Zitto, imetosha sasa

Zitto, imetosha sasa

Tatizo hapa ni Zitto kusemea hili jambo au ni NSSF kupewa Kiwira?

Inawezekana kwamba tunapinga kwa sababu Zitto kasema au tunakubali kwa sababu Zitto kasema.

Sisi, mimi na wewe, tunasemaje?

Na Zitto hawezi kutoa amri, naamini hilo analijua na nafasi yake ya kushauri kama kamati anaifahamu. Mawazo yake ndio ya kujadiliwa. Kwa nini anasema hivi na sio vile.

Mwisho, tunawasiwasi na NSSF kutokana na uwezo au tunawasiwasi kuna watu watakula hapo katikati?

Kama ni sababu ya pili, basi tuna tatizo zaidi. Kwa nini mtu ambaye tunawasiwasi nae ndie amekabidhiwa fedha zetu na ndie anaendelea kupokea makato yetu? Kwa nini tusisafishe huo uozo tunaoungelea?

Nitarudi nikishaielewa vizuri hii mada.
 
I dont understand. Kwanza hapa umeme umekatika, washeni Dowans halafu tumzime.:hug:
 
[B said:
Lu-ma-ga[/B];1748530] Augustino Lyatonga Mrema ameamrisha kukamatwa kwa afisa wa Halmashauri ya Rombo eti kwa ubadhirifu

"boundaries" za majukumu ya kamati za bunge. waziri wa nishati na madini, kuwa ni nani kati ya William Ngeleja na January Makamba.

Hawa wenyeviti wa kamati za Nishati na Madini (Makamba), mahesabu ya Serikali za Mitaa (Mrema) na mahesabu ya Mashirika ya Umma (Zitto) QUOTE]

Tuwaache Zito, Mrema, Makamba etc wafanye kazi zao. Serikali (Executive) inafanya kazi ya Bunge na Mahakama(Judiciary). tumeona mara kadhaa serikali ikiiaamulia Bunge/Mahakama. Tanzania ya C** haina utawala wa kuzingatia hii mihimili. Ingelikuwa hivo mkwere asingalikuwa hapo alipo.
Kama mawaziri husika (executive) wameshindwa kazi wache kina Makamba et al.. (Parliament) iwasaidie. Ni kwa maslahi ya nani iyo kitu ingine.
 
Kwanza niliposikia kuwa Zitto ametoa ushauri huo nilihisi kizunguzungu! Haya Mashirika yanawakamua wananchi na sasa wanataka wawakamue hata kwenye umeme?? Kwanini wasishauri Kiwira apewe mtu au kampuni yenye uzoefu katika masuala ya umeme? Mfuko wa hifadhi ya jamii na kufua umeme, tena wa makaa ya mawe, wapi na wapi? Hapa kuna jambo limefichika!
 
Rafiki Zitto.
Nakuandia ushahuri huu kwa dhati kabisa, una haki ya kuuchukua au kuupuuza.
Nakushauri kwamba kwa jitihada ambazo umekwisha kuzifanya mpaka sasa juu ya N.S.S.F kuuziwa Mgodi wa Kiwira, ni bora ukaishia hapo ulipofikia, umesema ya kutosha, kama kweli ni ushahuri ama wako binafsi ama wakamati yako ya Bunge ni vyema ukawaachia wote unaowashauri waufanyie kazi ushauri wako ama waukatae sababu hili swala litakuchafua zaidi.

Kumbuka kwamba Watanzania wenye nia ya kurejesha ustaarabu katika utawala wa nchi yetu wamekwishapoteza imani na wewe kutokana na actions zako za muda mrefu sasa, lakini kutokana na imani kubwa sana ambayo bado wanayo kwako wanakuchukulia poa hasa kwa imani kwamba Binadamu hatujakamilika na kukosea ni sehemu ya kujifunza hasa mkosaji anapoonyesha jitihada na kisha mafanikio katika kuhakikisha harudii kosa.

Mtazamo wangu ni kwamba, nguvu za mafisadi zinakuzidia nguvu kadri ziku zinavyokwenda, na Imani yangu ni kwamba hawakuzidi nguvu by coincidence bali ni strategically kwa kukutumia, na unawasiliana nao katika hatua zako zote ambazo wewe binafsi naona kama unadhani hiyo nafasi uliyonayo ya uenyekiti wa kamati ya bunge ni kinga tosha ya kusingizia kwamba unafanya kazi za taifa.

Unayo nafasi ya kujirekebisha, japo uwezo huo sidhani kama unao tena, hasa kutokana na uko ulikofikia sasa, umefika deep water my comrade.ZITTO mafisadi wamekuzidia kiasi kwamba sasa hauna nguvu kabisa za kuisonta serikali ukiwa katika spirit ya UMA/CHADEMA, sasa hata ukijitutumua kuisonta serikali unajificha kwenye kamati ya Bunge ya nini sijui!! Sio wewe

Sasa kwa kifupi ni kwamba, N.S.S.F wanayo idara inayojishughulisha na utoaji taarifa kwa UMA, waache wao wenyewe waje (Kama haujatumwa) na kuzungumza nasi ama kwa kutupa taarifa za mpango wao wa kununua Kiwira au kwa Mapendekezo,ila hii deal uliyonayo sasa ya kujustify kwa nini wao wapewe Kiwira mimi ntakuuliza swali, kwa nini wasipewe PPF, kwa nini wasipewe PSPF.Unatakiwa kuwa consistent kama unataka tuendelee kuamini kwamba akili yako bado ni nzuri na unathink Big. Idea nzuri kabisa lakini why do you narrow to NSSF.

Kazi ya Kamati yako ya Bunge sio kuwa maafisa miradi wa Mashirika ya UMA, toa ushauri then stop there, Kama watu wanapewa ushauri mzuri alafu wanaupuuza na wao hawaji na mbadala wa mawazo na matendo shauri waondolewe. Lula MwanaNzela na Mwanakijiji wametoa hoja za msingi kama maoni yao ya kupinga mpango huu na naona tayari Umeanza kupambana nao.

Hapo Nyuma tulimpenda sana Mkwere, Tulimpenda sana Lowasa walipotugeuka na sisi tumewakataa.
Wewe sio exceptional
Hii ni camouflage lakini ushauri wangu ni kuwa mkiendelea mtaanguka zaidi sababu yake. Kwenu nyie upinzani ni kuchukia kila kitu kinachofanywa na Serikali.
 
Hii ni camouflage lakini ushauri wangu ni kuwa mkiendelea mtaanguka zaidi sababu yake. Kwenu nyie upinzani ni kuchukia kila kitu kinachofanywa na Serikali.

Fuatilia hotuba mbalimbali za viongozi wa CDM kwenye maandamano, yalikuwa ni ya ku-identify problems na kusuggest solutions. CCM kwa upande wake inaona tu watu wanaandamana wanahatarisha amani. Kinalalamika tu kwa kila jambo. CCM imekuwa kama chama cha upinzani.
 
Kaka majimshindo,

Anachosema Taifa kwanza mi nimekielewa vzuri. sidhani anakataa uwekezaji,anachozungumza ni yeye Zitto kushadadia suala hilo la NSSF kupewa hiyo kitu, na kama ukiangalia ni kweli sasa kuna mkanganyiko kati ya kamati za bunge na wizara husika kimajukumu/madaraka. Kamati zinaonekana kuwa ndio executives sasa, hata issue ya Makamba January.

All in all Zitto Zuberi si yule ambaye nilitokea kumkubali sana hapo awali kwa ukali wake dhidi ya mafinyango ya serikali/CCM. I wonder what has changed him, kama ni mafisadi ndo walivo basi nomaaaaa!
 
ndiyo maana uenyekiti wa kamati nyeti za bunge ulipangwa na kupangika vilivyo,lakini katika kutekeleza majukumu lazima tuwamulike,hatukuwa na uwezo wa kuwazuia mkalie hivyo viti wale ambao hatukiridhika na uwezo wenu
 
Napata shida kidogo kujua "boundaries" za majukumu ya kamati za bunge. Niliwahi kuanzisha thread iliyohoji nafasi ya waziri wa nishati na madini, kuwa ni nani kati ya William Ngeleja na January Makamba. Naona kuna mkanganyiko mkubwa sana wa muingiliano wa majukumu kati ya kamati na wizara. Na hii si kwa kamati ya nishati na madini pekee bali ni kwa kamati zote za bunge za msimu huu.

Inaonekana wenyeviti wa kamati na kamati zao kwa ujumla wamekuwa na sauti kubwa kushinda hata mawaziri husika. Tukichukulia kamati ya zito kwa mfano, inaitwa kamati ya hesabu za mashirika ya umma. Iweje leo iwe mstari wa mbele katika kuhakikisha ubinafsishwaji wa shirika? Hata kama hilo ni moja ya jukumu lake lakini naamini wanachopaswa ni kutoa ushauri tu na si kurasimisha ushauri wao kuwa matekelezo. Nadhani zito umenisikia.

Ndg;
those are politician they have a strategy to create public attention.
Kwa nini aite waandishi wa habari kutoa ushauri kwa shirika ambalo anajua mahali zilipo ofisi zake? na endapo utachunguza waweza gundua hajawahi hata kupeleka hayo mapendekezo in writing!!
NA HUO NDIO UBABABISHAJI UNAOTUWEKA HAPA TULIPO!!
HATUNA UTARATIBU!! TUNAJIENDEA TU KAMA KONDOO MALISHONI!!!
 
Vijana mnanifurahisha mnavyomkaushia Majimshindo, hahahaaaaa Safi sana. Kuna wawili watatu ambao inabidi kuwakumbusha kuwa kuna watu humu ndani haifai kujibizana nao wala kuongea nao. BIG UP.

Kwa wanaomtetea Zitto kwa hili, naona hawaelewi tatizo liko wapi.

Tatizo si kuwa hatuna imani na NSSF. Ukweli mbona umeandikwa tangu jana?

NSSF hawana wataalamu wa kufua umeme ila wana hela zetu sisi. Sasa watakapoamriwa kutengeneza umeme/kuchimba makaa ya mawe basi watakuwa na option mbili: Kuchukua wabia wa serikali ambao ni TANESCO au kuchukua mbia mwingine ambaye ni ********.

Huyo ****** wengi wetu tuna wasiwasi kuwa atakuwa Richmonduli aka Dowans ambaye milele ofisi zake zipo Mirambo Street na kampuni mama ni CASPIAN. Huyu bwana huyu ni kama Boomerang. Kila ukimrusha na kumtupilia mbali, yeye anakurudia. Na hapo ndipo mzizi wa fitina kalala maana UFISADI wote wanaotaka kuufanya basi utaanzia hapo.

Barabara ya Chalinze hadi Msata ilikuwa ijengwe na Wakorea. Ila wakalazimishwa wawe na Sub-contactor ambaye alikuwa ni shirika la JKT kama sikosei na huku Kikwete Mdogo akiwa kajipachika kama kupe. Cha ajabu, hela zote walipewa hawa Wabongo ambao ni Sub-Contactor na jamaa wakalala mbele na hela. Matokeo yake ni kuwa hadi leo haijajengwa wala kipande (kupanulia). Mkorea kalizwa maana hajapata hata senti tano pamoja na kuingia Bongo na vifaa vyao.

Hii ndiyo Bongo ambao inabidi kuwamulika hawa jamaa kwelikweli. Sintashangaa hawa wanaokuja kutetea hapa na kuonyesha kuwa akina Zitto na Makamba wanafanya kazi kwelikweli, ndiyo hao hao wanaozisubiri hela zitoke. HAKUNA KULALA mwaka huu. Tutakupigieni kelele hata kama mtakuja JF na kusema huu ni USHENZI, UTOTO, UPUUZI, UJINGA na kila aina ya tusi mnalolifahamu. Wengine tukiwa JKT tumetukanwa sana na hatutajali sana.

Kama mkija na mapendekezo ya KUIPA NGUVU Tanesco na kuwaachia hatimaye wenyewe wafanye kazi na nyie mkisimamia tu, tutakuwa na nyie milele. Tanesco wamekuwa wakisumbuliwa tangu Mkapa aje na ile kampuni yake ya South Africa na wakala hela mwishoni mkawafukuza. Mkaja na mbinu nyingine nyingi tu na hadi leo mmeshaona kula kwenu kuko TANESCO tu.

Ingekuwa vema KUPIGA marufuku hawa wawezekaji wengine wa UMEME na Tanesco wabaki peke yao na huku akina Zitto, Makamba, Shelukindo nk nk wakisimamia tu. Kama kazi/umeme hauzalishwi, si mfukuzani tu CEO wa Tanesco na mlete mwingine? Badala ya kuwasikiliza akina CEO, kwa nini msiwalete Wahandisi na wao watoe maoni yao?

Kibaya kinachoniudhi hapa Tanzania ni hii tabia ya viongozi waliosoma mambo ya ABUSHIRI na Tip Tip, kukaa na kuamua mambo ya Umeme, barabara, mitambo, viwanda nk wakati hata Mwanga wa nini kinaongelewa hawana. Heri wizara ya Nishati angeliwekwa Prof. Mwandosya maana akikaa na Wahandisi wenzie, wanapeana mambo in detail. Sasa hawa akina Makamba, ukiwauliza hata Transformer inavyofanya kazi hajui. Ukimwuuliza Jet Injine inafanya kazi vipi hajui. Na huyu ndiye aagize mitambo ya umeme nje au kutafuta kampuni la kuzalisha umeme Tanzania. Kweli tatizo la umeme ni Tanzania ni UONGOZI (by Mwanakijiji).
 
Hata ukiniuliza sasa hivi ni nini jukumu la bunge nadhani nitapata sifuri na kichwa kitaniuma hadi nikalazwe hospitali
 
WENYEVITI KAMATI ZA BUNGE, ACHENI KUWAGASI MAWAZIRI NA KUTUKERA WANANCHI
KWA UPAYUKAJI NA KUBWABWAJA MIDOMO KILA DAKIKA


Wenyeviti wa Kamati za Bunge, jamani nyinyi si Mawaziri chonde waacheni mawaziri wafanye kazi zao Tanzania nzima ila kwenu nyinyi eneo lenu la kazi ni mle mle ndani ya bunge na wala hatutaki kuwasikia sauti zenu mkirandaranda huku mitaani na mikogo ya ajabu.

Nyote msiojua kazi ya mwenyekiti wa kamati yoyote ya bunge basi nendeni mkachukue darasa kule Bumbuli kwa Mzee Shelukindo na jinsi UPAYUKAJI NA KUDANDIA KILA JAMBO KANA KWAMBA MMEKUA VIRANJA KATIKA DARASA LA MAWAZIRI usivyohitajika. Mtakomaaga lini nyinyi watu?? Ukimuona Lowassa Gongolamboto utadhani ama ni Waziri wa Ulinzi au wa Mambo ya Ndani.

Ukimuona Februari Ma-Ropes ndio kabisaa utadhani siku hizi William Ngeleja hana kazi tena. Ukimtazama Zitto Kabwe aka Mzee wa Michongo ya HILA ndio kabisa utadhani wizara ya fedha kiongozi wake si yule tunayemfahamu siku zote - jamani tulieni na muache UBONGO FLAVA wenu katika kazi za umma.

Japo mkanda mzima Uwenyeviti wa kamati mbalimbali bungeni ulivyotolewa na malengo yake hasa bado yanatafutiwa majibu lakini upayukaji na mikogo ya kujihisi rais waziri anapokuja kwako au wakuu wa mashirika muache. Kama unafanya kazi vizuri, hata ukiwa kimya, sisi wananchi tutajua tu na wala msilazimike kuwa PUBLI NUISANCE kiasi hiki kila leo kwa vyombo vya habari!!

Hata hivyo wakati tunapoendelea kutafuta majibu juu ya mpango mzima Uenyeviti wa Kamati Mbalimbali za bunge na jinsi zilivyogawiwa kama chapati kwa wateule, mpaka hivi sasa wengine tayari tumeshaguswa akilini kwamba wateule hawa wengi wao ni VIBARAKA AMBAO KUNGETAMANIKA WAPEWE UWAZIRI KAMILI kwenye serikali hii ya kifisadi na uchakachuaji lakini kwa kuona NOMA kwetu sisi wananchi ndio mkapewa short-cut hiyo ambayo wengine tayari mnadhania kwamba ni mabosi wa mawaziri kama si marais kwa nafasi zenu hizo.

Huruma kweli Zitto, February Ma-Ropes na Lowassa kwa mienendo yenu hii!!!!
 
Uongozi wa nchi hii ni wa ajabu sana.
Hivi hakuna job discriptions za hawa wenyeviti, mawaziri na hata wataalam katika fani mbalimbali?
Sasa hivi hawa wenyeviti wa kamati za bunge hasa hawa waliowekwa na mafisadi ni waropokaji sana kana kwamba wao ndio wasemaji wakuu, wakutoa amri za utekelezaji, wataalamu nk. Wanatia kichefuchefu. Hii kasi, ari ya kutufilisi kweli ni zaidi ya mlivyodai.
Ushauri wangu kwa hawa vijana ni kuwa uchawi hufundihswa tangu utotoni lakini kuupractice ni mpaka ufikie umri mkubwa (kungwi) angalia kama kuna akina mama vijana wanauuawa kule shinyanga. Ninyi mumepewa ufisadi kama baba zenu lakini kasi hiyo hamfiki, mtaliwa nyama kabla ya wakati.
 
Hivi Kiwira kununuliwa na NSSF kuna tatizo lipi? au Kiwira ibaki ikijifia bila mtaji na wapewe wawekezaji wa nje bila ubia na Taasisi au mashirika ya ki Tanzania ndio vyema?

Nawashangaa sana wanaoona kuwa NSSF haipaswi kuwekeza Kiwira.

Hapa issue ya Msingi na ambayo hata wewe unajifanya hujaiona ama kwa makusudi au tu we ni kilaza ni kwa nini NSSF???may be Zitto angesema Mifuko ijitolee kuwekeza na si ku pendekeza NSSF,hii ni Logic kabisa,Mawazo ya Zitto kupendekeza NSSF ipewe Kandarasi hiyo yanatofauti gani na Force za Lowassa Kuipa Richmond Kandarasi,tofauti yake ni kuwa Lowassa alikuwa PM na Zitto ni just Mwenyekiti wa Kamati tu,lakini Maudhui yao unawezakusema kuwa ni sawa,Lowasa alitaka na alishinikiza Richmond ipewe Kandarasi ya Kufua Umee,alikuwa na Personal interest pale, je Zitto akitaka NSSF ipewe hiyo Kandarasi tumueleweje??
Ifikie Mahali hata Mkeo unayempenda vp akikosea umwambie ukweli na sio kumchekea chekea tu
 
Rafiki Zitto,

Nakuandia ushahuri huu kwa dhati kabisa, una haki ya kuuchukua au kuupuuza.

Nakushauri kwamba kwa jitihada ambazo umekwisha kuzifanya mpaka sasa juu ya N.S.S.F kuuziwa Mgodi wa Kiwira, ni bora ukaishia hapo ulipofikia, umesema ya kutosha, kama kweli ni ushahuri ama wako binafsi ama wakamati yako ya Bunge ni vyema ukawaachia wote unaowashauri waufanyie kazi ushauri wako ama waukatae sababu hili swala litakuchafua zaidi.

Kumbuka kwamba Watanzania wenye nia ya kurejesha ustaarabu katika utawala wa nchi yetu wamekwishapoteza imani na wewe kutokana na actions zako za muda mrefu sasa, lakini kutokana na imani kubwa sana ambayo bado wanayo kwako wanakuchukulia poa hasa kwa imani kwamba Binadamu hatujakamilika na kukosea ni sehemu ya kujifunza hasa mkosaji anapoonyesha jitihada na kisha mafanikio katika kuhakikisha harudii kosa.

Mtazamo wangu ni kwamba, nguvu za mafisadi zinakuzidia nguvu kadri ziku zinavyokwenda, na Imani yangu ni kwamba hawakuzidi nguvu by coincidence bali ni strategically kwa kukutumia, na unawasiliana nao katika hatua zako zote ambazo wewe binafsi naona kama unadhani hiyo nafasi uliyonayo ya uenyekiti wa kamati ya bunge ni kinga tosha ya kusingizia kwamba unafanya kazi za taifa.

Unayo nafasi ya kujirekebisha, japo uwezo huo sidhani kama unao tena, hasa kutokana na uko ulikofikia sasa, umefika deep water my comrade. ZITTO mafisadi wamekuzidia kiasi kwamba sasa hauna nguvu kabisa za kuisonta serikali ukiwa katika spirit ya UMA/CHADEMA, sasa hata ukijitutumua kuisonta serikali unajificha kwenye kamati ya Bunge ya nini sijui!! Sio wewe

Sasa kwa kifupi ni kwamba, N.S.S.F wanayo idara inayojishughulisha na utoaji taarifa kwa UMA, waache wao wenyewe waje (Kama haujatumwa) na kuzungumza nasi ama kwa kutupa taarifa za mpango wao wa kununua Kiwira au kwa Mapendekezo,ila hii deal uliyonayo sasa ya kujustify kwa nini wao wapewe Kiwira mimi ntakuuliza swali, kwa nini wasipewe PPF, kwa nini wasipewe PSPF.Unatakiwa kuwa consistent kama unataka tuendelee kuamini kwamba akili yako bado ni nzuri na unathink Big. Idea nzuri kabisa lakini why do you narrow to NSSF.

Kazi ya Kamati yako ya Bunge sio kuwa maafisa miradi wa Mashirika ya UMA, toa ushauri then stop there, Kama watu wanapewa ushauri mzuri alafu wanaupuuza na wao hawaji na mbadala wa mawazo na matendo shauri waondolewe. Lula MwanaNzela na Mwanakijiji wametoa hoja za msingi kama maoni yao ya kupinga mpango huu na naona tayari Umeanza kupambana nao.

Hapo Nyuma tulimpenda sana Mkwere, Tulimpenda sana Lowasa walipotugeuka na sisi tumewakataa. Wewe sio exceptional
Zitto,
mimi nasema hivi tamaa mbaya huwa mwisho wake ni mbaya.tamaa zako za kupenda ukubwa na mambo makubwa mwisho wake siyo mzuri.anayejiinua mwenyewe Mungu humshusha daima sitashangaa kama tayari umeshahaidiwa mabilioni kama ya TANAPA.
 
Wakuu, nadhani mpango wa NSSF kununua Kiwira haukuanzishwa na Mh. Zitto, mbona hatuwasakami hao hao NSSF wanaotaka kuwekeza kwenye mradi wa kujenga bomba la gesi toka Mtwara kwenda Mombasa na Mwanza?, mradi wa kujenga UDOM, magorofa ya Mchikichini, daraja la Kigamboni etc, etc, etc...

Mimi si msemaji wa mh. Zitto isipokuwa naamini kabisa yeye binafsi amekuwa mshabiki wa suala hili kutokana na performance ya NSSF kwenye miradi yao mingine waliyokwisha fanya.

Pia imani yake inaweza kuwa inachangiwa na uwezo wa kifedha wa NSSF ukilinganisha na wawekezaji wengine ambao malengo yao makubwa ni kuchota pesa za mradi badala ya kuwekeza pesa. Mfano mzuri ni hiyo kampuni iliyoshindwa hapo Kiwira iliyokuwa ikimilikiwa na comradi Nkapa....

Mwisho nawaombeni tumuache kijana afanye kazi...ingawaje kumkosoa ni vizuri lakini ingekuwa vizuri zaidi kumkosoa pale alipo haribu na sio kumfuatilia kwa kila jambo. Kwanza kumbukeni huyu ni member mwezetu hapa jamvini, tusimfanye achukie na mwisho ajitoe jamvini...:washing:
 
Najua hii ilipoanzia!

Ule mchezo wa kulipua jengo la Uwekezaji Nairobi na kufahamisha umma kuhusu mifuko mingine kutaka kutumika. Sasa naona mmeanza kuona NSSF inaelekea kupata faida kubwa na hivyo sifa kwa utawala wake mnaanza kushambulia watu wanaotazama mema ya nchi. Siasa wekeni kando na kamwe cha juu hamtapata kwa kuwa NSSF hatutoi rushwa.

Narudia sisi ni zero corruption zone na Hosseah anajua. Zitto achana na hawa

NSSF DAMU
Join Date11th March 2011Last Activity

Naona umeamua kujiunga JF Kusafisha Mambo.
Ila tumia akili ndugu,hapa Tanzania ni NSSF tu ndo wanauwezo wa kuwekeza kiwira????
HATA HIYO YA ZITTO KUWAPIGIA CHAPUO NI RUSHWA TOSHA.... LOH
 
Nafikiri pia si kusema mifuko ijitolee. Ila la muhimu ni kuwa waje na maelezo yote kuwa NSSF watakuwa na ubiya na fulani. Na fulani huyo awe na utaalamu wa kutengeneza umeme ambalo kwa Tanzania wanabaki Tanesco peke pake.

Kwangu mie ingelikuwa busara zaidi kufanya kwamba:

"NSSF wanatoa hela na KUSIMAMIA na TANESCO wanazalisha umeme na kurudisha hela NSSF."


Hali ikiendelea hivi, basi Ikulu, Serikali na Bunge wafukuzwe na NSSF wapewe hiyo mihimili.
Hapa issue ya Msingi na ambayo hata wewe unajifanya hujaiona ama kwa makusudi au tu we ni kilaza ni kwa nini NSSF???may be Zitto angesema Mifuko ijitolee kuwekeza na si ku pendekeza NSSF,hii ni Logic kabisa,Mawazo ya Zitto kupendekeza NSSF ipewe Kandarasi hiyo yanatofauti gani na Force za Lowassa Kuipa Richmond Kandarasi,tofauti yake ni kuwa Lowassa alikuwa PM na Zitto ni just Mwenyekiti wa Kamati tu,lakini Maudhui yao unawezakusema kuwa ni sawa,Lowasa alitaka na alishinikiza Richmond ipewe Kandarasi ya Kufua Umee,alikuwa na Personal interest pale, je Zitto akitaka NSSF ipewe hiyo Kandarasi tumueleweje??
Ifikie Mahali hata Mkeo unayempenda vp akikosea umwambie ukweli na sio kumchekea chekea tu
 
Tatizo hapa ni Zitto kusemea hili jambo au ni NSSF kupewa Kiwira?

Inawezekana kwamba tunapinga kwa sababu Zitto kasema au tunakubali kwa sababu Zitto kasema.

Sisi, mimi na wewe, tunasemaje?

Na Zitto hawezi kutoa amri, naamini hilo analijua na nafasi yake ya kushauri kama kamati anaifahamu. Mawazo yake ndio ya kujadiliwa. Kwa nini anasema hivi na sio vile.

Mwisho, tunawasiwasi na NSSF kutokana na uwezo au tunawasiwasi kuna watu watakula hapo katikati?

Kama ni sababu ya pili, basi tuna tatizo zaidi. Kwa nini mtu ambaye tunawasiwasi nae ndie amekabidhiwa fedha zetu na ndie anaendelea kupokea makato yetu? Kwa nini tusisafishe huo uozo tunaoungelea?

Nitarudi nikishaielewa vizuri hii mada.
Mkuu hata mm sikuona tatizo mawazo ya zitto juu ya kiwira lakini inashtua kuona wenye mawazo tofauti kushambuliwa na kamati ya zitto tena tukiamini kwa baraka zake! Nilishatabiri bado kuna kitu nyuma ya zitto na mwisho wa siku atatushangaza! The means justify the end.Tanzania nakupenda sana na tutakufia bila woga.
 
Back
Top Bottom