Zuio la mahindi nje litawanufaisha wachache na kuwapa hasara wengi

Molembe

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
9,821
11,527
Baada ya tamko la Rais kuzuia mahindi kwenda nje malori yenye shehena za mahindi yamezuiwa kwenda nchi za nje, Ukitembelea maeneo mengi ya mpakani hasa kule Sirari na Namanga kuna malori mengi sana yamezuiwa kuingia Kenya.

Zuio hili la mahindi litawanufaisha wachache maana Tanzania sio kisiwa, haiwezekani mahindi gunia Tanzania liuzwe 50,000/- halafu Kenya liuzwe 150,000/- sisi Tanzania tuwe salama, kwa vyovyote vile mahindi hayo yatatoroshwa kwenda nje maana nchi yetu sio kisiwa.

Zuio hili litaleta hasara kubwa kwa wakulima maana wajanja wachache watalangua mahindi hayo kwa bei ndogo na kuyatorosha kwenda nje matokeo yake nchi itakosa mapato pia na wakulima kupata hasara, Ukitembelea maeneo ya mpakani tayari imeishakuwa dili la polisi na watu wa Tra.

Wito wangu kwa serikali iruhusu mahindi yaende nje tupate mapato na vile vile wakulima wetu wapate faida na kufurahia matunda ya kazi, hii pia itaweza kuwavutia wengi kujishughulisha na shughuli za kilimo na ile dhana ya kudharau kilimo na wakulima itafutika.

Lakini pia serikali ikumbuke gharama za kilimo zimepanda sana mathalani kulima ekari moja mkulima hutumia wastani wa 700,000/-~ 900,000/-, ekari moja hutoa wastani wa gunia 15~20, hivyo mkulima akiuza mazao yake kwa bei ndogo atapata hasara na msimu unaofuata hatajihusisha tena na kilimo au atapunguza uzalishaji.

Serikali itumie hii kama fursa kuhakikisha tunaboresha kilimo chetu ili tuweze kuwaalisha majirani zetu, na kutengeneza ajira pia.
 
Zuio hili litaleta hasara kubwa kwa wakulima maana wajanja wachache watalangua mahindi hayo kwa bei ndogo na kuyatorosha kwenda nje matokeo yake nchi itakosa mapato pia na wakulima kupata hasara, Ukitembelea maeneo ya mpakani tayari imeishakuwa dili la polisi na watu wa Tra.
Tangu hapo kabla hao wakulima hawanufaiki na uuzwaji wa mahindi nje ya nchi. Waishio mpakani wana ushahidi huo. Wakulima wengi ni walalahoi wanaofaidika ni walanguzi.

Baadae wakulima haohao wanakuja kununua chakula kwa bei ghali.
 
Hapn tunawapenda wakulima ila wakulima watuvumilie kwanzamwakani chakula kitatoka nnje
 
Mtoa mada hebu acha kuongeza chumvi katika gharama ya kulima ekari 1, umesema inagharimu laki 7 mpaka laki 9. Mimi ni mkulima mzoefu hebu lete mchanganuo ikifika laki 7 nakupa milioni moja ya usumbufu.
 
Tangu hapo kabla hao wakulima hawanufaiki na uuzwaji wa mahindi nje ya nchi. Waishio mpakani wana ushahidi huo. Wakulima wengi ni walalahoi wanaofaidika ni walanguzi.

Baadae wakulima haohao wanakuja kununua chakula kwa bei ghali.
Wakulima wananufaika ebu uliza bei ya mahindi kwa sasa kule Mpanda na kabla ya tamko, bei zimeshuka sana baada ya tamko.
 
Kama serikali ilitoa taarifa mapema kuwa tarehe fulani mipaka itafungwa ni sahihi.
Sometimes lazima serikali iingilie forces za demand na supply kwa manufaa ya jamii.

Ila kama hakukuwa na taarifa rasmi, yaani mipaka imefungwa ghafla. Hiyo ni changamoto hasa kwa waliokuwa wakisafirisha kwenda nje.
 
Kiko wali kiburi Cha waziri Bashe leo Samia ameingilia Kat ameona Hali itakuwa mbaya mwa kuwanenenepesha wafanya biashara wachche wasio fika hata elf 30


Hali Ni mbya sna ya chakula safari hi wee tembeeleaa gairo na kibaigwa utaona Hali halisi mashambani
Hivi mpaka sasa hamjajua ni sababu gani iliyo sababisha serikali izuie mahindi kwenda nje?
Serikali haijazuia mahindi kwa kuofia njaa bali imeyazuia kwa sababu imeona haina uwezo wa kushindana na wafanya biashara katika kutoa bei kwa mkulima,na wenda huu ushauri kautoa Bashe mwenyewe.

Serikali ina taka kununua mahindi zaidi ya tani laki tano hivi unategemea wakiruhusu yaende nje ni mkulima au mfanya biashara gani atakaye kubali kuiuzia serikali mahindi ?
Hata hayo mahindi yamezuiwa makusudi kabisa mpakani ili kuwa razimisha wafanya biashara wayauze kwa serikali.

Ukitaka kuamini hili ww subili wamalize kununua mahindi uone kama hili zuio litaendelea kuwepo,hivyo ni vyema kutumia furusa hii kununua akiba ya mahindi ya kutosha kwa ajili ya familia tofauti na hapo tutatia adabu.
 
Back
Top Bottom