Zitto kufukuzwa CHADEMA siku chache zijazo

Zitto kufukuzwa CHADEMA siku chache zijazo

chikutentema

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2012
Posts
7,730
Reaction score
5,013
Ndg. wanajamvi,

Ni wazi kuwa huu msuguano ndani ya CHADEMA kuhusu kuvuliwa nyadhifa zote Bw. Zitto Kabwe ndani ya chama zitakoma.

Taarifa za kuaminika ni kwamba kikao kijacho cha Kamati Kuu (CC) kati ya tarehe 3-4 Januari, pamoja na mambo mengine kitakuwa na agenda ya kumvua uanachama mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Kaskazini.

Source: Gazeti la Raia Tanzania.
 
Kwa watanzania wanaoipenda nchi hii wataunga mkono ZZK akifukuzwa rasmi uanachama.

CC ifuate taratibu zote muhimu zilizopo, ili huyu kijana aungane rasmi na waliomtuma kudhoofisha ukombozi.
 
Natamani cc ya CDM ingemfuta uanachama hata leo. But ushauri wangu kwa wanachadema ni vizuri pia kuheshimu maamuzi yatakayotolewa na cc ya CDM. naamini watafikia maamuzi sahihi ambayo kimsingi hayatatufurahisha wote.
 
Ngoja tupo kwenye kikao cha ukoo huku moshi pamoja nakula sherehe za mwisho wa mwaka tukishatoka huku tutakuwa na maamuzi mazito. Kamati kuu ndio sisi .
 
Tena wamechelewa sana kumvua uanachama huyu dogo, ilibidi muda huu awe anaomba ubunge wa mahakama, mpigeni chini haraka hatakuwa na madhara yeyote, abaki akiwahutubia chadeccm kwa mikutano inayoratibiwa na mwigulu na nape

Kweli kabisa mimi nikiulizwa leo Mapungufu ya chama changu ktk mwaka 2013 pungufu mojawapo nitasema kuchelewa kumtoa nyoka (zzk) ndani ya nyumba(cdm)
 
Afukuzwe ili akaimalishe safu ya kumpindua mwenyekiti wa Nccr kwa kushirikiana na Kafulila.

Jamani wakati mwingine tujadili haya masuala kwa undani Kafulila (kumpindua Mbatia) na Zitto kumpindua Kamanda Mbowe. Hawa watu pia ni marafiki. Mmmmh kutakuwa kunatatizo kwa watu hawa hata hivi vyama vikishika dola waangsaliwe vizuri wanaweza kuja kupindua serikali(Ubinafsi ndilo hasa linalowatesa na usariti)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom