Zitto: Tusimpelekeshe sana Rais Samia, tumpe muda

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameingia madarakani kutokana na msiba, hivyo asipelekeshwe sana na badala yake apewe muda

Ameeleza Samia ambaye awali alikuwa Makamu wa Rais hakujiandaa kuwa Rais, bali msiba umetokea na amechukua mamlaka kwa mujibu wa Katiba

Aidha, amesema kuna masuala ambayo ni mapendekezo ya watu wengi Rais ameanza kuyachukulia hatua. Ameeleza, ni muhimu Rais kutafuta wataalamu ili kutazama namna ya utekelezaji wa bwawa la Mwalimu Nyerere, SGR, uboreshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na mengineyo
 
Hapa Jambo la Msingi ni Mchako wa Katiba Mpya, Maswala ya Mibunge ya CCM ya darasa la Saba kuingia bungeni kwa Mbereko ya Mwendazake Liliiumiza nchi sana, Issue hapa ni kudeal na Katiba Maana Kwa katiba hii tuliyonayo Mibunge ya CCM inaona imeshajitwalia umiliki wa nchi hii.
 
Ukishakua Makamu wa Rais unahitaji kujiandaa nini tena wakati Katiba iko wazi? Maneno haya angesemewa Mh Mpango tungeelewa hakuna kujiandaa kuwa Makamu wa Rais maana ni yeyote mwenye sifa hizo katika muda husika anaweza kuteuliwa. Ila kwa Makamu wa Rais kuassume kazi ya Urais si hivyo analazimika kwa mujibu wa Katiba maadamu hakusema kikombe hiki kiniepuke.

Katika utendaji wake Mh Rais na hili na rudia tena kumnasihi, Hayati JMP kafa mwili tu lakini anaishi katika nyoyo za Watanzania walio wengi isipokuwa majizi,mafisadi na mawakala/wapambe wao, hili haliepukiki. Huyu ni zaidi ya ule wimbo wa " Kama isinge kuwa juhudi zako Nyerere..." Ambao Watanzania wakidhulumiwa huimba wakiwa wamejikunyata ili kujifariji. Kwa Hayati JPM hawataimba tena kama watoto yatima na kujikunyata watachukua hatua za kutenda kwa ujasiri.
 
Ukishakua Makamu wa Rais unahitaji kujiandaa nini tena wakati Katiba iko wazi? Maneno haya angesemewa Mh Mpango tungeelewa hakuna kujiandaa kuwa Naibu wa Rais maana ni yeyote mwenye sifa hizo katika muda husika abaweza kuteuliwa. Naibu wa Rais si hivyo analazimika kwa mujibu wa Katiba maadamu hakusema kikombe hiki kiniepuke.

Katika utendaji wake Mh Rais na hili na rudia tena kumnasihi Hayati JMP kafa mwili tu lakini anaishi katika nyoyo za Watanzania walio wengi hili haliepukiki. Huyu ni zaidi ya ule wimbo wa " Kama isinge kuwa juhudi zako Nyerere..." Ambao Watanzania wakidhulumiwa huimba kujifariji. Kwa Hayati JPM hawataimba tena kama watoto yatima watachukua hatua za kurenda kwa ujasiri.
Labda alitaka apigiwe simu, Zitto ni mchumia tumbo kama akina Mwigulu na CCM wenzake
 
MAMA YETU RUDISHA FAO LA KUJITOA..Zitto atuache kwanza yeye kama mbunge mstaafu alipewa mafao yake kila muhula unapoisha...ila kuna kijana anaambiwa asubiri azeeke ndo apewe hela yake akiwa mzee..ili imsaidie nini? Aache watu watoe maoni yao ...Rais ni Taasisi sio yeye atayafanya anaweza agiza watu wake wafanye .....
 
Zito anaamini kuna watu wanamsikiliza mpaka ageuke kuwashauri? Anaposema mama alikuwa makamu hivyo hakujiandaa kuwa rais, ni sawa na mchezaji yuko benchi, kisha aliyeanza akashindwa kuendelea na mchezo, halafu aseme haukuwa amejiandaa kucheza!

Zito anajiwekea mazingira ya kuwa karibu na mama ili afaidike na madaraka yake. Ndio maana chama chake kiko kwenye uchaguzi wa marudio huko Muhambwe, wameambiwa na tume ya uchaguzi wasitishe kampeni hadi may 1, na kweli wamesitisha ili waonekane ni watiifu, kisha wapewe hilo jimbo kwa hisani ya mama.
 
Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameingia madarakani kutokana na msiba, hivyo asipelekeshwe sana na badala yake apewe muda

Ameeleza Samia ambaye awali alikuwa Makamu wa Rais hakujiandaa kuwa Rais, bali msiba umetokea na amechukua mamlaka kwa mujibu wa Katiba

Aidha, amesema kuna masuala ambayo ni mapendekezo ya watu wengi Rais ameanza kuyachukulia hatua. Ameeleza, ni muhimu Rais kutafuta wataalamu ili kutazama namna ya utekelezaji wa bwawa la Mwalimu Nyerere, SGR, uboreshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na mengineyo
Mbona JPM haukumpa muda? Zitto huo udini wako hauna tija kwa Taifa. Ni haki kumpa muda Mama lakini wewe siyo msemaji wa Ikulu wala serikali au hata siyo msemaji wa CCM. Jifunzeni kuwa mnaficha upumbavu wenu. Msifikiri waTanzania wote huwa hawafikiri. Mwambie na mpuuzi mwenziyo Assad.

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameingia madarakani kutokana na msiba, hivyo asipelekeshwe sana na badala yake apewe muda

Ameeleza Samia ambaye awali alikuwa Makamu wa Rais hakujiandaa kuwa Rais, bali msiba umetokea na amechukua mamlaka kwa mujibu wa Katiba

Aidha, amesema kuna masuala ambayo ni mapendekezo ya watu wengi Rais ameanza kuyachukulia hatua. Ameeleza, ni muhimu Rais kutafuta wataalamu ili kutazama namna ya utekelezaji wa bwawa la Mwalimu Nyerere, SGR, uboreshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na mengineyo
*TUHUMA ZA MBOWE ZINAACHA MASWALI MENGI.
*
Mbowe kabla hata ya kujisafisha na uongo wake wa kulewa na kuangushwa na konyagi nyumbani kwa hawara Joyce Mkuya kisha kulitangazia taifa kwamba amepigwa na wasiojulikana, amekuja na igizo jingine kwamba alifilisiwa na akaunti zake zote zilifungwa na TRA!!

Kama ni kweli alikuwa wapi kuyasema haya? Badala yake akawa anaitisha press conference akiwa amevaa gloves feki huku akiwa amejifungia kwenye lockdown hewa.

Ina maana Mbowe alikuwa tayari kuita waandishi wa habari na kuwaelezea alivyokimbia bunge na kwenda lockdown uchwara kuliko kuwaelezea alivyofungiwa akaunti zake zote ikiwemo ya mshahara?

Mbowe hili ni taifa la watu wanaojitambua na kamwe hutafanikiwa kwenye hiyo biashara yako mpya uliyokula 10% ili ulete chanjo ya corona nchini.
 
Back
Top Bottom