Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, ametoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, akisisitiza kuwa kususia uchaguzi ni kosa kubwa litakalogharimu taifa kwa miaka mingine mitano ya mateso ya kisiasa na kiuchumi.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji wa Tukuyu, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya siku ya Jumamosi, Zitto amesema ingawa wananchi wamechoshwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kupinga kwao hakutakuwa na maana yoyote iwapo hawatajipanga kushiriki katika uchaguzi kwa ajili ya kuiondoa CCM madarakani kupitia sanduku la kura.
Zitto amesema kuwa ni wazi Watanzania wamechoshwa na vitendo vya wizi wa kura, upuuzwaji wa sauti zao na ufisadi wa kisiasa unaodhoofisha demokrasia. Hata hivyo, ameonya kuwa suluhisho la hayo yote siyo kukaa nyumbani au kususia uchaguzi bali kupambana kupitia ushiriki wa moja kwa moja kwenye uchaguzi.
Katika hotuba yake, Zitto ameonya wale wanaoamini kuwa mabadiliko yanaweza kuletwa bila kushiriki kwenye mchakato wa uchaguzi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwa na wagombea kutoka vyama mbadala ambao wataweza kuleta mabadiliko ya kweli kwa wananchi, huku akisema chama kinachoshiriki uchaguzi ndicho kinachopewa nafasi ya kuleta mabadiliko, si kile kinachokaa pembeni.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji wa Tukuyu, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya siku ya Jumamosi, Zitto amesema ingawa wananchi wamechoshwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kupinga kwao hakutakuwa na maana yoyote iwapo hawatajipanga kushiriki katika uchaguzi kwa ajili ya kuiondoa CCM madarakani kupitia sanduku la kura.
Zitto amesema kuwa ni wazi Watanzania wamechoshwa na vitendo vya wizi wa kura, upuuzwaji wa sauti zao na ufisadi wa kisiasa unaodhoofisha demokrasia. Hata hivyo, ameonya kuwa suluhisho la hayo yote siyo kukaa nyumbani au kususia uchaguzi bali kupambana kupitia ushiriki wa moja kwa moja kwenye uchaguzi.
Katika hotuba yake, Zitto ameonya wale wanaoamini kuwa mabadiliko yanaweza kuletwa bila kushiriki kwenye mchakato wa uchaguzi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwa na wagombea kutoka vyama mbadala ambao wataweza kuleta mabadiliko ya kweli kwa wananchi, huku akisema chama kinachoshiriki uchaguzi ndicho kinachopewa nafasi ya kuleta mabadiliko, si kile kinachokaa pembeni.