Zoezi la uandikishaji lahamia kwa wanafunzi wa sekondari

Kingjr2

JF-Expert Member
Sep 8, 2018
644
1,271
Hakika ukistaajabu ya Musa utayaona ya firauni!

Wakati Dar es Salaam Mkuu wao wa Mkoa akijinasibu kwa kuongoza mikoa mingine zoezi la uandikishaji, Halima Mdee anaibuka na tuhuma kwamba majina mengi hayana saini za wahusika

Sasa kituko ni huko Morogoro, baada ya juzi kupenyezewa kwamba wajumbe wa mtaa wanapita nyumba kwa nyumba kuorodhesha watu wote wenye miaka 18 na kuendelea, sasa zoezi limehamia kwa wanafunzi

Ili kuendana na kasi, waandikishaji wamepewa target ya watu 40 kwa siku. Wanachokifanya wanadaka yeyeto anayepita mbele yao, na wanaorodhesha wanafunzi kuanzia kidato cha pili na kuendelea wanaosoma ndani ya shule iliyomo ndani ya kata husika au jirani ilimradi tu wafikishe target.

Pia Wakuu wa shule wameambiwa wawahimize watoto wakajiandikishe na kila siku wanatoa taarifa ya idadi kwa mkurugenzi.

Shule zenye idadi ndogo ya wanafunzi waliojiandikisha Wakuu wa shule hupewa maneno yenye mwelekeo wa vitisho. Nani atakubali kutishiwa kisa watoto hawajiandikishi na uwezo wa kuwalazimisha anao!? Kinachotokea ni watoto kupigwa biti wakajiandikishe hata kama hawana miaka 18 ilimradi idadi iwe kubwa

Hizi taarifa wanazo walimu na watendaji wa mitaa.
 
Kwan kama hao wanafunz wamefikisha umri wa miaka 18 yupo form three kuna shida gani?
Hainashida kabisa ila shida inakuja pale ambapo hawaulizwi miaka yao na wanapohoji kwamba hawajafika miaka 18 wanaambiwa sio lazima wao wanataka majina na sahihi zao
 
Kwan kama hao wanafunz wamefikisha umri wa miaka 18 yupo form three kuna shida gani?
Kama wapo wanaweza kuwa mmoja, wawili au watatu hasa kwa shule za serikali...hapo ni form three, form two sio rahisi kuwa na miaka 18! Ni mara chache sana, labda shule za private.

Sasa unadhani Mkuu wa shule atakubali kupeleka majina ya wanafunzi 10 au 15 kwamba ndio waliojiandikisha wakati shule ina wanafunzi zaidi ya mia tisa!?

Unaweza kujua atakachoambiwa na bosi wake
 
Kuna shule boarding, form four waligomea kwa kuwa wataondoka kabla ya kupga kura. Wakaambiwa wao wanajuwa wanachokifanya.
 
Hawa ni wanafunzi wa sekondari hapa Makambako mtaa wa Sigrid wamesombwa kwenda kuandikishwa kwenye daftari la wapiga Kura. Swali ni Je wana miaka 18 na huu utaratibu wa kusomba watoto wa shule kwenda kuwaandikisha umeanza lini?


Nchi hii shetani anatutafuta..

By RC
FB_IMG_1571257945012.jpeg
 
Back
Top Bottom