Sorry madam (Destination of my enemies)

SORRY MADAM (39)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
“Moja, hakikisha kwamba unaurudisha uhai wa
Eddy Godwin”
“Mbili ndani ya masaa 48, Eddy awe amerudi
madarakani la sivyo bomu hili litaisambaratisha
ikulu yako”
Simu hiyo ikakata, huku video iliyo kuwa
inaonekana kwenye tv hiyo ikapotea na kubakisha
mwanga wa bluu wa tv hiyo kubwa, watu wote
waliomo ndani ya ofisi
hiyo wakabaki wakimtazama raisi Praygod
azungumze kitu juu ya hilo.
ENDELEA
Jasho jingi likazidi kumwagika raisi Praygod,
hakuwa na jambo la kuweza kuzungunza na wala
hakuweza kutambua ni wapi alipo Eddy.
"Muheshimiwa Eddy si amesha kufa sasa
itakuwaje?"
Mmoja wa wafanyakazi wake walinuuliza
"Yupo hai"
Kila mmoja akabaki akiduwaa, baada ya kulisikia
hilo swala, raisi alipo ligundua hilo akakohoa
kidogo.
"Endeleeni na kazi"
Akatoka ndani ya ofisi yake na kuelekea katika
eneo lake la kulala, kichwani mwake akazidi
kujiuliza ni nani aliye weza kuufanya mchezo huo
kwani wataalamu wake walipo jaribu kutafuta ni
eneo gani simu hiyo ya vitisho ni wapi ilipo tokea
hawakuweza kuipata. Kitu kilicho zidi kumuumiza
zaidi ni wapi alipo kuwepo mke wake kipenzi
Shamsa, kwani inasadikika tangu atoke jana majira
ya asubuhi kutokana na taarifa aliyo pewa,
hakuweza kurejea kabisa hadi majira haya ya
asubuhi.
Akafungua moja ya droo yake na kutoa vidonge
viwili na kuvimeza pasipo hata kunywa maji,
akavisukumiza kwa mafumba kazaa ya mate kisha
akasimama mbele ya kioo kikubwa kilichopo
mbele ya chumba chake na kujitazama uso wake
ulio jaa wasiwask, iliyo changanyikana na hasira
kali sana.
"EDDY, EDDY, EDDY"
Raisi Praygod alizungumza huku jazba ikizidi
kuongezeka kifuani mwake. Taratibu akakisogelea
kitanda na kujilaza, huku akihema taratibu taratibu.
***
Mwanga mkali wa jua ukaanza kupenya kwenye
macho ya mtubaliye lala kitandani huku mwilini
mwake akiwa amebakiwa na boksa tu. Akajaribu
kunyanyuka kitandani ila maumivu makali ya paja
yakamfanya kurudi tena kitandani. Kwa sekunde
kadhaa akatumia kuchunguza kufahanu ni wapi
alipo, ila ikawa ni swali gumu sana Kwakwe
kuweza kufahamu alipo, kwani chumba hicho
kimetawaliwa na mitambo mingi ya kushangza.
Kitanda alicho lalia pembeni yake kuna bomba lililo
ning'inizwa dripu ya maji iliyo peleka mrija wake
moja kwa moja hadi kwenye mkono wake wa kulia
na kisindano kidogo kilicho weza kuunganishwa na
mrja huo, kimeingia moja kwa moja kwenye
mshipa wake wa damu.
"Hapa ni wapi?"
Alizungunza huku akijaribu kujikaza kunyanyuka,
mguh wake ulio fungwa bandeji zilizo badikika
rangi kutokana na dawa akiyo pakwa, ukazidi
kumuuma. Akiwa katika kutazama tazama mlango
wa chumba hicho kikubwa kinacho onekana
kwamba kipo juu ya gorofa kubwa, ukafunguliwa.
Akaingia mwanaume aliye valia koti jeupe pamoja
na miwani kubwa kiasi. Katika kumtazama kwa
haraka haraka ni lazima utagundua kwamba mtu
huyo ni daktari.
"Karibu tena duniani Mr Eddy Godwin"
Mtu huyo mwenye asili ya kizungu izungumza
kiswahili sahihi kilicho mshangaza hata Eddy
mwenyewe.
"Wewe ni nani?"
Lilikuwa ni swali la kwanza la Eddy huku akimkazia
macho daktari huyo aliye zidi kupiga hatua
kumfwata katika kitanda alicho lala.
"Kuna hofu ya kuhofia, mimi ni rafiki yako wa
karibu. Naitwa dokta William"
Alizungumza huku akigeuza geuza dripu linalo
endelea kushusha maji kwenye miishipa ya Eddy.
"Unajisikiaje?"
"Nina maumivu kwenye mguu. Kwanza hapa ni
wapi?"
"Hapa upo Mosscow Russia"
"Nilifikaje hapa?"
Eddy aliiza huku akizidi kumkazia macho daktari
huyo kwani jibu lake tayari lilianza kumpa wasiwasi
mkubwa.
"Nilikutoa Tanzania siju chache za nyuma. Niweza
kukufwatilia wewe kwa ukaribu mkubwa hadi
nikafanikiwa kukupata"
"Ulinijuaje mimi?"
"Nilikujua kupitia mama yako, alikuwa ni rafiki
yangu wa karibu sana. Kiufupi mama yako alikuwa
ni mwema sana kipindi nilipo kuwa nikiifanya kazi
ya kuwafundisha madktari wa jeshi nchini
Tanzania.
"Usiwe na shaka kwani Tanzania ni moja ya nchi
niliyo ipenda sana na ni nchi ambayo viongozi
wake baadhi ni wakatili sana wakiongozwa na raisi
Praygod"
Eddy akastuka kusikia jina jilo, katika
kumchunguza chunguza dokta William kwa haraka
haraka akatambua kwamba ni mtu ambaye hakuwa
na nia mbaya sana kwake japo hakuhitaji kuliamini
hilo kwa asilimia mia moja.
"Nil stori ndefu sana mimi na Tanzania pamoja na
viongozi wake na sasa nipo katika mpango wa
kuhakikisha kwamba nina lipa kisasi kwa nchi
hiyo."
"Kwa nini unahitaji kulipa kisasi?"
Dokta William akaivua miwani yake taratibu, kwa
mbali machozi yakawa yanamlenga lenga,
hakuhitaji kuzungumza kitu cha aina yoyote.
Akaondoka na kusimama kwenye moja ya mashine
inayo ongozwa na kompyuta aina ya Laptop.
Akaanza kuiminya minya batani zake kwa mwendo
wa kasi akionekana kuseti baadhi ya vitu katika
mtambo huo. Kila alivyo zidi kuminya batani za
kumpyuta hiyo asira dhidi ya Tanzania hususani
raisi Praygod zikazidi kumpanda mara dufu.
***
Kwa mwendo wa boti waliyo kuwa nayo,
haikuwasaidia sana kuweza kupasua mawimba
makubwa ambayo yanaendelea kuikumba bahari ya
hindi mara mwa mara. Upepe mkali na wenye
nguvu wa kuyumbisha hata meli kubwa ulizidi
kuirusha boti hiyo waliyo panda Shamsa na Briton
kutoka upande mmoja kwenda mwengine.
Halo hiyo kikaifanya boti hiyo kuzima gafla, hofu
ya kufa ndani ya maji ikaanza kumtawala Shamsa
ambaye kwa Mara kadhaa alionekana kumkumbatia
Briton huku akilia sana. Alihisi hakuwa na bahati
ya kuishi jwani familia yake aliyo kuwa akiitegemea
tayari ilisha fariki kuanzia Eddy hadi mtoto wake
Junio.
"Bray tunakufa mpenzi wangu"
"No hatuwezi kufa, tusonge Mbele"
Briton alizungumza huku akiendelea kujitahidi
kuhakikisha kwamba boti huyo inasonga Mbele.
Bahari ikazidi kuchafuka, hats akari ambao
walikuwa doria katika maji waka waliamriwa
kughairisha msako huyo kwank hali ilitisha sana.
Mvua taratibu ikaanza kunyesha jambo lililio zidi
kuwachanganya Briton na Shamsa. Radi zikaanza
kutawala kila kona. Gafla boti yao ikabenuliwa na
kuzamishwa ndani ya maji, kila mmoja akaangukia
upande wake. Hali ikazidi kuwa mbaya kwani radio,
mawimbi Na upepeo vikazidi kuongezeka kadri ya
muda ulivyo zidi kwenda ndivyo ikawa afadhali ya
dakika moja nyuma.
Kila mmoja alijikuta akiwa katika upande wake,
baridi kali ikazidi kuunynyasa mwili wa Shamsa,
maumivu makali ya tumbo yakarejea gafla mwilini
mwa Shamsa na kumfanya aanze kuishi wa nguvu,
dakika kadhaa mbeleni akapoteza fahamu.
***
Hali ya usalama ikazidi kuimarishwa maeneo mbali
mbaali ndanj na nje ya jiji la Dar es Salaam.
Wanaanchi kupitia katika vyombo vya habari.
Video, redio na magazetini raisi Praygod
akatangaza hali ya usalama katika maeneo yote
yanchi, akiendelea kuwahakikishia kwamba hakuto
kuwa na jambo lolote bays litakalo weza
kujitokeza. Wanaanchi pamoja na wafanya biashara
wakarudi katika maeneo yao ya kazi.
Kitu kilicho zidi kimchanganya raisi Praygod ni
wapi alipo mke wake kipenzi Rahab. Msako wa
kuhakikisha kwamba mke wa raisi anapatikana
ukazidi kuendelea. Kwa siku ya pili mfululizo
hapakuwa na askari akiye weza kulaza kichwa
chake kwenye kitanda chake kama ilivyo siku za
nyuma. Kuanzia wakuu wa majeshi hadi waliopo
ngazi za chini, kazi ikawa ni kuhakikisha kwamva
mke wa raisi anapatikana. Hapakuwa na mtu
mwenye wazo la kujua kwamba mke wa raisi yupo
kwenye pango ambalo lilitumiwa Na waasi
wanawake ambao kwa sasa baadhi yao wapo
katika mikono ya wamarekani.
"Madam tutaendelea kukaa humu hadi lini?"
"Hadi siku ambayo nitaamua mimi kutoka ndani ya
handaki hili"
"Ika utakuwa unampa wasiwasi muheshimiwa
raisi"."Nalitambua hilo ila sinto hitaji kurudi ikulu
hadi nihakikishe ninampata Eddy, iwe kwa kuua au
kufanya lolote ni kuhakikisha kwamba tunampata
Eddy"
Priscar hakuwa na kitu chochote cha kuzungumza
zaidi ya kuyasikiliza matakwa ya bosi wake.
"Ila kuna kitu kimoja nahitaji tuweze kukifanya kwa
pamoja"
"Kitu gani madam"
"Nilazima kuhakikisha kwamba tunapata pesa tena
pesa ya kutosha"
"Kama ni pesa mbona mume wako anazo za
kutosha?"
"Ndio anazo ila nitahitahi za kwangu, BOT ipo
kwenye mpango wangu wa kuchukua pesa zote
zilizomo ndani ya benki hiyo"
Rahab izungunza huku akiishika bastola yake,
akiigeuza upande mmoja hadi mwingine, heshima
ya kuwa mke wa riasi akaiweka kando na kuamua
kurudi katika kazi yake aliyo kuwa akiifanya miaka
kadhaa ya nyuma.
***
Mpango wa kuwahamisha wafungwa watatu, ambao
wanachuliwa kama magaidi katika nchi ya
Marekani. Ikawadia, vikosi vyabulinzi vilivyo
kabidhiwa kazibya kuwatoa wafungwa hao ambao
ni Fetty, Halima na Anna. Ulinzi mkali
ukaimarishwa kuanzia kwenye helcoptar zao
wakihakikisha kwamba hakuna jambo lolote ambalo
litaweza kujitokeza. Helcoptar zipatazo sita zilizo
jaa askari wa kikosi cha FBI, zikazidi kukizunguka
eneo la kikosi, huku ndege moja kubwa inayo
tumika kubeba wafungwa kuwatoa katika gereza
hilo, ikawekwa tayari.
Ulinzi ndani ya gereza ukazidi kuimarika. Fetty,
Halima na Anna wakawekwa tayari kwa kutolewa
katika vyumba vyao maalumu walivyo kuwa
wamefungiwa kwa kipindi chote hicho. Walifungwa
pingu mikononi na kufungwa cheni ngumu kwenye
miguu yao. Kila sehemu walipo pita wafungwa
wezao waliweza kuwashangilia kwa jinsi wanavyo
tolewa kwenye gereza hilo. Japo miili yao
imedhohofika sana ika tayari walisha jijengea
umaarufu mkubwa ndani ya gereza hilo. Hii
nikutokana na msaada ambao mara kadhaa
waliweza kuwapatia wafungwa wezao ambao mara
kadhaa walikuwa wakionewa vikali wa wasichana
wengine wababe ndani ya jengo hilo. Kabla
hawajafikishwa nje kulipo na uwanja mkubwa sana
wa ndege. Wakavalishwa vigunia vyeusi
wakatolewa nje ya gereza wakiwa katika ulinzi
mkali, wakizungukwa na askari walio jazatiti kila
idara, ili kuhakikisha tu kwamba magaidi hao
ambao ni tishio hawawezi kufanya kitu chochote
cha ajabu.
Wakiwa njiani wakielekea kwenyebuwanja wa ndege
katika eno hilo, gafla moja ya helcoptar ikalipuliwa
hewani na kuwafanya askari na watu wote kustuka
ni kitu gani kilicho tokea huku askari wapatao kumi
na mbili, walio kuwa wakiwasindikiza Fetty, Halima
na Anna, wakawazingira na kuwalaza chini huku
mitutu yao ya bunduki wakielekezea juu na pande
zote kutazama maadui wapo eneo gani.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 40YA SIMUHILI HII. ENDELEA
Hadithi tamu sanaa
 
Hizi tabia za kumaliza stori na kutelekeza uzi inaonyesha tabia za wanaume kwa wapenzi. Wanawafuatilia kwa kasiiiiii akisha funua tu nakumaliza kula basi anamtelekeza asee
 
Back
Top Bottom