Malata Junior
JF-Expert Member
- Nov 29, 2011
- 3,108
- 2,553
Heshima kwenu wakuu.
Wakati Zitto kabwe akikwaruzana na viongozi wenzake ndani ya CHADEMA alidai kuwa anapambana na mfumo WA kihafidhina ndani ya chama na kwamba alikuwa anapigania chama kuendeshwa kama taasisi na si kwa maamuzi ya MTU mmoja au watu wachache.
Baada ya kutimuliwa CHADEMA na kujiunga na ACT Zitto alijitanabaisha kwamba watajenga taasisi ya kidemokrasia yenye kutoa haki sawa kwa wanachama wote. Hivi karibuni Halmashauri kuu ya chama hicho ilitoa ratiba ya uchukuaji fomu na uteuzi wa wagombea WA nafasi za udiwani, ubunge na urais kwa tiketi ya chama hicho.
Cha ajabu hata kabla wanachama hawajaanza kuchukua fomu Zitto ameshateua na kuwatangaza watu wake watakaogombea ubunge kwenye baadhi ya majimbo bila kufuuta utaratibu wala kuteuliwa na kikao chochote! Wamefanya hivyo kwenye majimbo ya Bukombe, Kahama, Mbowe, Biharamulo na sasa baadhi ya wanachama wanaotaka kugombea kwenye majimbo hayo wameanza kulalamika.
Kwa demokrasia hii ya Zitto ni halali kweli au ndiyo udikteta unaanza kukijenga kwenye chama hicho?
Wakati Zitto kabwe akikwaruzana na viongozi wenzake ndani ya CHADEMA alidai kuwa anapambana na mfumo WA kihafidhina ndani ya chama na kwamba alikuwa anapigania chama kuendeshwa kama taasisi na si kwa maamuzi ya MTU mmoja au watu wachache.
Baada ya kutimuliwa CHADEMA na kujiunga na ACT Zitto alijitanabaisha kwamba watajenga taasisi ya kidemokrasia yenye kutoa haki sawa kwa wanachama wote. Hivi karibuni Halmashauri kuu ya chama hicho ilitoa ratiba ya uchukuaji fomu na uteuzi wa wagombea WA nafasi za udiwani, ubunge na urais kwa tiketi ya chama hicho.
Cha ajabu hata kabla wanachama hawajaanza kuchukua fomu Zitto ameshateua na kuwatangaza watu wake watakaogombea ubunge kwenye baadhi ya majimbo bila kufuuta utaratibu wala kuteuliwa na kikao chochote! Wamefanya hivyo kwenye majimbo ya Bukombe, Kahama, Mbowe, Biharamulo na sasa baadhi ya wanachama wanaotaka kugombea kwenye majimbo hayo wameanza kulalamika.
Kwa demokrasia hii ya Zitto ni halali kweli au ndiyo udikteta unaanza kukijenga kwenye chama hicho?