Zitto utamkoma Rais Magufuli

RUSTEM PASHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2016
3,590
8,475
ZITTO UTAMKOMA RAIS MAGUFULI

Mwaka 2013, CAG katika ripoti yake, alitoa hati chafu kwa Wizara ya Ujenzi, kutokana na fedha kiasi cha Sh253 bilioni ambazo wizara hiyo iliziomba kwa ajili ya utekelezaji wa miradi maalum, lakini matumizi yake yalijaa giza.

Waziri wa Ujenzi alikuwa Dk John Magufuli. Hivyo kashfa hiyo ikawa inamwelekea yeye.

Zitto Kabwe akiwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), aliibebea bango kashfa hiyo. Bungeni pakachimbika. Zitto akashikilia mshahara wa Magufuli.

Kashfa hiyo ilimtesa sana Magufuli ambaye alihangaika kutoa maelezo na kusambaza kwenye mitandao ya kijamii kujisafisha. Zitto alimkalia kooni.

Zitto akiwa Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, aliwakataza wabunge wa Chadema wakati huo kumsifia Magufuli. Wabunge wengi wa Chadema walikuwa wakisimama wanamsifu Magufuli kwa utendaji wake, Zitto akawaonya kuwa Magufuli alizitumia vibaya sifa hizo kwa kuushusha hadhi upinzani.

Kimsingi Magufuli na Zitto hawajawahi kuiva chungu kimoja. Ni Zitto aliyeahidi kuwa Magufuli atakuwa Rais wa muhula mmoja. Kwamba mwaka 2020 atakataliwa na wananchi.

Leo hii Magufuli ndiye Rais wa Tanzania. Zitto ni Kiongozi wa ACT-Wazalendo, chama kichanga ambacho kinahitaji uwekezaji imara ili kiimarike na kukua.

Ni wakati huu sasa Magufuli anavuna vichwa ACT. Alimtwaa mshauri wa chama, Prof Kitila Mkumbo, akampa Ukatibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, sasa amemtwaa Mwenyekiti wa ACT, Anna Mghwira, kampa Ukuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Kitila na Mghwira walikuwa nguzo hasa za ACT. Magufuli kawatwaa na kukiachia pengo chama, kisha kukijaza kashfa kuwa viongozi wake wana nasaba na CCM.

Kipindi hiki Zitto lazima ajue Magufuli ni nani. Magufuli ni Rais. Anatumia mamlaka yake kisayansi kukidhoofisha na kukipa wasifu mbaya chama cha ACT. Watu wakione chama ni ndugu na CCM, jambo ambalo ni sumu mbaya kwa siasa za upinzani Afrika.

Zitto wewe endelea kukomaa na usahihi wa sheria za madini, endelea kupambana kudai utawala wa sheria, endelea kunadi maono yako kuwa Magufuli ni Rais wa muhula mmoja, halafu yeye anakupiga kwa vitendo tu.

Ni sawa Magufuli kuwapa kazi wapinzani maana nchi ni ya wote, lakini uteuzi wa Kitila na Mghwira siyo afya kwa ACT.

Pole Zitto. Sisemi kuwa Rais Magufuli anakukomoa au anakulipizia kisasi, ila kiukweli utamkoma. Nakuhurumia sana.

Ndimi Luqman MALOTO.
 
amkome mara nagapi, ni juzi tu alimsema anatuuzia ndege terrible teen, akaiacha na kutengeneza mpya, ni juzi tu katukanwa kuwa kuna watu wamepewa fedha kuwatetea accasia
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Aliyesikia Tamko la Zito kuhusu uteuzi wa M/Kiti wake atusogezee hapa
 
  • Thanks
Reactions: SDG
amkome mara nagapi, ni juzi tu alimsema anatuuzia ndege terrible teen, akaiacha na kutengeneza mpya, ni juzi tu katukanwa kuwa kuna watu wamepewa fedha kuwatetea accasia
Kama ni hivyo, basi Zito ni MTU mhimu sana kwa Taifa maana anambana Mkuu mpaka anashindwa kufanya mambo ya hovyohovyo. Kama kweli ilikuwa inunuliwe Terrible teen, baadae ikaachwa ikanunuliwa mpya ili kumkomoa Zito ! Nijambo jema maana tumepata kilichobora.
 
Kila nikijaribu kuvaa viatu vya mwanasiasa Zitto kabwe naona kuna kuandamwa na mitihani mizito ambayo inaleta kizungumkuti katika future yake kisiasa...naona anguko kubwa la ZITTO KABWE linakuja
 
Zitto yuko imara!!
Cdm mlimtupa sasa Mungu anamwinua - ni mbunifu na mlezi mzuri

Ukiona kwa muda mfupi tu katoa viongozi wa kitaifa wawili basi hiyo ni ishara njema kwake

Kubali ukikubali siasa ni dynamic na hii itawatesa cdm mnaofikiri ktk njia moja
 
Inasaidia vipi ACT. Juzi juzi hapa ZKK alitangaza kuwa ataungana na wapinzani wote. Hili tamko lilikuwa tishio pia kwa chama kubwa.
 
Hii inaitwa ombea adui yako aishi siku nyingi ili ukifanikiwa ajionee kwa macho. Zitto Kabwe ni msomi nguli ambaye hakuthamin sacrifices ambazo chama cha upinzani kinalazimika kuzifanya ili kiweze kuwa imara. Ni mtu aliyechukulia poa harakati na jitihada za chadema kwa kiburi cha usomi kwa sababu tu kawa maarufu na kapata mafanikio makubwa kuliko hata wakongwe kwenye siasa.

Kwa kuamua kujiunga na ACT, Zitto sasa atapata fursa ya kujifunza gharama ya kujenga chama kwa vitendo. Gharama yake haitakuwa ndogo, jasho na damu vitamtoka. Na hapa bado hatujafika uchaguzi wa 2020. Naamini baada ya 2020 hatakuwa na siasa za ushindani tena, bali siasa za kujikimu kimaisha kwa sababu uchaguzi wa 2020 ni vita ya giants, sio midgets.
 
Hii inaitwa ombea adui yako aishi siku nyingi ili ukifanikiwa ajionee kwa macho. Zitto Kabwe ni msomi nguli ambaye hakuthamin sacrifices ambazo chama cha upinzani kinalazimika kuzifanya ili kiweze kuwa imara. Ni mtu aliyechukulia poa harakati na jitihada za chadema kwa kiburi cha usomi kwa sababu tu kawa maarufu na kapata mafanikio makubwa kuliko hata wakongwe kwenye siasa.

Kwa kuamua kujiunga na ACT, Zitto sasa atapata fursa ya kujifunza gharama ya kujenga chama kwa vitendo. Gharama yake haitakuwa ndogo, jasho na damu vitamtoka. Na hapa bado hatujafika uchaguzi wa 2020. Naamini baada ya 2020 hatakuwa na siasa za ushindani tena, bali siasa za kujikimu kimaisha kwa sababu uchaguzi wa 2020 ni vita ya giants, sio midgets.
Masahahihisho Zitto alifukuzwa hakuhama.
 
Masahahihisho Zitto alifukuzwa hakuhama.
Kwa suala la Zitto, maneno kufukuzwa au kuhama yalikuwa na maana moja. Baada ya wazee wa chama kumzuia kugombea alipojaribu mara ya kwanza, mara ya pili alishakuwa ameamua kuwa lazima awe mwenyekiti wa Chadema au 'Mwenyekiti' wa ACT. Maana yake alikuwa na plan B, ndo maana alikuwa bold zaidi kuliko awali. Watu wenye akili kama Zitto huwa hawafukuzwi, 'kufukuzwa' ni mtaji wa kuianzisha ACT.
 
Mara tu baada ya kuteuliwa watu walianza kutaka kupata maoni ya mkuu wa chama cha ACT umwami Zitto. Naye alijitetea kwa kusema kamati kuu itakaa na kutoka na tamko.

Kabla hata ya kamati kuu kukaa na kutoa tamko tayari aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha ACT ambaye sasa ni mkuu wa mkoa akaapishwa.

Bila shaka Zitto alifahamu A-Z kuhusu uteuzi huo. Lkn ktk kutuliza wafuasi wake anajitia kutojua na kuandaa kikao. Hii ni zuga tu. Zitto anacheza na akili za watu tu hapa.

Chama chake kiliibuka kipindi cha uchaguzi kwa lengo moja tu, kupunguza kura za kawa. Malipo yake ndiyo haya. Kama mtakumbuka Zitto alianza kumkomalia sana JPM kwa kumkosoa kwa nguvu zake zote. Hii ni baada ya Zitto kuona kana kwamba ccm imegoma kutoa malipo kwa kazi aliyoifanya.

Vuteni subira muone rangi kamili ya Zitto baada ya viongozi wake 2 wa ngazi za juu kuingizwa ktk serikali ya JPM. Atakuwa mtetezi wa kila jambo.

Kwahiyo ACT imepata maana mpya:

Àkiba ya Chama Tawala (ACT)
 
Zitto bado hajakomaa kuongoza chama, lazima wamchezee. Asipoangalia naye atachotwa tu
 
Back
Top Bottom