Zitto, ungana na wapinzani wenzako...

Zitto, ungana na wapinzani wenzako...

Zito sio mjinga hivyo! mwaka jana wengine walitapeliwa ooohhh tuwe kitu kimoja badala yake amri inatoka cdm mnakuwa wanachama mnakufwata yao sio mliokubaliana.
 
Kiukweli siasa kwenye inchi imekuwa drama sielewi wap tunaelekea na sizani kama hii ndo njia yakutekeleza matakwa ya katiba katk inch
 
Tuanzie na majibu ya maswali haya kwanza:

1. Zitto anahitaji UKAWA au UKAWA inamuhitaji Zitto?

2.Zitto kwa UKAWA ni LIABILITY au ni ASSET?
 
Zitto rudi CDM, yule babu aliyekutoa nduki naye kashatoka nduki, huko uliko ni kama upo peke yako - hutasonga!!
 
CCM wana mkuu wa kitengo cha fitna,uchakachuaji na kamati za Ufundi, huyo mtu ana bajeti kubwa sana na akitaka pesa mda wowote anapewa toka Hazina,kazi yake kubwa ni kuwakoroga Wapinzani kwa kuwachonganisha,kuwahujumu kwa njia mbalimbali ili wakose umoja na kuaminiana kisha CCM wanapenya humo humo,January leo hii amekuwa bilionea kupitia Kitengo hicho kwani pesa nyingi inayobaki huishia tumboni mwake.
 
Zitto alishaonyesha mara kibao nia ya ACT kushirikiana na UKAWA, lakini Kila akiwaandikia barua washirikiane hawamjibu!. Sasa yeye afanyeje zaidi ya kwenda solo?

Pili ni ujinga kutaka kumfanya Zitto awe Subordinate wa Mbowe kwenye muungano wowote, ni lazima uwe muungano of equals bila kujali Chadema kwa sasa ni chama kikubwa kuliko ACT Wazalendo.
 
Zitto alishaonyesha mara kibao nia ya ACT kushirikiana na UKAWA, lakini Kila akiwaandikia barua washirikiane hawamjibu!. Sasa yeye afanyeje zaidi ya kwenda solo?

Pili ni ujinga kutaka kumfanya Zitto awe Subordinate wa Mbowe kwenye muungano wowote, ni lazima uwe muungano of equals bila kujali Chadema kwa sasa ni chama kikubwa kuliko ACT Wazalendo.
Utashirikianaje na chama chenye kiongozi mmoja?
 
Zito sio mjinga hivyo! mwaka jana wengine walitapeliwa ooohhh tuwe kitu kimoja badala yake amri inatoka cdm mnakuwa wanachama mnakufwata yao sio mliokubaliana.
CCM wana mbinu nyingi za kuwavuruga Wapinzani mfano sasa wamewekeza kwa Lipumba wanakula pesa za Umma kuanzia Msajili na Madalali wa siasa kwa kisingizio kuwa wanazitumia kuua CUF na kudhoofisha ukawa, kufa kufaana Wajanja CCM wanaishi kwa pesa ya kuwakoroga Wapinzani.
 
Upinzani umekosa agenda tena za kifisadi hehe sasa ime angalia fursa ikaona size mlopokaji kama mugabe hehehe ufisadi na kipi bora hehehe lakini angalieni msije nanyi mkawa walipokaji hasa tundu lissu mnyika kimyaa amewashika vibaya
 
CCM wana mkuu wa kitengo cha fitna,uchakachuaji na kamati za Ufundi, huyo mtu ana bajeti kubwa sana na akitaka pesa mda wowote anapewa toka Hazina,kazi yake kubwa ni kuwakoroga Wapinzani kwa kuwachonganisha,kuwahujumu kwa njia mbalimbali ili wakose umoja na kuaminiana kisha CCM wanapenya humo humo,January leo hii amekuwa bilionea kupitia Kitengo hicho kwani pesa nyingi inayobaki huishia tumboni mwake.

Hiyo pia ni mbinu ya kisiasa inahitaji magenius maana ingekuwa rahisi upinzani wangetumia
 
Wapinzani Tanzania wamekuwa mladi mzuri kwa Wajanja kule CCM kwani mda wote wanabuni mbinu mbalimbali za kuwasambalatisha Wapinzani wapate pesa toka hazina,Tanzania bila upinzani kuna watu watakufa njaa .
 
Wachaga watakubali au hiyo zit to anajisaulisha u mimi wa kaskazini watakubali lowasa ana taka yeye asimame yeye220 zit to utakubali ovyoooo upinzani bado sana tz m bwembwe tu hizo
 
Hiyo pia ni mbinu ya kisiasa inahitaji magenius maana ingekuwa rahisi upinzani wangetumia
Wapinzani hawana pesa lakini CCM wana serikali ni rahisi kuchota pesa hazina kimya kimya kama walivyofanya kwenye mkutano mkuu wa CCM baada ya kuwa umekwama kwa kukosa pesa, mkuu wa Kitengo February huchota pesa hata toka kwa wahindi matajiri wanachama wa CCM na hata wale wasio na chama.
 
Mimi nadhani isitumike nguvu kubwa kumshawishi Zitto kutambua hilo Bali itumike nguvu kuwafumbua macho watu walio ndani ya Ccm kuondoa woga na kumpinga yule bwana hadharani kwa afanyayo.
Ni wazi kuwa hata ndani ya chama chake wengi hawakubaliani na afanyayo bali wanaishi kwa hofu tuu hivyo hadharani kumuunga mkono.lakini sio moyoni. Hata yule mama makamu wake na kiranja wa mjengoni hawako radhi naye
 
Mnajitoa fahamu tu,hivi mmeisha sahau kwamba zitto(ACT) aliwaandikia UKAWA kuomba kujiunga nao na hajajibiwa mpaka leo.
 
Mnafiki tu huyo, yeye ana sababu zake Binafsi za Kumchukia Magufuli, sasa hivi kapata loop holes za kupitisha malengo yake,
siku ile ya raisi kulihutubia Bunge, wabunge wote wa UKAWA walifukuzwa yeye akabakia na Raisi akamsifia kuwa ni mwanasiasa mkomavu na yeye akabaki kukenua meno tu

Wenzie walishayaona Mapungufu ya JPM yeye akuyaona?, iweje leo umshauri aingie kwenye huo UKAWA?
Unaonaekana unapenda sana kulishwa siasa za chuki badala ya wewe mwenyewe kuwa objective!! Unatia aibu unapohusisha siasa na chuki binafsi... unaweza kutuambia hizo sababu binafsi unazodai ndizo zinamfanya Zitto "amchukie" JPM?

Mosi, hivi sababu ambazo zilipelekea UKAWA kutolewa nje ni kwa sababu ya Magufuli personally au ilikuwa kuonesha kwamba hawakukubalina na mchakato wa upigaji kura ambao hatimae ulimwingiza JPM madarakani?!

Btw, alikuwa na sababu gani za leo kuonesha unafiki kwamba humkubali xyz kwamba ni rais halafu kesho unaenda kwa huyo huyo uliyemkataa?! Hata huyo JK ambae kwa unafiki wa watu hapa wanajifanya kumkumbuka, CHADEMA hawakutoka bungeni siku JK anaenda kufungua bunge?!

Pole sana kumbe ni mfuasi wa political drama!

By the way, hivi kabisa kabisa unaamini kinachomsukuma Zitto ni chuki dhidi ya JPM? SERIOUSLY? Yaani yanayopingwa yapo wazi kabisa na yanaweza kuonekana hata na mtoto mdogo lakini bado kuna watu mnaamini hizo ni chuki tu za Zitto dhidi ya JPM?!

I hate to say this but what I sense ni chuki zako dhidi ya Zitto kwavile ulishazoea kulishwa siasa za chuki!

Ni kweli Zitto Kabwe mwanzoni alikuwa anamuunga mkono JPM pale JPM alipoonesha nia ya kupambana na ufisadi!! Binafsi, nilimuunga mkono JPM kwa 100%. Sasa ni nani mwenye akili timamu ambae anaweza kuacha kuunga mkono vita dhidi ya ufisadi? Kinyume chake, wewe ulitaka zile siasa za kijinga za kupinga kila kitu!!!!!

Kwa kumbukumbu zangu, Zitto alianza kutofautiana na serikali ya JPM lilipoanza suala la Bunge Live na upigaji marufuku wa mikutano ya kisiasa!!

Sasa ni nani mwenye akili timamu ambae angeunga mkono ujinga kama huo?! Kwahiyo kwa akili yako, pale Zitto alipoanza kupinga masuala ya wazi kabisa kumbe hiyo ni chuki binafsi dhidi ya JPM?!!

Tofauti yako na Zitto na hii: Wakati watu kama nyinyi mmekula yamini kuunga mkono X na kuipinga Y no matter what, Zitto ataunga mkono na kupinga kutegemeana na hali halisi na sio kupinga tu kama mwehu na kuunga mkono tu kama kipofu!!!
 
Mnafiki tu huyo, yeye ana sababu zake Binafsi za Kumchukia Magufuli, sasa hivi kapata loop holes za kupitisha malengo yake,
siku ile ya raisi kulihutubia Bunge, wabunge wote wa UKAWA walifukuzwa yeye akabakia na Raisi akamsifia kuwa ni mwanasiasa mkomavu na yeye akabaki kukenua meno tu

Wenzie walishayaona Mapungufu ya JPM yeye akuyaona?, iweje leo umshauri aingie kwenye huo UKAWA?
Hivi nikuulize Zitto akiletwa na Mbowe ndani ya ukawa wewe utamzuia?......

Kumbuka hata lowassa mlikuwa mbamtukana hivyo hivyo lakini alipokuja mkamsafisa............

Uliona Obama na Hillary walivyokuwa wakigombana 2008 lakini juzi Obama ameach ikulu na kwenda kumpigia kampeni Hillary.......

Mtu kama Trump anasima kwenye kapeni anawaambia watu kuwa akishinda anamshitaki Hillary watu wanamshangilia lakini baada ya kushinda anasema sitafanya hivyo pia hao hao wanamshangilia .........

Sasa hivi umoja Wa ulaya unaweka vikwazo Kwa Burundi Kwa Rais kuongeza muhura Wa tatu wakati Chancellor Wa ujerumani anataka kujiongezea muhura Wa tatu lakini huko kwao ni sawa tu lakini Kwa Burundi si sawa.....

Hiyo ndio siasa, siasa ni unyumbu mtupu.............

Ndio maana watu wengine tulijitenga na siasa za vyama tunapenda watu personally akifanya vizuri tunampongeza akikosea tunamwambia ukweli ........

Kiufupi siasa ni ngumu sana duniani kote ............
 
Hivi nikuulize Zitto akiletwa na Mbowe ndani ya ukawa wewe utamzuia?......

Kumbuka hata lowassa mlikuwa mbamtukana hivyo hivyo lakini alipokuja mkamsafisa............

Uliona Obama na Hillary walivyokuwa wakigombana 2008 lakini juzi Obama ameach ikulu na kwenda kumpigia kampeni Hillary.......

Mtu kama Trump anasima kwenye kapeni anawaambia watu kuwa akishinda anamshitaki Hillary watu wanamshangilia lakini baada ya kushinda anasema sitafanya hivyo pia hao hao wanamshangilia .........

Sasa hivi umoja Wa ulaya unaweka vikwazo Kwa Burundi Kwa Rais kuongeza muhura Wa tatu wakati Chancellor Wa ujerumani anataka kujiongezea muhura Wa tatu lakini huko kwao ni sawa tu lakini Kwa Burundi si sawa.....

Hiyo ndio siasa, siasa ni unyumbu mtupu.............

Ndio maana watu wengine tulijitenga na siasa za vyama tunapenda watu personally akifanya vizuri tunampongeza akikosea tunamwambia ukweli ........

Kiufupi siasa ni ngumu sana duniani kote ............

Kwa nini unaninasibisha mimi na Ukawa?

Kweli siasa ni ngumu, ila ya Tanzania ni kiboko, imejaa unafiki kuliko maelezo, Hivi mtu kama Lipumba nae utasema ni mpinzani?
 
Back
Top Bottom