Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Mbeya kimesema kimekamilisha maandalizi ya kufanyika kwa maandamano ya amani yanayotarajiwa kufanyika Jumanne, Februari 20.2024 ambapo viongozi wa chama hicho ngazi ya Taifa wakitarajiwa kuongoza maandamano hayo
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Mbeya mjini Fokile Mwadende Shitambala wakati akizungumza na wanahabari katika Ofisi za chama hicho Kanda ya Nyasa jijini Mbeya kuhusu maandalizi ya maandamano hayo
Shitambala amesema tayari wamefanya maandalizi hayo kwa asilimia kubwa ambapo kutakuwa njia kubwa tatu za Mbalizi, Uyole na Isanga zikikusanya watu kwenda katikati ya jiji kisha mkutano wa hadhara katika uwanja wa Ruanda Nzovwe
Mwenyekiti huyo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuungana pamoja kwenda kufikisha ujumbe wao kwa serikali ambayo anadai haizingatii haki na utawala bora wala kuheshimu haki za watu wake ambao ndio wenye nchi
Kwa upande wake Katibu wa CHADEMA mkoa wa Mbeya Hamadi Mbeyale amesema hali ngumu ya maisha, madai ya Katiba mpya na kupinga miswada mitatu iliyopitishwa Bungeni hivi karibuni sambamba na masuala mengine yanayokuwa kero kwa wananchi
Mbeyale amewaasa wananchi kujitokeza Februari 20.2024 ili kuandamana kwani ni haki yao kikatiba ambayo itawezesha kufikisha ujumbe wao.
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Mbeya mjini Fokile Mwadende Shitambala wakati akizungumza na wanahabari katika Ofisi za chama hicho Kanda ya Nyasa jijini Mbeya kuhusu maandalizi ya maandamano hayo
Shitambala amesema tayari wamefanya maandalizi hayo kwa asilimia kubwa ambapo kutakuwa njia kubwa tatu za Mbalizi, Uyole na Isanga zikikusanya watu kwenda katikati ya jiji kisha mkutano wa hadhara katika uwanja wa Ruanda Nzovwe
Mwenyekiti huyo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuungana pamoja kwenda kufikisha ujumbe wao kwa serikali ambayo anadai haizingatii haki na utawala bora wala kuheshimu haki za watu wake ambao ndio wenye nchi
Kwa upande wake Katibu wa CHADEMA mkoa wa Mbeya Hamadi Mbeyale amesema hali ngumu ya maisha, madai ya Katiba mpya na kupinga miswada mitatu iliyopitishwa Bungeni hivi karibuni sambamba na masuala mengine yanayokuwa kero kwa wananchi
Mbeyale amewaasa wananchi kujitokeza Februari 20.2024 ili kuandamana kwani ni haki yao kikatiba ambayo itawezesha kufikisha ujumbe wao.