Kwani lazima kuoana?

Mulama, kuoa ni jambo jema kwa jamii na kwa wawili wapendanao. Kuna halalisha na kuhakikisha kuwa, watoto watakaopatikana kwenye ndoa watapata malezi bora zaidi. Na pia kunathibitisha uwezo, na nia ya wawili kuendelea kupendana, kuvumiliana na kuheshimiana.

Ndoa ni mzigo kwa wanaoingia bila kuwa na sababu za msingi za kufanya hivyo. Kuingia kwenye ndoa ili kuifurahisha jamii peke yake, ni sawa na kujinyima furaha ya maisha. Ndoa lazima itokane na nia thabiti inayosukuma mioyo ya watu wawili kuona maisha bila kuwa karibu hayana raha. Ndoa ya namna hiyo haizuiliki.

Mulama, sio lazima kwa yeyote kuoa au kuolewa. Mtu anaweza na ni haki yake kuamua aina ya maisha anayotaka kuishi (ndoa au bila ndoa). wapo watu wengi walioteseka sana ndani ya ndoa, na wapo waliofurahia sana kuwa ndani ya ndoa. Maisha ni kupanga, na kupanga ni kuchagua.

Ili kuwa na watoto, si lazima kuoa au kuolewa. Hakuna ndoa iliyofungwa wakati Adam na Hawa walipopewa amri ya kwenda na kuijaza dunia. Lakini ili maisha yawe ya kistaarabu, na ili watoto wapate malezi bora, ni vyema wawili wenye nia ya kuzaa wakaoana.
 
Dunia njema wawili wawili, hata ndege hukaa wawili....sasa litawezekana hili la wawili wawili bila ya kuwepo ndoa?

YouTube - Leona Lewis - I Got You

Linawezekana sana, kwani siku hizi hujaona wawiliwawili kabla ya ndoa? Hivi watu jamani mboni hamuelewi sledi yangu???!!! khaa mii nachukia bwanaaa! Nimeuliza hiviii ikiwa siku hizi mambo yanayofanyika kwenye ndoa tunayafanya kabla ya ndoa je kuna haja tena ya kuwa na ndoa siku hizi???? kwa maana ni changamoto kuwa ikiwa tunathamini uwepo wa ndoa basi ni kheri yatendwayo katika ndoa yawe yanasubiri ndoa kwa maana nyingine ndoa itakuwa na thamani ikiwa tutaacha kuendekeza pre marriages tunazofanya sasa.
 
Kuoa na kuolewa kuna heshima yake na mtoto wa ndoa siku zote huwa na baraka zake,

Ni imani yako tu mkuu! tukihesabu walio na baraka duniani utakuta wengi ni wa nje ya ndoa unamuonaje Obama? au hujui kama babake anga alikuwwa university akamtwanga ujauzito Ann Stanley Dunham mama yake Obama na mchezo ukaishia hapo mama akazaa prezidaa wa taifa kubwa sasa!
 
Ni imani yako tu mkuu! tukihesabu walio na baraka duniani utakuta wengi ni wa nje ya ndoa unamuonaje Obama? au hujui kama babake anga alikuwwa university akamtwanga ujauzito Ann Stanley Dunham mama yake Obama na mchezo ukaishia hapo mama akazaa prezidaa wa taifa kubwa sasa!
Hapa nimekusoma boss
 
Linawezekana sana, kwani siku hizi hujaona wawiliwawili kabla ya ndoa? Hivi watu jamani mboni hamuelewi sledi yangu???!!! khaa mii nachukia bwanaaa! Nimeuliza hiviii ikiwa siku hizi mambo yanayofanyika kwenye ndoa tunayafanya kabla ya ndoa je kuna haja tena ya kuwa na ndoa siku hizi???? kwa maana ni changamoto kuwa ikiwa tunathamini uwepo wa ndoa basi ni kheri yatendwayo katika ndoa yawe yanasubiri ndoa kwa maana nyingine ndoa itakuwa na thamani ikiwa tutaacha kuendekeza pre marriages tunazofanya sasa.
Umesomeka boss
 
Mulama, kuoa ni jambo jema kwa jamii na kwa wawili wapendanao. Kuna halalisha na kuhakikisha kuwa, watoto watakaopatikana kwenye ndoa watapata malezi bora zaidi. Na pia kunathibitisha uwezo, na nia ya wawili kuendelea kupendana, kuvumiliana na kuheshimiana.

Ndoa ni mzigo kwa wanaoingia bila kuwa na sababu za msingi za kufanya hivyo. Kuingia kwenye ndoa ili kuifurahisha jamii peke yake, ni sawa na kujinyima furaha ya maisha. Ndoa lazima itokane na nia thabiti inayosukuma mioyo ya watu wawili kuona maisha bila kuwa karibu hayana raha. Ndoa ya namna hiyo haizuiliki.

Mulama, sio lazima kwa yeyote kuoa au kuolewa. Mtu anaweza na ni haki yake kuamua aina ya maisha anayotaka kuishi (ndoa au bila ndoa). wapo watu wengi walioteseka sana ndani ya ndoa, na wapo waliofurahia sana kuwa ndani ya ndoa. Maisha ni kupanga, na kupanga ni kuchagua.

Ili kuwa na watoto, si lazima kuoa au kuolewa. Hakuna ndoa iliyofungwa wakati Adam na Hawa walipopewa amri ya kwenda na kuijaza dunia. Lakini ili maisha yawe ya kistaarabu, na ili watoto wapate malezi bora, ni vyema wawili wenye nia ya kuzaa wakaoana.

Hakika umetoa mushraf jadidi mkuu, haya na mengine ndio yapendezayo kujadiliwa katika m,uktadha huu manake tunatakiwa kufikia mahala pa kuwa na msimamo wa llipi lifanyike kati ya kuoana au kutooana na kila anayehamua aina mojawapo awe amejihoji yakini kama amechagua njia sahii na anayoapa kuitumikia siku zote za maisha yake.
 
Mulama ulipata ngapi kwenye kiswahili maana naona km una F hv

Binti watafuta twalaka kwa nguvu weye!! utamuhoji vipi mumeo khabari za maksi shuleni wakati ulitakiwa kumuuliza mkiwa bado wachumba?????!
 
Kuhusu mimi:Male 22 yrs,cna girlfriend and No plans to have one,i'm happy with my life.Kuna kitu kinanikera sana,hivi kwani ni lazima kila mtu aoe?????? kwanini nikisema nataka kuadopt mtoto watu wananiona mutant?:typing: i've seen people do it(stay single and they are happy)i'm not ready for Relationship Stress and i'm not sure if i will someday.:and one thing; I HATE MARRIAGE!!!!!!!!MARRIAGE SUCKS!!!!!!!!lol!
 
Hakuna ulazima wa kuoa au kuolewa,ila maandiko matakatifu yanasemaje kuhusu hilo?ni agizo la mwenyezi mungu!kwanza we bado dogo sana,soma kwanza,usikimbilie mambo ya utu uzima.
 
"Basi kuhusu mambo yale mliyoniandikia: Ni vema mwanaume asimguse mwanamke. Lakini ili kuepuka zinaa, kila mwanaume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe."

"Kwa wale wasiooa na kwa wajane, ingekuwa vizuri wabaki kama mimi nilivyo. Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe na kuolewa, kwa maana ni afadhali kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa.'

"Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote."
 
Kuhusu mimi:Male 22 yrs,cna girlfriend and No plans to have one,i'm happy with my life.Kuna kitu kinanikera sana,hivi kwani ni lazima kila mtu aoe?????? kwanini nikisema nataka kuadopt mtoto watu wananiona mutant?:typing: i've seen people do it(stay single and they are happy)i'm not ready for Relationship Stress and i'm not sure if i will someday.:and one thing; I HATE MARRIAGE!!!!!!!!MARRIAGE SUCKS!!!!!!!!lol!

Ni maamuzi yako tu hakuna atakayekulazimsha ufanye vile ambavyo wewe hupendi. Kuna wengine wanapenda sana kuolewa au kuoa kutokana na faida mbali mbali zilizomo kwenye ndoa pamoja na kuwa zina machungu yake, lakini miaka ya karibuni idadi ya wale ambao hawataki kuoa au kuolewa imeongezeka kwa kasi sana. Hata kuadopt mtoto si kitu kibaya maana kuna watoto wengi ambao ni yatima hivyo itakuongezea thawabu nyingi. Kila la heri.
 
sio lazima kuoa.Maishani usikubali kufuata mkumbo hata siku moja.Ila ni afdhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.Halafu Mungu alione si vema mtu awe single!.
Hebu pata kitu hiki:"Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa. Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa. Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee. " (Mathayo 19:10-12).
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
MMMh! kuna walaakin hapo si bure.kina Baba na kina mama wa JF mpoo kijana wenu anaulizaa neno zitooooooooo!
 
Mi nadhani kwa umri wako waweza kuconcentrate na mambo mengine kwanza ila najua umri ukifika utakuja kuomba ushauri jinsi gani nzuri ya kuingia kwenye ndoa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom