Zombe aomba kustaafu

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Jeshi la polisi nchini limesema kwamba Kamishna Abdalah Zombe bado ni mtumishi wake ila amelazimika kuomba kustaafu kutokana na mazingira ya kesi iliyomkabili na kwamba anasubiri majibu kutoka Utumishi.
 
Alikiwa anasubiri nini cku zote hizi, kwani kurudishwa kazini by all means itakuwa vigumu, hata kama atashinda rufaa
 
For whatever decision he takes, he is in for it, na jamii haitamkubali anymore!
Aache kazi, akimbilie kokote anakotaka, mkono wa sheria utamfuata, na hata akishinda rufaa, hukumu ya hakimu-ULIMWENGU ipo juu yake tayari.
 
Ulikuwa wapi Swahiba? mbona na mimi nilikushauri siku nyingi? Kama ni kweli unasubiri nini? Barua kutoka Ikulu au Utumishi????? Lakini bado hukumu ya God ipo Pale pale kwa wale uliowatesa na kuwaua pasipo na Makosa. Kila la Kheri usubiri Hukumu
 
Mimi nafikiri Utumishi wasubiri kwanza hatima ya rufani kwanza. Kwa sababu kama akikubaliwa kustaafu inamaanisha atalipwa pia mafao yake. Sasa itakuwaje kama serikali iliyokata rufani ikashinda na huyu jamaa akafungwa huku akiwa amevuta kiinua mgongo? Mimi naona Utumishi wasubiri hatima ya rufani kwanza kabla ya kuanza mchakato wa aina yoyote ile.

Shadow.
 
Hii barua aliiandika siku nyingi na akaipeleka pale Makao makuu ili ipitishwe, kinachotokea ni timing, ya kutaka kumrudisha tena selo akiwa mtumishi ili kumnyima baadhi ya stahili zake iwapo atatiwa hatiani maana itampasa kufukuzwa kazi, maana ipo rufaa ya serikali itakamilika punde.
 
Ulikuwa wapi Swahiba? mbona na mimi nilikushauri siku nyingi? Kama ni kweli unasubiri nini? Barua kutoka Ikulu au Utumishi????? Lakini bado hukumu ya God ipo Pale pale kwa wale uliowatesa na kuwaua pasipo na Makosa. Kila la Kheri usubiri Hukumu

mkuu pastor wewe ukiwa kama original mchungaji si ulitakiwa umkumbushe kutubu?mimi naamini kuna toba ya ukweli ambayo akitubu na kujutia madhambi yake[kama anayo]mola atamsikia
 
Hii case iwe isiwe, Zombe hana hatia ya kuua, hakufyatua risasi kuua mtu. Labla wamtie hatiani kwa makosa ambayo hakushitakiwa nayo ya kuficha na kupindisha ukweli na kufundisha wahalifu jinsi ya kuongea kwenye Tume ya Kipenka.

Waendesha mashitaka wetu ni mbumbumbu, walitakiwa kuleta counts kama 50 kwa zombe na wenzake, saa hizi tungekuwa tumeshasahau kama kulikuwa na kesi ya Zombe na wenzake. Maana wasingetiwa hatiani kwa mauaji ila wangetiwa hatiani kwa counts nyingine.

Mwacheni Zombe aombe kustaafu, ajichukulie stahili zake, mapema. Na kesi zote za ufisadi zitashindwa kama hii ya Zombe na wenzake. Tumesha mwagiwa pilipili za macho na waendesha mashitaka wa kisiasa. Sasa baada ya kuona wananchi wanakuja juu na uchaguzi unakaribia wanajifanya kumshikia bango Zombe. Mwacheni ajipumzikie baada ya kusota mahabusu kwa muda mrefu
 
Haki ya malipo yake ipo palepale! Hata ajichimbie chini ya ardhi itamfuata alipo! Aombe kustaafu na uraia wa TZ basi
 
The man is lucky, nani alitegemea kwamba hukumu ya awali ingekuwa hivi? Nadhani atashinda tena kama ilivyotokea hapa mwanzo. Tatizo letu kama nchi hakuna tofauti kati ya SIASA na SHERIA!!
 
Zombe hana hatia ya mauaji. Hii haihitaji PhD ya Oxford kujua hilokwa mujibu ya kesi za mauaji.

Pili, kama Zombe kwa hiyari yake mwenyewe ameamua kuomba kustaafu na anacheleweshewa majibu yake, basi tulitakiwa kuikema tabia hii ya ucheleweshaji kwa nguvu zote. Leo tunaona ucheleweshaji kwa Zombe kwa vile media bado ina mmulika, je ni watanzania wangapi wanafanyiwa hivyo sasa hivi?
 
Back
Top Bottom