Zitto na PAC yake waliteleza?


Mkuu mbona skuelewi?
hebu nifumbue macho mwenzio kipofu hivi nisheria ipi inasema mikataba ya rasilimali za nchi ni siri ya serikali?.
 
Uko smart mkuu ile ni drama huyu msaliti anatumia kila njia kujibua lakini ndio keshapima kina cha tope kwa miguu miwili, atajaribu kila aina ya u-senge lakini hataweza kujiokoa.

Akili yako nindogo mno!!!
hivi unahisi hao unao ona c wasaliti wana mzidi uwezo wakujenga hoja zitto?
acha ujinga wa kumezeshwa chuki na wajinga ...kaa chini umiza kichwa kutafiti ujuee ukwel..

kipindi kile zitto katangaza kuwania urais kupitia chadema mli mezeshwa sumu eti ana vuruga chama na ni msaliti wapumbavu mka kubali kauli za mazuzu..
hapa juzi Tundu lisu amesema anaweza kugombea uraisi kupitia chadema hakuna mbwa hata mmoja alie sema Lisu ni msaliti..ila ipo sku tuta ujua ukweli.
 

We kweli akili hazikutoshi....kama anapindisha sheria kwa maslah ya nchi we unaumia nn?
Au ulitaka apindishe sheria kwa maslah binafsi ndo umuone mzuri?...yaan kuna mijitu mingine huwa c ielew ni mitanzania au mikenya...hayana jema hhata sku mmoja kila linalo fanywa na zitto kwao ni nongwa afanyej ili mlizike?
 
Ni ukweli ulio dhahiri kuwa mambo haya yanafanyika maksudi na wanaofanya hivi wanafanya maksudi kwa sababu wamezoea kutumika,lengo nikutupoteza katika swala ka msingi la katiba,ndio maana huwez kusikia yule jamaa akizungumzia swala la katiba...
 
Na huo ndo ukweli Zitto alikuwa anatafuta "comeback" imegoma!

Unatuhamisha kiboyo Aiseeee... Ishu ni Mikataba, na sio Ujio wa Zitto... Tunapoteza Energy kubwa kujadili MTU mmoja, badala ya Kuumiza kichwa kwenye Mambo Ya Msingi, Huu Ni Ujinga.
 
kwanza inaonyesha kila dalili kuwa wale jamaa waliandaliwa kiaina kabisa kwamba watapelekwa polisi then wataachiwa, inaonyesha huo mpango uliandaliwa mahsusi tangu awali ili kuanza kuliinua jina la msaliti juu, bahati mbaya halijainuka,

Hivi watu kama huyu ni Great Thinker au ndio ......!!!
 
Hivi watu kama huyu ni Great Thinker au ndio ......!!!

Hii sio issue ya kuthink,ni issue ya ku observe.

Jamaa wamepelekwa mahakamani au bado polisi wanafanya uchunguzi?
 

Sisi hatuangalii anachokisema huyo mjinga wenu tunaangalia anachokifikiria.

Jipangeni.
 

Mkuu mikataba alisaini prof KJ alipokuja prezidaa wa China kama unakumbuka,sasa kama wanaitaka c wangemuuliza mukulu ametunza wapi?au prof muongo?hao jamaa wameonewa sababu wanauwezo wa kumbana waziri wa nishati na madini bungeni!
 

Mkuu kwani hujui TPDC wako chini wa wizara ya nishati na madini na maelekezo yanatoka huko?kwanini waziri mwenye dhamani asibebeshwe mzigo wa kuleta mikataba bungeni?mikataba alisaini mkuu wa kaya alipokuja prezidaa wa china na mwanasheria Mkuu alikuwepo kwanini hao wasiiweke wazi kwa wananchi tukaijua?Napinga hao watu kukamatwa sababu wenye mikataba wanajulikana!
 
Hivi Wadau , ktk katiba inayopendekezwa suala la mikataba limewekwaje? Maana mikataba ya rasilimali ya nchi inabidi iridhiwe na Bunge kwa niaba ya wananchi.
 

Nimekuelewa Mkuu..
 
Mkuu mikataba alisaini prof KJ alipokuja prezidaa wa China kama unakumbuka,sasa kama wanaitaka c wangemuuliza mukulu ametunza wapi?au prof muongo?hao jamaa wameonewa sababu wanauwezo wa kumbana waziri wa nishati na madini bungeni!

So wamefanya Ze comedy show ....kuchukulia Kiki wakijuwa wazi mikataba ufunguo kwa baba
 
Ahsante mkuu. Kama watu wangekuwa wanachangia kama wewe, this way, jukwaa hili lingekuwa na maana maradufu. Ahsante sana kaka. Sina la kuongeza

 
Nakumbuka zitto aliomba mwongozo kwa mwakilishi wa katibu wa bunge ambae wakiambatana nae kuhusu hili swala. Na huyo mwakilishi wa katibu wa bunge alisema PAC ina haki ya kuzipata hizi nyaraka zilizoombwa.
 

Sangarara,

Acha kukurupuka, unatakiwa usome mwanzisha uzi huu amejadili nini na mimi nimemjibu nini.

Kama umemsoma vizuri mtoa mada amesema akina Zito na PAC hawana mamlaka ya kuwafikisha wale viongozi wa Polisi na akatoa mpaka na kifungu cha sharia.

Mimi nimemjibu hata PAC wana mamlaka hayo kwani hawakukurupuka bali walipokea maelekezo hayo toka kwa wanasharia wa bunge na mmoja wa wanasharia hao alitoa ufafanuzi hapo.

Sasa kumbuka kila mtu ana haki kwa maana PAC au Bunge na watuhumiwa waliodhalilishwa kama alivyobainisha mtoa mada.

Mimi nikatoa hitimisho kuwa kama hawakuridhia na maamuzi ya PAC ambayo hatima ya kuwafikisha mahakamani ipo kwa SPIKA basi na wao wana haki ya kulishitaki Bunge (PAC ni kamati ya Bunge) kwa kuwadhalilisha.

nafikiri nimekupa mwanga kidogo wa muradi wa andiko langu.

Usikubali kuongozwa na chuki wala ushabiki utateteleka kiumsimamo.

Pole sana

 

Kisa zitto roho mbaya itakua
 

Mkuu

Nashukuru kwa maelekezo yako.

Lakini naomba nikuweke sawa, mimi sichangii hapa kishabiki, Lakini natambua kwamba msimamo wangu juu ya Zitto ni Negative, na sidhani kama hilo ni Kosa.

Sasa turudi kwenye hoja yako?

Unamaanisha kwamba Mwanasheria wa Bunge aliwapa akina uzito ushauri kwamba wanaweza wakaruka taratibu za kupeleka mahitaji yao kwa speaker ili ayawasilishe serikalini na hata kuruka ngazi zingine za kiserikali na kwenda moja kwa moja polisi? sababu hicho ndio walichokifanya kina Zitto.

Na Je, lengo lao la kuwaitia jamaa polisi ni nini? Wote tunajua polisi ni njia tu ya kufika mahakamani, sasa PAC walikuwa wamechukua maamuzi ya kuwapeleka jamaa mahakamani?

Ndio maswali yangu hayo, labda ungenijibu na mimi, sababu majibu yako kwa mleta mada nimeyaelewa.

Ama sivyo kama issue imeisha, inabidi tujue lengo lilikuwa ni nini? Sababu kama waliteleza Je, wameanzisha mchakato stahili? Kama hawajaanzisha ni kwa nini? au wameishapewa hiyo mikataba?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…