Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,582
- 113,795
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo ni kuhusu umuhimu wa viongozi wetu na haswa wakuu wa Mihimili lazima sio tuu wawe wasomi, weledi na wachapakazi, bali lazima wawe Bright, brilliant na wabobezi wa fani husika.
Niko mahali nafuatilia Bunge Live, kiukweli kabisa nimekuwa very impressed na jinsi Madam Spika Dr. Tulia Akson anavyoliongoza Bunge.
Juzi aliifanua vizuri Ripoti ya CAG na kuifafanua ile kauli ya hasira ya Mama ya stupid na "Watupishe", ni walioongeza "cha juu" kwenye ununuzi wa ndege ya mizigo, na sio wote waliotajwa kwenye ripoti ya CAG.
Leo Mbunge wa Liwale kaibua kubwa kuliko Bungeni kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere, JNHPP japo liko Rufiji, bwawa hilo liko wilaya ya Liwale mkoani Lindi, na sio Mikoa ya Pwani na Morogoro, hivyo wilaya ya Liwale inastahili asilimia 60% ya mgao wa fedha za CSR ya JNHPP, lakini Liwale haikupata hata senti 5!.
Spika Tulia akaingilia kati kwa kumuuliza Mhe. Mbunge athibitishe Bwawa la JNHPP liko Liwale, Mbunge akasema lipo Liwale!.
Dr. Tulia akafafanua tofauti ya mahali Bwawa lilipo na the catchment area maji ya kulijaza bwawa yanakotoka!. Mhe. Mbunge akang'ang'ana bwawa liko Liwale!.
Dr. Tulia akamwambia Mhe Mbunge kuwa yeye na wabunge wamekwenda lilipo na hadi kubonyeza kitufe kukajaza maji, bwawa liko Rufiji na sio Liwale, hivyo akamwambia mbunge akae kwanza.
Kisha akauliza wahusika kama wapo waeleze Bunge bwawa la JNHPP liko wapi, ndipo akasimama Naibu Waziri wa Nishati, Byabato, akasema kwa mujibu wa ramani zao, bwawa la JNHPP liko Rufiji na Morogoro, ila kama Mbunge anayo ramani yake inayoonyesha bwawa liko Liwale, ailete na kuwaelimisha wengine tuko tayari kujifunza!.
Mbunge mwingine akasimama kuchangia kuwa bwawa liko Rufiji ila the catchment area ya maji ya bwawa hilo yanatoka Liwale.
Ndipo Spika Tulia akampiga darasa Mbunge huyo kuwa bwawa la JNHPP liko Rufiji ila maji ya kulijaza yanaweza kutiririka kutoka popote na kumruhusu kumalizia kuchangia.
Hii ndio faida ya kuwa na Spika msomi wa sheria, natumaini wengi unakumbuka uendeshaji wa Bunge enzi za Spika Sitta pia alikuwa ni msomi wa sheria.
Kwa vile mimi ni mtu wa mastori mastori
Ngoja niwape mastori ya Mimi na Dr. Tulia Akson, kwa msiopenda mastori jump kule chini
Tanzania tunakwama baadhi ya maeneo kwasababu tuna viongozi vilaza!. We can afford kuwa na wabunge vilaza, ndani ya Bunge la JMT but we can't afford kuwa na wabunge vilaza kwenye Bunge la EALA! Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo
Ili Tanzania tuweze kupata viongozi bora,, the best of the best, hatuwezi kuuendeleza ule ujinga uliochomekewa ndani ya katiba yetu kiubatili, kuwaachia kakikundi ka watu wachache kuamua huyu ni wenzetu mpe uongozi, hata kama ni vilaza!, na huyu sii wenzetu kata jina tupa kule, hatumuhitaji, hata kama ni the best bright and Brilliant
Kwa maoni yangu, nashauri Spika asitokane na ukanda wa chama cha siasa, Spika Dr. Tulia huyu, tunayemsifu leo, kuwa anakwenda kuwa Spika bora ndio Dr. Tulia yule yule aliye naibu Spika chini ya bora Spika, na alinyamaza kimya wakati katiba yetu ikikanyagwa Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?
Hitimisho,
Nahitimisha kwa lile swali, la msingi la makala hii, kufuatia Spika Sitta na Spika Dr. Tulia Akson, ambao ni wanasheria, kuwa so good kwenye uendeshaji wa Bunge la JMT, kwasababu, they are smart, bright & brilliant! kuna haja sasa, kuanzia sasa kuhakikisha MaSpika wetu wote lazima wawe wanasheria?.
Wasalaam
Paskali
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo ni kuhusu umuhimu wa viongozi wetu na haswa wakuu wa Mihimili lazima sio tuu wawe wasomi, weledi na wachapakazi, bali lazima wawe Bright, brilliant na wabobezi wa fani husika.
Niko mahali nafuatilia Bunge Live, kiukweli kabisa nimekuwa very impressed na jinsi Madam Spika Dr. Tulia Akson anavyoliongoza Bunge.
Juzi aliifanua vizuri Ripoti ya CAG na kuifafanua ile kauli ya hasira ya Mama ya stupid na "Watupishe", ni walioongeza "cha juu" kwenye ununuzi wa ndege ya mizigo, na sio wote waliotajwa kwenye ripoti ya CAG.
Leo Mbunge wa Liwale kaibua kubwa kuliko Bungeni kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere, JNHPP japo liko Rufiji, bwawa hilo liko wilaya ya Liwale mkoani Lindi, na sio Mikoa ya Pwani na Morogoro, hivyo wilaya ya Liwale inastahili asilimia 60% ya mgao wa fedha za CSR ya JNHPP, lakini Liwale haikupata hata senti 5!.
Spika Tulia akaingilia kati kwa kumuuliza Mhe. Mbunge athibitishe Bwawa la JNHPP liko Liwale, Mbunge akasema lipo Liwale!.
Dr. Tulia akafafanua tofauti ya mahali Bwawa lilipo na the catchment area maji ya kulijaza bwawa yanakotoka!. Mhe. Mbunge akang'ang'ana bwawa liko Liwale!.
Dr. Tulia akamwambia Mhe Mbunge kuwa yeye na wabunge wamekwenda lilipo na hadi kubonyeza kitufe kukajaza maji, bwawa liko Rufiji na sio Liwale, hivyo akamwambia mbunge akae kwanza.
Kisha akauliza wahusika kama wapo waeleze Bunge bwawa la JNHPP liko wapi, ndipo akasimama Naibu Waziri wa Nishati, Byabato, akasema kwa mujibu wa ramani zao, bwawa la JNHPP liko Rufiji na Morogoro, ila kama Mbunge anayo ramani yake inayoonyesha bwawa liko Liwale, ailete na kuwaelimisha wengine tuko tayari kujifunza!.
Mbunge mwingine akasimama kuchangia kuwa bwawa liko Rufiji ila the catchment area ya maji ya bwawa hilo yanatoka Liwale.
Ndipo Spika Tulia akampiga darasa Mbunge huyo kuwa bwawa la JNHPP liko Rufiji ila maji ya kulijaza yanaweza kutiririka kutoka popote na kumruhusu kumalizia kuchangia.
Hii ndio faida ya kuwa na Spika msomi wa sheria, natumaini wengi unakumbuka uendeshaji wa Bunge enzi za Spika Sitta pia alikuwa ni msomi wa sheria.
Kwa vile mimi ni mtu wa mastori mastori
Ngoja niwape mastori ya Mimi na Dr. Tulia Akson, kwa msiopenda mastori jump kule chini
Mimi nimejiunga Radio Tanzania mwaka 1990 wakati huo Tulia ndio kwanza anamaliza darasa la 7 Shule ya Msingi ya Mabonde na kupasi na kujiunga Form I Shule ya Sekondari ya Loleza ile mwaka 1991 mimi tayari nina mwaka mmoja kazini.
Ile mwaka 1994 wakati jina la Tulia linaingia kwenye wanafunzi kumi bora wa Tanzania, ni mimi nili cover story na picha ya Tulia akifanana copy right na mwandishi mmoja wa habari wa RTD Tumaini Mwakosya (RIP)
Tulia akapasi kwenda Shule ya sekondari ya Zanaki na Mwaka 1997 wakati anafumua points 3, mimi tayari naendesha kipindi cha Kiti Moto, Tulia alijoin UDSM kupiga LL.B na kufumua GPA kali, infact alikuwa apate 1st Class kama AshaRose Migiro lakini wakambania, akaunganisha LL.M. na kuajiriwa UDSM as tutorial assistant. Kipindi cha Kiti Moto from time to time tulikiendeshea Ukumbi wa Nkruma Hall.
Mwaka 2003 mimi nilipotinga UDSM kupiga LL.B, mwaka wetu wa kwanza, kipindi chetu cha kwanza ni LW : 101 mwalimu wetu wa kwanza kuingia darasani kwetu ni Tulia Akson.
Sisi tuliosoma tukiwa watu wazima, tuna changamoto kweli kweli, unafundishwa na vialimu vibinti vidogo vibichi!, sometimes concentration ni changamoto!.
Mwaka 2004 kwenye top ten ya wanafunzi bora pale Ukumbi wa Karimjee Hall nikakutana na Tulia, kumbe last born wao kabinti pia kametinga top ten!.
Kuna familia Wanafanya vizuri na kutinga top ten kwasababu wanatoka familia bora, wazazi wana uwezo, nyumbani asubuhi ni breakfast chai maziwa, mkate siagi, sousages, mayai, cornflakes, Shule ni academy, zina walimu, all facilities vitabu vya kiada na ziada, mtoto asipofanya vizuri huyo ni vilaza!. Ndio maana kuna wakati niliwahi kumtumia barua Baba Jesca Wito kwa Baba Jesca: Watendee haki kina Jesca wote ili nao wapate bahati kama Jesca!
Lakini kuna familia wao akili zao ni za nature, watu waliosoma St. Kayumba, kisha kusoma Government schools halafu kutinga top ten ujue hizi ni akili za Nature, ili Tanzania tupate maendeleo ya kweli ni lazima viongozi wetu wa taasisi muhimu wawe the best, the bright and brilliant, Bunge la Dr. Tulia, hataki ujinga ujinga!.
Kuna siku nilikutana na Spika Dr. Tulia kule Mbeya, nilipomsalimia na kujitaja mimi nilikuwa mwanwfu wake, yeye alirudisha salaam yangu kwa kuitikia Marahaba!, as if mimi nilimwamkia shikamoo!
She is almost 10 years mdogo kwangu!.
Unapotokea kumpongeza mtu kama huyu baada ya kuingia kwa dhana ya uchawa, mijitu mijinga inaweza kudhani hili ni bandiko la kusifu kwa UCHAWA!. No!. Tofauti pekee kati ya kusifu kwa ukweli bonafide genuine na kusifu kwa UCHAWA, kusifu bonafide genuine ni utasifu mazuri tuu, hivyo siku huyo uliemsifia leo akiboronga, una mkosoa.
Kusifu kwa machawa, kazi yao ni kusifu tuu.
Hivyo japo ni mimi niliyemtabiria Dr. Tulia uspika, Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...
Fursa ya Spika mpya ilipojitokeza, niliwaomba CCM Kujiuzulu kwa Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili tupate Spika Bora. CCM itateua Spika Bora au Bora Spika kama kawa?
Hivyo Dr Tulia aliposhinda nikamshauri Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!
Tanzania tunakwama baadhi ya maeneo kwasababu tuna viongozi vilaza!. We can afford kuwa na wabunge vilaza, ndani ya Bunge la JMT but we can't afford kuwa na wabunge vilaza kwenye Bunge la EALA! Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo
Ili Tanzania tuweze kupata viongozi bora,, the best of the best, hatuwezi kuuendeleza ule ujinga uliochomekewa ndani ya katiba yetu kiubatili, kuwaachia kakikundi ka watu wachache kuamua huyu ni wenzetu mpe uongozi, hata kama ni vilaza!, na huyu sii wenzetu kata jina tupa kule, hatumuhitaji, hata kama ni the best bright and Brilliant
Kwa maoni yangu, nashauri Spika asitokane na ukanda wa chama cha siasa, Spika Dr. Tulia huyu, tunayemsifu leo, kuwa anakwenda kuwa Spika bora ndio Dr. Tulia yule yule aliye naibu Spika chini ya bora Spika, na alinyamaza kimya wakati katiba yetu ikikanyagwa Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?
Hitimisho,
Nahitimisha kwa lile swali, la msingi la makala hii, kufuatia Spika Sitta na Spika Dr. Tulia Akson, ambao ni wanasheria, kuwa so good kwenye uendeshaji wa Bunge la JMT, kwasababu, they are smart, bright & brilliant! kuna haja sasa, kuanzia sasa kuhakikisha MaSpika wetu wote lazima wawe wanasheria?.
Wasalaam
Paskali