Zitto Kabwe: Msimlinganishe Bernard Membe na Edward Lowassa

Zitto Kabwe: Msimlinganishe Bernard Membe na Edward Lowassa

wanasiasa wana tabia za kimalaya hawana msimamo bahati nzuri tunaopiga kura ni sisi tunawajua vizuri wote wanafanana kitu kimoja wanakuja upinzani si kwa sababu wanapenda mageuzi bali waliamini kuwa wanastahili kuwa marais wa Tanzania na kwa sababu wapinzani wenyewe akili zao kama za kina Zitto wanajithidi kuwapamba waoneka wanamageuzi.
Zitto alikuwa anadai muda mrefu anataka kuwa mgombea urais kinachomzuia sasa hivi ni nini wakati umri unamruhusu au kwa sababu kipindi kile alikuwa anatumiwa kuvuruga upinzani?

Zito hana ujanja lazima akubali masharti ya Membe. ACT ni chama kilichoundwa kwa ufadhili wa JK, Membe, Mwigulu nk. Na lengo lilikuwa ni kupambana na cdm. Baada ya Magufuli kuingia madarakani amekata supply yote ya kundi la kina JK, Membe nk. Hapo ndio uadui wa Zito na serikali ya ccm chini ya Magufuli ulipoanzia.

Zito anajua fika cdm ndio yenye wapiga kura wengi wa upinzani, kutokana na ukweli huu, Membe anamuagiza Zito kuwashawishi cdm ili waungane kisha Membe awatumie wapinzani kama ngazi. Ila tatizo liko kwetu sisi wapiga kura hasa wa cdm, kwani bado tunaugulia uhuni wa Lowassa, na hatuko tayari kurudia kosa. Na tumeapa kuwa hatuko tayari tena kusupport muhuni yoyote toka ccm.

Nyuma ya pazia inaonekana Cdm na ACT wanapokea hela za Membe na ccm asilia isiyo upande wa Magufuli, ili agombee urais kupitia upinzani. Tatizo ni kuwa Membe kuja cdm ni kurudia kosa la Lowassa, hivyo Zito ndio anatumika kama kete. Hao akina Membe ndio wameshawishi vyama vya upinzani viache kudai tume ya uchaguzi, ndio maana unaona hakuna kelele za kudai tena tume huru, ila kushiriki uchaguzi hivyo hivyo. Hapa bila wananchi kusimama kidete, ni lazima aletwe muhuni mwingine kama Lowassa.
 
Katika hili tafakuri yangu ipo hivi:
1. Membe hana ushawishi mkubwa, na hawezi kuusaidia upinzani kwa kiwango kikubwa kufikia athari chanya zilizoletwa na Lowasa, ikiwemo kuongezeka kwa kura za upinzani na hadi kupata wabunge. Hili hata Zitto Kabwe na Maalim Seif wanalifahamu.

2. Malengo ya ACT-Wazalendo katika uchaguzi huu sio kuchukua dola, ni kupata wabunge wengi. kwa hiyo, wakimpata Membe anaweza akawasaidia kuongeza wabunge hasa ukanda wa kusini anakotokea.

3. Kwa kuwa ACT-Wazalendo wanataka wabunge tu, wako radhi kushawishi Membe apewe nafasi ya kugombea urais wakijua kuwa hawezi kupata, lakini akawasaidia kupata wabunge wengi.
Nini cha kufanya?

4. Kama Membe anataka ajiunge na upinzani kweli, basi aje bila sharti hilo la kutaka agombee urais kwa sababu ataharibu saikolojia ya wapiga kura ambao wamejipanga kupigia kura mtu ambaye wanaamini kabisa ana roho ya upinzani piga ua! Wapiga kura walioko upinzani na CCM ambao wameamua mpaka sasa kumpigia mtu mwingine, lakini sio Magufuli wanatamani kumpigia kura mtu mwenye kumudu vilivyo Magufuli jukwaani na nje ya jukwaa, kama vyombo vya dola vinawekwa kando, na huyo hawezi kuwa Membe.

5. ACT-Wazalendo waachane na mtazamo kwamba Membe anaeza kuwasaidia kupata wabunge wengi, bali wajisimamie wenyewe kwa kuwatumia akina Bwege na watu mashuhuri ndani ya CCM ambao kiroho hawapo pamoja na CCM katika kupata Rais 2020, ambao ni wengi tu huko kusini kwenyewe ambako ni target yao.

6. Kama Zitto atalazimisha, kama inavyoonekana, kumvuta Membe kwa ahadi ya urais ataharibu kwa sababu ataanza kuandaa mapema utengano wa wapinzani ambao wameanza kuaminika kuelekea uchaguzi, yaani ACT-Wazalendo na Chadema.

lakini kubwa la mwisho katika ninachokiona sasa, na ambacho kinapaswa kutopuuzwa ni kwamba: Zitto ana historia ya kutumiwa na TISS, hivyo tusipuuze mtazamo kwamba Membe na Zitto wanaweza kushirikiana kupunguza threat kwa CCM. lazima mjue kuwa tofauti na wengi wanavyojidai, ukweli ni kwamba this time CCM kina wakati mgumu sana kuelekea uchaguzi mkuu. Hizo mbwembwe zinazoonyeshwa ni za nje tu ambazo ni sehemu ya propaganda, lakini anguko lake linaweza kuwa mwaka huu kupitia sanduku la kura!
 
Naona anamvuta vuta ila CCM kiboko wameweza kuninyooshea yule alokuwa anaogopeka hata na rais aliepita
 
Katika vitu nisivyotaka kusikia ni wanasiasa yaan ningekua na uwezo wote wangeenda chini chap
 
Katika hili tafakuri yangu ipo hivi:
1. Membe hana ushawishi mkubwa, na hawezi kuusaidia upinzani kwa kiwango kikubwa kufikia athari chanya zilizoletwa na Lowasa, ikiwemo kuongezeka kwa kura za upinzani na hadi kupata wabunge. Hili hata Zitto Kabwe na Maalim Seif wanalifahamu.

2. Malengo ya ACT-Wazalendo katika uchaguzi huu sio kuchukua dola, ni kupata wabunge wengi. kwa hiyo, wakimpata Membe anaweza akawasaidia kuongeza wabunge hasa ukanda wa kusini anakotokea...


Mpaka sasa wagombea potential wa upinzani ni watatu tu,nawapanga kwa potentiality yao.
1.Tundu Lissu
2.Bernard Membe
3.Zitto Kabwe

Waliobaki ni Pumba tupu. Kama Tundu Lissu atafanikiwa kurudi huyo ndiyo mgombea bora kabisa wa upinzani,akishindwa kurudi asimamishwe Bernard Membe, ikishindikana asimame Zitto Kabwe. Otherwise kila chama kisimamishe mgombea ili kujiimarisha.
 
Membe hana Hype kama ya Lowasa.

Hilo ni tatizo, Upinzani watatumia nguvu nyingi sana kumnadi badala ya yeye kuwabeba.

Lowasa aliubeba upinzani.

Membe atabebwa na upinzani.
 
Kama Lowasa tu,Membe hawezi kukubali hayo mambo ya kwenda kushindanishwa tena na watia nia wa kwenye hivyo vyama vyenu! Never.

Uwezekano wa kushindwa ni 100% akishindanishwa na Lisu ( kama hakutakuwepo maelekezo kutoka juu lakini) na Membe hawezi kukubali hiyo fedheha ya kuwa reject hadi huko!

Isitoshe tu Zitto anapaswa atambue wenzie walishafunga pazia la kutia nia urais toka June 15.
Pointi zako zinamashiko bro! Zito amegeuka kuwa mwanasiasa uchwara thanks to mbinyo wa Magufuli. Alifika bei enzi za JK, Unfortunately, the odds have changed.
 
Back
Top Bottom