GE2025 Zitto: CCM Watueleze wamefanya nini Miaka Mitano

GE2025 Zitto: CCM Watueleze wamefanya nini Miaka Mitano

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amehoji utendaji wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, akieleza kuwa yeye tayari ameonesha dira (vision) yake kwa Ujiji na kueleza mambo ya msingi yanayopaswa kufanyika ili mji huo urejeshe heshima yake ya kihistoria

Akihutubia mkutano wa kampeni katika Kata ya Kitongoni, Septemba 26, 2025 Zitto alisema:

"Sisi si tumeondoka 2020, wenyeviti wa serikali za mitaa walikuwa wa chama gani? Madiwani walikuwa chama gani? Mbunge chama gani? Rais chama gani? Soko wamejenga? Sasa kwanini mhangaike na miaka mitano ile ya juzi, miaka yenu mitano hamsemi mmefanya nini."

Soma pia

 
Zitto aache upuuzi. Anataka ubunge kupitia mbeleko ya mwenyekiti wa CCM halafu bado anajifanya hajui kilichofanywa na CCM kwa miaka mitano? Ni wajibu wa Zitto kuwaambia wananchi mambo makubwa yaliyofanywa na CCM chini ya Mama Samia.
 
Ipo siku uyu Bwa mzito atakosa pa kuficha sura yake, niseme ukweli kama uchaguzi huu ungekua wa haki , binafsi ningeenda jimboni mwake kuomba wananchi wampe kura yoyote ila sio uyu Bwana mzito, ujinga mwingi sana, hivi kigoma tulimkosea nini Mungu why tumejaa unafiki sana,,sio kwa wanasiasa , wasanii ,tuna mambo ya kijinga sana,

Watani zetu wahaya tunawasemaga ni wajuaji ila hawatuzidi sie waha
 
Back
Top Bottom