Maandamano ya CHADEMA Jiji la Mbeya-Picha na Matukio

Serikali ya CCCM imekuwa ikiwapatia CDM mamilioni ya shilingi kama ruzuku ya chama hicho kujijenga kidemokrasia na kuleta chachu ya maendeleo nchini lakini CDM wamekuwa wakitumia fedha hizo za walipa kodi kwa kutalii mikoa kadhaa huku wakipoteza nguvu ya rasilimali watu, nchi hii inahitaji wachapakazi na wenye kuleta chachu ya maendeleo na si watalii.

Matumizi mabaya ya ruzuku ni kuanzisha shirika lake la ujasusi na si maandamano
 
pesa ya ruzuku inayolipwa kwa vyama vya siasa kazi yake ni kusaidia shughuli za siasa ktk hivyo vyama. Vyama vya siasa vina shughuli mbalimbali kutegemeana na sera itikadi mrengo mission na vision za vyama na kila chama kinatakiwa kutumia hiyo ruzuku kwa shughuli zake za chama na sio vinginevyo. Kwa upande wa CDM maandamano na mikutano ya hadhara ni mojawapo ya shughuli zake za siasa yakiwa na lengo la kuweka awareness kwa watz pamoja na kutafuta wapenzi na wanchama wapya na hapo ndo matumizi ya ruzuku yanapoingia unaposema ni matumizi mabaya ya kodi hizo ni cheap propaganda, kwan CCM wanatumia ruzuku kufanyaje? Ka sio kulipa mishahara ya makatibu ambayo hatujui ni shs ngapi na kulipana posho za vikao ila sisi hatusemi. Halafu kama una uchungu sana na kodi za watz ungeaza na matumizi mabovu ya serikali ktk chai na viwarsha, ununuzi wa mashangingi, mishahara ya wabunge na tbc kutumika ka chombo cha itikadi cha chama.
Tatizo lenu hamtaki kuona watz wakijua haki zao wakitaka kuelimishwa kidogo kuhusu upuuzi unaofanywa na serikali tayari mshaanza kubwabwaja ooh mara eeh matumizi mabaya eeeh uvunjifu wa amani na ujinga kibao, huku nyie mkiendelea kutumbua kodi zetu kwa starehe zenu huku watz wa kawaida wakisafa acheni hizo njooni na hoja
 
Mtachoka tu kuandamana li-nchi likubwa sana hili. Kodi zetu ndio zinateketea hivo. Tofauti kati yenu na CCM kwa matumizi ya fedha za UMMA haipo. Watoto wetu waendelee kusoma chini ya miti na kukalia mawe. Tuendelee kuigharamia SIASA mpaka basi.
mimi nafikiri ujui unachoonge.maandamano yamesaidia kwa kwa kiasi kikubwa na cha umuhimu watu wapate elimu na watambue haki zao ili itapofikia wakati wa uchaguzi wafanye maamuzi boro.
 
Hivi hawa Chadema sisi Watanzania tunawashangaa sana kila kukicha maandamano, saizi watu wapo makazini, viwandani, mashambani, wao wapo barabarani wanafanya usumbufu kwa Watanzania, wanatumia vibaya pesa zetu walipa kodi 'ruzuku' wanagawana posho kila baada ya maandamano. viongozi wa juu Dk Slaa na wenzake kila mmoja poso yake milioni mbili, hawa wengine kina Lema na wenzake milioni moja, huyo dada mbunge wa kupewa wa maandamo Regia Mtema yeye na wenzake laki tano, huyu dada yeye kila kukicha kiguu na njia kwenye maanamano, hili swala Zitto akubaliani nalo ndio maana umuoni kwenye maandamano yao, Chadema wamefanikiwa lakini kwenye maandamano kimekuwa chama cha kwanza dunia kufanya maandamano mengi wastani kila mwezi wanaitisha maandamano. wamo kwenye Guinness book Record in the World, chama cha maandamano

EEEEEEEEEEEh, kweli chama cha MAFISADI. Kimewadanganya watanzania tangu uhuru; na kuwa wafanya kuwa wagumu wa kuelewa kama wewe. Think??? wewe utapata pinats kwa kuwasaliti watanzania.
 
CDM walivyoanza maandamano walisema ni kwa ajili ya kupinga ulipwaji wa DOWANS, je na Nyanda za juu kusini ni nini, DOWANS pia, tunataka ruzuku itumiwe katika kuleta chachu ya maendeleo na si kununua magwanda na kutalii mikoani.
 
Kwa wanafunzi mmekwisha wawini. Matawi mnafungua sana kisha mnayatelekeza. Ruzuku yote kwenye maandamano na uendeshaji makaomakuu!
Tusimpuuze WildCard,
Yuko na agenda ya muhimu, CHADEMA wanatakiwa wasambaze hii Ruzuku mpaka kwenye ofisi zao za vijijini sio pesa kutumika makao makuu tu.
 
Wakuu,

Hivi sasa ndio tunajipanga ili kuanza Maandamano yetu. Mji umejaa hamasa kubwa kila ukipita bendera za CHADEMA na ishara ya vidole viwili ndio vimetawala.

Watu wamependeza sana na Kombati na Sare nyingine za Chama. Tunatarajia kuanza Maandamano mida ya saa sita. Magari yote ya msafara yako hapa Forest yakipiga nyimbo mbalimbali za chama. Maandamano yanatarajiwa kuanza maeneo ya Mafiat njia ya Uwanja wa Ndege yataelekea Viwanja vya Ruandanzovwe Mwanjelwa.

Leo tutatembea Kilomita Mbili tu.

Pata picha za Awali.




Aluta Continua
Kutoka Mbeya Forest

Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Duh ! ww mama bado una post vitu humu JF ? watu hawana imani na ww humu kwa upotoshaji unaofanya na kulinda maslahi yako badala ya taifa
 
Tathmini ya haraka haraka...mheshimiwa Godbless Lema, MB ndio star wa leo hapa Mbeya..
 
Nawambieni CHADEMA msipoonyesha kwa vitendo kufanya yale ambayo CCM yamewashinda, watu wa kawaida watashindwa kuwatofautisha nao. Maandamano hata CCM wanayaweza sana. Onyesheni kwa vitendo na kauli zenu kwamba mnaweza kuyabadili maisha ya Watanzania hata kwa ruzuku hii ndogo mnayopata.
Wazo zuri ni kweli maandamano yaendane na kuonyesha kwamba wanaweza kuaminiwa kwa vitendo
 
Hivi sasa ndo tumetoka kuzindua tawi la wanafunzi chuo kikuu cha Teofilo Kisanji.Tunaelekea kuzindua Ofisi yao Majengo tukitoka hapo tunaendelea na maandamano kuelekea uwanjani.Watu ni wengi sana.Aluta Continua.
Asante Dada Regia Mtema,
Kwa ushauri wangu fungueni hayo matawi na muhakikishe yanajiendesha,Nilishawahi kufika ofisi moja ya tawi nikakuta hakuna hata kiti cha ziada zaidi ya kile alichokalia mwenyekiti wa tawi,Fungueni matawi na muwaweze watendaji,sio hiyo ruzuku kuishia mikononi mwa wajanja makao makuu.
 
Serikali ya CCCM imekuwa ikiwapatia CDM mamilioni ya shilingi kama ruzuku ya chama hicho kujijenga kidemokrasia na kuleta chachu ya maendeleo nchini lakini CDM wamekuwa wakitumia fedha hizo za walipa kodi kwa kutalii mikoa kadhaa huku wakipoteza nguvu ya rasilimali watu, nchi hii inahitaji wachapakazi na wenye kuleta chachu ya maendeleo na si watalii.
CHADEMA sio CCM tumeona ilivyojengwa na jinsi gani wamezitumia rasilimali zetu kwa ajiri ya kuendeleza matubo yao na familia zao(UFISADI)Kwa ziara za kwenda nje na kuwakumbuka wananchi wakati wa uchaguzi kwa kuwazadia walalahoi pea za khanga fulana na pilau.Utakijengaje chama kwa kukaa Dar na kutanua.HAMA KWELI CCM KICHEKESHO HAWA VIWAVI ILIOWATUMA HAPA JAMVINI KUWATEA HAWANA HOJA WANAKURUPUKA .
 
WildCat, Sikulaumu kwa uelewa wako finyu kwani huo ndio uwezo uliopewa na Mungu, kufanya zaidi ya hapo uwezo wa uelewa wako ulipoishia ni sawa na kukusulubu tu.
Hivi unadhani fedha za maendeleo ya Halmashauri zinatolewa na Chama! Elewa kuwa fedha za maendeleo hazitolewi na chama chochote kiwacho cha siasa. Kazi ya chama kinachoongoza Halmashauri ni kuhakikisha kuwa pesa zinatumika kwa kadri ya bajeti walizozipangia na kuzuia Ufisadi ili kile kilichokusudiwa kifanyike na si vinginevyo. Wewe unataka CDM waende kufanya maendeleo katika maeneo yanayoongozwa na ccm kwa pesa gani waliyopewa kama bajeti ya hizo halmashauri zinazofisadiwa na ccm!
 
Nazidi kushangaa wadau, kuna babu mmoja hapa nimekaa naye jirani anaonekana anawasubiri kwa mori viongozi wakuu wa chama, muda wote macho barabarani na jukwaani, naona pia kuna mama watu wazima wana mori sana pia na mabadiriko, kuna mabinti wenye wenye ari, akina mama wanazidi kuongezeka, wanavyoonekana wamekuja kwa dhamira za kweli kabisa, vijana ndo wengi zaidi, mabango yalikuwepo mengi sana, baadhi yalikuwa yana bedha hatua ya kujivua magamba ccm wakati nyoka ataendelea kuwa yuleyule, pia yamembedha shitambala kwa unafiki na njaa yake, uwanja unazidi kujaa kwa kasi hapa.

Safi, endelea kutuhabarisha mkuu. Kama kuna uwezekano tuwekeeni picha wakuu.
 
Back
Top Bottom