Zitto, kama umeshindwa kumheshimu Rais Magufuli kwa dhamana yake basi mheshimu kwa umri wake

MASIGA

Senior Member
Aug 29, 2015
130
281
Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe ni kijana ambaye miaka ya 2015 nyuma ulikuwa ni miongoni mwa vijana mahiri na wenye kujenga hoja kweli kweli, binafsi mbali na kutokufuatilia Itikadi zenu za kivyama nilikupenda na kukuheshimu sana.

Hukuwahi kuwa na siasa za kushambulia utu wa mtu, ila ulikuwa na siasa za kushambulia hoja ya mtu, " politics of agenda not inhuman politics".

Nimesoma tweet yako, binafsi nimeumia sana, na niseme tu ningekuwa na uwezo nadhani ulikuwa ni wakati muafaka wa kuvunja katiba na kukushughulikia wewe mtu mmoja ambaye unahatarisha amani ya watanzania milioni 50 na kujenga taharuki kwa kutunga uongo.

Busara inaweza tumika kukuacha uendelee na maisha yako ila nakuhakikishia Kaka yangu na kijana mwenzangu dhambi hii haitokuacha salama kama sio leo basi kesho.

Umenukuu kifungu cha katiba 37 (2) ambacho kwa hakika ni dhihaka kubwa kwa kiongozi wa nchi.

Marekani wana Demokrasia ila hawafanyi hivi,
Uingereza wana Demokrasia ila hawafanyi hivi,
Urusi wana Demokrasia ila hawathubutu kufanya hivi.
Hapa Tanzania kuna nini watu wanavuka mipaka na kudhalilisha utu tena wa Kiongozi Mkuu wa nchi?
Uhuru gani wa kuongea tunaoutaka? Ni huu wa kudhihaki na kudhalilisha utu wa Viongozi tena Mkuu wa nchi.

Zitto umeteleza tena umeteleza sana, binafsi nimeumia sana ila bado naendelea kutafakari je ni wewe ninayekufahamu uliyepita mpaka nyumbani kwetu kuomba kura kwa akili zako unafanya haya ama wewe ni kitangulizi tu?

Zitto kama umeshindwa kumuheshimu Rais Magufuli kwa dhamana aliyonayo basi muheshimu kwa umri wake.

Naamini sana katika uhuru wa mawazo na demokrasia lakini si katika kuutumia kwa ajili ya kutweza utu, kuzusha, kutunga uongo au kujenga taharuki kwa maslahi binafsi ya kisiasa.

Daud Lukanya
Kigoma Ujiji.
Daudlukanya@gmail.com
IMG-20180923-WA0086.jpeg
 
Kuzungumzia kwako kunaisapoti ile kauri ya zitto maana yule ambae hakuiona kule kaiona kwako na kumfanya aendee kuitafuta hivyo kwa kuwa umesema zitto ni wa kigoma ungemtafuta inbox ukamkumbusha na sio kufanya hivi ulivyofanya kwa hichi ulichokofanya kila mwenye akili anataungana na Mimi kukukosowa wewe kwa hili
 
Naamini hakuna sheria hata moja yenye chembe chembe ya udhalilishaji au yenye chembe za dharau. Hasa ukizingatia sheria mama ya nchi (Katiba Ya Nchi).

Sasa wewe kama unahisi hicho kifungu cha katiba kina chembe za dharau au kina dhalilisha, ungekwenda "bungeni" au "mahakamani" au "tume ya katiba na sheria" kukipinga, kifutwe ili kisiwepo kabisa.

Imekua tabu sasa, mtu ukifuata sheria za nchi ni kosa, ukivunja ni kosa.
 
Kuzungumzia kwako kunaisapoti ile kauri ya zitto maana yule ambae hakuiona kule kaiona kwako na kumfanya aendee kuitafuta hivyo kwa kuwa umesema zitto ni wa kigoma ungemtafuta inbox ukamkumbusha na sio kufanya hivi ulivyofanya kwa hichi ulichokofanya kila mwenye akili anataungana na Mimi kukukosowa wewe kwa hili
hata me nmeiona hapa
 
Mkuu umeshawahi kufika Marekani au hata kusoma au kuangalia habari zao kwenye vyombo vya habari!? Ulaya,Marekani maraisi wanafika mpaka kupigwa mayai viza na raia,....Raisi sio Mungu wananchi ndio wamemchagua kama hafanyi vile wanavyotaka wananchi ni haki ya wananchi kumsulubu Raisi wao,unakumbuka Magufuli alivyokuwa akilia alipiokuwa anaomba Kura za wananchi!!??

Sasa hivi video iliyoenea kwenye mitandao ya kijamii ni mama mmoja alieingilia mkutano wa mshauri wa Trump ambayo ilkuwa na agenda ya kuiwekea vikwazo vikubwa au mpaka kuivamia Iran kama itawezeka,...

Nimefatilia nini kimeukuta huyu mama baada ya yale aliyoyafanya,habari za kuaminika yule mama hakufunguliwa mashtaka ya aina yoyote yale,...Aliyoyafanya yule mama katika ule mkutano ni Uhuru wa kujieleza,uhuru wa kuzungumza,uhuru wa kutoa maoni, kitu ambacho Tanzania kinakosekana,..

Zitto kama mtanzania ana uhuru wa kutoa maoni yake kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania...Haya mambo ya kuheshimiwa mtu kwa mujibu wa umri ni huku Afrika na Nchi nyengine za Kiarabu wazungu hawana itikadi wala utamaduni wa kumuheshimu mtu kwa Umri...
 
Back
Top Bottom