Charles Ignatio
Senior Member
- Oct 9, 2010
- 133
- 52
*ZOEZI LA KUPOKEA TAARIFA ZA WALIMU WOTE NCHINI WA SHULE ZA BINAFSI AMBAO WAMEKUMBWA NA TATIZO LA MISHAHARA YAO KUTOLIPWA KUTOKANA NA JANGA LA UGONJWA WA CORONA LINAENDELEA VIZURI*
Zoezi hili linaratibiwa na chama cha walimu wa shule za binafsi Tanzania- *TPTU* mpaka muda huu linaendelea vizuri na mwitikio wa walimu nvhini wanaotoa taarifa zao kwetu ni mkubwa, inatia moyo sana na inatupa ari kutafuta majawabu ya tatizo hili kwa busara na hekima kubwa, hii ni inashiria kuwa tatizo hili ni kubwa kuliko tunavyoweza kufikiria.
Tunalazimika kusimama katika hili kwa walimu wote wa shule za binafsi nchini ambao wapo katika tatizo hili bila kujali ni wanachama waliosajiliwa au sio wanachama waliosajiliwa tunasimama nao wote kama ilivyo wajibu wa chama hiki kisheria.
Tunakiri wazi kabisa kuwa tatizo hili limeathiri *walimu,wazazi,waajiri na wanafunzi* lakini katika hawa wote, mwalimu wa shule binafsi ambaye hajapata mshahara wake ndiyo anaeumia zaidi,chama kinawatoa hofu walimu wote nchini kuwa busara kubwa itatawala katika kutafuta suluhisho la hili tatizo baina ya *chama,waajiri na serikali* ili kupata mwarobaini wa walimu hawa kwani kila mtu katika janga hili hana hatia ila ni muhimu tukashirikiana bega kwa bega wakati huu wa shida kama ilivyokuwa wakati wa amani.
Tarehe *19/4/2020* siku ya jumapili ni mwsho wa kupokea taarifa za walimu wenye changamoto hii ili tuende kwenye hatua zingine ambazo chama kimejipanga kuzipitia kuhakikisha ufumbuzi wa tatizo hili kwa walimu unapatikana haraka.
Wasiliana nasi kwa simu namba *0767664494* tupate taarifa zako kama unapitia changamoto hii, share ujumbe huu kadiri uwezavyo uwafikie walengwa wengi zaidi wa tatizo hili hapa nchini.
*UMOJA NA MSHIKAMANO DAIMA*
Na Mwl JULIUS MABULA.
KATIBU MKUU.
CHAMA CHA WALIMU WA SHULE ZA BINAFSI TANZANIA-TPTU.
MAKAO MAKUU-MWANZA.
Zoezi hili linaratibiwa na chama cha walimu wa shule za binafsi Tanzania- *TPTU* mpaka muda huu linaendelea vizuri na mwitikio wa walimu nvhini wanaotoa taarifa zao kwetu ni mkubwa, inatia moyo sana na inatupa ari kutafuta majawabu ya tatizo hili kwa busara na hekima kubwa, hii ni inashiria kuwa tatizo hili ni kubwa kuliko tunavyoweza kufikiria.
Tunalazimika kusimama katika hili kwa walimu wote wa shule za binafsi nchini ambao wapo katika tatizo hili bila kujali ni wanachama waliosajiliwa au sio wanachama waliosajiliwa tunasimama nao wote kama ilivyo wajibu wa chama hiki kisheria.
Tunakiri wazi kabisa kuwa tatizo hili limeathiri *walimu,wazazi,waajiri na wanafunzi* lakini katika hawa wote, mwalimu wa shule binafsi ambaye hajapata mshahara wake ndiyo anaeumia zaidi,chama kinawatoa hofu walimu wote nchini kuwa busara kubwa itatawala katika kutafuta suluhisho la hili tatizo baina ya *chama,waajiri na serikali* ili kupata mwarobaini wa walimu hawa kwani kila mtu katika janga hili hana hatia ila ni muhimu tukashirikiana bega kwa bega wakati huu wa shida kama ilivyokuwa wakati wa amani.
Tarehe *19/4/2020* siku ya jumapili ni mwsho wa kupokea taarifa za walimu wenye changamoto hii ili tuende kwenye hatua zingine ambazo chama kimejipanga kuzipitia kuhakikisha ufumbuzi wa tatizo hili kwa walimu unapatikana haraka.
Wasiliana nasi kwa simu namba *0767664494* tupate taarifa zako kama unapitia changamoto hii, share ujumbe huu kadiri uwezavyo uwafikie walengwa wengi zaidi wa tatizo hili hapa nchini.
*UMOJA NA MSHIKAMANO DAIMA*
Na Mwl JULIUS MABULA.
KATIBU MKUU.
CHAMA CHA WALIMU WA SHULE ZA BINAFSI TANZANIA-TPTU.
MAKAO MAKUU-MWANZA.