Zitto Kabwe: Soko la mahindi limeharibiwa na Serikali

Zitto Kabwe: Soko la mahindi limeharibiwa na Serikali

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,198
Reaction score
162,739
Rais Magufuli amelalamikia wasaidizi wake kwanini hawakununua Mahindi.Namkumbusha Rais kuwa marais wenzake waliotangulia walikuwa wananunua Mahindi kumlinda Mkulima ( tazama picha Hii Ripoti ya BoT ).Yeye tangu aingie hatengi fedha kwa NFRA. Tatizo Kuu la Rais ni J P Magufuli

Magufuli alipoingia madarakani alikuta NFRA Ina Reserve ya Mahindi tani 253,000. Sasa hivi kuna tani 62,000 tu. NO kuuza mahindi nje na Serikali haikununua matokeo yake bei imeshuka kutoka 120,000 kwa gunia mpaka 20,000. Kama Korosho, soko la mahindi limeharibiwa na Serikali
mahindi.jpg
 
Mambo mengi yanachangia kushuka kwa bei ya mahindi hata barabara zikuwa nzuri inachangia!
 
Alafu anatumia nguvu kubwa kutaka aonekane mzalendo huku akilaumu wasaidizi wake kumbe baadhi ya mambo yeye ndio chanzo.

Majinga hayaelewi na wala hayafuatilii kazi kushangilia tu na kusifu ujingaujinga!
sema kwa sasa mkuu 75% ya wananchi wamemstukia
 
Zitto ni mshirikina hadi anapoteza kumbukumbu amesahau kuwa yeye alitangaza baa la njaa....hahahaha na serikali ilichukua hatua ya kuuza mahindi nje na kama inge ruhusu kama kawa kabla ya kuangalia uzalishaji hakika bei ya unga ingekuwa haishikiki kabisa...
 
Zitto ni mshirikina hadi anapoteza kumbukumbu amesahau kuwa yeye alitangaza baa la njaa....hahahaha na serikali ilichukua hatua ya kuuza mahindi nje na kama inge ruhusu kama kawa kabla ya kuangalia uzalishaji hakika bei ya unga ingekuwa haishikiki kabisa...

We ni mpuuzi sasa kwanini tuzuie kuuzwa nje kwa mahindi badala ya kuongeza uzalishaji? Unawateja halafu unalalamika kuwa wateja ni wengi huo ndo upuuzi wa kiwango cha flyover ya mfugale
 
Tuna rais wa ajabu haijawahi tokea. Tatizo kubwa la pombe hana mipango yeye ni KUKURUPUKA tu litalomjia ndo hilo hilo matokeo yake mambo mengi yatakwama vibaya.
 
Huyu huyu Zitto Kabwe alibwabwaja wakati bei ya mahindi ipo juu..Ana ndimi mbili, tumtazame vizuri!
IMG_20181112_181159.jpeg
IMG_20181112_181155.jpeg
 
Back
Top Bottom