Sioni kama ni tatizo mradi wao wote January, Zitto na Said Bagaile wanapigania maslahi ya Taifa. Acheni majungu
Zito anajibagua sana na wana mabadiliko wenzake,tulisha mzoea yule,nafikiri udini unamsumbua sijui kwa nini asirudi ccm
Jamani wadau mimi ninawasiwasi sana na ukaribu na utendaji kazi wa Zito Kabwe yaana urafiki aliokuwa nao na wanamagamba unatia wasiwasi suala moja lakujiuliza kwanini asishirikiane na watu
kamaMnyika,lema,msigwa,kasulumbayi,mbilinyi na makamanda wengine huu ukaribu wake na wakina January na kigwangala hatusemi wawe maadui ila tu kisiasa ukifanyakazi na watu mnaotofautiana itikadi hasa ikiwa wapo wenzako ambao mnaitikadi sawa wengi tu unaoweza kufanyanao kazi inatia sana mashaka lakini pia kuna dalili ya agenda ya chinichini kuunganisha nguvu hii ni kwa maslahi ya naani? NAWEKA WAZI MASHAKA YANGU ILI KUWEKA KUMBUKUMBU VIZURI JUU YA HILI
Hakuna ubaya wowote Zitto kufanya kazi Janauri, kinachotakiwa ni kuwa mzalendo na nchi yako kwa mustakabali wa taifa letu.
Lack of credibilityWana JF
Mimi ni miongoni mwa wale wanao amini kuwa siasa kati ya vyama na vyama si uadui bali ni kutofautiana kwa hoja katika kusukuma gurudumu la maendeleo. Hivyo ni muhimu kwa wanasiasa wetu wapingane kwa hoja lakini yanapokuja katika kusimamia maslahi ya taifa wayasimamie kwa pamoja bila kujali itikadi zao. Pia si vibaya kwa wanasiasa wetu kushirikana iwe kwa wale wa upinzani na wa chama tawala.
Bada ya kusema hayo nataka kutoa angalizo kwa CHADEMA juu ya ushirikiano wa kisiasa kati ya Makamba na Zitto niseme tuu huu ni mtazamo wangu naweza kuwa sahii au laa. Ukitazama kwa sasa juu ya harakati za kisiasa za hawa mabwana ni kama vile utadhani wako chama kimoja,huoni wakipingana kwa hoja wao kwa wao pia utaona kuwa vyombo vyote vya habari vile vinavyoshabikia propaganda mbovu kwa CHADEMA kama Jombo leo, TAZAMA, na Clauds FM vipo mstari wa mbele katika kuwashabikia hawa wawili kwa mfano ukiridi kwenye suala la posho za wabunge utaona kuwa CHADEMA na wabunge wake wote wamekuwa wakipinga hoja ya poshao za wabunge hadharani sijawahi kumwona Januari akipinga jambo hilo nje ya vikao vya bunge lakini imejengwa dhana na vyombo hivi vya habari kuwa hawa tuu ndio wapingaji wa suala la posha katika msingi huo ndipo ninapojenga hisia na angalizo kwa CHADEMA kuwa makini na urafiki huu yawezekana ukawa ni mkakati maalumu wa CCM kumbuka wamesema wamefungulia mbwa kwa sasa na hakuna kulala mpaka 2015.Nirudie tu niseme huo ni mtazamo wangu naweza kuwa sahihi au kinyume chake na hili ni angalizo tuu.
Wote hapo ni corrupt leaders ndio maana wanajidai kupinga posho huku wakijua kuna mahali wanavuta pesa kisirisiri.Mkuu kwenye itikadi hapo; Zitto na January wana itikadi moja in common: Wote wanapinga posho za vikao ila hao makamanda wengine unaosema hawana nia thabiti ya kuzipinga posho.