwani
anamfahamu vizuri sana Eddy, akiamua lake huwa
anaamua hata liwe jambo la kuhatarisha maisha
yake basi atafanya hivyo ili mradi aweze
kufanikiwa. Swali la kwanza alilo jiuliza endapo
Eddy atagundua kwamba yeye yupo hai itakuwaje,
swali hilo halikupata jibu zaidi ya kujifajiri atajua
mbele ya safari
***
“Eddy kwa nini umejuzulu?”
“Sikia Samson, katika serikali hii nina maadui
wengi sana, na nikiwa katika kiti cha uongozi sinto
weza kufanya kazi yangu vizuri. Nahitaji kurudi
kuwa Eddy, Eddy yule niliye zoea mateso na
machungu ya haya maisha”
“Ila huoni hivi itakuwa ni hatari sana kwako?”
“Natambu ila nikiendelea kuwa katika uongozi
itakuwa ni hatari sana kwani D.F.E wananitafuta
kulilo kitu chochote”
“D.F.E ndio nini?”
Swali la Samson likamfanya Eddy kumtazama
Samson usoni, hapo ndipo alipo amini kwamba
D.F.E bado ni chama cha siri sana na
hakijajulikana kwa watu wengi ndani ya Tanzania
“Usijali nitakuambia”
Wakiwa ndani ya handaki, wakasikia mngurumo wa
gari kusimama, ikamlazimu Samson kuanza kutoka
ndani ya handaki hilo na kupanda juu, akiwa
makini kutazama ni nani aliye fika katika eneo hilo.
Akamkuta Rahab akiwa na mlinzi wake wa kike,
wamesimama nje ya gari walilo jia, lenye namba sa
usajili T288 DCS, ambayo si gari ya ikulu
“Karibu Madam”
“Asante Eddy yupo wapi?”
“Yupo chini huko”
“Nisubirini hapa”
Rahab akawaacha Samsonm na mlinzi wake wa
kike yeye akshuka chini, ikiwa nio baada ya miaka
mingi sana kupita tangu alipo ondoka ndani ya
handaki hilo. Gafla akastukia ngumi nzito ilioyo
mfwata, kwa wepesi wake akajikuta akiikwepa na
kupita pembeni.
“Eddy ni mimi?”
Rahab alizungumza mara baada ya kumuona Eddy
akijitokeza kwenye kona aliyo kuwa amejificha
akihisi kuna uvamizi umetokea kwani hakumuona
Samson kushuka sehemu walipo.
“Umefwata nini huku?”
“Eddy hata salamu”
“Nijibu kilicho kulete wewe huku ni nini?”
“Nimekuja kukuona mpenzi wangu”
“Rahba sinto hitaji kuwa na wewe tena, nahitaji
kuishi maisha yangu. Huyo memwa wako
amemteka mwanangu kisa ni wewe, huoni unazidi
kuniweka mimi matatani?”
Eddy alizungumza kwa kufoka hadi Rahab akatulia
tuli, akimsikiliza mwanaume huyo aliye anza kufura
kwa hasira na taratibu kifua chake kikianza kujaa.
“Eddy……”
“Eddy nini, unahisi kwamba nitakuelewa kwa
utakacho niambia eheee?”
“Nisikilize basi mpenzi wangu, nipo tayari kufanya
chochote kwa ajili yako, ili mradi nisikupoteze
wewe”
“Upo tayari eheee?”
“Ndio niambie mimi nitafanya”
“Niletee Shamsa mwanangu hapa, kisha ndio
tutaendelea na mambo mengine”
“Sawa”
Rahab akajisogeza karibu na Eddy akataka
kumpiga busu la mdomoni, ila Eddy akamzuia
kukataa busu hilo.
“Fanya hivyo umenielewa?”
“Sawa mpenzi”
Rahab alijibu huku machozi yakimlenga lenga,
akatoka ndani ya pango huku akiwa na hasira kali
ni kwanini mume wake amefikia mbali hadi hatua
ya kumteka binti asiye na hatia katika vita hiyo
inayo endelea kimya kimya.
“Madam….”
Samson aliita baada ya kumuona Rahab akiwapita
kwa hasira na kuingia ndani ya gari na kuubamiza
mlango kwa nguvu, mlinzi wake akaingia kwenye
gari na yeye, akakiweka vizuri kioo chake cha
mbele kinacho muwezesha kuweza kumuangalia
abiria wake wa nyuma, kwa mara ya kwanza
akamshuhudia bosi wake akimwagikwa na
machozi, hakuelewa ni nini kilicho mfanya atokwe
na machozi.
“Muheshimiwa tunaelekea wapi?”
“Popote enmdesha gari?”
Mlinzi wake akabaki akiduwaa, kwani jibu hilo
lilimfanya ashindwe kujua ni nini cha kufanya
“Prisca endesha gari unashangaa nini?”
Rahab alifoka kwa hasira na kumfanya Prisca
kuwasha gari, akaligeuza na kuondoka katika eneo
hilo, lililopo katikati ya msitu wenye miti mingi
sana. Priscar akaamua kuelekea jijini Dar er
Salaam, ikiwezeklana weende ikulu kabisa.
Kutokana safari yao ilikuwa ni ya siri, pamoja na
gari wanayo itumia haina usajili wa namba za
ikulu, ikawalazimu kusimama kwenye foleni kama
watu wengine wanavyo simama, huku akilini
mwake Rahab akifikiria kumuonyesha mume wake
jinsi uhatari wake ulipo pale anapo jaribu kuingia
katika anga zake hususani anga za mapenzi
***
“Una itwa nani?”
Dulla alimiiliza binti aliye mpakiza kwenye gari lake
kwa mara ya pili wakiwa katika foleni ya mataa
maeneo ya Ubungo maji.
“Jina langu halite kusaidia chochote”
Shamsa hakuhitaji kumuamini Dulla moja kwa
moja kwani wasiwasi wa usalama wake bado anao.
Wakiwa kwenye foleni pembeni yao gari nyeusi
aina ya land cruser, ilisimama, huku vioo vyake
vikiwa ni vyeusi, na si rahisi kwa mtu yoyote
kuweza kuona ndani. Brian akiwa katika dibwi
kubwa la mawazo ni jinsi gani anaweza kumpata
Shamsa ambaye hajui ni jinsi gani ametoroka,
kwani kwa dawa aliyo muwekea kwenye kitambaa
alicho mziba puani, huwa inachukua hata masaa
48 kuweza kuondoka mwili mwa mtu na kumfanya
azinduke katika usingizi mzito. Katika kupitisha
pistisha macho yake kutazama huku na kule,
pembeni yake akaona gari ndogo, ila katika
kutazama vizuri akamuona Shamsa akiwa amekaa
pembeni ya siti ya dereva, kijana ambaye hajawahi
kumuona. Ili kuhakikisha kwamba ndio Shamsa
anaye mtafuta ikalazimu kushushakioo kumtazama
vizuri, hapo ndipo macho yake yakagongana na
Shamsa, aliye achia tabasamu pana.
“Mlinzi wetu yule pale ngoja nishuke”
Ikambidi Dullah kumtazama mlinzi mwenyewe ni
nani, alipo muona kumbukumbu kichwani kwake
ikarejea haraka kwamba huyo ndio mlinzi ambaye
aliye mteka Shamsa, ambaye tayari amesha fungua
mlango kwa ajili ya kushuka.
“Noo usiendeeeeeee”
Dulla alizungumza huku akimuwahi kumshika
mkono Shamsa, na alipo geuka kumtazama mlinzi
huyo, akakuta akiwa amenyooshewa bastola ya
uso, huku mlinzi huyo akimueleza kwa ishara ya
mdomo amuachie Shamsa aondoke naye.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 30 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (30)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“Mlinzi wetu yule pale ngoja nishuke”
Ikambidi Dullah kumtazama mlinzi mwenyewe ni
nani, alipo muona kumbukumbu kichwani kwake
ikarejea haraka kwamba huyo ndio mlinzi ambaye
aliye mteka Shamsa, ambaye tayari amesha fungua
mlango kwa ajili ya kushuka.
“Noo usiendeeeeeee”
Dulla alizungumza huku akimuwahi kumshika
mkono Shamsa, na alipo geuka kumtazama mlinzi
huyo, akakuta akiwa amenyooshewa bastola ya
uso, huku mlinzi huyo akimueleza kwa ishara ya
mdomo amuachie Shamsa aondoke naye
ENDELEA
“Unatatizo gani wewe Dulla?”
Shamsa aliuliza kwa sauti ya ukali, huku
akichungulia kwenye gari kumtazama Dulla aliye
mshika mkono. Brian akairudisha bastola yake
haraka, kitendo ambacho Shamsa hakuweza
kukiona.
“Shamsa huyo jamaa ndio aliye kuteka wewe”
Gari za mbele yao zikaanza kuondoka taratibu,
Shamsa akafunga mlango huku akiwa na wasiwasi
mwingi, akilitazama gari la Brian walilo liacha
nyuma kidogo. Wakakunja na kuelekea njia
iendayo Mwenge, ikamlazimu Brian na yeye
kujichochomeka kwenye magari yanayo kunja
kuelekea mwenge, nusu asababishe ajali ila
hakulijali sana jambo hilo.
“Una uhakika kwamba ndio yeye aliye niteka?”
“Ndio ninauhakika, ndio yeye siwezi kukudanganya
nilimuona kwa macho yangu mawili, akikuteka”
Shamsa akatazama nyuma huku akitazama kama
gari ya Brian inawafwata, hakuweza kuiona kwani
nyuma yao kuna gari ya abiria iendayo Kawe.
Wakafika maeneo ya Mlimani City, wakaingia
kwenye eneo hilo na moja kwa moja akatafuta
eneo lenye nafasi ya maegesho na kulisimamisha
gari lao, Brian akiwa katika mwendo kasi,
aliwashuhudia Shamsa na Dulla wakishuka maeneo
ya mlimani City na kuingia ndani,
“Shittiiii………”
Brian alijikuta akiminya honi, kumuashiria dereva
wa mbele alipishe gari lake huku macho yake
akitafuta sehemu ambayo anaweza kuligeuza gari
lake, akafanikiwa kufika kwenye eneo ambalo
aliweza kuligeuza gari lake na kurudi katika eneo la
mlima city huku akiwa na hasira kali sana
“Humu ndani tutampoteza hawezi kutufwatilia
huku”
Dulla alizungumza huku wakijichanganya katikati
ya watu wanai ingia katika jengo kubwa hilo,
Shamsa kazi yake ikawa ni kutazama kila eneo,
kuona kama Brian anawafwatilia.
“Una simu hapo?”
“Ndio”
Brian akatoa simu yake na kumkabidhi Shamsa
aliye minya minya baadhi ya namba na kuiweka
simu yake sikioni. Majibu aliyo kutana nayo ni
kwamba namba ya simu ambayo anaipigoa
haipatikani kwa muda huo, akarudia tena kuipiga
ila jibu likawa ni moja kwamba namba anayo ipiga
haipitikani kwa wakati huo.
“Baba hapatikani”
“Hembu jaribu kumpigia tena inawezekana ikwa ni
mtandao unasumbua”
Shamsa akajaribu kuipige tena namba ya Eddy ila
haikuwa hewani, wakatafuta moja ya mgahawa na
kutafuta sehemu iliyo jificha na kukaaa. Hapakuwa
na aliye kuwa na hamu hata ya kuweka kitu
chochote mdononi mwake.
“Ila unajua serikali ya Tanzania inavituko sana”
Kijana mmoja aliye kaa pemebi yao pamoja na na
mwenzake alisikika akizungumza huku akiwa
ameishika simu yake mkononi aina ya Samsung
Note 3.
“Kwa nini?”
“Sijui ni sababu zipi zilipelekea hadi yule waziri wa
ulinzi kujiudhuru hadharani”
Taarifa hiyo ikamstua kidogo Shamsa na kujikuta
akiwatazama vijana hao kwa macho ya kuiba huku
masikio yake akiwa moja kwa moja ameyeelekezea
kwa vijana hoa.
“Serikali yetu bwana ina mambo, unajua jamaa
alikuwa mkweli, inawezekana amaeona upuuzi
unaoa endelea akaamua kujiudhuru”
“Niwasaidiea nini?”
Dada mmoja aliye valia sketi fupi huku kitambaa
cha rangi nyekundu akiwa amekifunga kiunoni
mwake, aliwauliza Shamsa na Dulla walio jikuta
wote wakimtazama.
“Mimi mimi maji”
Dulla alibabaika kujibu swali hilo jepesi, dada huyo
alimtazama Shamsa akisubiria kulipata jibu lake
“Dada na wewe nikuletee nini?”
“Juisi yoyote”
Dada huyo aliandika kwenye kikaratasi chake
kidogo na kuondoka, kwa mwendo wa kawaida,
akafika sehemu ya vinjwaji, akatoa simu yake na
kumpigia Brian.
“Bosi wapo hapa”
Maneno hayo yalitosha kabisa kumjulisha Brina ni
wapi walipo vijana anao watafuta. Brian akageuza
mulekeo wake, akaenza kutembea kwa mwendo wa
kasi kuelekea kwenye mgahawa, hata kabla hajafika
kwenye mgahawa huo simu yake ikaita, ikaitoa
mfukoni haraka haraka na kuipokea.
“Umefikia wapi?”
“Mkuu nipo mlimani City, ndio ninawafwatilia”
“Sasa kuna vijana wnafika hapo, kuna plani
nimeipanga sasa wewe wasubirie”
“Plan, Plan gani muheshimiwa”
“Subiria”
Sauti ya mmoja wa viongozi waliopo ikulu ya raisi
praygod ilisikika kwenye simu ya Brina, kisha
ikakatika, Brian akajikuta akiwa amesimama huku
akiwa hafahamu ni nini cha kufanya.
“Ina maana baba yangu amejiudhuru?”
“Baba yako yupi?”
“Waziri Eddy”
“Ina maana waziri Eddy ni baba yako?”
“Ndio”
Dulla akabaki akiwa amemtumbulia macho
Shamsa, huku akiwa kama haamini fulani kwamba
Shamsa ni mtoto wa waziri Eddy.
***
Hali ngumu ya mateso makali ikazidi kuongezeka
siku hadi siku kwa kina Fetty na wezake wawili,
manyanyaso ya kupigwa shoti za umeme pamoja
na sindano za maumivu makali zilifanyika mara
kwa mara wakiwa ndani ya gereza. Yote hayo
walihitajika kuweza kusema ni wapi ilipo ngome
yao ya walio kuwa wakiwatumikia. Hapakuwa na
mtu aliye weza kusema lolote si Fetty, Halima wala
Anna.
Afya zao siku hadi siku zikazdi kuzorota kwa
mateso hayo makali wanayo yapata, kila mmoja
alijiapiza moyoni mwake ni bora kufa kuliko
kusema ni wapi walipo kuwa wakitokea isitoshe,
kila mmoja tayari alisha pata mateso yakutosha.
Ulinzi mkali ulizidi kuwekwa dhidi yao, hadi
vyumba vya kulala kila mmoja aliweza kuingizwa
kwenye chumba chake tofauti ambacho kina
kamera ya ulinzi inayo mmulika masaa yote
atakapo kuwa ndani ya chumba hicho.
Hapakuwa na mwana harakati aliye weza kutokea
kuzitetea haki zao, kwani manyanyaso yalipita
kikomo. Mpango wa kuwahamisha katika gereza
hilo na kuwapeleka katika gereza jengine, lenye
mateso makali kupindukia ukaanza kupangwa
taratibu, kikosi cha FBI, kikiwa kinahusika katika
kusimamia kusafirishwa huko kwa waalifu watuta
wambao wanasadikika ni kati ya wale walio husika
katika kifo cha waziri wao wa mambo ya nje bwana
Paul Henry Jr.
“Ni lini wana hamishwa gereza”
Agnes aluliza kwa shahuku kubwa mara baada ya
kusikia taarifa hiyo kutoka John.
“Siku maaalumu bado haijapanmgwa, ila kuna watu
wentu wanaendelea kulifwatilia hilo swala
kuhakikisha wanatupa taarifa kwa kila jambo
ambalo litaendelea ndani ya gereza hilo”
“Ila wanasafirishwa kwa usafiri gani, kutokana wao
wapo katikati ya kisiwa”
Jaquline aliuliza huku akimtazama John usoni
“Hapo kweli ndipo hata sisi tunapo takiwa kuwa
makini napo, kufahamu siku ambayo
wanasafirishwa peke yake haitoshi kujifariji kama
tunaweza kuwaokoa”
John akamuamuru mpambe wake ambaye muda
wote anatembea naye kuwapa baasha ya kaki
Agnes na mwenzake kutazama baadhi ya picha
zilizopo ndani ya bahasha hiyo. Kila picha ambayo
Agnes aliitazama akajikuta machozi yakimwagika
kwa wingi, wezake hao walio kuwa mabinti
warembo wa kuvutia sana, wamechakaa kiasi cha
kuonekana kama vizee omba omba sana. Nywele
zao na miili yao ilizidi kudhohofika na kuwa
wembama sana, mithili ya watu ambao ni
wagonjwa sana. Kwa hasira Agnes akajikuta
akikunja moja ya picha ya Halima, aliye chakaa
kupita wote, kisha akaondoka kwa hasira huku
akilia, Jaquline naye akaondoka kwa haraka
kuelekea alipo kwenda Agnes
***
“Sasa unahisi madam anaweza kufanikisha
kumpata mwanao?”
“Natambua anaweza kumpata mwanangu, kutokana
mume wake yeye ndio aliye nyuma ya tukio zima
hili”
Samson akabaki kimya hakuwa na swali jengine
kwa Eddy, aliye kaa kwenye kiti pembezoni mwa
computer zilizomo ndani ya handaki hilo. Eddy
akaendelea kuperuzi peruzi kwenye mtandao,
habari ya yeye kujiudhuru ndio habari inayo
zungumziwa kwa sana katika mitandao mingi ya
kijamii. Gafla sura yake ikaanza kubadilika, huku
akiikazia macho cumputure hiyo akisoma habari
ambayo ameiona kwa wakatia huo katika moja ya
ukurasa wa kituo kikubwa cha habari.
“Samson njoo uone”
Samson kwa haraka akasogea eneo ambalo yupo
Eddy, kitendo cha yeye kuisoma taarifa hiyo naye
sura yake ikabadilika na kujikuta akishangaa
***
Moshi mkali wa gesi na unao nuka vibaya ukaanza
kusambaa ndani ya jengo kubwa la kibiashara la
Mlimani City. Milio ya risasi ikaanza kurindima kila
mhala jambo lililo wafanya wananchi wengi walio
kuwemo ndani ya jengo hilo kuanza kutawanyika
huku wakipiga kelele, na kila mmoja akijitahidi
kuyaokoa maisha yake.
Amri moja ikatolewa watu wote walale chini ya
sakafu huku mikoo yao ikiwa kichwani, na
wananchi nao wakafanya hivyo kwani aliye kuwa
mbishi katika hilo aliambulia kupigwa risasi hadi
kufa. Watu wapatao ishirini walio valia nguo nyeusi
pamoja na vitambaa vyeusi usoni mwao vilivyo
wabakisha macho, walitawanyika na kulizunguka
eneo zima la jengo la Mlimani City, wakiwa na
silaha nzito mikononi mwao. Polisi pamoja na
walinzi wote walio kuwepo katika jingo hilo
waliuawa kikatili. wengine walichinjwa na wengine
walipigwa risasi za vichwa na kupoteza maisha
yao.
Vijana wawili wakamtafuta Brian alipo
wakamnyanyua mzoga mzoga hadi kwenye moja
ya vyoo, kisha wakavua vitambaa vyao usoni.
“Samahani muheshimiwa mimi ninaitwa Ahemed”
“Mimi ninaitwa Briton, ndio viongozi wa kundi hili,
tuliingia jana usiku hapa Tanzania tukitokea
Somalia, sisi ni miongoni mwa wafuasi wa D.F.E,
tukishirikiana na Al-Shabab”
Hapo ndipo Brian akatambua maana ya simu aliyo
pigiwa na kiongozi wake kutokea ikulu
“Kazi nzuri vijana, sasa mpango ni upi unao
endelea kati yenu”
“Ngoja tukuonyeshe”
Briton akapiga simu ya upepo kwa jamaa anaye
itwa Lukuma, wakamuelekeze sehemu walipo,
ndani ya dakika tatu jamaa akwa ameingia kwenye
vyoo hivyo na kukutana na wezake.
“Vua kitambaa chako muheshimiwa akuone”
Lukuman akafanya hivyo, Brina akajikuta
akimshanga sana Lukuma.
“Huu ndio mpango wetu kwa sasa”
Briton alizungumza huku akimruhusu Lukuman
kuvaa kitambaa chake. Wakatoka na Brian
wakijifanya kama wamemshikilia mateka moja kwa
moja wakaelekea kwenye chumba cha kamera za
ulinzi za jengo zima ambapo wezaowengine wawili
tayari walisha waweka wafanyakazi wote ndani ya
chumba hicho chini ya ulinzi.
“Unganisha tv zote za humu ndani zionyeshe viseo
hii”
Briton alimuamrisha mmoja wa mafundi mitambo
wanao shuhulika ndani ya chumba hicho, jamaa
akaminya minya kwenye computer yake, Tv zote
zilizomo ndani ya jengo zima zikawa zinaonyesha
kitu kimoja tu, mistari mistari myekundu, njano,
myeupe na bluu. Ahmed akavua begi lake dogo
alilo kuwa amelivaa mgongoni akatoa kamera moja
ndogo pamoja na vimuguu vya kusimamishia
kamera hizo. Wakaiunganisha na mtambo unao
ungoza tv zote ndani ya jengo la Mlimani City.
Lukuman akasimama mbele ya kamera hiyo huku
akiwa ameshika bastola, kwa ishara ya vidole
Briton akaanza kuhesabu moja hadi tatu, Lukuma
akavua kitambaa cheka cha usoni.
Kukohoa kwake kidogo kukawafanya baadhi ya
watu kunyanyua vichwa vyao kutazama tv zilizomo
kwenye maeneo yao, akiwemo Shamsa, aliye stuka
sana kumuona Eddy kwenye Tv hizo, akionekana
yeye ndio kiongozi wa kundi hilo lililo teka jengo
zima la Mlimani City
“Baba…………………!!!”
Shamsa alizungumza huku akikinyanyua kichwa
chake juu kabisha bila hata ya kuhofia ulinzi mkali
walio wekewa, hapo ndipo alipo mfanya Dulla naye
kunyanyua kichwa chake na kumuona waziri Eddy
akiwa katika mavazi mengine ya kikazi zaidi tofauti
na asubuhi alivyo kuwa amevaa, pale alipokuwa
akitangaza kujiudhulu.
Vyombo vyote vya habari vikarusha tukio zima,
ikiwa ni habari ya dharura(breaking news). Kwa
kamera moja ya muandishi wa habari aliye kuwemo
ndani ya jengo hilo na kujibanza kwenye moja ya
kona pasipo kuonekana, aliitegesha kuelekea moja
ya tv kubwa, na mawasiliano yakaruka moja kwa
moja kwenye kituao anacho kifanyia kazi, na
kwakupitia video hiyo vituo vyote vya televishion
nchini Tanzania vikawa vinaonyesha tukio hilo
walilo liita la kigaidi, likiongozwa na waziri mstafu
bwana Eddy Godwin, jambo lililo wastua wananchi
wengi na kutambua maana ya waziri huyo
kujiudhuru ndio hiyo.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 31 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (31)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Vyombo vyote vya habari vikarusha tukio zima,
ikiwa ni habari ya dharura(breaking news). Kwa
kamera moja ya muandishi wa habari aliye kuwemo
ndani ya jengo hilo na kujibanza kwenye moja ya
kona pasipo kuonekana, aliitegesha kuelekea moja
ya tv kubwa, na mawasiliano yakaruka moja kwa
moja kwenye kituao anacho kifanyia kazi, na
kwakupitia video hiyo vituo vyote vya televishion
nchini Tanzania vikawa vinaonyesha tukio hilo
walilo liita la kigaidi, likiongozwa na waziri mstafu
bwana Eddy Godwin, jambo lililo wastua wananchi
wengi na kutambua maana ya waziri huyo
kujiudhuru ndio hiyo.
ENDELEA
Shamsa akasimama wima pasipo kuwa na woga
wowote
“Kaa chini wewe binti, kaa chini nitakupasua
ubongo wako huo”
Mmoja wa watekeaji alizungumza huku bunduki
yake akiwa ameielekezea kwa Shamsa, Dulla kwa
haraka akamshika mkono Shamsa na kumvutia
chini.
“Shamsa unataka kufanya nini, watakuua hawa
watu”
“Nahitaji kuzungumza na baba yangu Eddy”
“Wasikilize watu wenyewe hawana akili kabisa
hawa”
Dulla aliendelea kulalama kwa sauti ya chini, huku
akiendelea kumshikilia Shamsa asiweze
kunyanyuka kutoka katika sehemu aliyo lala.
“Funga mabakuli yenu wana haramu nyinyi”
Mtekaji huyo alizungumza kwa sauti ya kufoka na
kuwafanya Dulla na Shamsa kunyamaza kimya.
***
“Madam”
Priscar alizungunza huku alimgeukia mdama
Rahab aliye keti siti ya nyuma, akamkabidhi simu
ambyo kuna ujumbe wa video uliingia. Rahab
akaichukua simu hiyo na kutazama video hiyo.
“Ndugu wananchi, ninaimani kwa kufanya hivi
serikali na wananchi kwa ujumla mutakuwa
mumenielewa nini dhamira yangu, baada ya
kujiudhuru”
Rahab akajikuta akistuka baada ya kumuona ni
Eddy akizungumza kwenye video hiyo akiwa
amevalia mavazi meusi pamoja.
“Eddy………!!”
Rahabu hakuamini macho yake kwani sura na sauti
vya mtu anaye zungumza ni Eddy mwenyewe, ila
kitu ambacho kinazidi kumshangaza zaid, Eddy
amemuacha kwenye kwenye handaki mbalo kipindi
walipo kuwa wakifanya kazi za ujambazi walikuwa
wakijificha huko yeye na wezake.
“Serikali isipo hitaji kufwata matakwa yangu basi
watu wote waliomo ndani ya jengo hili wateteketea
kwa kupigwa risasi hadi kufa”
Ujumbe huo wa sauti ukaishia hapo, magari
kwenye foleni yakaanza kuruhusiawa huku Rahab
akiwa amepoteza amani ndani ya moyo wake.
Kwani hiyo ni moja ya skendo ambayo itakuwa ni
ngumu sana kuweza kujisafisha mbele ya
wananchi ya Watanzania.
Raisi Praygod akaitisha kikao cha dharura kwa
maofisa wote wa ngazi za juu katika jeshi. Hali ya
hatari inayo endelea katika jiji la Dar es Salaam
kuhusiana na kutekwa kwa jengo la kibiashara la
Mlimani City, ndio mada kuu ya kuweza
kuzungumziwa ni jinsi gani ya kuweza kuwaokoa
mateka wote wanao sadikika kutekwa na waziri wa
ulinzi, pasipo kujua kwamba mtu aliye panga
mpango huo ni miongoni mwa washauri wa raisi
walio panga kufanya kazi hiyo.
Vikosi vya vitengo vyote vya jeshi kuanzia polisi,
jeshi, zima moto pamoja na usala wa taifa,
waliweza kutumwa katika jengo la Mlimani City
kuhakikisha kwamba wanaweza kuwaokoa watu
wote walio weza kutekwa ndani ya jengo hilo,
Waandishi wa habari, karibia vituo vyote vya habari
nchini Tanzania wakaweka kambi katika jengo la
Mlimani City kuweza kurusha habari kwa mambo
ambayo yanaendelea katika eneo hilo. Sio
waandhishi pekee wa Tanzania, bali hata kutoka
mashirika makubwa kama BBC, Sky news pamoja
na CCN, waliweza kuweka kambi ili kuitaarifu dunia
juu ya kuwepo kwa tukio hilo la ugaidi ambalo
limejitokeza nchini Tanzania, huku tukio hilo
walikifananisha na tukio lililo tokea nchini chini
Kenya miaka kadhaa iliyo pita kwa kutekwa kwa
jengo la kibiashara, ambapo ni watu wengi
waliweza kutekwa na wengine waliweza kupoteza
maisha yao katika shambulio hilo.
Ulinzi mkali ukazidi kuimarishwa nje ya jengo la
Mlimani City, barabara inayo pita kuelekea Mwenge
pamoja na Ubungo zote ziliweza kufungwa,
hawakuruhusiwa watu kuweza kukatiza katika
maeneo hayo.
Simu ya mezani iliyopo ndani ya chumba cha
kuongozea kamera zate ndani ya jengo hilo,
ikaanza kuita Briton na watu wake wote
wakaitazama, kila mmoja akiwa katika hali ya
kujiuliza ni nani anaye ipiga simu hiyo kwani
hapakuwa na mtu aliye weza kufikiria kwa muda
huo kuna simu ambayo inaweza kupigwa katika
eneo hilo. Briton akajikaza na kuipokea simu hiyo,
ila hakuzungumza kitu chochote.
“NYOTE MUMEKUFAAAAA”
Sauti nzito inayo kwaruza kwaruza ilisikika upende
wa pili wa simu hiyo, jambo lililo muogopesha
Briton na kujikuta akiutoa mkonga huo wa simu
sikioni mwake na kuutazama kwa macho ya
mshangao.
***
“Eddy…………!!”
Manka alijikuta akishangaa huku akitazama taarifa
inayo rushwa kituo cha CNN, kuhusiana na
kutekwa kwa jengo la Mlimani City.
“Ndio maana nikakuambia Eddy ni mtu hatari hafai
kwenye hii jamii”
Mzee Godwin alizungumza huku akimtazama
Manka machoni mwake, muda wote John alikaa
kimya akiitazama taarifa hiyo kwani hakujua
kwamba huo ni mchezo. Kitu kinacho muumiza
kichwa zaidi ni jinsi gani ambavyo Eddy anaoeneka
kuwa ni mtu hatari sana kwenye mipamgo yake
kwani hadi kufikia hatua ya kuweza kuteka jengo
hilo kubwa la biashara nchini Tanzania, basi
amekamilika katika mipango yake, ila ukweli ni
kwamba mpango huo wote mzee Godwin
anaufahamu, ni njia moja ambayo inaweza
kumfanya adui yake huyo kukimbia kimbia ndani
ya nchi yake kama aliyo kuwa akiandamwa yeye
kipindi Eddy alipo kuwa madarakani.
Katika taarifa hiyo, inayo endelea kuruka, hewani
kukaonyeshwa kiongozi huyo ambaye amevalia
sura inayo endana na Eddy, akiwachukua wanaume
wawili alio wasimamisha mbele ya kamera pasipo
huruma akawatandika risasi za kichwa, jambo lililo
zidi kuwastua watu wote.
***
“Eddy kuna tatizo”
Samson alimuambia Eddy aliye kuwa amesimama
mbali kidogo na computer hizo mara baada ya
kupiga simu ya vitisho kwa watekaji hao, kwa
haraka akaelekea sehemu alipokuwa amekaa
Samson, akashahudia watu wawili wakiwa
wameuwa kwa kupigwa risasi kisha kiongozi wao
huyo akizungumza kitu.
“Atendelea kufa mmoja baada ya mwengine”
Ujumbe huo mfupi ukazidi kuwachanganya Eddy na
Samson ambao hawakujua wafanye nini kwa wakati
huo, Eddy akaingia kwenye chumba alicho kuwa
amelala, akachangua changua kwenye nguo zililzo
wekwa bila ya mpangilio juu ya meza, akabahatika
kuweka kulpata koti moja jeusi refu kuanzia chini
hadi juu, ambapo lina kofia kubwa, na mtu akilivaa
si rahisi kuweza kujulikana. Akalivaa, alipo ona
limemtosha vizuri akatoka nje ya chumba hicho na
kumuuliza Samson jinsi anavyo onekana.
“Unaonekana upo vizuri”
“Basi inatupasa kuweza kuifanya hii kazi ya
kuwaokoa mamia ya watu walio weza kutekwa
nyara ndani ya jengo hilo”
“Tutaifanya vipi hii kazi ikiwa, usalama
umeimarishwa kila kona”
“Tutajua ni jinsi gani ya kuweza kufanya ila kwa
sasa inatupasa kuweza kuondoka katika eneo hili,
hakuna muda mwengine wa kuweza kupoteza”
Wakatoka na Samson na kuingia kwenye gari,
safari ya kurudi jijini Dar es Salaam ikaanza, akilini
mwa Eddy, akawa anafikiria ni jinsi gani anaweza
kuifanya kazi hiyo ya kisiri pasipo mtu yoyote
kumtambua. Mwendo wa masaa manne
wakafanikiwa kufika katika jumba lake la kifahari,
ambapo hapakuwa na mlinzi wa aina yoyote anaye
linda hapo, macho ya askari yote yapo kwenye
jengo la Mlimani City. Wakaingia kwenye moja ya
chumba cha siri cha Eddy kilichopo chini ya ardhi
na chumba hicho mara nyingiu huwa anaficha
silaha zake za siri za kupambana endapo
kunakuwa na tatizo kubwa.
Samson akabaki akishangaa silaha nyingi za kivita
zilizomo ndani ya chumba hicho, akaanza kukagua
silaha moja baada ya nyingine, zote zinaonyesha
zina uwezo mkubwa pale zinapo tumiwa katika
mapambano ya kuzitoa roho za watu.
“Hizi silaha zote umezitolea wapi?”
“Kipindi nipo madarakani nilikuwa nikiwa
namtumia dokta mmoja wa kiisrael, ndio alikuwa
akinitafutia wataalamu ambao walizitengeneza hizi
silaha.”
“Walizitengeneza kisiri bila ya serikali kuweza
kufahamu?”
“Ndio pasipo serikali kuweza kufahamu kwani ni
ulinzi wangu binafsi”
Eddy akalivua koti ambalo amelivaa na kuchukua
moja ya bastola, yake na kutoa magazine akakuta
risasi za kutosha, kisha akairudishia, akafungu
moja ya kabati linalo funguliwa kwa namaba za
siri, akatoa visu vidogo vipatavyo ishirini vilivyomo
kwenye moja ya mkanda mrefu.
“Unaweza kutumia visu?”
“Ndio kama hivi”
Kwa haraka sana, Eddy alichomo moja na
kukirusha kwenye moja nguzo iliyomo ndani ya
chumba hicho, kuonyesh umahiri wake wa kuweza
kutumia visu hivyo.Eddy akavua nguo zake zote
na kuvalia nguo nyeusi tupu kisha akachukua moja
ya jaketi la kuzuia risasi na kulivaa, kisha
akamalizia na jaketi kubwa lenye kofia.
“Hivyo ndivyo unavyo vaa?”
“Ndio, nahitaji kuifanya hii kazi pasipo mtu
mwengine kunifahamu kwani ni hatari sana”
“Unaonaje ukasubiria kuifanya kazi hii usiku?”
“Ndio mpango ni lazima kuifanya kazi hii usiku”
“Tutaongozana, nipe tano”
Eddy akagonganisha ngumi yake na ngumi ya
Samson, kuashira kuungana kwao kuifanya kazi ya
kuwaokoa watu wali tekwa kwenye jengo la
Mlimani City
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 32 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (32)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Kwa haraka sana, Eddy alichomo moja na
kukirusha kwenye moja nguzo iliyomo ndani ya
chumba hicho, kuonyesh umahiri wake wa kuweza
kutumia visu hivyo.Eddy akavua nguo zake zote
na kuvalia nguo nyeusi tupu kisha akachukua moja
ya jaketi la kuzuia risasi na kulivaa, kisha
akamalizia na jaketi kubwa lenye kofia.
“Hivyo ndivyo unavyo vaa?”
“Ndio, nahitaji kuifanya hii kazi pasipo mtu
mwengine kunifahamu kwani ni hatari sana”
“Unaonaje ukasubiria kuifanya kazi hii usiku?”
“Ndio mpango ni lazima kuifanya kazi hii usiku”
“Tutaongozana, nipe tano”
Eddy akagonganisha ngumi yake na ngumi ya
Samson, kuashira kuungana kwao kuifanya kazi ya
kuwaokoa watu wali tekwa kwenye jengo la
Mlimani City
ENDELEA
Hadi majira ya usiku hapakuwa na jambo lolote
lililo weza kufanywa na askari katika kuwaokoa
mateka katika jengo la Mlimani City, watu wenye
ndugu zao wakakesha wakiomba Mungu ndugu
zao waweze kutoka humo ndani, vilio vya
wamama, vilizidi kutawala kila muda jinsi unavyo
zidi kwenda kwani hapakuwa na jibu lolote lililo
weza kutolewa na jeshi likawaridhisha.
Kitu kilicho zidi kuwaumiza zaidi vichwa serikali
kwa ujumla ni kundi kubwa la watoto wadogo na
wanawake waliomo ndani ya jengo hilo,
hawakuhitaji kuweza kuwaona wakiendelea
kuteseka, ikamlazimu raisi Praygod Makuya
kuwasiliana na watekaji hao, kuwauliza ni kitu gani
wanancho kihitaji zaidi ili kuweza kuwaachia
baadhi ya watu watakao wahitaji.
“Muheshimiwa raisi, hakuna ambalo unaweza
kulifanya juu ya hili, hatuhitaji pesa wala silaha.
Tunacho hitaji ni roho za binadamu wote waliomo
ndani ya jengo hili.
Simu ikakatwa, nusu raisi Praygod aangusha
machozi chini, hasira kali dhidi ya Eddy ikazidi
kumpanda kwani ndio mtu aliye weza kuipokea
simu yake na kuzungumza ujinga wa aina hiyo.
“Muheshimiwa raisi tuna fanyaje sasa?”
“Andaeni vikosi vyote kuweza kuvamia, hatuwezi
kuendelea kusubiria kuona wanawake, watoto na
vijana wakiendelea kuumia na kuteseka ndani ya
jengo hilo. Kama wangekuwa wanahitaji pesa nipo
tayari kutoa kiasi chochote cha pesa ila hawapo
tayari, wanataka roho inaniumaaa.”
Raisi Praygod alizungumza kwa uchungu huku
machozi yakimlenga lenga, ofisi nzima watu wote
wakabaki kimya, kwani wazo alilo litoa kiongozi
wao sio wazo baya ila ni wazo ambalo roho za
watu zitazidi kuteketea.
“Baby huwezi kufanya hivyo”
Sauti ikasikika ikitokea mlangoni, watu wote
wakageuza macho yao kutazama ni nani aliye
zungumza, wakamkuta ni mke wa raisi. Watu wote
wanamfahamu Rahab uwezo wake alio weza
kuuonyesha kipindi cha kuweza kumpindua
makamu wa raisi aliye jaribu kumpindua mume
wake kwa uroho wa madaraka. Rahaba akazidi
kutembea hadi mbele kwenye televishen kubwa
iliyomo ndani ya ofisi hiyo ya Ikulu, inayo onyesha
matukio moja kwa moja kwenye jengo hilo la
Mlimani City
“Mume wangu hapa si ishu ya kutumia nguvu, ni
ishu ya kutumia akili sana, kuahkikisha watekaji
wanaanguka mmoja baada ya mwengine.”
“Ukiseme nguvu itumike, tazama wamama, tazama
watoto, tazama mabinti wadogo tazama watu wote
kwa ujumla ndani ya jengo hilo, watakufa. Damu
hiyo itakayo mwagika utailipia wapi mume wangu,
fikiri kabla ya kutenda tafadhali.”
Rahab alizungumza kwa sauti ya upole na
unyenyekevu, iliyo anza kutengua taratibu
maamuzi ya Raisi Praygod ndani ya moyo wake.
Kamanda anaye ongoza vikosi vyote vya
oparesheni, ikamlazimu kusimamisha kwanaza
swala zima kushambulia, kuhofia watu wengi
kuendelea kufa kwa kupigwa risasi.
“Ni saa ngapi sasa hivi?”
Eddy alimuuliza Samson huku wakiwa
wamesimama juu kabisa kwenye moja ya gorofa
lililopo karibu na maeneo ya Mlimani City, huku
wakiwa wamevalia nguo nyeusi tupu, huku Eddy
sura yake akiwa ameifunika na kofia kubwa la koti
alilo livaa, ambapo sio rahisi sana kwa mtu kuweza
kumfahamu. Samson yeye amevalia kitambaa
cheusi usoni kilicho weza kuificha sura yake na
kumbakisha macho yake tu, kidogo amefanania na
watekeji hao.
“Ni saa saba na robo usiku”
“Tunatakiwa kutumia dakika kumi tuwe tumesha
maliza”
“Ndio muheshimiwa”
“Kuanzia sasa usiniite muheshimiwa?”
“Ila nikuite nani?”
“BLACK SHADOW”(KIVULI SHEUSI)
“Nimekupata Black Shadow”
Kwa kutumia mshale mrefu wenye kamba ngumu
sana. alio urusha Samson na kwenda kukita moja
ya kuta ya jengo la Mlimani City, waliweza
kuitumia kamba hiyo, kupitia huku wakiburuzika
kwa kutumia mikono yao hadi sehemu ya juu
kabisa ya jengo la Mlimani City pasipo mtu yoyote
kuweza kuwaona wala kustukila jambo lolote.
Wakaanza kutafuta sehemu ya kuweza kuingilia
kupitia juu katika jengo hilo, haikuwachukua muda
sana wakafanikiwa kuipata na kuzama ndani ya
jengi hilo kimya kimya pasipo mtu yoyote kuweza
kufahamu uwepo wao ndani ya jengo hilo.
Samson akatoa ramani ya jengo zima ambayo
aliweza kutumia wa Rahabu masaa machache
yaliyo pita, kupitia email, kisha wakaitoa nakala
yake na ndio hiyo wanayo itumia kwa wakati huo,
mpango wa kuvamia jengo hilo kisiri, anafahamu
Rahab peke yake na hakuhitaji kuweza kumueleza
mtu yoyote juu ya mpangui huo kwani, mtu
wanaye muhisi ndio mtekaji ndio mtu anaye
kwenda kuokoa mamia ya wananchi ya watu
waliomo ndani ya jengo hilo, kazi kubwa ya Rahab
ni kuhakikisha kwamba hakuna pua yoyote ya
askari inahusika kwenye mpango wa kwenda
kuwaokowa wananchi hao kwani tangu asubuhi
walikuwepo nje ya jengo jilo ila walishindwa
kuweza kufanya lolote dhidi ya magaidi hao.
“Hapa ndilo eneo walipo wananchi wengi, huku
ndipo kwenye ofisi za mawasiliano, sasa tuanze na
wapi?”
“Tugawane, nenda chumba cha mawasiliano mimi
acha niende kwenye eneo la wananchi, kumbuka
hakuna kutumia bunduki, nakukumbusha katika
hilo”
“Sawa Mr black Shadow”
Samson akaikunja ramani hiyo na kuiruidisha
mfukoni alipo itoa, na kila mtu akapita nji yake
anayo iweza kupita. Kwa kutumia visu vidogo
ambayo vinasumu kali, inayo ua ndani ya dakika
mbili na kumkausha mtu na kuwa kama mkaa,
Eddy akaanza kuvitumia kwa kukirusha kwa
mmoja wa watekaji walio weza kusimama akipiga
doria katia eneo ambalo ilikuwa ni bahata mbaya
kwake kupita kwani ndipo alipo kuwepo bwana
Black Shadow(Eddy Godwin)
Mauaji ya kimya kimya yakaendelea kufanyika
ndani jengo la Mlimani City, Eddy akitumia visu
vyake kuwaangusha watekaji nyara hao kisiri siri,
huku Samson akitumia nguvu zake kuweza
kuvunja shingo ya kila aliye weza kukutana naye
kwenye kumi na nane.
“Mama”
Mtoto mmoja wa kike mwenye umri yapata miaka
minne alimtingisha mama yeka, baada ya kumuona
mtu aliye valia mavazi meusi akimrushia kisu cha
shingo mmoja wa watekaji aliye anguka kimya
kimya pasipo mwenzake kutazama. Mama huyo
alipo tupia macho yake katika eneo alilo onyeshwa
na mwanaye, macho yake yakakutana na macho ya
mtu huyo ambaye hawakujua ni nani, ila alicho
kifanya mtu huyo ni kuweka kidole chake mdomoni
kuwaashiria kwamba wasizungumze chochote, kwa
haraka mama huyo akamzima mdomo mwanae,
asije akamwaga mchele kwenye kuku wengi na
mambo yakaharibika.
Mmoja wa watekaji katika kupita pita, akawakuta
wezake wakiwa wamekufa kifo cha kuogopesha
sana kwani miili yao iliweza kubadilika na kuwa
myeusi tii.
“Muheshimiwa tumevamiwa”
Mtekaji huyo alizungumza na Briton, aliyemo
kwenye chumba cha mawasiliano. Kwa haraka
akawaamuru mafundi mitambo walio waweka chini
ya ulinzi kutama kupitia kamera zote ni kitu gani
ambacho kinacho endelea ndani ya jengo hilo.
“Fu***”
Briton alijikuta akitukana huku akichanganyikiwa
kwani, watu wake wengi waliweza kuangushwa
chini, huku mtu aliye valia koti kubwa jeusi lenye
kofia ndio akiifanya kazi hiyo.
“Wote sasa jiandaeni kwa mashambulizi kuna hali
ya hatari narudia, tupo kwenye hali ya hatari”
Briton alizungumza kupitia simu ya upepo huku
akichukua bunduki yake, Lukuman na Briton
wakatoka ndani ya chumba hicho na kuwacha
vijana wawili pamoja na Brian, ili kuweza
kuendelea kumtazama muuaji huyo anapita
ameneo gani.
Kitendo cha Lukuman aliye jitengenezea sura kama
ya Eddy pamoja na Briton kutoka na kutokomea
karibu na eneo hilo lachumba cha mawasiliano
ndipo Samson alipo weza kufika. Akautazama
mlango huo ulio andikwa na maandishi madogo ya
rangi nyeusi
(Security control room)
Mmoja wa mafundi mitambo alipo gundua, kupitia
kamera iliyopo njee ya mlango wa chumba hicho
kama kuna mtu amesimama nje ya mlango kwa
haraka akaweza kubadilisha video hiyo na
kuihamishia kwenye kamera nyingine inayo
waonyesha Briton na Lukuma sehemu wanapo
pita.
“Wewe wewe hembu rudisha kwenye kamera uliyo
itoa”
Brian alizungumza huku akimnyooshea bastola
fundi mitambo huyo, aliye anza kutetemeka mwili
mwiza, kwani miili ya watu wawili walio
washuhudia wakipigwa risasi mbele yao, bado imo
ndani ya chumba hicho wakiwa wamelala sakafuni
na endapo atafanya kama kinyume na alicho weza
kuamrishwa basi kifo kitamuhusu. Kitendo cha
fundi mitambo huyo kurudisha picha inayo
onyeshwa na kamera iliyopo mlango, wote
wakastukia mlango wa chumba hicho unao fungwa
kwa kutumia umeme ukiangushwa chini wote kwa
kuvunjwa, taa zote zilizomo ndani ya chumba
hicho zikazimika gafla, jambo lililo wachanganya
Brian na vijana wake wawili walio baki ndani ya
chumba hichi wakimlinda yeye kama kiongozi
mkubwa, japo sio yeye anaye ongoza kundi hilo.
Brina na watu wake wakaanza kupiga risasi pasipo
na mpangilio wowote, mafundi mitambo wapatao
sita wote kila mmoja akajitafutia sehemu yake
ambayo anaweza kujificha, wengine wakaingia chini
ya meza, wengine wakilala chini, mmoja kwa
kiwewe alicho nacho akajikuta akijilazisha kujificha
kwenye kindoo kidogo cha kuwekea mataka taka.
Brian na watu wake wakajikuta risasi zikiwaishia
kwa kuweza kupiga piga ovyo pasipo kuweza
kumuona mtu mwenyewe wanaye mpiga.
Mngurumo mzito kama simba, ukasikika ukitokea
mlangoni, Brian na watu wake wakazidi kuogopa
“Muheshimiwa kuna nini kinacho endelea”
Sauti ya Lukuman kupitia simu ya upepeo ilisikika
kwenye redio moja ya upepo iliyo anguka chini,
hapakuwa na mtu aliye weza kuijibu zaidi kila
mmoja aliisikilizia sauti hiyo kama ya simba
ikiendelea kunguruma ndani ya chumba hicho, hadi
fundi mitambo aliye jificha kwenye ndoo ya taka
mkojo ukamtoka pasipo kujizuia.
***
Kwa kamera ya mwandishi wa habari aliyemo ndani
ya jengo aliweza kuchukua moja ya tukio la mtu
anaye toa msaada ndani ya jengo hilo na kuirusha
moja kwa moja hadi kwa kitu cha habari chake
anacho fanyia kazi, ambapo vituo karibia vyote
vilivyo kuwepo kwenye eneo la Mlimani City
waliweza kurusha tukio hilo, jinsi mtu huyo
mwenye ujuzi wa kurusha visu jinsi akiendelea
kuwaua watekaji hao mmoja baada ya mwengine.
Taarifa hiyo ikafufua matumaini kwa viongozi
walimo ndani ya ikulu ya Tanzania, raisi Praygod
akajikuta akilegeza tai yake shingoni, akishuhudia
mtu huyo akishusha chini watekaji hao.
“Huyu ni nani?”
Raisi aliuliza baada ya habari hiyo kuisha baada ya
kurushwa kwa muda wa kama dakika tano.
Hapakuwa na mtu aliye weza kutoa jibu la uhakika
kwani kila mmoja ndio kwanza anamuona mtu
huyo ambaye wanaamini ni mkumbozi wa watu
mamia waliomo ndani ya jengo hilo. Rahab
akajikuta akitabasamu usoni mwake, kwani
mwanaume anaye mkubali na kumpenda ndio
anaye fanya kazi hiyo iliyo washinda mamia ya
askari wanaume walipo nje ya jengo la Mlimani
City wakijidai wanaimarisha ulinzi usio na faida
Hasira kali ikampanda gafla mzee Gdowin baada ya
kuiona taarifa hiyo, akajikuta akichomoa bastola
yake na kupiga moja Tv, iliyomo kwenye ofisi yake,
na kuwafanya watu wote kustuka kwa tukio hilo.
“Shitiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii………………………….!!!”
Mzee Godwin alizungumza huku akiendelea
kutetemeka kwa hasira, kwani mpango wake
umesha ingia doa.
“Nahitaji muniletee kichwa cha huyo
mwanaharamu”
Mzee Godwin aliondoka ndani ya ofisi hiyo kwa
hasira na kuwaacha John wakiwa wanashangaa,
ikambidi Manka atoke na kumgwata baba yake
sehemu alipo elekea.
“Baba baba”
Manka alimuita Mzee Godwin anaye tembea
kwenye kordo hiyo kwa mwendo wa kasi sana
huku akiwa amefura kwa hasira
“Baba sasa hicho kichwa cha huyo mwanaaramu
tutakipataje?”
“Manka fanyeni kama nilivyo waambia sihitaji
maswali zaidi”
“Sawa baba hauhitaji maswali ila nahitaji kujua
yule mtu ni nani hadi ukasirike kiasi hicho?”
“Ni EDDYndio anaye waokoa hao watu”
Mzee Godwin akaondoka na kumuacha kwenye hali
ya maswali mengi kwani, Eddy ndio mtekaji wa
jengo hilo la bishara, sasa itakuwaje ni Eddy huyu
huyo ndio anaye waokoa watu aliyo wateka. Manka
akageuka akiwa amechoka kwa jibu alilo pewa na
baba yake, akamkuta John akiwa yupo mbali
kidogo pamoja na mpambe wake huku naye akiwa
amesikikia kila kitu kwamba muokoaji huyo ni Eddy
Godwin, wote wakabaki wakiwa wametazamana
pasipo kufahamu ni nini kinacho endelea.
***
Eddy akasimama katikati ya eneo walilo wananchi
wengi chini, akatazama kila mahali akajiridhisha
watu wapo salama, hata kabla hajazungumza kitu
cha aina yoyote mlio wa risasi iliyo pita karibu na
kifua chake ukamstua, ikawa ni kazi yake sasa
kuanza kupambana na watekaji wawili hao ambao
ni Briton na Lukuman. Eddy akajaribu kurusha visu
vyake vyote ila vikamuishia pasipo kuwapata
watekaji hao ambao nao wanajiweza sana kwenye
swala zima la kupambana. Roho ya Shamsa ikazidi
kumuuma kumuona baba yake Eddy akiwa ni
miongoni mwa watekaji hao walio waua watu
wasio na hatia.
Lukuma na Briton wakamuweka Eddy mtu kati
huku kila mmoja akiwa amechomoa panga lake
refu linalo waka kwa kung’ara, kwa bahati mbaya
risasi zote ambazo walizo kuwa wakimpiga Eddy
aliye kuwa akifanya kazi ya kujaribu kuziweza
kuzikwepa, ni moja tu iliyo weza kumpiga kwenye
paja la mguu wake wa kushoto, na kumfanya Eddy
asimama huku akichuchumia.
Kitendo hicho kikiwa kinaendelea Shamsa aliweza
kushuhudia damu ikimtoka mtu ambaye anaamini
amekuja kuwasaidia na kuwaokoa.Bila ya uwoga
na wala pasipo kuhofia maisha yake, Shamsa
akasimama wima na kuanza kupiga hatua za
kwenda walipo simama watu hao walio muweka
kati mtu aliye valia mavazi meusi tupu.
Eddy akabaki akiwa katika mshangao mkubwa,
baada ya kumuona Shamsa akikaribia katika eneo
hilo ambalo ni hatari kwa maisha yake. Eddy
akajaribu kutingisha kichwa chake kumzuia
Shamsa asiweze kusogelea eneo hilo, ila ndio
kwanza Shamsa akaongeza mwendo wa
kuwasogelea akiwa amejiandaa tayari kwa
kupigania watu wote waliomo ndani ya jengo hilo.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 33 YA SIMUHILI HII.
 
SORRY MADAM (33)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Kitendo hicho kikiwa kinaendelea Shamsa aliweza
kushuhudia damu ikimtoka mtu ambaye anaamini
amekuja kuwasaidia na kuwaokoa.Bila ya uwoga
na wala pasipo kuhofia maisha yake, Shamsa
akasimama wima na kuanza kupiga hatua za
kwenda walipo simama watu hao walio muweka
kati mtu aliye valia mavazi meusi tupu.
Eddy akabaki akiwa katika mshangao mkubwa,
baada ya kumuona Shamsa akikaribia katika eneo
hilo ambalo ni hatari kwa maisha yake. Eddy
akajaribu kutingisha kichwa chake kumzuia
Shamsa asiweze kusogelea eneo hilo, ila ndio
kwanza Shamsa akaongeza mwendo wa
kuwasogelea akiwa amejiandaa tayari kwa
kupigania watu wote waliomo ndani ya jengo hilo.
ENDELEA
“Am sorry dady”(Samahani baba)
Shamsa alizungumza huku akiruka hewani na
kushusha teke zito kwa Lukuman akitambua
kwamba ni baba yake. Eddy akataka kuzungumza
kitu ila akastukia akipigwa mtama na Briton, ulio
mpeleka chini, hakutaka kupoteza hata sekunde
moja kwa kofia lake kuweza kuanguka alicho
kifanya ni kuliweka sawa na kunyanyuka huku
akichechemea.
“Baba kwa nini umeamua kufanya hivi?”
Shamsa alizungumza huku machozi yakimwagika
usoni, Lukuman akabaki akiwa ameshangaa kwa
kuitwa baba, ili kupotezea akarusha ngumi nzito
kifuani mwa Shamsa, na kumfanya binti huyo kuto
ukelele wa maumivu huku akianguka chini na
kujikunja. Briton na Eddy wakajikuta wote
wakimtazama Shamsa anaye garagara chini kwa
maumivu makali. Kumbukumbu na sura ya
Shamsa vikaanza kumjia Briton, akaanza kufikiria
ni wapi alipo isikia sauti hiyo ya maumivu ya
msichana huyo mwenye asili ya kiasia.
Kumbukumbu zake zikatua kipindi ambacho,
walikuwa ni miongoni mwa mateka walio weza
kuingizwa katika kambi ya kundi la Al-Shababu,
akiwa ni kijana mdogo mwenye umri wa miaka
kumi na tano. Miongoni mwa mateka ambao
waliokuwa kipindi hicho, Shamsa ni mmoja wapo
kipindi hicho Shamsa alikuwa bado binti mdogo.
Anakumbuka siku moja wakiwa katika mazoezi ya
lazima, Shamsa alipewa kijana mwengine ambaye
walimkuta ndani ya kambi hiyo, apambane naye,
kutokana Shamsa hakuwa mzoefu na alikuwa ni
binti mdogo na mpole sana, kijana huyo pasipo
huruma aliweza kumbutua vya kutosha Shamsa, na
kitu ambacho anakikumbuka zaidi, ni pale kijana
huyo alipo mpiga Shamsa ngumi ya kifuani na
binti huyo akaanguka hivyo hivyo kama alivyo
anguka sasa hivi. Britona akakumbuka alipo jitoa
katikati ya vijana wezake walio zunguka duara hilo
wakiwatazama Shamsa na kijana mwengine jinsi
walivyo kuwa wakipigna. Akamvaa kijana huyo na
kumshindilia ngumi za hasira hadi kijana huyo
akapoteza maisha yake.
‘Naitwa Shamsa’
Sauti hiyo ilipita masikioni mwa Briton na
kukumbuka siku alipo muuliza jina bintyi huyo na
kutokea kumpenda, kupita maelezo. Briton
akastushwa na buti zito la Lukuman lililo tua
tumboni mwa Shamsa, dadi akanyanyuka kidogo
juu na kutua chini puu.
“Ahagraaaaaaaaaa”
Briton akamuacha Eddy na kwenda kumvaa
Lukuman, na kumuangusha chini kama mzoga,
hadi Eddy akabaki akishangaa. Briton akaanza
kumshindilia mangumi ya uso Lukuman, kila alivyo
zidi kumshindilia mangumi mazito hayo ndivyo
alivyo kuwa akikumbuka tukio la Lukuman kumpiga
msichana ambaye alizama ndani ya moyo wake na
kuahidi atamtunza ndani ya moyo wake hadi siku
ambayo atakuja kumuona. Eddy kwa haraka
akapiga goti moja chini na kumnyanyua Shamsa
aliye poteza fahamu.
“WOTE TOKENI NJEEEEEE”
Ikawa kama fungulia mbwa, kila mmoja aliye jiweza
alijitahdi kutoka nje akikimbia, hapakuwa na mtu
aliye hitaji kujihusisha na ugovi wa watekaji hao
wawili, kila mtu alijitahidi kuizingatia roho yake
kwanza mambo mengine yatafwata baadaye. Eddy
akamuweka Shamsa kwenye moja ya meza, baada
ya kugundua yupo hai, kisha yeye akandoka
akihofia askari walio anza kuingia ndani ya jengo
hilo kuweza kumkuta na kumtambua.
Ndani ya dakika moja Brina na watui wake wote
wawili, walijikuta wakiwa wamelala chini, kila
mmoja akishika eneo la mwili wake lililo tole
pande la nyama, kwa kucha kali ambazo Samson
alizitumia katika kuwadhuru waasi hao. Mmoja wao
koromeo lake liliweza kutolewa nje, na yupo katika
hatua za mwisho mwisho za kuiaga dunia huku
mikono yake miwili ikiwa imeshika sehemu
koromeo lake lilipo chomolewa, ili damu isitoke.
Mwengine alitobolewa tumboni na utombo wake
wote ukavutwa nje pasipo huruma. Brian miguu
yake yote miwili, ilivunjwa vunjwa vipingili pingili
zaidi ya kumi kwa kila mguu, na kuacha akiendelea
kulia kwa maumivu makali. Samson alipo
hakikisha kazi yake imekamilika akatoka ndani ya
chumba hicho na kuwaachia woga mwingi mafundi
mitambo, kila mmoja akiwa haamini kama
amepota, na hapakuwa na aliye weza kutoka katika
sehemu aliyo jificha hadi walipo sikia sauti za
polisi,walio jitambulisha mara baada ya kuingia
ndani ya chumba hicho.
“Upo salama?”
Samson alimuuliza Eddy mara baada ya kumkuta
akiwa amesimama juu ya paa akiwatazama jinsi
wananchi wanavyo pokelewa na ndugu zao walio
weka kambi katika eneo hilo kuhakikisha kwamba
wanawaona ndugu zao. Japo si desturi ya watu
wengi kukumbatiana ila kila aliye muona ndugu
yake alijikuta akimkumbatia kwa furaha, wengine
wakiendelea kuita majina ya ndugu zao wakizidi
kuwatafuta katikati ya mamia ya watu walio weza
kutoka ndani ya jengo hilo. Wachache kati ya
waliopo nje ya jengo, walijikuta wakiingiwa na
wasiwasi mwingi na wengine wakiangua vilio
baada ya kupata taarifa au kuona miili ya ndugu
zao walio fariki.
“Ndio japo si sana”
Eddy alizungumza kwa ufupi huku akiendelea
kutazama huku na huku, akabahatika kuweza
kumuona Shamsa akiwa amebebwa kwenye
machela na kuingizwa ndani ya gari ya wagonjwa,
hapo roho yake ikaweza kutulia
“Tuondoke zetu muheshimiwa”
“Usiniite muheshiwa niite……..”
“BLACK SHADOW”
***
“I.T.V:WANANCHI WALIO TEKWA WAMEACHIWA
USIKU HUU”
“T.B,C:MAMIA YA WANANCHI WALIO TEKWA NDANI
YA JENGO LA BIASHARA MLIMANI CITY WAACHIWA
HURU”
“Star Tv:GAIDI MMOJA AKAMATWA, NA ALIYE
KUWA WAZIRI WA ULINZINA NDIO MTEKAJI MKUU
AMEKUTWA AMEKUFA”
Kila muandishi wa kitua cha habari aliye kuwepo
katika eneo la tukio la Mlimani City aliweza
kuzungumza taarifa hiyo kwa jinsi ya habari aliyo
weza kuipata kwa wakati huyo. Watu wote walio
kuwemo ndani ya ofisi ya maalumu ya matukio ya
raisi Praygod Makuya wakajikuta wakipiga makofi
wakifurahia tukio hilo, kila mmoja alikumkumbatia
raisi kwa furaha, wakimpongeza kwa kazi nzuri,
Rahab naye wakampongeza kwa kuwa pamoja nao
katika kazi nzito ya kushinda kwenye mativ
makubwa yaliyomo ndani ya ofisi hiyo wakilifwatilia
tukio zima.
“Ila hili ni fundisho inaonyesha ni jinsi gani serikali
yetu haijajipanga katika kuimarisha ulinzi. Hivyo
basi kuanzia leo maeneo yote ya mipaka
nitahakikisha ninaongeza vikosi vya ulinzi na
usalama, ili kuhakikisha hawa maharamia
hawawezi kuingia tena ndani ya nchi yetu”
Raisi Praygod alizungumza kwa sauti ya juu, watu
wote wakampiga makofi kwa wazo hilo alilo weza
kulitoa.
‘KUSEMA KWELI MIMI NIMSHUKURU YULE MTU
ALIYE VALIA NGUO NYEUSI, KWELI ALIAMUA
KUJITOA YAANI HUWEZI AMINI MWANANGU
ALIMUONA AKI…………”
Dada huyo anaye hojiwa na mundishi alijikuta
akimwaga machozi huku akiwa ameshikilia mkono
mwanye wa kike, akajipungusa machozi kidogo
kisha akendelea kuzungumza,
‘YAANI KUSEMA KWELI YULE KAKA NI JASIRI
SANA, NITAMSHUKURU TENA SANA’
Muandishi wa habari akamuhoji mtu mwengine
aliye vua shati lake na kulishika mkononi,
akionekana kuwa katika hali ya furaha.
‘AISEE CHALAA WANGU MIMI HUKU DAR SIRUDI
TENE, YAANI NIMEKUJA FANYA SHOPING HATA
UKINIULIZA SASA HVI SIKUMBUKI NI KIPI KILICHO
NILETA HAPA, TENA YULE MAN WANGU
ALIYEKUWA ANARUSHA RUSHA MATEKE YANII
YULE MAN NIME MMAINDI KICHIZI, YAANI CHALAA
ANARUSHA VISU HUYO, JAPO NILIKUWA NIMELALA
CHINI, ILA NIKAWA NACHABO MARA KWA MARA
KUONA JINSI JAMAA ANAVYO WAANGUSHA WALE
NGEDERE YANII CHALAA WANGU NAKUKUBALI
SANA’
Kijana huyo mwenye lafudhi ya kichaga
alizungumza bila hata ya kupumzika kwa furaha
aliyo kuwa nayo hadi ikamlazimu muandishi wa
habari kumkatisha na kumuhoji mtu mwengine.
***
Eddy na Samson wakafika nyumbani, moja kwa
moja wakelekea kwenye chumba cha siri cha Eddy,
ikawa ni kazi ya Samson kuhamisha vitu baadhi
vilivyomo ndani ya chumba hicho na kuviingiza
ndani ya gari. Mamumivu makali yakazidi kuutesa
mguu wa Eddy, jasho jingi likanza kumwagika
mwilini mwake, kwani hakuweza kumumbia
Samson kama ana jeraha kwenye mguu wake, kwa
kiasi cha damu kilicho weza kumtoka akajikuta
akilegea na kupoteza fahamu.
“Eddy Eddy”
Samson aliita huku akimtingisha Eddy aliye jilaza
kwenye kochi mara baada ya kuingia ndani ya
chumba hicho, akitoka kupoleka baadhi ya vitu.
Katika kumtazama vizuri suruali yeka mguu mmoja
umelowana na damu nyingi, katika kumkagua
kagua akakuta shimo lililo ingia risasi.
“Shitttttt”
Samson akanyanyuka kwa haraka na kukimbilia
kwenye kabati lenye sawa pamoja na vifaha vya
kutibia majeraha kwa haraka akaanza
kumuhudumia kujaribu kuitoa risasi iliyomo ndani
ya paja kabla hata sumu yake kusambaa kila eneo
la mwili. Ndani ya muda mchache akafanikiwa
kuitoa risasi hivyo na kulifunga jeraha hilo.
“Damu”
Samson akataka kutoa damu yake ili amuongezee
Eddy, ila akasita akachukua simu yake na kumpigia
Rahab ila simu yake haikuwa hewani, ikabidi atume
ujumbe wa maandishi mafupi(massage). Akataka
kumbeba Eddy na kumpeleka ndani ya gari, ila
akasikia vishindi vya kama watu wakikimbia nje ya
nyumba, kwa haraka akaufunga mlango, akachukua
moja ya kiti cha chuma kilichopo ndani ya chumba
hicho, akakisogeza karibu na ukutani kisha
akapanda juu yake kuchungulia kwenye kijidirisha
kidogo kilichopo upande wa juu kabisa wa dirisha
hilo. Kundi kubwa la wanajeshi wenye silaha wapo
nje ya nyumba ya Eddy wakijiandaa kuvamia ndani
ya nyumba hiyo.
***
Raisi Praygod baada ya kutoka ofisini kwake majira
ya saa kumi na moja alifajiri moja kwa moja
akaelekea ndani kwake, akiwa ameongozana na
mke wake. Kitendo cha kuingia ndani, wakanza
kunyonyana midomo yao taratibu, hisia za
kimapenzi zikapenda katikati yao, kila mmoja
akaoeneka kuwa na hamu kali na mwenzake,
Rahab akanza kumvua nguo mume wake, alipo
bakiwa mtu, naye akachojoa za kwake na wote
wakaangukia kitandani. Furaha ya raisi Praygod ni
kusikia mwizi wa penzi lake amefariki na yupo
katika chumba cha kuhifadhia maiti Muhimbili,
huku akipanga kukipambazuka vizuri aende
kumuona mwizi wake huyo aliye fariki na aibu
kubwa kama gaidi.
Furaha ya Rahab,, ni jinsi ambavyo Eddy aliweza
kuahakikisha ameifanya kazi hiyo pasipo kuweza
kujulikana. Kwa furaha zao kwa ujumla wakajikuta
wakipiga mechi kana kwamba hawajachoka kabisa,
Hadi mechi inafikia mwisho, Rahab akashuka
kitandani huku akiwa anapepesuka kwa kuchoka,
moja kwa moja akelekea bafuni kujimwagia maji.
Raisi Praygod akiwa amejilaza chali huku akihema
kama mtu aliye fukuzwa, akajikuta akishangilia
kimya kimya kwa Eddy kuweza kufariki. Akashuka
kitandani na kujinyoosha, kabla hata hajapiga
hatua mbele simu ya mke wake iliyo anguka chini
ikaingia ujumbe wa maandishi, akaiokota taratibu
na kuirushia kitandani, akapiga hatua mbili
kuelekea bafuni, ila roho yake ikasita, akarudi hadi
kitandani na kuichukua simu ya Rahab. Pasipo
kujishauri mara mbili akaufungua ujumbe ambao
jina limejitokeza kwa ufupi ‘SAM’. Akatingisha
kichwa mara mbili kuyaweka macho yake sawa,
kurudia kuusoma ujumbe huo wa meseji.
{MADAM EDDY, AMEPIGWA RISASI YA MGUU NA
ANAHITAJI DAMU NIMUWEKEE YAKWANGU?}
“EDDYYYYYY………………………???”
Raisi Praygod akabaki akiwa amejiuliza, kugeuza
shingo yake nyuma akamkuta Rahab akiwa
amesima nje ya mlango wa bafuni akijifuta maji
kwa taulo.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 34 YA SIMUHILI HII.
 
Back
Top Bottom