Zitto, Makamba wautaka urais?

Tusiwe kama punguawani wa akili. Hivi Zitto angeongoza ujumbe wa CDM kumuona Rais kuhusu mapendekezo ya rasimu ya katiba si ndio mngesema kuwa anajipendekeza kwa Rais. Nashukuru Zitto hakuwepo na waliokuwepo ni wale mnaoamini ndio CDM damu. Kila jambo akifanya Zitto na watu wa CCM bila nyie kuangalia manufaa yake kwa taifa anaonekana msaliti, kwanini tumefikia hapa?. Ama kweli waswahili walisema 'Kunyata anyate kinyonga, akinyata kicheche anavizia kuku'. Zitto nakusihi kuwa endelea kuweka mbele maslahi ya taifa, sababu watu hawajui kuwa unatekeleza maslahi ya chama chako CDM.
 
Kadhalika, Zitto, aliwaasa vijana kuachana na siasa za kulalamika bila ya kutoa majawabu ya matatizo wanayoyalalamikia na kwamba enzi hizo zimepitwa na wakati.

"Siasa za vijana wa sasa ni za kutoa masuluhisho ya kukabiliana na changamoto zilizopo bila ya kuangalia itikadi za kivyama, kama ambavyo tumekuwa tukifanya mimi na Makamba katika mambo ya msingi yenye maslahi kwa nchi. Ni lazima palipo na maslahi ya nchi, tusimame pamoja kwa kuwa bila ya kufanya hivyo, watu wengine watatusemea," alisema.
Hapa ndipo ninaposhindwa kuwaelewa wanasiasa!
 
Mavijana kama haya yanapoanza kuonyesha uchu wa madaraka mapema hivi napata shaka. Kuna mengi ya kujadili sasa kupunguza umri wakupiga kura ndo nini! kutoka 18 hadi 16! upuuzi kabisa. Hili ndo tatizo la democrasia nchi hii!? ukiwa kwenye mfumo wa kimaandazi unakuwa maandazi tu, huyu Zitto nae aangalie asidhani kafika, atashangaa
 
Sioni sababu ya kuweka umri wa kugombea urais uanzie miaka 40.Ni vigezo gani vinatumika kuweka age limit?Najua kuna baadhi ya wazee na vijana wenye fikra mgando watakaopinga hili.Huwezi kupinga notion ya kizuzu kwamba vijana ni taifa la kesho kisha ukaendekeza hoja ya age limit iwe miaka 40,huko ni kutokujitambua.

Naamini katika uwezo wa mtu lakini pia umri ni kigezo muhimu.Nikipewa watu wawili wenye uwezo sawa (ceteris peribus) basi nitachagua mmoja ambaye ni the youngest among the two....!

Unaweza vipi kupima uwezo wa watu wawili na kufanya uamuzi kuwa wana uwezo sawa. Dunia hakuna mtu anafanana na mwingine katika uwezo.

Ni kama unaweza kupiga uwezo, je ni sababu gani zitakufanya uchague the youngest?
 
Yaache magugu na ngano vikue pamoja. Wakati wa mavuno, ndipo Bwana wa Mavuno atakapo ibagua ngano na magugu, na atayafunga magugu matita matita na kuyatupa motoni, na ngano ataihifadhi katika ghala lake. Hapo ndipo kitakuwa ni kilio na kusaga meno.

Amini nawambieni, kizazi hiki hakitapita kabla ya utabiri huu kutokea.

Mwenye masikio na asikie.
 
Tutatayaona na kuyasikia mengi kutoka kwa Zitto .Sio yeye anayekanusha kila kukicha kuwa hataki urais 2015 kwa kuwa kipindi hicho atakuwa na miaka 39!!!!?
Sasa hizo ni strategic mpya.Ila apewe nafasi ya kuelezea anayofikiri kichwani mwake tutamuhukumu kwa kauli zake muda ukifika
 
Sioni sababu ya kuweka umri wa kugombea urais uanzie miaka 40.Ni vigezo gani vinatumika kuweka age limit?Najua kuna baadhi ya wazee na vijana wenye fikra mgando watakaopinga hili.Huwezi kupinga notion ya kizuzu kwamba vijana ni taifa la kesho kisha ukaendekeza hoja ya age limit iwe miaka 40,huko ni kutokujitambua.

Naamini katika uwezo wa mtu lakini pia umri ni kigezo muhimu.Nikipewa watu wawili wenye uwezo sawa (ceteris peribus) basi nitachagua mmoja ambaye ni the youngest among the two....!

Nadhani mambo mengi huwa yanafanywa na kuwekewa baraka za maamuzi pale ambapo tafiti za kina zimefanyika na suluhu zikawekwa bayana kulingana na ukweli uliyopatikana.Kwa mtazamo wangu sizani kama ni sahihi kutokuwa na kigezo cha umri,tunaposema watoto kuna tafiti zilishafanyika kuwa umri wa miaka _ mpaka_ ni mtoto hali kadhalika kwa watu wazima hivyo hivyo.Tafiti gani zilizofanyika mpaka kuwaweka mtu mwenye umri wa miaka 35 na 40 kuwa wapo sawa kimawazo na kimtazamo wa kimawazo?.Huwa kuna watu hususani vijana waliyopata nafasi ya kusikika wanajaribu kupindisha mambo kutokana na uelewa wao kwa manufaa yao.Hii zana ya umimi kwa zama hizi inabidi ipigwe vita tena kwa nguvu zote.Naamini kamwe hawa wenye fikra na mitazamo ya umimi hawatachukua round wataanguka vibaya sana.

Tukisema umri wa kugoombea uwe miaka 35 utawagundua haraka sana hao naowataja kuwa wananafasi ila wanatumia philosophy ya umimi na kwa nini watu fulani walikuwa wanang'ang'ania hii hoja.Yote haya yanaendana na umri kwani tafiti zimefanyika na zikawakusanya watu wa umri fulali kutokana na tabia zinazoshabihiana pia mabadiliko ya kibiolojia.Ni kweli kuna baadhi ya watu wana umri mdogo ( 30-40) na wanakuwa wamekomaa kifikra na hata maamuzi yao yanatija zaidi ta wazee (45-65).

Ila si vyema kundi fulani likawa linashawishi mambo ambayo yanaoonekana wazi yanataka kuwafaidisha wao binafsi ,hii ni sumu kali sana kwa maendeleo hususani jamii ambayo inaelekea kwenye mabadiliko ya kujikomboa kifikra na kiuongozi.Hakika kila jambo lazima lifuatwe kulingana na mitazamo chanya, yenye tija kwa jamii kwa ujumla na si kwa mtu mmoja mmoja. Hili swala la umri linaonekana kama vile ni suala dogo ila kama wanaharakati na watu wenye mitazamo ni vyema kulijadili kwa umakini sana.
 
Jamani Zitto ni kigeugeu. Huyu jamaa ni mmojawapo wa vijana watiivu sana kwa Jk. Nyote mnajua namna alivyojipambambanua kwa wingi kuitetea urais wa JK baada ya uchaguzi 2010 ikiwa ni pamoja na kidai kuwa kura za Dr. Slaa hasijachakachuliwa. Huyu jamaa hana uwezo wa kuongoza nchi kwa level ya urais, maana hana mzimamo na ni mmoja wana cdm wanafaida walau makombo ya ufisadi kwenye secta ya madini. Huyu jamaa kama atapitishwa na cdm kugombea urais kwa tiketi ya cdm basi cdm kushney!!!
 
Uwezo mdogo wa kufikili na ufahamu mdogo kuhusu multiparty system , kuwa vyama tofauti haina maana mnatofautiana kila kitu, makamba na zito wana common understanding katika issue nyingi zenye maslahi ya taifa hili.
nyie ndio wale wae mnapinga tu hata kama jambo lina maslah na taifa.
 
Elezea, siyo unaandika kwa ufupi. Na si kila mtu atajua ulichoandika, sisi tunatumia kiswazi kwa mawasiliano, hivo uloandika ni uchafu kwa sababu maneno ulopigia mstari yameandikwa kiswahili, nawe jibu hivo.
Lack of credibility
 
Ujumbe wa Zitto huu hapa!

Baadhi ya vyombo vya habari vimehusisha kauli yangu ya kutaka kupunguza umri wa kugombea urais na mimi ‘kuutaka urais’. Mimi nikiwa mwanachama na kiongozi wa chama chama changu cha CHADEMA naelewa na kuziheshimu taratibu na kanuni tulizojiwekea za kuomba nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo nafasi ya urais. Nafasi ya uongozi ndani ya CHADEMA haiombwi kwenye warsha. Iwapo chama change, wakati muafaka ukifika na kutokana na matakwa ya jamii, kikiona nipewe jukumu lolote sitasita kutekeleza wajibu huo niwe au nisiwe mgombea.2. Kwa hivyo, nilichozungumza jana ni kutoa maoni yangu kwamba muda umefika kwa Taifa letu kupunguza umri wa kugombea urais. Maoni yangu haya yanatokana na ukweli kwamba hakuna sababu zozote za kisayansi zinazomfanya mtu aliye chini ya umri wa miaka 40 akose sifa za kuwa Rais. Msimamo huu nimekuwa nao tangu zamani nikisoma shule na haujawahi kubadilika. Hakuna mahala popote katika maoni yangu niliyotoa jana niliposema kwamba nataka umri wa urais upunguzwe ili nipate fursa ya kugombea nafasi ya urais. Pia siwezi kutaka katiba iandikwe kwa ajili yangu. Vilevile kamwe isionekane kwamba matakwa ya muda mrefu ya vijana ya kutaka umri wa kugombea Urais kupunguzwa yanalenga kunipa fursa mimi kwani mimi ni binaadamu naweza nisiwe na sifa za kuwa Rais lakini kukawa na vijana wengine wengi wenye umri chini ya miaka 40 wenye Uwezo na Uzalendo wa kutosha kushika usukani wa nchi yetu. Ni maoni yangu kwamba tupate mabadiliko ya vizazi katika uongozi wa nchi yetu ili kukabili changamoto za sasa zinazokabili Taifa letu.3. Tunapojiandaa kutoa maoni kuhusu Katiba Mpya ni vizuri vyombo vya habari vikajikita kutoa taarifa bila kuweka tafsiri au kuwatafasiria maoni ambayo wananchi na viongozi watakuwa wanayatoa kuhusu maudhui ya Katiba Mpya.Dar es Salaam29 Februari 2012

From Michuzi blog
 
Ndio ukweli wenyewe kuna mkakati maalumu kuna picha inachorwa Zitto alikuwa Tanga jee Lushoto kwa maana ya Bumbuli alifika,think twice
 
Naomba mfahamu ki2 kimoja kuwa nili neno"MUSTAKABALI WA TAIFA" ndio lilomzika seif ahmad na cuf yake, kumbuka mrema naye alipokuwa upholder wa ili neno na sasa yupo wapi, hebu kumbukeni moto wa zitto kabla ya hapa alipo, pia ni huu mstakabli wa kipumbafu ambao mnaita wa kitaifa ndo ulomfanya zitto azidiwe kura za mtandaoni na na kamanda Lema" so hiyo ni ishara ya madhara ya hii sumu ambayo mmeibatiza jina na kuiita eti ni mstakabali wa taifa.
 
Source: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Kampeni ya kupunguza umri wa urais haina uhusiano na mimi kutaka kugombea urais 2015 « Zitto na Demokrasia


KABWE ZUBERI ZITTO,
MP
KIGOMA KASKAZINI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kampeni ya kupunguza umri wa urais haina uhusiano na mimi kutaka kugombea urais 2015
Baadhi ya vyombo vya habari vimehusisha kauli yangu ya kutaka kupunguza umri wa kugombea urais na mimi ‘kuutaka urais'. Mimi nikiwa mwanachama na kiongozi wa chama chama changu cha CHADEMA naelewa na kuziheshimu taratibu na kanuni tulizojiwekea za kuomba nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo nafasi ya urais. Nafasi ya uongozi ndani ya CHADEMA haiombwi kwenye warsha. Iwapo chama changu, wakati muafaka ukifika na kutokana na matakwa ya jamii, kikiona nipewe jukumu lolote sitasita kutekeleza wajibu huo niwe au nisiwe mgombea.


Kwa hivyo, nilichozungumza jana ni kutoa maoni yangu kwamba muda umefika kwa Taifa letu kupunguza umri wa kugombea urais. Maoni yangu haya yanatokana na ukweli kwamba hakuna sababu zozote za kisayansi zinazomfanya mtu aliye chini ya umri wa miaka 40 akose sifa za kuwa Rais. Msimamo huu nimekuwa nao tangu zamani nikisoma shule na haujawahi kubadilika.

Hakuna mahala popote katika maoni yangu niliyotoa jana niliposema kwamba nataka umri wa urais upunguzwe ili nipate fursa ya kugombea nafasi ya urais. Pia siwezi kutaka katiba iandikwe kwa ajili yangu. Vilevile kamwe isionekane kwamba matakwa ya muda mrefu ya vijana ya kutaka umri wa kugombea Urais kupunguzwa yanalenga kunipa fursa mimi kwani mimi ni binaadamu naweza nisiwe na sifa za kuwa Rais lakini kukawa na vijana wengine wengi wenye umri chini ya miaka 40 wenye Uwezo na Uzalendo wa kutosha kushika usukani wa nchi yetu. Ni maoni yangu kwamba tupate mabadiliko ya vizazi katika uongozi wa nchi yetu ili kukabili changamoto za sasa zinazokabili Taifa letu.


Tunapojiandaa kutoa maoni kuhusu Katiba Mpya ni vizuri vyombo vya habari vikajikita kutoa taarifa bila kuweka tafsiri au kuwatafasiria maoni ambayo wananchi na viongozi watakuwa wanayatoa kuhusu maudhui ya Katiba Mpya.


Dar es Salaam
29 Februari 2012
 
Zito anajibagua sana na wana mabadiliko wenzake,tulisha mzoea yule,nafikiri udini unamsumbua sijui kwa nini asirudi ccm

zito alishapoteza mvuto, mimi binafsi simwamini japokuwa ni mtu aliyeinua chama chetu na kuvutia vijana wengi.
 
Nani atawachagua january makamba na zitto?mimi siwezi kupanga mstari masaa zaidi ya mnne kwa ajili ya hao vijana wanafiki .si bora nikaangalie tamthlia yangu ya Merlin!
 
Zito anajibagua sana na wana mabadiliko wenzake,tulisha mzoea yule,nafikiri udini unamsumbua sijui kwa nini asirudi ccm
Sio anajibagua na hilo la udini liko akilini kwako tu. Hebu tuseme ukweli, zitto akae na Lema au Sugu kweli wataelewana? Si bora hata akae na mnyika. Kweli sugu au Lema anaweza kuchangia kitu gani cha maana? Ushauri wao mkubwa ni TUANDAMANE.

Mnyika wamemuweka busy sasa Zitto kaona kijana aliebaki msomi mwenzake ni January.Hata kama chama tofauti, muhimu Taifa kwanza
 
na mimi sijaona kabisa sababu ya kumshambulia Zitto. juzi tu hapa walikuwa na Mnyika Tanga huko, kwani alikipigia debe ccm? mbona watu mnaogopa vivuli vyenu hivyo? Au kwa kuwa ................................................................................................ (jaza mwenyewe)
 
Back
Top Bottom